Atheism sio kuamini Hakuna Mungu, ila ni kutoamini kuwa kuna Mungu

Atheism sio kuamini Hakuna Mungu, ila ni kutoamini kuwa kuna Mungu

Mcqueenen

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2019
Posts
6,843
Reaction score
11,702
Wanaoamani Mungu hutumia uumbaji kama hoja kuu ya kuamini Mungu yupo, siwalaumu because after all bila uumbaji tusingekuwepo kubishana hapa kama mungu yupo au la! Na uwepo wake usingekuwa na maana.

Hoja yao ipo hivi:

1. kila kitu kilichopo kina chanzo hakiwezi kutokea from nothing,

2. Hivyo Ulimwengu una chanzo, hiko chanzo lazima kitakuwa nje ya ulimwengu na kitakuwa na uwezo zaidi ya ulimwengu

3. Kwahyo ulimwengu umeumbwa na huyo aliyeuumba tunamwita Mungu

Kuna matatizo kwenye kila statement hapo,. Ngoja tuzichambue

1. Kila kitu kilichopo kina chanzo hakiwezi kutokea from nothing,

Hatuna ushahidi wa hili.

Kwanza tunaishi kwenye sayari ndogo inayozunguka nyota moja kati ya nyota billioni 100 zinazounda galaxy. Ulimwengu unaoonekana tu una galaxy billion 100-200. Kwahyo hapo idadi ya nyota ni kama billioni 100 mara billioni 100 kwa idadi ya chini, na bado kuna ulimwengu ule ambao hatuuoni ambao unaweza kuwa mkubwa kuliko huu tunaouona kwa vifaa vyetu.

Kwahyo hatuwezi kuhitimisha kitu hakiwezekani kwenye huu ulimwengu kwa kutumia reference ya sheria tunazoziona kwenye haka kapocket kadogo ka ulimwengu tunakoishi. Inawezekana huko nyota ya mbali kuna viumbe wameweza kutengeneza something from nothing.

Sisi hatuwezi kuhitimisha chochote itakuwa ni sawa na mgeni kutoka Kigoma afikie kwa shemeji yake Chanika, aitalii nyumba ya shemeji kuanzia sebuleni,uani mpaka chooni halafu aseme ameshaijua Dar nzima na hakuna nyumba ya muundo tofauti na hiyo ya shemeji yake. Hakuna TV kama ya shemeji yake na hakuna gari kama la shemeji yake Dar nzima.

Pili, hata kwenye hiki kipoketi cha ulimwengu tunachoishi hatuna uhakika kuwa tunajua sheria zote za ulimwengu.

Ukimwambia mzee aliyekufa miaka 50 iliyopita kuwa Kuna teknolojia ya kuongea na mtu ana kwa ana sekunde hiyohiyo huku mkisikiana kama mko pamoja(Videocall) Atabisha kuwa hiko kitu hakiwezekani kama tunavyobisha kuwa something hakiwezi kutoka from nothing.

Hivyo hatuna ushahidi wowote wa kuhitimisha kuwa haiwezekani kitu kitokee bila chanzo.

2. Hivyo Ulimwengu una chanzo, hiko chanzo lazima kitakuwa nje ya ulimwengu na kitakuwa na uwezo zaidi ya ulimwengu

Hata kama tukikubali kuwa Ulimwengu una chanzo,bado haithibitishi kuwa hiko chanzo lazima kiwe nje ya ulimwengu au kiwe na uwezo zaidi ya ulimwengu…Maji kwenye glass hayana madhara lakini yakiungana kutengeneza bahari yanaweza kuzamisha meli na kuleta Tsunami.

Pia hiko Chanzo kinaweza kuwa ulimwengu wenyewe,
Hizo sifa unazompa Mungu inawezekana ni sifa za ulimwengu.Yani ikiwa ulimwengu umejitengeneza,upo kila sehemu na unaweza kila kitu.
Maana Mtu ukibisha kwa kusema ulimwengu lazima uwe na chanzo kwasababu kila kitu kina chanzo basi ntakuambia na mungu pia yupo kwenye hiyo “kila kitu kinahitaji chanzo” na ukibadilisha kuwa kila kitu kinahitaji chanzo kasoro Mungu tu basi ntakuuliza nini kinampa Mungu hiyo kasoro?? Kwanini isiwe kila kitu kinahitaji chanzo kasoro ulimwengu wenyewe? Au chanzo kingine kisicho huyo ‘Mungu’?

3. Kwahyo ulimwengu umeumbwa na huyo aliyeuumba tunamwita Mungu

Na hata kama tukikubali ulimwengu umeumbwa bado haitoshi kujua kuwa huyo aliyeumba ni Mungu na wengine huenda mbali hadi kumpa sifa zingine kama i)aliwahi kuwa binadamu akaja kufa duniani, au wengine husema huyo ii)Mungu haelewi lugha tofauti na kiarabu

Haya yote mmejuaje? Je kama hiko chanzo ni kitu kingine ambacho hakipo tena ulimwenguni,yani kiliumba halafu kikaondoka kikauacha ulimwengu ujiendeshe kwa sheria kilizouwekea? Una uthibitisho gani kuwa hiko chanzo cha ulimwengu ndio hiki unachoita Mungu na si kingine??

Kwasababu kusema ulimwengu uliumbwa haitoshi kuwa kama ushahidi wa kuwa aliyeuumba ni Mungu.

Au una ushahidi kuwa lazima kiwe Mungu na especially huyo Mungu wako na sio Mungu wa Zumaridi? Au kitu tofauti na Mungu?? Vipa kama Mungu aliumba Ulimwengu halafu akaondoka akaendelea na mishe zake akawcha ujiendeshe na tukifa ndio imetoka hiyo?? Kwanini iwe ni Mungu wako tu?? Una uthibitisho?

Nachosema Mimi ni kuwa Mungu anaweza kuwepo, ila hatuna ushahidi wa hilo. Na hatuna sababu za kuamini hilo kama unao naomba

Maana ukisema ushahidi ni kitabu chako cha dini kilikuambia hivyo basi hiko hiko kitabu naomba ukiulize haya maswali unipe majibu
 
Tumuite Mungu, japo nikiulizwa kwanini awe ni Mungu na si kitu kingine tu nisichokijua, nitakuwa sina jibu.
Hii dunia ni full mysterious, actually hakuna anajua chanzo cha ulimwengu na uhai but kuna Imani ina make logic sense ukisikiliza, sihitaji kuelezea isije semwa ninaihubiri.

Kuna nguvu inaendesha hii dunia na haijali hisia zetu,it acts accordingly na haitafuti waumini wa kuiamini.

Sikumbuki mwaka, coz ni kitambo niliwai ona watu wakitembea kwenye mbalamwezi wakati nimetoka nje kukojoa.
Nilihisi ni wenge BCBG, Nikarudi ndani kumuambia Mama kuwa kuna kitu cha ajabu nje, watu wanatembea kwenye mwezi.. Ilimchukua sekunde kadhaa kuhisi kuwa uenda kuna kitu si cha kawaida nimekiona nje ndiyo maana ninamuamsha ili akakione. akaamuka na Dada zangu wakaamka kwenda kushuhudia nilichokuwa nina kisema!!.
Ni yale majira ya mwezi Unatokeza fully, umbo lote unaliona.. Ni kama vile sinema watu wanatembea kwenye mwezi.
Niliowaita kuona ilo tukio waliogopa sana!! dada yangu ninaemfuta mara 3 akasema " twende kwa mzee wa kanisa, uenda leo ni siku ya mwisho".
Baada ya hapo ile sinema ikakata mwezi ukarudi katika hali yake.
Hadi leo wengine wamezeeka, nikijalibu kuwa kumbushia hiyo ilo tukio kila mmoja ana maoni yake.
Hivi juzi nimekuja kujua kuhusu mradi wa blue beam, uenda tulichokishuhudia ni blue beam ama ni tukio la miujiza tu kama miujiza mingine.. But definitely nimewai ona watu wakitembea kwenye mwezi. mwezi huu huu UnAujua, nimeona bila vifaa vya kitaalamu.
Ulimwengu ni zaidi ya unavyoelezwa na atheists ama believers.
 
Tumuite Mungu, japo nikiulizwa kwanini awe ni Mungu na si kitu kingine tu nisichokijua, nitakuwa sina jibu.
Hii dunia ni full mysterious, actually hakuna anajua chanzo cha ulimwengu na uhai but kuna Imani ina make logic sense ukisikiliza, sihitaji kuelezea isije semwa ninaihubiri.

Kuna nguvu inaendesha hii dunia na haijali hisia zetu,it acts accordingly na haitafuti waumini wa kuiamini.

Sikumbuki mwaka, coz ni kitambo niliwai ona watu wakitembea kwenye mbalamwezi wakati nimetoka nje kukojoa.
Nilihisi ni wenge BCBG, Nikarudi ndani kumuambia Mama kuwa kuna kitu cha ajabu nje, watu wanatembea kwenye mwezi.. Ilimchukua sekunde kadhaa kuhisi kuwa uenda kuna kitu si cha kawaida nimekiona nje ndiyo maana ninamuamsha ili akakione. akaamuka na Dada zangu wakaamka kwenda kushuhudia nilichokuwa nina kisema!!.
Ni yale majira ya mwezi Unatokeza fully, umbo lote unaliona.. Ni kama vile sinema watu wanatembea kwenye mwezi.
Niliowaita kuona ilo tukio waliogopa sana!! dada yangu ninaemfuta mara 3 akasema " twende kwa mzee wa kanisa, uenda leo ni siku ya mwisho".
Baada ya hapo ile sinema ikakata mwezi ukarudi katika hali yake.
Hadi leo wengine wamezeeka, nikijalibu kuwa kumbushia hiyo ilo tukio kila mmoja ana maoni yake.
Hivi juzi nimekuja kujua kuhusu mradi wa blue beam, uenda tulichokishuhudia ni blue beam ama ni tukio la miujiza tu kama miujiza mingine.. But definitely nimewai ona watu wakitembea kwenye mwezi. mwezi huu huu UnAujua, nimeona bila vifaa vya kitaalamu.
Ulimwengu ni zaidi ya unavyoelezwa na atheists ama believers.
Mwezi hauko chumbani kwako,Kitu chochote kwenye mwezi kingeonekana dunia nzima.
Wewe kuona na dada zako mauzauza sio uthibitisho wa kuwepo kwa Mungu.

Kuna kipindi watu wa Mwanza waliona usiku kuna mwanga mkali angani unatembea ukizunguka anga.. wakasema ni yesu anarudi lakini kumbe zilikuwa zile taa za club ya Villa park.
 
Mwezi hauko chumbani kwako,Kitu chochote kwenye mwezi kingeonekana dunia nzima.
Wewe kuona na dada zako mauzauza sio uthibitisho wa kuwepo kwa Mungu.

Kuna kipindi watu wa Mwanza waliona usiku kuna mwanga mkali angani unatembea ukizunguka anga.. wakasema ni yesu anarudi lakini kumbe zilikuwa zile taa za club ya Villa park.
Ni wapi nimesema nilichokiona/tulichokiona ni uthibitisho wa Mungu ?
Kwanini umekimbia kwenye uwepo aa Mungu na si project ya blue beam?.
Hukuona pahara nilipoongelea project ya blue beam?
Huku ona pahari nilipoongelea juu ya mawazo ya atheists na believers?.
Ni nini kimekutia upofu katika sentisi zingine za comment yangu hata ukoanna swala la Mungu na si kitu kingine?.
Upo obsessed na maswala ya Mungu ndiyo maana umekimbia uko, ingelikuwa ni kinyume chake usingekimbilia uko.
Nb:- ujifunze kusoma kwa ufahamu.
 
Mimi na Mungu iko hivi..
Huwa mimi na yeye Tunazungumza.
Namuuliza swali ananijibu, ananimbiaga hapendi nini na anapenda nini na kuna vitu kanipa na kuna vitu kaniahidi atanipa.

Sifa yake kubwa yeye ndie kaniumba. na Kaumba dunia yote na ulimwengu.
 
Wanaoamani Mungu hutumia uumbaji kama hoja kuu ya kuamini Mungu yupo, siwalaumu because after all bila uumbaji tusingekuwepo kubishana hapa kama mungu yupo au la! Na uwepo wake usingekuwa na maana.

Hoja yao ipo hivi:

1. kila kitu kilichopo kina chanzo hakiwezi kutokea from nothing,

2. Hivyo Ulimwengu una chanzo, hiko chanzo lazima kitakuwa nje ya ulimwengu na kitakuwa na uwezo zaidi ya ulimwengu

3. Kwahyo ulimwengu umeumbwa na huyo aliyeuumba tunamwita Mungu

Kuna matatizo kwenye kila statement hapo,. Ngoja tuzichambue

1. Kila kitu kilichopo kina chanzo hakiwezi kutokea from nothing,

Hatuna ushahidi wa hili.

Kwanza tunaishi kwenye sayari ndogo inayozunguka nyota moja kati ya nyota billioni 100 zinazounda galaxy. Ulimwengu unaoonekana tu una galaxy billion 100-200. Kwahyo hapo idadi ya nyota ni kama billioni 100 mara billioni 100 kwa idadi ya chini, na bado kuna ulimwengu ule ambao hatuuoni ambao unaweza kuwa mkubwa kuliko huu tunaouona kwa vifaa vyetu.

Kwahyo hatuwezi kuhitimisha kitu hakiwezekani kwenye huu ulimwengu kwa kutumia reference ya sheria tunazoziona kwenye haka kapocket kadogo ka ulimwengu tunakoishi. Inawezekana huko nyota ya mbali kuna viumbe wameweza kutengeneza something from nothing.

Sisi hatuwezi kuhitimisha chochote itakuwa ni sawa na mgeni kutoka Kigoma afikie kwa shemeji yake Chanika, aitalii nyumba ya shemeji kuanzia sebuleni,uani mpaka chooni halafu aseme ameshaijua Dar nzima na hakuna nyumba ya muundo tofauti na hiyo ya shemeji yake. Hakuna TV kama ya shemeji yake na hakuna gari kama la shemeji yake Dar nzima.

Pili, hata kwenye hiki kipoketi cha ulimwengu tunachoishi hatuna uhakika kuwa tunajua sheria zote za ulimwengu.

Ukimwambia mzee aliyekufa miaka 50 iliyopita kuwa Kuna teknolojia ya kuongea na mtu ana kwa ana sekunde hiyohiyo huku mkisikiana kama mko pamoja(Videocall) Atabisha kuwa hiko kitu hakiwezekani kama tunavyobisha kuwa something hakiwezi kutoka from nothing.

Hivyo hatuna ushahidi wowote wa kuhitimisha kuwa haiwezekani kitu kitokee bila chanzo.

2. Hivyo Ulimwengu una chanzo, hiko chanzo lazima kitakuwa nje ya ulimwengu na kitakuwa na uwezo zaidi ya ulimwengu

Hata kama tukikubali kuwa Ulimwengu una chanzo,bado haithibitishi kuwa hiko chanzo lazima kiwe nje ya ulimwengu au kiwe na uwezo zaidi ya ulimwengu…Maji kwenye glass hayana madhara lakini yakiungana kutengeneza bahari yanaweza kuzamisha meli na kuleta Tsunami.

Pia hiko Chanzo kinaweza kuwa ulimwengu wenyewe,
Hizo sifa unazompa Mungu inawezekana ni sifa za ulimwengu.Yani ikiwa ulimwengu umejitengeneza,upo kila sehemu na unaweza kila kitu.
Maana Mtu ukibisha kwa kusema ulimwengu lazima uwe na chanzo kwasababu kila kitu kina chanzo basi ntakuambia na mungu pia yupo kwenye hiyo “kila kitu kinahitaji chanzo” na ukibadilisha kuwa kila kitu kinahitaji chanzo kasoro Mungu tu basi ntakuuliza nini kinampa Mungu hiyo kasoro?? Kwanini isiwe kila kitu kinahitaji chanzo kasoro ulimwengu wenyewe? Au chanzo kingine kisicho huyo ‘Mungu’?

3. Kwahyo ulimwengu umeumbwa na huyo aliyeuumba tunamwita Mungu

Na hata kama tukikubali ulimwengu umeumbwa bado haitoshi kujua kuwa huyo aliyeumba ni Mungu na wengine huenda mbali hadi kumpa sifa zingine kama i)aliwahi kuwa binadamu akaja kufa duniani, au wengine husema huyo ii)Mungu haelewi lugha tofauti na kiarabu

Haya yote mmejuaje? Je kama hiko chanzo ni kitu kingine ambacho hakipo tena ulimwenguni,yani kiliumba halafu kikaondoka kikauacha ulimwengu ujiendeshe kwa sheria kilizouwekea? Una uthibitisho gani kuwa hiko chanzo cha ulimwengu ndio hiki unachoita Mungu na si kingine??

Kwasababu kusema ulimwengu uliumbwa haitoshi kuwa kama ushahidi wa kuwa aliyeuumba ni Mungu.

Au una ushahidi kuwa lazima kiwe Mungu na especially huyo Mungu wako na sio Mungu wa Zumaridi? Au kitu tofauti na Mungu?? Vipa kama Mungu aliumba Ulimwengu halafu akaondoka akaendelea na mishe zake akawcha ujiendeshe na tukifa ndio imetoka hiyo?? Kwanini iwe ni Mungu wako tu?? Una uthibitisho?

Nachosema Mimi ni kuwa Mungu yupo, ila hatuna ushahidi wa hilo.kama unao naomba

Maana ukisema ushahidi ni kitabu chako cha dini kilikuambia hivyo basi hiko hiko kitabu naomba ukiulize haya maswali unipe majibu
Argument from ignorance hizo. Ndo Yale mambo ya Thomas Aquinas kwamba first mover must be God. Ni ujinga tu na uvivu wa kufikiri. Kuumbwa na Mungu na kufata sheria za muarabu ni vitu 45682 tofauti. Nakubaliana na hoja yako
 
Kinachonipa Imani kwa Mungu wangu ni kuwa, Huwa mimi na yeye Tunazungumza.
Namuuliza swali ananijibu, animbiaga hapendi nini na anapenda nini na kuna vitu kanipa na kuna vitu kanihaidi atamipa.

Sifa yake kubwa yeye ndie kaniumba. na Kaumbo dunia yote na ulimwengu.
Huyo Mungu wako unayemsema na akili yako ndo maana hawezi kukuambia kitu ambacho hutaki. Kama unabisha mwambie akuambie ujikate paja..
 
Tumuite Mungu, japo nikiulizwa kwanini awe ni Mungu na si kitu kingine tu nisichokijua, nitakuwa sina jibu.
Hii dunia ni full mysterious, actually hakuna anajua chanzo cha ulimwengu na uhai but kuna Imani ina make logic sense ukisikiliza, sihitaji kuelezea isije semwa ninaihubiri.

Kuna nguvu inaendesha hii dunia na haijali hisia zetu,it acts accordingly na haitafuti waumini wa kuiamini.

Sikumbuki mwaka, coz ni kitambo niliwai ona watu wakitembea kwenye mbalamwezi wakati nimetoka nje kukojoa.
Nilihisi ni wenge BCBG, Nikarudi ndani kumuambia Mama kuwa kuna kitu cha ajabu nje, watu wanatembea kwenye mwezi.. Ilimchukua sekunde kadhaa kuhisi kuwa uenda kuna kitu si cha kawaida nimekiona nje ndiyo maana ninamuamsha ili akakione. akaamuka na Dada zangu wakaamka kwenda kushuhudia nilichokuwa nina kisema!!.
Ni yale majira ya mwezi Unatokeza fully, umbo lote unaliona.. Ni kama vile sinema watu wanatembea kwenye mwezi.
Niliowaita kuona ilo tukio waliogopa sana!! dada yangu ninaemfuta mara 3 akasema " twende kwa mzee wa kanisa, uenda leo ni siku ya mwisho".
Baada ya hapo ile sinema ikakata mwezi ukarudi katika hali yake.
Hadi leo wengine wamezeeka, nikijalibu kuwa kumbushia hiyo ilo tukio kila mmoja ana maoni yake.
Hivi juzi nimekuja kujua kuhusu mradi wa blue beam, uenda tulichokishuhudia ni blue beam ama ni tukio la miujiza tu kama miujiza mingine.. But definitely nimewai ona watu wakitembea kwenye mwezi. mwezi huu huu UnAujua, nimeona bila vifaa vya kitaalamu.
Ulimwengu ni zaidi ya unavyoelezwa na atheists ama believers.
Hicho mlichoona ni hallucinations, Ureno watu 3000 waliona jua linacheza cheza.
 
Ni wapi nimesema nilichokiona/tulichokiona ni uthibitisho wa Mungu ?
Kwanini umekimbia kwenye uwepo aa Mungu na si project ya blue beam?.
Hukuona pahara nilipoongelea project ya blue beam?
Huku ona pahari nilipoongelea juu ya mawazo ya atheists na believers?.
Ni nini kimekutia upofu katika sentisi zingine za comment yangu hata ukoanna swala la Mungu na si kitu kingine?.
Upo obsessed na maswala ya Mungu ndiyo maana umekimbia uko, ingelikuwa ni kinyume chake usingekimbilia uko.
Nb:- ujifunze kusoma kwa ufahamu.
Andiko lako tu umeanza kwa kusema tumuite Mungu, halafu unasema mimi ndo niko wrong kukimbilia Mungu na sio project blue beam.
Kama ulikuwa huongelei mungu ulipoongelea supernatural kwenye mwezi bali ulikuwa unaongelea project blue beam basi sasa hiyo inahusiana nini na hii mada??

Nimeeleza hata hizi simu tunzotumia kuwasiliana na watu wa mbali,, kwa zamani ungemweleza mtu hiko kitu angesema ni supernatural
 
Andiko lako tu umeanza kwa kusema tumuite Mungu, halafu unasema mimi ndo niko wrong kukimbilia Mungu na sio project blue beam.
Kama ulikuwa huongelei mungu ulipoongelea supernatural kwenye mwezi bali ulikuwa unaongelea project blue beam basi sasa hiyo inahusiana nini na hii mada??

Nimeeleza hata hizi simu tunzotumia kuwasiliana na watu wa mbali,, kwa zamani ungemweleza mtu hiko kitu angesema ni supernatural
Hakika, sikupingi
 
Mimi na Mungu iko hivi..
Huwa mimi na yeye Tunazungumza.
Namuuliza swali ananijibu, animbiaga hapendi nini na anapenda nini na kuna vitu kanipa na kuna vitu kanihaidi atamipa.
Hauzuiwi kuwa hivi,, mi mwenyewe nilipokuwa mdogo nilikuwa nina imaginary friend yani rafiki wa kufikirika..Nilikuwa nina uwezo wa kupiga naye story mpaka watu wa karibu wakaanza kuamini kuwa yupo kweli,, nilikuwa naweza kumuomba ushauri na sometimes alikuwa ananikataza vitu..

Mtu angeweza kuniagiza kitu nikakataa kwa kusema imaginary friend wangu amenikataza.
Na of course nilikuwa nakataa vitu nisivyovipenda,, asingeweza kunikataza kula nyama.
Kuna muda nilizama kwenye hiyo delusion npaka mimi mwenyewe niliamini huyo imaginary friend yupo.
Sifa yake kubwa yeye ndie kaniumba. na Kaumbo dunia yote na ulimwengu.
Sasa hapa ndo unakosea kuhitimisha bila kuweka ushahidi.,., Unaweza kuthibitisha hizi claims??
 
Sasa hapa ndo unakosea.,., Unaweza kuthibitisha hizi claims??
Sijasema ninavithibitisho vyovyote kuhusu uwepo wa Mungu wangu.

Sinaaaa

Kwasababu nikiwa naongea nae wewe huwezi kusikia.

Wewe huyo rafiki yako uliyekua unaongea nae kakupa nini ?? Maana mimi wakwangu kuna vitu vingi sana kanipa.
 
Wanaoamani Mungu hutumia uumbaji kama hoja kuu ya kuamini Mungu yupo, siwalaumu because after all bila uumbaji tusingekuwepo kubishana hapa kama mungu yupo au la! Na uwepo wake usingekuwa na maana.

Hoja yao ipo hivi:

1. kila kitu kilichopo kina chanzo hakiwezi kutokea from nothing,

2. Hivyo Ulimwengu una chanzo, hiko chanzo lazima kitakuwa nje ya ulimwengu na kitakuwa na uwezo zaidi ya ulimwengu

3. Kwahyo ulimwengu umeumbwa na huyo aliyeuumba tunamwita Mungu

Kuna matatizo kwenye kila statement hapo,. Ngoja tuzichambue

1. Kila kitu kilichopo kina chanzo hakiwezi kutokea from nothing,

Hatuna ushahidi wa hili.

Kwanza tunaishi kwenye sayari ndogo inayozunguka nyota moja kati ya nyota billioni 100 zinazounda galaxy. Ulimwengu unaoonekana tu una galaxy billion 100-200. Kwahyo hapo idadi ya nyota ni kama billioni 100 mara billioni 100 kwa idadi ya chini, na bado kuna ulimwengu ule ambao hatuuoni ambao unaweza kuwa mkubwa kuliko huu tunaouona kwa vifaa vyetu.

Kwahyo hatuwezi kuhitimisha kitu hakiwezekani kwenye huu ulimwengu kwa kutumia reference ya sheria tunazoziona kwenye haka kapocket kadogo ka ulimwengu tunakoishi. Inawezekana huko nyota ya mbali kuna viumbe wameweza kutengeneza something from nothing.

Sisi hatuwezi kuhitimisha chochote itakuwa ni sawa na mgeni kutoka Kigoma afikie kwa shemeji yake Chanika, aitalii nyumba ya shemeji kuanzia sebuleni,uani mpaka chooni halafu aseme ameshaijua Dar nzima na hakuna nyumba ya muundo tofauti na hiyo ya shemeji yake. Hakuna TV kama ya shemeji yake na hakuna gari kama la shemeji yake Dar nzima.

Pili, hata kwenye hiki kipoketi cha ulimwengu tunachoishi hatuna uhakika kuwa tunajua sheria zote za ulimwengu.

Ukimwambia mzee aliyekufa miaka 50 iliyopita kuwa Kuna teknolojia ya kuongea na mtu ana kwa ana sekunde hiyohiyo huku mkisikiana kama mko pamoja(Videocall) Atabisha kuwa hiko kitu hakiwezekani kama tunavyobisha kuwa something hakiwezi kutoka from nothing.

Hivyo hatuna ushahidi wowote wa kuhitimisha kuwa haiwezekani kitu kitokee bila chanzo.

2. Hivyo Ulimwengu una chanzo, hiko chanzo lazima kitakuwa nje ya ulimwengu na kitakuwa na uwezo zaidi ya ulimwengu

Hata kama tukikubali kuwa Ulimwengu una chanzo,bado haithibitishi kuwa hiko chanzo lazima kiwe nje ya ulimwengu au kiwe na uwezo zaidi ya ulimwengu…Maji kwenye glass hayana madhara lakini yakiungana kutengeneza bahari yanaweza kuzamisha meli na kuleta Tsunami.

Pia hiko Chanzo kinaweza kuwa ulimwengu wenyewe,
Hizo sifa unazompa Mungu inawezekana ni sifa za ulimwengu.Yani ikiwa ulimwengu umejitengeneza,upo kila sehemu na unaweza kila kitu.
Maana Mtu ukibisha kwa kusema ulimwengu lazima uwe na chanzo kwasababu kila kitu kina chanzo basi ntakuambia na mungu pia yupo kwenye hiyo “kila kitu kinahitaji chanzo” na ukibadilisha kuwa kila kitu kinahitaji chanzo kasoro Mungu tu basi ntakuuliza nini kinampa Mungu hiyo kasoro?? Kwanini isiwe kila kitu kinahitaji chanzo kasoro ulimwengu wenyewe? Au chanzo kingine kisicho huyo ‘Mungu’?

3. Kwahyo ulimwengu umeumbwa na huyo aliyeuumba tunamwita Mungu

Na hata kama tukikubali ulimwengu umeumbwa bado haitoshi kujua kuwa huyo aliyeumba ni Mungu na wengine huenda mbali hadi kumpa sifa zingine kama i)aliwahi kuwa binadamu akaja kufa duniani, au wengine husema huyo ii)Mungu haelewi lugha tofauti na kiarabu

Haya yote mmejuaje? Je kama hiko chanzo ni kitu kingine ambacho hakipo tena ulimwenguni,yani kiliumba halafu kikaondoka kikauacha ulimwengu ujiendeshe kwa sheria kilizouwekea? Una uthibitisho gani kuwa hiko chanzo cha ulimwengu ndio hiki unachoita Mungu na si kingine??

Kwasababu kusema ulimwengu uliumbwa haitoshi kuwa kama ushahidi wa kuwa aliyeuumba ni Mungu.

Au una ushahidi kuwa lazima kiwe Mungu na especially huyo Mungu wako na sio Mungu wa Zumaridi? Au kitu tofauti na Mungu?? Vipa kama Mungu aliumba Ulimwengu halafu akaondoka akaendelea na mishe zake akawcha ujiendeshe na tukifa ndio imetoka hiyo?? Kwanini iwe ni Mungu wako tu?? Una uthibitisho?

Nachosema Mimi ni kuwa Mungu yupo, ila hatuna ushahidi wa hilo.kama unao naomba

Maana ukisema ushahidi ni kitabu chako cha dini kilikuambia hivyo basi hiko hiko kitabu naomba ukiulize haya maswali unipe majibu
Think out of the box. Ukienda Korea Kaskazini, Mungu wao ni Kim Il Sung na uzazi wake. Ukienda India kwa Wahindu kuna Miungu lukuki kila mmoja ana nafasi yake katika maisha. Na wote wanaishi vizuri kwenye imani zao. Point hapa usijikite tu kwenye imani za Ukristo/Uislamu. Hii dunia imani zipo nyingi sana na tofauti na maisha yanasonga kwa maelfu ya miaka. Funguka akilini.
 
Andiko lako tu umeanza kwa kusema tumuite Mungu, halafu unasema mimi ndo niko wrong kukimbilia Mungu na sio project blue beam.
Kama ulikuwa huongelei mungu ulipoongelea supernatural kwenye mwezi bali ulikuwa unaongelea project blue beam basi sasa hiyo inahusiana nini na hii mada??

Nimeeleza hata hizi simu tunzotumia kuwasiliana na watu wa mbali,, kwa zamani ungemweleza mtu hiko kitu angesema ni supernatural
Imagine!! What if nilichokiona ilikuwa ni sehemu ya project ya blue beam?.
Ukiwa hutaki/uwezi onyesha wapi nimesema ni Mungu basi chochote unachokiandika ni invalid.
Hukuona sehemu nilposema ' sitaki kuiongelea isije sema ninaihubiri? " kwanini umei- out singled sentensi ya Mungu na kuacha zingine?.
Bure kabisa.
 
Sijasema ninavithibitisho vyovyote kuhusu uwepo wa Mungu wangu.

Sinaaaa

Kwasababu nikiwa naongea nae wewe huwezi kusikia.

Wewe huyo rafiki yako uliyekua unaongea nae kakupa nini ?? Maana mimi wakwangu kuna vitu vingi sana kanipa.
Alinipa confidence ya kuongea na crush wangu darasa la 5.
Ni kitu kikubwa sana kwangu
 
Back
Top Bottom