Awamu ya Tano iliua UDART, hili tuliseme wazi si kumung'unya maneno

Kisena yule Fisadi! Enzi za JK alikuwa na nguvu hatari,aliwahi kumpiga OCD wa Maswa mtama lol.huyu atakuwa alikamatwa kwa uhalali.
Uko sahihi. Serikali ilikuwa sahihi sana kutafuta pesa yake iliyochotwa na mtu kama huyu kwa urafiki tu na rais. Akaachiwa eti naye akajiita mfanyabiashara.
Kuna mengi ya kuipa sifa awamu ya 5, badala ya kubeza.
 
Mawazo ya kimaskini kabisa haya! Serikali sio mwizi imeleta tija gani na kama huyo alietaka kuchukua alikuwa mwizi kwanini Serikali ilishindwa kutafuta mwekezaji mwingine


Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Sijawahi kujiuliza kwanini hiyo kampuni haipo, ila nimejiuliza sana ni kina nani walikuwa nyuma ya hiyo kampuni.
MaxMalipo ni sehemu ya ufisadi wa wakuu waliokuwa Benki kuu miaka hiyo. Akina Idrissa. Wakajidai kumuweka huyo Max kama mbunifu. Ila kwa ujumla imesaidia mambo ya e-commerce sana.
 
Uzuri sisi wengine tupo humu JF kitambo na akili zetu ni zile zile hatuendi na upepo. Soma huu uzi na comments zake alafu umpe JPM heshima yake.


 
Sijawahi kujiuliza kwanini hiyo kampuni haipo, ila nimejiuliza sana ni kina nani walikuwa nyuma ya hiyo kampuni.
 
Hili jambo mimi nilishindwa kabisa kulielewa, vifaa ambavyo vinaenda kusaidia wananchi serikali inagoma kabisa kuvitoa! Sasa walipata faida gani? Kodi hawajapata, wananchi huduma hawajapata. Si wangeweka special agreements, kila siku 50pc ya revenue iende kulipa kodi, how difficult was that! Watanzania hatujui ni namna gani Mungu ametuokoa na lile jitu.

Na huu ujinga wa BRT Phase 1 ndio umetunyima pesa ya Phase II na III, World Bank waligoma kutoa pesa tena. Maana hii ya kwanza tumechemka.
 
Serikali haiwezi kufanya biashara ndiyo maana hata ATCL ni hasara tupu pamoja na majigambo yooote ya mwendazake
 
Kwa hiyo magu akaamua kumkomoa sio?
Acheni porojo someni huu uzi, msifikiri mambo mengi nchi hii ni mapya. Uzuri mengi yametokea technology tayari ipo juu.

 
Robert Kisena yuko jela mke wake yuko jela, buses 70 ziko tra, mkurugenzi wa fedha umemfukuza kazi, unasema mkajadiliane na tra kuhusu nini? hivi mumekuwaje? ndio maana ngosha alikuwa anawatukana pumbavu, mumwachie Kisena aje aendeleze shirika lake alipe na kodi aajiri watu aboreshe usafiri, hivi kweli ceo wa udart angekuwa mmarekani mngemfanyia haya?
 
Nani yuko kwenye hiyo Kampuni sio issue .. issue ni kuhusu performance

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
Sina uhakika kama performance yao iko juu au chini, maybe you can explain more.

Nachojua mimi sera ya Tanzania ikija kwenye private sector, hakuna sekta itakuwa dominat player. Baadhi ya kampuni za simu wamejaribu kutumia mabavu na kuwa dominant lakini wameshindwa, kama Maxmalipo walidhani wanaweza kuliteka soko, itabidi wajipange upya. Hata mwendo kasi pia, makampuni mengine yanajipanga kujiingiza kwenye biashara.
 
Ukiyaangalia haya yote, hakika utawala wa Hayati Magufuli umeleta hasara zaidi kuliko faida. Ni machache mno mazuri ya kuyaendeleza kutoka kwenye utawala wa awamu ya 5.

Itachukua miaka zaidi ya 10 kuondoa athari mbaya zilizosababishwa na utawala wa awamu ya 5.
 
Inawezekana ni kweli mwekezaji alikuwa na matatizo, lakini kwa uhakika Serikali ilikuwa na matatizo makubwa zaidi kwa sababu haikuwa inaelewa kabisa inachofabya na athari zake.
 
Naona hata Amerika huijui! Angekuwa Mmarekani ktk awamu ya 2, 3, na 4 angepeta tu si wapo waliokuja na suti na wakaondoka na utajili? Mmarekani ktk awamu ya 5 au Mmarekani akiwa amerika hawezi kujitutumua kwa upuuzi kama wa Kisena unayemtaja. Amerika angefilisiwa na kufungwa, no nonsense!

Unawezaje kujimilikisha shirika la umma bila kuangalia mambo ya kisheria yanayokupa nguvu hiyo? Mtu anategemea 'misheni tauni' ili kufanikiwa maisha! Baadaye akibanwa na sheria unaanza oooh Kisena, Ooh mke wake! that is fallacy! Kwanza huyo Kisena ni stupid na foolish kabisa! aliingizaje familia nzima kwenye illegals mama wa watu akajikuta anaingia magereza kwa utapeli wa mume.
 
Kisena aliwekwa kama chambo tu. Ile kampuni ya SIMON GROUP ina wahusika wengi sana wakubwa, akiwepo Profesa Kapuya na Marehemu Idd Simba. Kuna vigogo kadhaa wamo mle. Ukipekua humu JF kuna mada inayoongelea SIMON GROUP, utayaona mengi sana
Hata kama walikuwemo, kuna ubaya gani? Si wawekezaji? Au kuna watu hawaruhusiwi kuwekeza?
 
Inawezekana ni kweli mwekezaji alikuwa na matatizo, lakini kwa uhakika Serikali ilikuwa na matatizo makubwa zaidi kwa sababu haikuwa inaelewa kabisa inachofabya na athari zake.
Kwani kati ya mwekezaji na serikali nani ana madaraka ya kumhukumu mwingine? Unawezaje kulinganisha mtu binafsi na serikali? Yaani mali ya umma inamilikiwa na ka-mtu binafsi halafu unasema kana nafuu!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…