Azam TV badilisheni Tamthilia zenye mlengo wa itikadi za kidini

Azam TV badilisheni Tamthilia zenye mlengo wa itikadi za kidini

We kama unaona AZAM TV inakukwaza achana nayo kaangalie ITV huko kila Jumapili mambo ya kanisani lakini Ijumaa hakuna mambo ya msikitini.Pia kaa angalie channel 10 yuko BULLDOZER Mwammposa ! Shida yako nini ??? Achana na AZAM shenz taip !
Uyu jamaa analock mind set sana. sasa iyo ni tamthilia,
 
Jana nimerudi nimechoka nikafikia kujitupa tu kwenye kiti hakukuwa na mtu sebuleni ila TV ilikuwa inaonesha chaneli ya Azam 2

Macho yangu yakaona kipande kimoja kwenye tamthilia ya kituruki bila shaka inaitwa Alpasalani nadhani, Sasa Kuna Binti alikuwa Yuko kwenye mtego na viongozi wa utawala mwingine inaonesha huo utawala una Ukristu maana askari wake wana misalaba kwenye mavazi yao.

Sasa hawa askari aisee ni midebwedo vibaya mno yaani mwanamke moja anaua infidels (humo wanaita wadhalimu) zaidi ya 20 mbele ya kiongozi wao halafu Yuko pekeake na bado anaendelea kusurvive!? Duuuh ina maana hao ni wanyonge kiasi hiko? Halafu mule inaonesha waislamu ni watu wema sana na wakristu ni watu wenye Roho mbaya mno na hii chanel secular ila inabagua Imani moja na kuipendelea ingine.

Ututuki ni nchi ambayo raia wake wengi ni waislamu hivyo ni sawa kuwa na maudhui kama Yale, Sasa Tanzania hii ni multi religion county huwezi kuwa na maudhui hayo hayo tu kila siku ya kukandamiza Imani moja na kuipendelea ingine kulikuwa na;
  • Ertugrul
  • Ottoman
  • Barbarossa na Sasa ni hii
  • Alpasalani
Zote hizi maudhui ni yaleyale.

Azam tv badilikeni acheni upumbavu wenu hela tunalipa sisi lakini mnatutibua nyingi makusudi kabisa. Na huu mwezi nitaacha kulipia hiki kisimbuzi kama ni ligi kuu nitaangalia bandani na kisimbuzi nitanunua cha startimes.

Azam tv mna mazoea sana aisée na kazi zenu, Imani hazilazimishwi kihivyo, mjifunze kwa wenzenu mbona wao wanajua mipaka yao.

Mnakera bwana aah!
Watanzania wengi huwa tunalalamikia udini lakini sisi ndo wadini wa kwanza.
Kuna kipindi nchi kwetu kwenye tv tamthilia nyingi ni za kifilipino na spanish/mexico hakukua na kelele, lakini sasahivi tamthilia nyingi ni kihindi na kituruki. Sasa hapa ndo kwenye shida mbona kelele za uhindu hakuna? Zipo kwenye hizi za kituruki🤣? Tolerance wakuu

Hapa sijaweka kabisa bongo movie mambo ya kina mtitu g game. "In God We Trust"

Ni sawa na ucheki historical korean series na ulalamike budhisim au confucianism

UVumilivu muhimu wakuu
 
We kama unaona AZAM TV inakukwaza achana nayo kaangalie ITV huko kila Jumapili mambo ya kanisani lakini Ijumaa hakuna mambo ya msikitini.Pia kaa angalie channel 10 yuko BULLDOZER Mwammposa ! Shida yako nini ??? Achana na AZAM shenz taip !
Kwa mwamposa ile ni non secular Azam tv ni secular
 
Watanzania wengi huwa tunalalamikia udini lakini sisi ndo wadini wa kwanza.
Kuna kipindi nchi kwetu kwenye tv tamthilia nyingi ni za kifilipino na spanish/mexico hakukua na kelele, lakini sasahivi tamthilia nyingi ni kihindi na kituruki. Sasa hapa ndo kwenye shida mbona kelele za uhindu hakuna? Zipo kwenye hizi za kituruki🤣? Tolerance wakuu

Hapa sijaweka kabisa bongo movie mambo ya kina mtitu g game. "In God We Trust"

Ni sawa na ucheki historical korean series na ulalamike budhisim au confucianism

UVumilivu muhimu wakuu
Kila jambo analitafsiri kidini, imekuwa kama Simba na Yanga sasa
 
Ila wangalatia mna nonngwa sana ktk kingamuzi cha Azam kuna channel za ungalaitiani nyingi sana kwa nin usifungue izo channel ukaskiliz mahubir ya kwenu ?
Mbona hata za kiislamu zipo ila hatuziongelei?
Si ipo iman tv, pia mahseen TV mbona hizo hatuzisemi?
 
naona kama azam wamewalenga watanzania wa hali ya chini kama wateja wao wakuu

tamthilia za kituruki ndo zinawafaa kwasababu sio ngumu kuelewa, mara nyingi ni mambo ya mapenzi tu na migogoro ya familia

ndo maana tamthilia za kihindi na kikorea zinapendwa sana pia, sio issue ya dini ni issue ya kuwapa wateja kitu wanataka
 
Kwa mwamposa ile ni non secular Azam tv ni secular
Kwa sababu ni secular ndio maana ina Tumaini TV, Arise and shine zote hizi za kikristo na kuna Islam TV hii ya kiislamu, kwahiyo ni juu ya mtazamaji kuchagua anacho penda, remote unayo kazi kwako
 
Unacho lalamika hapa hakina mantiki, kwenye Azam TV kuna Tumaini TV ya kikristo na kuna Arise and shine ya kikristo, kama hizi tamthilia zina uislamu weka hizo za kikristo ule injili, hakuna anaeweza kumfurahisha kila mtu , isipokuwa unafanya vitu sahihi tu
Kitu sahihi ni nini?
Azam two siyo ya kidini ni ya wote
Kuna Iman tv na mahseen TV zote za kiislamu mbona hatuziongelei si tunajua ni kidini?
 
Back
Top Bottom