Azam TV wazindua mitambo mipya ikiwemo VAR, kamera moja tu imegharimu Tsh. Milioni 500

Huwezi kununua viatu kama huna miguu.
 
Azam hawezi pata nafasi kuonyesha EPL. Kumbuka purchasing power ya Afrika Mashariki ni ndogo Azam ina watazamaji wengi ila njaa kali ukiweka fee kubwa wanazima TV. Sasa uwekezaji utarudi vipi kwa kulipia mabilioni EPL wakati subscribers wake wachache. Ndio hapo tunadai DSTV wana bei, Azam ili warudishe gharama itabidi wawe na bei sana kuizidi mbali DSTV sababu wana wateja wachache.

Na Azam tatizo lake ni kutumia Kiswahili kama main language.
Kiswahili hakikwamishi wabongo tu kwenye soko la ajira nje, hata wawekezaji wa kibongo wanapata changamoto kidogo. Unaanza na domestic market ni Waswahili unaenda nje kujitanua inabidi sasa uanze kuwa na contents zotezote. Na unapata ugumu kuingia.

Ila kwa investment Azam inaenda vizuri. Dstv inashuka kila mwaka labda iuzwe
 
Pamoja sana masta.
 
Watz wengi ni vichwa maji wao wakiona juisi nyingi wanajua thamani ndo hiyo.
Kwa ufupi Multichoice ina thamani kuliko kampuni zote za ssb
Multichoice ni kampuni kubwa. Tanzania hatujawa na level ya kuwa na kampuni too demanding kwenye uboreshaji. Dstv wanateseka sababu hawakuwekeza kwenye online streaming kama Netflix. Ukitazama gharama za kuwekeza uko ni tatizo, sasa sisi hapa wazee wa Channel 10 na ITV iko vilevile tangu niko darasa la kwanza hatuwezi furukuta sana kimataifa.
 
Supersport wanalipa Paundi Milioni 168 kwa mwaka kuonyesha mechi zote za msimu kwa sub-saharan countries....mbona ni pesa nyingi sana.?
 
Hapa bongo Azam anaingiza pesa nyingi kuliko huyo dstv
 
Duh,hivi watu hela mnazitoa wapi? Mbona hatupeani ramani my zangu. Yan gari zishafika hadi EGU mi sijui. πŸ™„πŸ™„ maana niliishiaga kwenye DTP, nikasikia hamna hela, maisha magumu, basi nikaacha kufuatilia, sa anashangaa hiyo gari namba yake πŸ˜₯πŸ˜₯πŸ™„. Daaaah, ngoja niamke aisee.
 
Ngoja chawa waje waseme mama amefungua nchi
 
Sio kama hawezi
Naendelea kusimamia hapo
Una maana gani kusema anatafuta sifa na kujinufaisha mwenyewe?

Mkuu kila kitu lazima ukipigie mahesabu
Ile ni biashara hivyo lazima kuangalia FAIDA!
Ikiwa hakuna faida utafanya ili iweje?

Issue sio azam kushindwa
Issue ni kua je mteja ataweza kulipia kifurushi cha juu?
Ikiwa hawezi basi azam pia hawezi kuingia huko

Hivi unadhan wao hawajui wastani wa wanaolipa kifurushi cha 35,25,15?
Wanajua ndio maan wanashindwa kuingia huko na si kama β€œHAWEZI”
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…