Azimio Bunge la kuridhia makubaliano kati ya Tanzania na Dubai kuboresha bandari ya Dar es Salaam

Serikali pia iwakodishie DP World, ikulu, bunge na mahakama kwa miaka 100 ili kuongeza ufanisi, na kutoa ajira kwa vijana wetu.
Kuna elimu, afya, kilimo, biashara, ccm... Yaani natamani wapewe wawekezaji binafsi kwa πŸ’―
 
Bandarini pale ni kiringe cha kukusanya mapato tuu.
Ina maana mbwa sisi hatuwezi kukusanya mapato yetu?
Kumbe vyuo vikuu vyetu vinazalisha vilaza na sii wataalamu.
 
Ukifuatulia watetezi Hawa wa DP world hatuelezi nini kinafanyika Moja kwa Moja kwenye Bandari.
Tukihoji mnasema
1.Bandari haijakodishwa.
2.Bandari haijabinafsishwa
3.Bandari haijauzwa

Wanajibu haya ni mashirikiano yapi katika Sasa?

Huo ufanisi unapatikanajaje?
Je? kwenye Kununua crane, serikali haina hela ya kununua crane million Mia mbili kwa crane Moja?

Watabomoa Bandari yote na kujenga upya na kujenga crane mpya?

Kwanini DP world wasiombe kandarasi kuboresha?

ulazima wa DP world kuomba mashirikiano badala consulting ni upi?

Mimi binafsi Bandari imeuzwa naona kabisa wazi. Na nani amechukua pesa za kuuza bandari?
 
Uchawi huko hapa kwenye hili neno "kuendelezwa"
 
Port efficiency will be maximized through functional integration in port logistics including 3PLs and 4PLs.
 
Faizafoxy and Lord denning wanakuja na ufafanuzi! NB; Hakuna mtanzania anaepinga uwekezaji bali terms za huo mkataba ni muhim kwa maenelezo yetu
 
L
Kwani hamuiendeshi? kuna ufanisi gani? kila siku mnapoteza wateja kwa Bandari ya Mombasa!!
Lakini wanateua Wakurugenzi wao hao hao kwanini Mkurugenzi asinye interview kabla ya kupewa bandarini? Yaani mnateua mtu Hana uwezo unakimbilia ufanisi.
 
Na kelele zote hizi mtandaoni kumbe hata mkataba hujausoma?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…