Azimio La Arusha: Why We Were Dead Wrong!

Azimio La Arusha: Why We Were Dead Wrong!

mkuu,
kwa hiyo tatizo siyo azimio la arusha ila watekelezaji wa azimio hilo.
naamini kabisa laiti kama utekelezaji ungekwenda kama azimio lilivyoelekeza basi azimio linabadilisha maisha ya watu na mienendo yao,na linaweza kabisa kuleta matokeo mazuri katika jamii husika.

Tutajie mtekelezaji wake mkuu tuanze kumkosoa kwa kutuaribia Azimio letu tukufu ambalo lingewafanya wananchi watanzania waondokane na umasikini na wasinyonywe tena na makabaila, makupe na mabepari?
 
Tutajie mtekelezaji wake mkuu tuanze kumkosoa kwa kutuaribia Azimio letu tukufu ambalo lingewafanya wananchi watanzania waondokane na umasikini na wasinyonywe tena na makabaila, makupe na mabepari?
CCM ya Mwinyi baada ya Azimio la Zanzibar...
 
mkuu,
kwa hiyo tatizo siyo azimio la arusha ila watekelezaji wa azimio hilo.
naamini kabisa laiti kama utekelezaji ungekwenda kama azimio lilivyoelekeza basi azimio linabadilisha maisha ya watu na mienendo yao,na linaweza kabisa kuleta matokeo mazuri katika jamii husika.

unataka kumtupia mpira nani? azimio la arusha author wake ni Nyerere, lilimfia yeye Nyerere, utekelezaji wake upi? kwani mahakamani kuna kurasa za azimio la arusha??
 
Hujaelewa mkuu wangu usikurupuke. Alichosema @Wabeloya ni kwamba Dira (Azimio) anamfunzwa kwa mtu tokeo akiwa mtoto, akisha kuwa kinachofanyika ni sheria tu (msemo wa samaki mkunje akingali mbichi) maana huwezi kuwa na sheria kama hukuwa na azma. Sasa kama wewe unapingana na hata kumfunza mtoto yalikuwa makosa utaweza vipi kusimamisha hizo sheria. halafu bado hujanijibu Sheria utaisimamisha vipi ikiwa huna miiko?

Unajua mchanganya sana mambo, kwa mfano unaweza kumfunza mtoto kwa kumkataza mabaya na asipofuata ukamcharaza bakora.. tatizo linakuwa maamuzi ya kumchapa mtoto bakora, tukasema ilikuwa abuse ama sii malezi mazuri, lakini sio kupinga hata kumkata mtoto kufanya vibaya..Sasa mnapozungumzia Azimio la Arusha ni pale mnapoona bakora zinawacharaza na kusema hata hayo mafunzo yake hayana hivyo kuwekewa miiko ni makosa, hapa ndipo tusipokubaliana.

Inaonyesha kuna watu mkiishaamua kuamini kitu kuwabadilisha kazi sana!!

huwezi kusema AA ni bakora mkuu!! AA ni kama biblia au quran, una hiyari ya kufuata au usifuate......kwani Azimio ukilisema kwa mdomo ndio inakuwa hivyo

wangapi wanaapa kabisa kuwa watakuwa waaminifu kwenye ndoa zao na bado wanatoka nje ya ndoa??

Kama mtu akifungwa jela anafungwa kwa AA , yaani hakimu au jaji anatumia AA kusema kwa kosa hili unaenda jela kwa kifungu xx cha azimio basi nitaliunga mkono..short of that is just blaha blah!!

mjadala hakuna hapa jamani
 
Hitimisho la Mjadala ..?

Azimio la Arusha was the right blue print of this nation. Wanaopinga hilo wana haki kufanya hivyo lakini cha ajabu ni kwamba kila ukiwasikia wakitoa hoja zao juu ya jinsi gani tumepotea kama nchi - kiuchumi, kiutawala na kijamii, wanajisahau kwamba mengi ya wanayo ongelea yaliwekewa misingi mizuri ndani ya azimio la arusha. Lakini muhimu zaidi ni kwamba wameamua ku 'work backwards': Wanaanza kwa 'kushambulia' MATOKEO YA SERA kutokana na kuwa na mtazamo na msimamo wao usio yumba kwamba 'development is path-dependent' (njia iliyotumiwa na mataifa tajiri kama marekani, UK n.k ndio njia pekee ya kuweza kuletea maendeleo binadamu), hivyo moja kwa moja wanajikita zaidi katika kukosoa na kutafuta madhambi ya MCHAKATO, na kuhitimisha kwa kukejeli na kutusi NIA YA AZIMIO LA ARUSHA. Kilichoshanganza wengi ni kwamba mtoa mada alikiri mwenyewe kwamba hajalisoma azimio la arusha na hakuona sababu ya kufanya hivyo. Sina uhakika kama yeye ni muumini wa dhana ya 'dont judge a book by its cover' au he has some reservations on that concept.

Vinginevyo Lets Agree to Disagree kwamba since the 'demise' of Azimio La Arusha, nchi yetu imepoteza mwelekeo na itakuwa vigumu sana kwa nchi yetu kuweza kujitambua tena kiutawala, kiuchumi na kijamii. It remains to be seen nini itakuwa source ya 'true emancipation' ya watanzania walio wengi chini ya Sera ya Azimio la Zanzibar, hasa walio vijijini, Azimio ambalo limekuwa likitekelezwa kwa miaka 20 sasa (1992-2012) na kuwa endorsed na wenzetu wanaolipinga Azimio la Arusha ambao in their humble opinion,Hatimaye Tanzania (ya watanzania wengi, hasa vijijini) sasa ipo kwenye njia sahihi ya kujipatia maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Mwisho, ni muhimu tu wakatambua kwamba mambo yafuatayo bado yataendelea kuwa muhimu katika harakati zetu za kutukomboa kiuchumi, kiutawala na kijamii: "ARDHI", "WATU", "SIASA/SERA SAFI", na "UONGOZI BORA".
 
Inaonyesha kuna watu mkiishaamua kuamini kitu kuwabadilisha kazi sana!!

huwezi kusema AA ni bakora mkuu!! AA ni kama biblia au quran, una hiyari ya kufuata au usifuate......kwani Azimio ukilisema kwa mdomo ndio inakuwa hivyo

wangapi wanaapa kabisa kuwa watakuwa waaminifu kwenye ndoa zao na bado wanatoka nje ya ndoa??

Kama mtu akifungwa jela anafungwa kwa AA , yaani hakimu au jaji anatumia AA kusema kwa kosa hili unaenda jela kwa kifungu xx cha azimio basi nitaliunga mkono..short of that is just blaha blah!!

mjadala hakuna hapa jamani
Mkuu wangu nakuelewa sana unachojaribu kusema. Dhambi zipo na hazitaweza kwisha lakini unapoharamisha dhambi ndipo unapoweza kutunga sheria kupambana nazo. Kwnai majambazi hawapo au wezi sii wapo na hawatakwisha mbona tunaweka sheria wakati haya ni maamuzi ya watu ambao mnadai wako huru.. Hakuna sheria inayotungwa pasipo kuwepo Dira ambayo hutunga mwongozo. AA sio Biblia au kura ila ni mwongozo kama Katiba maana Biblia na Kuran zimeandikwa baada ya imani za dini kufundishwa tena kwa karne nyingi zimepita, waumini walijua wanasali kwa ajili gani wanaabudu nini na hatua gani wazifuate ili waokoke kinyume cha sheria za Romans kina Pilato.

Katiba ndiyo inatunga sheria wakati dira ndiyo blueprint inayotangulia katiba maana huwezi andika katiba kama huna kitu mkononi, na katiba hubadilika kulingana na mazingira ya kidunia japo safari ni ile ile naha ktk dini toka Abraham hadi leo hii kuna vitabu kibao vimeandikwa vya sheria na tofauti. Sheria za imani ya dini zilitungwa baada ya imani hizi kuwepo kwa muda mrefu sana na zimewekwa kutokana na matukio, siku kwa siku, mweuzi hadi miaka sheria ziliendelea kutungwa ili kulinda waumini wake kutokana na all evil around them ikiwa wanataka kwenda Mbinguni. Jiulize kwa nini tunataka kukusanya mawazo ya watu kabla ya kuandika katiba mpya?.. kaa sii kujitmabua sisi ni nani, muungano wetu, kero zetu na kadhalika na tunaazimia kufanya nini.. Kwa nini tusitumie tu sheria kuandika katiba mpya au copy and paste.

Hivyo kwa muumini wa dini, dira yake ni maisha ya hapa duniani, hiyo safari ya kutoka hapa kwenda mahala pema peponi unatakiwa ufanye nini ili upate uzima wa milele na mwongozo na sheria zikawekwa kuwalinda waumini ili wapate kufika huko. Hivyo kinachotangulia ni who U are, WHY unabadilika toka ulivyokuwa na unataka kuwa nani.. Kitaifa tunasema kwa nini unataka kuwa HURU, ili uwe nani na kama ni Liberty ni mfumo gani utumike kulingana na mazingira yaliyokuzunguka, hivyo unaweza kutumia hata negative Liberty inategemea na WATU na ktk MAZINGIRA waliyopo, kisha sheria ina govern. Ukipoteza la kwanza sheria inakuwa haina msingi tena. Leo hii tunaweza mrudisha mkoloni tukatawaliwa na kwa sheria hizihizi zinazotumika leo, ila itapoteza UHURU wetu na tutajuliknana kama tunatawaliwa.

Sheria inalinda tu ile sababu ya WHY, kwa hiyo yule anayetembea nje ya ndoa kama AZIMIO linakataza watu kutembea nje ya ndoa na sababu zake, basi ni rahisi kutunga sheria lakini huwezi kuzuia watu wote wasitembee nje ya ndoa kwa sheria tu. Hata wizi na kifungoi cha miaka 10 au 20 inatokana na uzito wa crime yenyewe ktk jamii na why mwizi hatakiwi ndipo unapotunga sheria.

Yesu alisema wakati fulani kuwaambia waja wake kwamba walipomuuliza kaa kula chakula bila kunawa ni haramu, naye akawajibu sii kitu kinachoingia tumboni ndio haramu bali imani yake. Kwetu sisi waislaam tunaitafsiri hii kwa kusema kwamba binadamu tumeumbwa na madhambi, from out of our hearts come evil thoughts. Na huwezi kuyazuia haya ikiwa hujaazimia kufuata imani hiyo. Kifupi ni kwamba kama unaamini kula bila kunawa mikono ni haramu basi huna sababu ya kuuliza kinachoinmgia tumboni maana uharamu unaanza na fikra zako. Kwa mfano, haramu sii nguruwe wala nyama yake bali imekatazwa, kama una imani ya roho hutakula wala bila kuuliza isipokuwa kama huna imani na hujaazimia kuokoka utakula na utajijengea sababu zako..

So in short is to say, AA isn't the solution but a blueprint of who we are, our sovereignty and against what. Then Law should govern in contrast to any evil thoughts. Sheria pekee haina maana yoyote maana hata Uingereza Malkia yupo juu ya sheria, KIna Sultan wa Saudia wapo juu ya sheria lakini ukiwauliza watakwambia wanafuata sheria kuwa juu ya sheria..Sheria means nothing ikiwa hujui unachokitaka na ndio maana tunaburuzwa kwa kusoma sana sheria wakati roho zetu zinaamini Ufisadi sio kosa - Ujanja kuwahi!..
 
Hitimisho la Mjadala ..?


Unofficially nitatumia nafasi kuelezea sababu za kushindwa kwa Azimio la Arusha.

1./ Tanzania ni jamuhuri. Na Jamuhuri inaongozwa na vitu viwili muhimu. Katiba na sheria za nchi. Hii ni mikataba kati ya wananchi na serikali yao. Azimio la Arusha ni document iliyotumbukizwa lakini haina uhalali wowote wa kisheria. Halmashauri ya TANU iliyopitisha Azimio hili iliwakilisha chama cha kisiasa cha TANU ambao walichaguliwa na wanachama wenye kadi za TANU. Document ya Taifa ni lazima ipitishwe na bunge ambalo limechaguliwa na wananchi wenye sifa za kupiga kura.

Tukumbuke pia kuwa wakati Azimio hili linapita, idadi ya wanachama wa TANU ilikuwa ndogo kuliko idadi ya watanzania. Na hata sasa idadi ya wanachama wa vyama vya siasa ni ndogo kuliko ya watanzania. Hivyo wanasiasa ni lazima wakumbuke kuwa taifa ni kubwa kuliko imani ya vyama vyao.

2./ Pili kurudishwa kwa mfumo wa vyama vingi, kuanza kurudisha katiba na sheria kwa wananchi. Katiba ya nchi na sheria za nchi hazikatazi mtanzania kuvunja baadhi ya kanuni muhimu ya Azimio la Arusha. Kwa mfano mtanzania anaweza kuwa mkurugenzi wa kampuni binafsi na akagombea ubunge kwa kupitia chama chochote cha siasa kisicho na kanuni za Azimio la Arusha.

Hivyo demise ya Azimio la Arusha haitokani na Azimio la Zanzibar. Inatokana na kuwa waliotunga Azimio la Arusha walitegemea chama kushika utamu daima na kusahau kulifanya Azimio hilo sheria ya nchi au extension ya katiba.

3./ Azimio halina walinzi. Nchi kama Iran au North Korea zinye kufuata itikadi zao zina watu walio tayari kutoa damu kulazimisha wengine au kulinda. Watu wengi ambao walisaidiwa na Azimio hili, ndio wao wa kwanza kuli-molest. Huwezi kujenga itikadi ukiwa huna wafuasi.

4./ Kila binadamu ana matamanio yake na hiyo ni haki aliyopewa na muumba wake. Azimio la Arusha linakiuka msingi huu na kufikiri kuwa serikali inaweza au mafundisho ya itikadi ya chama yanaweza kuwafanya binadamu wafikiri sawa sawa. Kilichotakiwa kuwaachia wananchi watimize matamanio yao mazuri bila kuvunja sheria.

5./ Utekelezaji wa mambo mengine ya azimio la Arusha ulikuwa advance kwa watanzania hata kwa mwandisi mkuu wa Azimio hilo. Kama kulikuwa na watanzania 12 wenye elimu ya juu wakati tunapata uhuru, nina uhakika namba haikuwa nzuri miaka ya 70 kusema kuwa tuendeshe viwanda vyetu au mabenki yetu. Kufanya hivyo ilikuwa ni kukataa education na kutumia ignorance.

6./Azimio liliongeza regulations ambazo zinazuia innovation and creativity.

7./ Leadership that bring results is an art form. You have it or you don't, and you don't need Azimio la Arusha to make things better.

Cau

Z10
 
Well, heshima mbele sana JF,

- Ninaomba kusema tena na tena, we were Dead wrong na idea za Azimio La Arusha, infact ndilo limetufikisha hapa tulipo yaani tumekwama hili taifa, hatujui tunakokwenda wala tulikotoka. Halafu wanatokea wasomi wanaodai eti turudi kwenye Azimio, hilo Azimio limetushinda mwanzoni kwa nini kuna wanaoamini tutaliweza sasa?

- Recently, nimeona wale wengi walioachwa kwenye uongozi wa juu yaani kwenye mlo, wakililia Azimio, halafu ninachukizwa sana ninapoona media inawapa free lunch hawa waliokosa mlo, sijawahi kuwasikia wakisema Azimio liliwahi kumfunga kiongozi gani wa juu mwizi, sijawasikia wakisema Azimio lilifanya nini cha maaana mpaka wanalilia!

- Mwalimu, yes was the greatest ever, lakini Mwalimu alikuwa na mapungufu makubwa mawili, hakujua;- !. Uchumi 2. Sheria, hivi vitu viwili Mwalimu simply hakuvijua kama alivijiua basi hakuvitilia maanani, na ndivyo vinavyolitafuna taifa letu sasa akiwa hayupo!

- WA-TANZANIA, KAMA TUNATAKA KUSONGA MBELE NA KIJIREKEBISHA TUACHANE NA MANENO YA AZIMIO LA ARUSHA, KWA SABABU NDILO HASA LIMETURUDISHA NYUMA SANA, LISIRUDI, LIENDE ZAKE, NA TUSILIJADILI MAANA NI SHETANI LILILOTURUDISHA NYUMA SANA, SASA TWENDE MBELE NA UBEPARI NA UTAWALA UNAOHESHIMU SHERIA NDIO THE BEST WAY MBELE!

RESPECT PEOPLE!

Mr. Willie @DSM City!

Mkuu mwalimu hakuwa na elimu kubwa, alikuwa na kipaji. Alijua mambo, lakini hakujua mengi, aliongoza nchi ambayo wananchi wake wengi walikuwa hawajaelimika na wengi walikuwa law abiding citizens, sio kama sasa ambako karibu more than half of cabinet wezi, hali ni tofauti sana.

Azimio la Arusha lilikuwa zuri kwa wakati ule, lilikuwa ni more than miiko ya utu na uongozi. tatizo ni kuwa it was strange idea to many, being strange is not same as being wrong.
 
Mchambuzi,
Mkuuwangu nimekuwa nakufuatilia sana kwa muda na naona unashusha vigongo vizuri sana ambavyo sisi wana Chadema ndio tunaviamini, sasa nashangaa sana unaposema unatatizwa na Itikadi ya Chadema ilihali mambo mengi ya Azimio la Arusha tunayasisitiza na isitoshe ktk uwajibikaji maswala ya Zakumi ndiyo yatakuwa kipimo cha uongozi. Mimi nadhani darasa hili lina mazuri yake na pengine William kaiweka mada hii bila kujua itatufikisha wapi ama alikusudia kuona tofauti zetu ktk mjadala mzito kama huu. Na nakuhakikishia mawazo yako yanaweza tu kupokelewa Chadema maana ndio chama pekee kinachosisitiza DIRA kwanza (wazo langu) na UWAJIBIKAJI Zakumi). Hawa wanaopinga Miiko na maadili wamejaa huko uliko na sii ajabu William anatetea mawazo baada ya kulishwa sumu hii.

Heshima sana Mkandara.... I once told Mchambuzi something similar!!!

Glad this seems to be very true
 
Azimio la Arusha was the right blue print of this nation. Wanaopinga hilo wana haki kufanya hivyo lakini cha ajabu ni kwamba kila ukiwasikia wakitoa hoja zao juu ya jinsi gani tumepotea kama nchi - kiuchumi, kiutawala na kijamii, wanajisahau kwamba mengi ya wanayo ongelea yaliwekewa misingi mizuri ndani ya azimio la arusha. Lakini muhimu zaidi ni kwamba wameamua ku 'work backwards': Wanaanza kwa 'kushambulia' MATOKEO YA SERA kutokana na kuwa na mtazamo na msimamo wao usio yumba kwamba 'development is path-dependent' (njia iliyotumiwa na mataifa tajiri kama marekani, UK n.k ndio njia pekee ya kuweza kuletea maendeleo binadamu), hivyo moja kwa moja wanajikita zaidi katika kukosoa na kutafuta madhambi ya MCHAKATO, na kuhitimisha kwa kukejeli na kutusi NIA YA AZIMIO LA ARUSHA. Kilichoshanganza wengi ni kwamba mtoa mada alikiri mwenyewe kwamba hajalisoma azimio la arusha na hakuona sababu ya kufanya hivyo. Sina uhakika kama yeye ni muumini wa dhana ya 'dont judge a book by its cover' au he has some reservations on that concept.

Vinginevyo Lets Agree to Disagree kwamba since the 'demise' of Azimio La Arusha, nchi yetu imepoteza mwelekeo na itakuwa vigumu sana kwa nchi yetu kuweza kujitambua tena kiutawala, kiuchumi na kijamii. It remains to be seen nini itakuwa source ya 'true emancipation' ya watanzania walio wengi chini ya Sera ya Azimio la Zanzibar, hasa walio vijijini, Azimio ambalo limekuwa likitekelezwa kwa miaka 20 sasa (1992-2012) na kuwa endorsed na wenzetu wanaolipinga Azimio la Arusha ambao in their humble opinion,Hatimaye Tanzania (ya watanzania wengi, hasa vijijini) sasa ipo kwenye njia sahihi ya kujipatia maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Mwisho, ni muhimu tu wakatambua kwamba mambo yafuatayo bado yataendelea kuwa muhimu katika harakati zetu za kutukomboa kiuchumi, kiutawala na kijamii: "ARDHI", "WATU", "SIASA/SERA SAFI", na "UONGOZI BORA".

Just to add to the point. Kweli tulipolitupa azimio la Arusha kule Zanzibar tulisema kuwa nchi yetu sasa ni uwanja wa fisi. Sasa hivi hata hiyo tunayoita Ardhi yetu inakuwa vigumu kuuita ardhi yetu, kwa kuwa inauzwa siku hizi, inawezekana akaja kaburu akasema ni ardhi yake na sisi tukakosa la kusema, siasa safi(sera) naweza kusema in papers tunazo nzuri labda hata kuliko za Marekani, lakini kitekelezaji ni 0 kabisa, ukisikia viongozi wanasema "maisha bora kwa kila mtanzania" utaona kuwa ni fix fix tu,no one is working to that end, kila mtu is working on fattening his bank account, hakuna kitu ambacho serikali inaweza kusema inafanya zaidi ya uendeshaji wa siku hadi siku, Uongozi bora hili siwezi hata kusema we see it day in day out. Sasa hakuna uongozi Tanzania, tuna viongozi lakini hakuna uongozi, hata viongozi wenyewe wanatia shaka kama kweli ni viongozi.

Unless we go back to Azimio la Arusha, unless we go back to the core principles or the main guiding principle of this country, we will still be in mess. Hatuwezi kuendesha nchi bila miiko ya uongozi na bila kuwa na guiding principle yeyote.
 
Mkuu wangu nakuelewa sana unachojaribu kusema. Dhambi zipo na hazitaweza kwisha lakini unapoharamisha dhambi ndipo unapoweza kutunga sheria kupambana nazo. Kwnai majambazi hawapo au wezi sii wapo na hawatakwisha mbona tunaweka sheria wakati haya ni maamuzi ya watu ambao mnadai wako huru.. Hakuna sheria inayotungwa pasipo kuwepo Dira ambayo hutunga mwongozo. AA sio Biblia au kura ila ni mwongozo kama Katiba maana Biblia na Kuran zimeandikwa baada ya imani za dini kufundishwa tena kwa karne nyingi zimepita, waumini walijua wanasali kwa ajili gani wanaabudu nini na hatua gani wazifuate ili waokoke kinyume cha sheria za Romans kina Pilato.

Katiba ndiyo inatunga sheria wakati dira ndiyo blueprint inayotangulia katiba maana huwezi andika katiba kama huna kitu mkononi, na katiba hubadilika kulingana na mazingira ya kidunia japo safari ni ile ile naha ktk dini toka Abraham hadi leo hii kuna vitabu kibao vimeandikwa vya sheria na tofauti. Sheria za imani ya dini zilitungwa baada ya imani hizi kuwepo kwa muda mrefu sana na zimewekwa kutokana na matukio, siku kwa siku, mweuzi hadi miaka sheria ziliendelea kutungwa ili kulinda waumini wake kutokana na all evil around them ikiwa wanataka kwenda Mbinguni. Jiulize kwa nini tunataka kukusanya mawazo ya watu kabla ya kuandika katiba mpya?.. kaa sii kujitmabua sisi ni nani, muungano wetu, kero zetu na kadhalika na tunaazimia kufanya nini.. Kwa nini tusitumie tu sheria kuandika katiba mpya au copy and paste.

Hivyo kwa muumini wa dini, dira yake ni maisha ya hapa duniani, hiyo safari ya kutoka hapa kwenda mahala pema peponi unatakiwa ufanye nini ili upate uzima wa milele na mwongozo na sheria zikawekwa kuwalinda waumini ili wapate kufika huko. Hivyo kinachotangulia ni who U are, WHY unabadilika toka ulivyokuwa na unataka kuwa nani.. Kitaifa tunasema kwa nini unataka kuwa HURU, ili uwe nani na kama ni Liberty ni mfumo gani utumike kulingana na mazingira yaliyokuzunguka, hivyo unaweza kutumia hata negative Liberty inategemea na WATU na ktk MAZINGIRA waliyopo, kisha sheria ina govern. Ukipoteza la kwanza sheria inakuwa haina msingi tena. Leo hii tunaweza mrudisha mkoloni tukatawaliwa na kwa sheria hizihizi zinazotumika leo, ila itapoteza UHURU wetu na tutajuliknana kama tunatawaliwa.

Sheria inalinda tu ile sababu ya WHY, kwa hiyo yule anayetembea nje ya ndoa kama AZIMIO linakataza watu kutembea nje ya ndoa na sababu zake, basi ni rahisi kutunga sheria lakini huwezi kuzuia watu wote wasitembee nje ya ndoa kwa sheria tu. Hata wizi na kifungoi cha miaka 10 au 20 inatokana na uzito wa crime yenyewe ktk jamii na why mwizi hatakiwi ndipo unapotunga sheria.

Yesu alisema wakati fulani kuwaambia waja wake kwamba walipomuuliza kaa kula chakula bila kunawa ni haramu, naye akawajibu sii kitu kinachoingia tumboni ndio haramu bali imani yake. Kwetu sisi waislaam tunaitafsiri hii kwa kusema kwamba binadamu tumeumbwa na madhambi, from out of our hearts come evil thoughts. Na huwezi kuyazuia haya ikiwa hujaazimia kufuata imani hiyo. Kifupi ni kwamba kama unaamini kula bila kunawa mikono ni haramu basi huna sababu ya kuuliza kinachoinmgia tumboni maana uharamu unaanza na fikra zako. Kwa mfano, haramu sii nguruwe wala nyama yake bali imekatazwa, kama una imani ya roho hutakula wala bila kuuliza isipokuwa kama huna imani na hujaazimia kuokoka utakula na utajijengea sababu zako..

So in short is to say, AA isn't the solution but a blueprint of who we are, our sovereignty and against what. Then Law should govern in contrast to any evil thoughts. Sheria pekee haina maana yoyote maana hata Uingereza Malkia yupo juu ya sheria, KIna Sultan wa Saudia wapo juu ya sheria lakini ukiwauliza watakwambia wanafuata sheria kuwa juu ya sheria..Sheria means nothing ikiwa hujui unachokitaka na ndio maana tunaburuzwa kwa kusoma sana sheria wakati roho zetu zinaamini Ufisadi sio kosa - Ujanja kuwahi!..


mkuu una moyo wewe!!

soma tathmini ya Nyerere ya AA baada ya miaka 10

http://www.tzonline.org/pdf/thearushadeclarationtenyearsafter.pdf


soma artcile hii ya mihangwa pengine itakufurahisha kidogo, lakini tatizo la msingi liko palepale tu.....kuwa Nyerere alikosea sana kuanzia mwanzo


Home*»*Insight





1. Nyerere alikosea ujamaa...haukuwa wakati wake na yy alijua hivyo
2. AA ilikuwa aidea yake baada ya miaka 10 likafa watu inaonyesha watu wake au vijana wake hawakujua lolote...unalosema azimio halikuwa azimio bali tamko!!
 
Hitimisho la Mjadala ..?

Hadi sasa tumepata mahitimisho matatu. Tunaomba tupate mengi inavyowezekana. Ninataka nieleze tuyatumieje.

Azimio la Arusha was the right blue print of this nation. Wanaopinga hilo wana haki kufanya hivyo lakini cha ajabu ni kwamba kila ukiwasikia wakitoa hoja zao juu ya jinsi gani tumepotea kama nchi - kiuchumi, kiutawala na kijamii, wanajisahau kwamba mengi ya wanayo ongelea yaliwekewa misingi mizuri ndani ya azimio la arusha. Lakini muhimu zaidi ni kwamba wameamua ku 'work backwards': Wanaanza kwa 'kushambulia' MATOKEO YA SERA kutokana na kuwa na mtazamo na msimamo wao usio yumba kwamba 'development is path-dependent' (njia iliyotumiwa na mataifa tajiri kama marekani, UK n.k ndio njia pekee ya kuweza kuletea maendeleo binadamu), hivyo moja kwa moja wanajikita zaidi katika kukosoa na kutafuta madhambi ya MCHAKATO, na kuhitimisha kwa kukejeli na kutusi NIA YA AZIMIO LA ARUSHA. Kilichoshanganza wengi ni kwamba mtoa mada alikiri mwenyewe kwamba hajalisoma azimio la arusha na hakuona sababu ya kufanya hivyo. Sina uhakika kama yeye ni muumini wa dhana ya 'dont judge a book by its cover' au he has some reservations on that concept.

Vinginevyo Lets Agree to Disagree kwamba since the 'demise' of Azimio La Arusha, nchi yetu imepoteza mwelekeo na itakuwa vigumu sana kwa nchi yetu kuweza kujitambua tena kiutawala, kiuchumi na kijamii. It remains to be seen nini itakuwa source ya 'true emancipation' ya watanzania walio wengi chini ya Sera ya Azimio la Zanzibar, hasa walio vijijini, Azimio ambalo limekuwa likitekelezwa kwa miaka 20 sasa (1992-2012) na kuwa endorsed na wenzetu wanaolipinga Azimio la Arusha ambao in their humble opinion,Hatimaye Tanzania (ya watanzania wengi, hasa vijijini) sasa ipo kwenye njia sahihi ya kujipatia maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Mwisho, ni muhimu tu wakatambua kwamba mambo yafuatayo bado yataendelea kuwa muhimu katika harakati zetu za kutukomboa kiuchumi, kiutawala na kijamii: "ARDHI", "WATU", "SIASA/SERA SAFI", na "UONGOZI BORA".

Unofficially nitatumia nafasi kuelezea sababu za kushindwa kwa Azimio la Arusha.

1./ Tanzania ni jamuhuri. Na Jamuhuri inaongozwa na vitu viwili muhimu. Katiba na sheria za nchi. Hii ni mikataba kati ya wananchi na serikali yao. Azimio la Arusha ni document iliyotumbukizwa lakini haina uhalali wowote wa kisheria. Halmashauri ya TANU iliyopitisha Azimio hili iliwakilisha chama cha kisiasa cha TANU ambao walichaguliwa na wanachama wenye kadi za TANU. Document ya Taifa ni lazima ipitishwe na bunge ambalo limechaguliwa na wananchi wenye sifa za kupiga kura.

Tukumbuke pia kuwa wakati Azimio hili linapita, idadi ya wanachama wa TANU ilikuwa ndogo kuliko idadi ya watanzania. Na hata sasa idadi ya wanachama wa vyama vya siasa ni ndogo kuliko ya watanzania. Hivyo wanasiasa ni lazima wakumbuke kuwa taifa ni kubwa kuliko imani ya vyama vyao.

2./ Pili kurudishwa kwa mfumo wa vyama vingi, kuanza kurudisha katiba na sheria kwa wananchi. Katiba ya nchi na sheria za nchi hazikatazi mtanzania kuvunja baadhi ya kanuni muhimu ya Azimio la Arusha. Kwa mfano mtanzania anaweza kuwa mkurugenzi wa kampuni binafsi na akagombea ubunge kwa kupitia chama chochote cha siasa kisicho na kanuni za Azimio la Arusha.

Hivyo demise ya Azimio la Arusha haitokani na Azimio la Zanzibar. Inatokana na kuwa waliotunga Azimio la Arusha walitegemea chama kushika utamu daima na kusahau kulifanya Azimio hilo sheria ya nchi au extension ya katiba.

3./ Azimio halina walinzi. Nchi kama Iran au North Korea zinye kufuata itikadi zao zina watu walio tayari kutoa damu kulazimisha wengine au kulinda. Watu wengi ambao walisaidiwa na Azimio hili, ndio wao wa kwanza kuli-molest. Huwezi kujenga itikadi ukiwa huna wafuasi.

4./ Kila binadamu ana matamanio yake na hiyo ni haki aliyopewa na muumba wake. Azimio la Arusha linakiuka msingi huu na kufikiri kuwa serikali inaweza au mafundisho ya itikadi ya chama yanaweza kuwafanya binadamu wafikiri sawa sawa. Kilichotakiwa kuwaachia wananchi watimize matamanio yao mazuri bila kuvunja sheria.

5./ Utekelezaji wa mambo mengine ya azimio la Arusha ulikuwa advance kwa watanzania hata kwa mwandisi mkuu wa Azimio hilo. Kama kulikuwa na watanzania 12 wenye elimu ya juu wakati tunapata uhuru, nina uhakika namba haikuwa nzuri miaka ya 70 kusema kuwa tuendeshe viwanda vyetu au mabenki yetu. Kufanya hivyo ilikuwa ni kukataa education na kutumia ignorance.

6./Azimio liliongeza regulations ambazo zinazuia innovation and creativity.

7./ Leadership that bring results is an art form. You have it or you don't, and you don't need Azimio la Arusha to make things better.

Cau

Z10

Just to add to the point. Kweli tulipolitupa azimio la Arusha kule Zanzibar tulisema kuwa nchi yetu sasa ni uwanja wa fisi. Sasa hivi hata hiyo tunayoita Ardhi yetu inakuwa vigumu kuuita ardhi yetu, kwa kuwa inauzwa siku hizi, inawezekana akaja kaburu akasema ni ardhi yake na sisi tukakosa la kusema, siasa safi(sera) naweza kusema in papers tunazo nzuri labda hata kuliko za Marekani, lakini kitekelezaji ni 0 kabisa, ukisikia viongozi wanasema "maisha bora kwa kila mtanzania" utaona kuwa ni fix fix tu,no one is working to that end, kila mtu is working on fattening his bank account, hakuna kitu ambacho serikali inaweza kusema inafanya zaidi ya uendeshaji wa siku hadi siku, Uongozi bora hili siwezi hata kusema we see it day in day out. Sasa hakuna uongozi Tanzania, tuna viongozi lakini hakuna uongozi, hata viongozi wenyewe wanatia shaka kama kweli ni viongozi.

Unless we go back to Azimio la Arusha, unless we go back to the core principles or the main guiding principle of this country, we will still be in mess. Hatuwezi kuendesha nchi bila miiko ya uongozi na bila kuwa na guiding principle yeyote.

Kwa kuwa Mjadala mrefu na wakina umeshafanyika na/au unaendelea, na kwa kuwa huo mjadala umekuwa kama kupasha misulu joto tu . Sasa tupate summaries ambazo tutazifanyia kazi ya kufanya a real CORE DISCUSSION ya Azimio La Arusha. Naweza kusema tulichofanya hapa mpaka sasa hivi ni Gereral Discussion ya Azimio La Arusha ambayo imekuwa inafanyika mara kwa mara sehemu mablimbali, naweza kuuita THE EXTERNAL DISCUSSION OF ARUSHA DECLARATION. Sasa tutumie hayo mahitimisho tufanye ESOTERIC DISCUSSION OF ARUSHA DECLARATION. Hii ni kwa sababu bado siamini kuwa AA ni Dhana nyepesi na ya kuchukuliwa juu juu tu! Kwa pande zote mbili "Kufanikisha" au "Kuzorotesha" Maendeleo ya Tanzania tunayoitaka. Kwa vyovyote vile, Azimio La Arusha Lina cha Kujibu, Sasa, wakati uliopita au wakati ujao!

Hivyo Kwa utulivu na bila kutawanyika sana, Tutengeneze summaries Kila Mtu Kwa maono yake then Tuachane na Long general discussion iliyotoa hizo summaries au abstracts. Kwani kiukweli hizo Long discussion zilizopatikana kwa mchakato makali wa wachangiaji kutoana JASHO wakati wa kutetea na Kuzijenga HOJA!

Hii ina maana gani?

Discussion itakuwa narrowed down and focused to A SPECIFIC CORE INNER DETAIL OF THE DECLARATION KATIKA KUJENGA THE TANZANIA WE WANT!!

Lakini kwanza tupate mahitimisho detailed ambayo yatakuwa rahisi kurejea, kama ya Za Kumi na Mchambuzi!
 
unataka kumtupia mpira nani? azimio la arusha author wake ni Nyerere, lilimfia yeye Nyerere, utekelezaji wake upi? kwani mahakamani kuna kurasa za azimio la arusha??

mkuu,
nyerere kuwa mwanzilishi asingeweza kulitekele peke yake wananchi na viongozi wa serikali pia wanahusika kulifanya kushindwa. hata hivyo sikweli kila kilichokuwapo katika azimio kilishindwa,
mfano utu,kufanya kazi kwa bidii,uzalendo na mengine kadha wa kadha
hivi unaweza kusema watu wa enzi za mwalimu waliosukwa na imani hii ya mwalimu i sawa na watu hawa tuliopo leo?
hivyo azimio usilitazame kwa upande mmoja bali kwa mapana na athari yake katika mapana hayo.
 
- WA-TANZANIA, KAMA TUNATAKA KUSONGA MBELE NA KIJIREKEBISHA TUACHANE NA MANENO YA AZIMIO LA ARUSHA, KWA SABABU NDILO HASA LIMETURUDISHA NYUMA SANA, LISIRUDI, LIENDE ZAKE, NA TUSILIJADILI MAANA NI SHETANI LILILOTURUDISHA NYUMA SANA, SASA TWENDE MBELE NA UBEPARI NA UTAWALA UNAOHESHIMU SHERIA NDIO THE BEST WAY MBELE

mkuu william
wasomi wanapotaka kurudi katika azimio la arusha wanataka kuyarudisha yale mazuri ya azimio, azimio halikuwa baya kabisa lilikuwa na mazuri yake na mapungufu pia,yale mazuri tukiyaenzi nafikiri taifa litakuwa pazuri haya ya kutokuwa na uadilifu ufisadi ukosefu wa uzalendo na hata uvivu ni matokeo ya kulitupa azimio la arusha.

kuhusu kilimo,
pengine mwalimu mnashindwa kumwelewa kwa wakati huo ilibidi kuhamasisha kilimo kwa namna yoyote ile kwani taifa lolote lililoendelea limepita katika hatua ya mapinduzi ya kilimo(agriculture revolution) ndio kuelekea huko katika viwanda na biashara zinginezo, labda kinachokuudhi wewe william ni kule kulazimishwa kwa watu kwenda vijijini kufanya kazi hizo lakini hata huko china ujerumani na kwingine kwingi watu wamekufa katika kujaribu kuleta maendelo ya nchi zao kwa naamna moja au nyingine, huko kuliwa na fisi halikuwa lengo la mwalimu bali lengo ni kujaribu kuwafanya watanzania kujizalishia ili tufike pale pa kupata malighafi za kuendeleza viwanda ambayo ingepekelea kuanza kukua kwa biashara sasa wewe ulitaka kilimo hicho kiendelezwe na nani kama si wananchi?

na kama ulitaka watu waanze kwa mabiashara hawakuwa na cha kutrade, ukumbuke pia hata technolojia ilikuwa bado chini hivyo yaliyotokea hayakuepukika.

Ila ulikuwa mwanzo mzuri, na uthubutu mzuri na msingi mzuri wa taifa letu, leo hii taifa halina dira, wala watu hawana kinachowaongoza.

Unaposema kuhusu kufwatwa kwa sheria kwani sasa hakuna sheria? Nini kimebadilika? Sheria pasipo uzalendo hakuna kitu, nachelea kusema baadhi ya mambo yaliopo katika azimio ni muhimu na yaendelezwe yatatufikisha pazuri
 
mkuu una moyo wewe!!

soma tathmini ya Nyerere ya AA baada ya miaka 10

http://www.tzonline.org/pdf/thearushadeclarationtenyearsafter.pdf


soma artcile hii ya mihangwa pengine itakufurahisha kidogo, lakini tatizo la msingi liko palepale tu.....kuwa Nyerere alikosea sana kuanzia mwanzo


Home*»*Insight





1. Nyerere alikosea ujamaa...haukuwa wakati wake na yy alijua hivyo
2. AA ilikuwa aidea yake baada ya miaka 10 likafa watu inaonyesha watu wake au vijana wake hawakujua lolote...unalosema azimio halikuwa azimio bali tamko!!

mkuu,
wewe unafikiri nini kilikuwa sahihi kwa wakati huo?
nchi imetoka kutawaliwa,watu wake hawakuwa na muelekeo wana machungu ya kunyonywa na mkoloni,hawana elimu ulifikiri mfumo gani ungefaa kuwatoa hapo na kwa namna gani? unafikiri huo ubepari unatekelezeka tu kirahisi katika jamii ya watu wa namna hii?
 
Heshima sana Mkandara.... I once told Mchambuzi something similar!!!

Glad this seems to be very true

Sehemu ya itikadi ya Chadema inayo nitatiza ni suala la kuwa 'mrengo wa kati' na nilishalijadili hili huko nyuma katika mazingira ya pro - poor economic growth ambayo ni muhimu sana given the level ya umaskini uliokithriri katika nchi yetu. Bila ya kuwa waangalifu, wananchi watakata tamaa haraka sana chini ya utawala wa Chadema unless itikadi ndani ya katiba yake iwe ni maneno tu lakini watekeleze sera za uchumi zenye kulenga kuleta maendeleo ya jamii kwa namna tofauti. Hata CCM wanasema itikadi yake ni ujamaa lakini utekelezaji wake ni tofauti kabisa. Pengine hii ni kawaida kwa vyama vyetu - kuweka itikadi yoyote kwenye katiba zao kama njia ya kutekeleza masharti ya usajili wa chama. Sina uhakika kama huwa wanakaa chini na ku 'brain storm' vyama vinahitaji kufuata itikadi ya/za namna gani ili kujipatia mafanikio ya kisiasa kutokana na kuwa na sera ambazo zina 'deliver'.

Tusisahau kwamba itikadi inatokana na matakwa ya jamii katika muda uliopo, haitungwi na chama i.e the process ya kupata itikadi ni bottom-up, sio top-down. Kinachotokea ni kwamba - chama kinaangalia jamii ina mtazamo gani, kisha kuweka mengi ya hayo katika package ya itikadi na kuendesha masuala yote ya kisera kwa mtazamo husika.

Otherwise Chadema ni Chama makini na kina nafasi kubwa sana ya kuleta mabadiliko nchini kuliko CCM. Tanzania inahitaji mawazo mapya na hayo hayawezi kutokea CCM hata siku moja. Ile kauli mbiui ya ARI MPYA KASI MPYA na NGUVU MPYA ilistahili itokee chama cha upinzani.
 
Sehemu ya itikadi ya Chadema inayo nitatiza ni suala la kuwa 'mrengo wa kati' na nilishalijadili hili huko nyuma katika mazingira ya pro - poor economic growth ambayo ni muhimu sana given the level ya umaskini uliokithriri katika nchi yetu. Bila ya kuwa waangalifu, wananchi watakata tamaa haraka sana chini ya utawala wa Chadema unless itikadi ndani ya katiba yake iwe ni maneno tu lakini watekeleze sera za uchumi zenye kulenga kuleta maendeleo ya jamii kwa namna tofauti. Hata CCM wanasema itikadi yake ni ujamaa lakini utekelezaji wake ni tofauti kabisa. Pengine hii ni kawaida kwa vyama vyetu - kuweka itikadi yoyote kwenye katiba zao kama njia ya kutekeleza masharti ya usajili wa chama. Sina uhakika kama huwa wanakaa chini na ku 'brain storm' vyama vinahitaji kufuata itikadi ya/za namna gani ili kujipatia mafanikio ya kisiasa kutokana na kuwa na sera ambazo zina 'deliver'.

Tusisahau kwamba itikadi inatokana na matakwa ya jamii katika muda uliopo, haitungwi na chama i.e the process ya kupata itikadi ni bottom-up, sio top-down. Kinachotokea ni kwamba - chama kinaangalia jamii ina mtazamo gani, kisha kuweka mengi ya hayo katika package ya itikadi na kuendesha masuala yote ya kisera kwa mtazamo husika.

Otherwise Chadema ni Chama makini na kina nafasi kubwa sana ya kuleta mabadiliko nchini kuliko CCM. Tanzania inahitaji mawazo mapya na hayo hayawezi kutokea CCM hata siku moja. Ile kauli mbiui ya ARI MPYA KASI MPYA na NGUVU MPYA ilistahili itokee chama cha upinzani.


ni kweli kabisa kauli mbiu hii haifanani na ccm kwani matendo wafanyayo na kauli hii n vitu tofauti kabisa. sasa kauli hii imesababisha watu kuichukia na kuidharau.
 
Mkuu wangu nakuelewa sana unachojaribu kusema. Dhambi zipo na hazitaweza kwisha lakini unapoharamisha dhambi ndipo unapoweza kutunga sheria kupambana nazo. Kwnai majambazi hawapo au wezi sii wapo na hawatakwisha mbona tunaweka sheria wakati haya ni maamuzi ya watu ambao mnadai wako huru.. Hakuna sheria inayotungwa pasipo kuwepo Dira ambayo hutunga mwongozo. AA sio Biblia au kura ila ni mwongozo kama Katiba maana Biblia na Kuran zimeandikwa baada ya imani za dini kufundishwa tena kwa karne nyingi zimepita, waumini walijua wanasali kwa ajili gani wanaabudu nini na hatua gani wazifuate ili waokoke kinyume cha sheria za Romans kina Pilato.

Katiba ndiyo inatunga sheria wakati dira ndiyo blueprint inayotangulia katiba maana huwezi andika katiba kama huna kitu mkononi, na katiba hubadilika kulingana na mazingira ya kidunia japo safari ni ile ile naha ktk dini toka Abraham hadi leo hii kuna vitabu kibao vimeandikwa vya sheria na tofauti. Sheria za imani ya dini zilitungwa baada ya imani hizi kuwepo kwa muda mrefu sana na zimewekwa kutokana na matukio, siku kwa siku, mweuzi hadi miaka sheria ziliendelea kutungwa ili kulinda waumini wake kutokana na all evil around them ikiwa wanataka kwenda Mbinguni. Jiulize kwa nini tunataka kukusanya mawazo ya watu kabla ya kuandika katiba mpya?.. kaa sii kujitmabua sisi ni nani, muungano wetu, kero zetu na kadhalika na tunaazimia kufanya nini.. Kwa nini tusitumie tu sheria kuandika katiba mpya au copy and paste.

Hivyo kwa muumini wa dini, dira yake ni maisha ya hapa duniani, hiyo safari ya kutoka hapa kwenda mahala pema peponi unatakiwa ufanye nini ili upate uzima wa milele na mwongozo na sheria zikawekwa kuwalinda waumini ili wapate kufika huko. Hivyo kinachotangulia ni who U are, WHY unabadilika toka ulivyokuwa na unataka kuwa nani.. Kitaifa tunasema kwa nini unataka kuwa HURU, ili uwe nani na kama ni Liberty ni mfumo gani utumike kulingana na mazingira yaliyokuzunguka, hivyo unaweza kutumia hata negative Liberty inategemea na WATU na ktk MAZINGIRA waliyopo, kisha sheria ina govern. Ukipoteza la kwanza sheria inakuwa haina msingi tena. Leo hii tunaweza mrudisha mkoloni tukatawaliwa na kwa sheria hizihizi zinazotumika leo, ila itapoteza UHURU wetu na tutajuliknana kama tunatawaliwa.

Sheria inalinda tu ile sababu ya WHY, kwa hiyo yule anayetembea nje ya ndoa kama AZIMIO linakataza watu kutembea nje ya ndoa na sababu zake, basi ni rahisi kutunga sheria lakini huwezi kuzuia watu wote wasitembee nje ya ndoa kwa sheria tu. Hata wizi na kifungoi cha miaka 10 au 20 inatokana na uzito wa crime yenyewe ktk jamii na why mwizi hatakiwi ndipo unapotunga sheria.

Yesu alisema wakati fulani kuwaambia waja wake kwamba walipomuuliza kaa kula chakula bila kunawa ni haramu, naye akawajibu sii kitu kinachoingia tumboni ndio haramu bali imani yake. Kwetu sisi waislaam tunaitafsiri hii kwa kusema kwamba binadamu tumeumbwa na madhambi, from out of our hearts come evil thoughts. Na huwezi kuyazuia haya ikiwa hujaazimia kufuata imani hiyo. Kifupi ni kwamba kama unaamini kula bila kunawa mikono ni haramu basi huna sababu ya kuuliza kinachoinmgia tumboni maana uharamu unaanza na fikra zako. Kwa mfano, haramu sii nguruwe wala nyama yake bali imekatazwa, kama una imani ya roho hutakula wala bila kuuliza isipokuwa kama huna imani na hujaazimia kuokoka utakula na utajijengea sababu zako..

So in short is to say, AA isn't the solution but a blueprint of who we are, our sovereignty and against what. Then Law should govern in contrast to any evil thoughts. Sheria pekee haina maana yoyote maana hata Uingereza Malkia yupo juu ya sheria, KIna Sultan wa Saudia wapo juu ya sheria lakini ukiwauliza watakwambia wanafuata sheria kuwa juu ya sheria..Sheria means nothing ikiwa hujui unachokitaka na ndio maana tunaburuzwa kwa kusoma sana sheria wakati roho zetu zinaamini Ufisadi sio kosa - Ujanja kuwahi!..

Mkuu Mkandara, I think this is the best I have seen from you! Gia aliyoingia nayo Waberoya ilinifanya kwa siku mbli niwe na usingizi mgumu. Lakini sasa nina weekend njema! Hoja ya kutokuwa na Mtizamo Murua na ulionyoka kwenye swala zima la SHERIA YA NCHI! MIIKO YA UONGOZI! MAADILI na KATIBA YA NCHI ...Imekuwa ndio FUNDO halisi la Mjadala huu na kwingineko na ni wachache wenye jeuri ya kuukabili!

Ngoja na Mimi nitengeneze hitimisho kwa ajili ya Fainali!!!! Maana wakati umefika lazima hili jambo lieleweke!!
 
Back
Top Bottom