Aziz Ali wa Gerezani na Mtoni Dar es Salaam

Aziz Ali wa Gerezani na Mtoni Dar es Salaam

Atakurushia sababu kama laki za kujustify hilo jina la Qafir
Hakuna jina la ki qafir,kuna majina Mazuri na Majina Mabaya,Kwenye uislamu hata kama ukiitwa rose ama joseph,ama diamond ama Edward ruksaa alimradi jina hilo liwe lina maana na asli nzuri,majina yasiyotakiwa ni yale yasiopendeza ama kutokuwa na maana mujarrab kama vile Shida,Masumbuko,Chuki,punda,(ashakum si matusi)[emoji482],mashaka etc,acha kueneza chuki baina yetu waislamu na wakristo ni ndugu moja watoto wa baba mmoja tusikwazane
 
Mbona reactions zako ni beyond kusahihisha ukweli!
Umetumia lugha za matusi/kukera mno!
Kama mleta mada amekosea kitu, historia hujengwa kwa kusahihisha, kwa kuwa kila mmoja wetu hapa atakuwa anaandika masimulizi, then yale yanayokubaliwa na wengi ndio huwa assumed kama maelezo sahihi Zaidi!
wewe, huji na version yako, umekuja na matusi tu!
Kama Mohamed Said asipoleta uzi wa historia hapa JF hakuna mwingine anayeleta, sasa masimulizi ya Tanganyika yatajulikana vipi!
Sidhani kama kuna anayeweza kuukataa mchango Julius, Rupia au Okello! lakini pia ni ukweli wenyewe lazima wachangie ktk ukombozi, hebu fikiria tu Julius kutoka Butiama aliishi mtaa gani hapa Dar Es Salaam, unadhani angewezaje kupambana na wazungu ktk mitaa ambayo hata chochoro hajui, Rupia alikadhalika!
Naona wote mnaongea kitu kimoja ktk spectrum 2 tofauti, ambapo hamna haja ya kutukana bali kuongezea nyama ktk historia zinazoletwa!
mkuu sikia mimi sina tatizo na historian wala history kitu ambacho hatuendi sawa ni style yake ya kuchomeka watu wasio na kichwa Wala mbele pengine hawakuhusika kabisa tena utakuta ndio walikuwa mashushu au wanafiki kwa wazungu katika harakati za Uhuru vibaraka huwepo... Sasa kuna walioondolewa kabisa na wengine waliostukiwa kwa sababu mbali mbali ikiwemo hiyo ya udini ambao mtoa Mada ndio msingi wake mkubwa Wa thread zake humu... Hao watu vibaraka walianzisha hadi vyama pinzani before uhuru... Ila Nyerere alikomaa na alikuwa hapendwi kwa kiswahili cha bara na kujua kwake kiingereza na ukristo wake Nyerere sasa huyu amerithi chuki tena nadhani ile misemo ya Mfumo kristo ndio Hawa walidhania Nyerere angejaza watu Wa msikitini kwenye serikali huku elimu hamna.. Hizo history za Uhuru na wapigania zipo mashuleni zimejaa waingereza wanazo Nyerere kaandika vitabu na kuna speech record TBC tele so acha uoga na story za huyu mzee hii nchi imepata Uhuru kwa kiongozi Ukristo. Yeye inamuuma. Anachofanya ni kutranslate vitabu na kuandika kwa kiswahili huku aliwachomekea sifa wahusika ambazo hazina misingi... Ati tayari akiwa mkristo oh mwafrika Wa kwanza kununua gari kujenga nyumba ya vitae n.k

Me sina chuki nae ila yeye anachuki na christian. Tulioleta Uhuru historia ndio ilivyo haibadilishiki hawezi rejesha ile hali yao ya chuki hadi wakristo kuishi kariakoo ni mission kota tu iliwezekana ila Tajili mkubwa Rupia anamuelewa
 
mkuu sikia mimi sina tatizo na historian wala history kitu ambacho hatuendi sawa ni style yake ya kuchomeka watu wasio na kichwa Wala mbele pengine hawakuhusika kabisa tena utakuta ndio walikuwa mashushu au wanafiki kwa wazungu katika harakati za Uhuru vibaraka huwepo... Sasa kuna walioondolewa kabisa na wengine waliostukiwa kwa sababu mbali mbali ikiwemo hiyo ya udini ambao mtoa Mada ndio msingi wake mkubwa Wa thread zake humu... Hao watu vibaraka walianzisha hadi vyama pinzani before uhuru... Ila Nyerere alikomaa na alikuwa hapendwi kwa kiswahili cha bara na kujua kwake kiingereza na ukristo wake Nyerere sasa huyu amerithi chuki tena nadhani ile misemo ya Mfumo kristo ndio Hawa walidhania Nyerere angejaza watu Wa msikitini kwenye serikali huku elimu hamna.. Hizo history za Uhuru na wapigania zipo mashuleni zimejaa waingereza wanazo Nyerere kaandika vitabu na kuna speech record TBC tele so acha uoga na story za huyu mzee hii nchi imepata Uhuru kwa kiongozi Ukristo. Yeye inamuuma. Anachofanya ni kutranslate vitabu na kuandika kwa kiswahili huku aliwachomekea sifa wahusika ambazo hazina misingi... Ati tayari akiwa mkristo oh mwafrika Wa kwanza kununua gari kujenga nyumba ya vitae n.k

Me sina chuki nae ila yeye anachuki na christian. Tulioleta Uhuru historia ndio ilivyo haibadilishiki hawezi rejesha ile hali yao ya chuki hadi wakristo kuishi kariakoo ni mission kota tu iliwezekana ila Tajili mkubwa Rupia anamuelewa
I don't get you!
Unamlalamikia mwenzio mdini wakati wewe unafanya the same!
Historia yako wewe ni ya ukristo na jamaa ya uislam!
Hebu changanyeni hizo historia 2 tupate version ya Tanzania!
Huwezi kubeza mchango wa waislam na uislam ktk uhuru wa Tanganyika! Lakini huwezi pia kukataa kuwa wakristo walikuwepo mstari wa mbele ktk uhuru!
Mapambano mazima hayakujengwa kwa misingi ya dini, nadhani uafrica ulitawala Zaidi ya kitu chochote, leo nyie vijukuu na vitukuu wa wapigania uhuru mnatazamana kwa dini mlizo rithishwa na wakoloni!
Ila I don't see you ukisema history, nakuona ukipinga tu!
Ukombozi wa kisiasa hauwezi kuwa na watu wawili, lazima kulikuwa na teams za kutosha!
upinzani ktk siasa usichukuliwe vibaya hata kidogo na hata kama mtu alikuwa mamluki lkn bado anapaswa kutajwa kwenye historia kwa nafasi yake!
 
Hakuna jina la ki qafir,kuna majina Mazuri na Majina Mabaya,Kwenye uislamu hata kama ukiitwa rose ama joseph,ama diamond ama Edward ruksaa alimradi jina hilo liwe lina maana na asli nzuri,majina yasiyotakiwa ni yale yasiopendeza ama kutokuwa na maana mujarrab kama vile Shida,Masumbuko,Chuki,punda,(ashakum si matusi)[emoji482],mashaka etc,acha kueneza chuki baina yetu waislamu na wakristo ni ndugu moja watoto wa baba mmoja tusikwazane
Wenye kuelewa walielewa

Mohamed anajulikana wewe hujui
 
Rose...
Unayo historia kinyume ya hivi?
Iweke hapa tuisome ikiwa unayo.

Sheikh Mohamed Said, hilo ombi ulilompa huyo Bi-mkubwa itapita Miaka 2000 mingine pasipo kuleta Historia tofauti na hii.
Na Yesu pia atarudi na kuingia hapa JF baada miaka 2000 mingine na Historia ataikuta hii hii.
Kinachotokea kuuchukia ukweli, Khalas.Neno Uislam kwa upande wa wenzetu ingewezekana Kwao walitamani lisitajwe popote inapotajwa Tanzania, huo ndio ukweli, ndio maana Sheikh Mohamed Said ukileta habari hizi watu wanakuona mdini, wanaweka ukweli pembeni wanasogeza jirani Udini, hawaleti historia yao ili tuone uongo wa Mohamed Said.
Nnazo picha za Miaka ya 1950 Nyerere yupo mitaa ya Magomeni, Mwinyimkuu au Takadiri kwenye ile picha Dini tofauti alikuwa Nyerere peke yake, na ni picha ambazo zilihusu harakati hizo za mambo ya vyama.
Mnaompinga mpinge tu, lakini huu ndio utabakia ukweli mpaka mtapoleta nanyi Historia ya Uhuru inayopingana na Mohamed Said kuwa waislam hawakuhusika na chochote kuhusu uhuru wa Tanganyika.
Baada ya hapo sasa tutaamini kweli Mohamed Said mdini maana kaleta Historia wengine kawaacha.
Mwenyezimungu akufanyie wepesi Sheikh Mohamed Said.
 
Sheikh Mohamed Said, hilo ombi ulilompa huyo Bi-mkubwa itapita Miaka 2000 mingine pasipo kuleta Historia tofauti na hii.
Na Yesu pia atarudi na kuingia hapa JF baada miaka 2000 mingine na Historia ataikuta hii hii.
Kinachotokea kuuchukia ukweli, Khalas.Neno Uislam kwa upande wa wenzetu ingewezekana Kwao walitamani lisitajwe popote inapotajwa Tanzania, huo ndio ukweli, ndio maana Sheikh Mohamed Said ukileta habari hizi watu wanakuona mdini, wanaweka ukweli pembeni wanasogeza jirani Udini, hawaleti historia yao ili tuone uongo wa Mohamed Said.
Nnazo picha za Miaka ya 1950 Nyerere yupo mitaa ya Magomeni, Mwinyimkuu au Takadiri kwenye ile picha Dini tofauti alikuwa Nyerere peke yake, na ni picha ambazo zilihusu harakati hizo za mambo ya vyama.
Mnaompinga mpinge tu, lakini huu ndio utabakia ukweli mpaka mtapoleta nanyi Historia ya Uhuru inayopingana na Mohamed Said kuwa waislam hawakuhusika na chochote kuhusu uhuru wa Tanganyika.
Baada ya hapo sasa tutaamini kweli Mohamed Said mdini maana kaleta Historia wengine kawaacha.
Mwenyezimungu akufanyie wepesi Sheikh Mohamed Said.
Amina, Sheikh apewe wepesi. Kuna figisu nyingi sana zimefanyika kuficha ukweli.
 
Amina, Sheikh apewe wepesi. Kuna figisu nyingi sana zimefanyika kuficha ukweli.
Lipyoto,
Kila aliyekisoma kitabu cha Abdul Sykes au kusikia historia hii kwa mara ya kwanza alipigwa na butwaa.

Baada ya mshtuko huo wapo waliokasirika na wapo pia waliofurahi.

Mimi sishangai hapa ninapoona hizi hamaki na wakati mwingine matusi.

Wangependa tubaki na ile historia rasmi iliyoandikwa na Chuo Cha Kivukoni.
 


Wednesday, 4 January 2017

Aziz Ali
Kleist Sykes alikuwa na duka la vyakula Kipata Street sasa mtaa huo umepewa jina lake unaitwa Mtaa wa Kleist. Hizi zilikuwa juhudi za Kitwana Selemani Kondo alipokuwa Meya wa Dar es Salaam kuwaadhimisha watu maarufu wa waliopata kuishi Dar es Salaam na wakaitumikia jamii. Nilipata kumsikia Mzee Kondo akisema, ‘’Hivi vipi litawekwa jina la mtu ambae hana nasaba yoyote na mji wa Dar es Salaam katika mji huu na kuwaacha wenye mji wao?’’ Hakika jambo hilo halikughalis. Mzee Kondo aliendelea na kusema, ‘’Hivi jina la Matola kwa nini lisiwekwe Dodoma lije liwekwe Dar es Salaam na wakati huo huo wakawasahau wazee wetu wa Dar es Salaam?

Turejee kwa Kleist Sykes. Hili duka lilikuwa nyumbani kwake na hapo ndipo ilipokuwa barza ya wazee maarufu wa mjini kukutana jioni inapoingia alasiri kuzungumza. Miaka ile Dar es Salaam kulikuwa na wauza kahawa wanapita mitaani na kahawa zao ndani ya madeli ya shaba yanayong’aa kwa kupigwa braso wakiuza kahawa na wao wenyewe wamevaa nadhifu, kikoi na kizubau na kofia kichwani. Basi baraza ile kila muuza kahawa akipita ataitwa na kuagizwa apige duru kwa wanabarza. Ikawa pale ile barza waungwana wale wanakunywa vikombe na vikombe vya kahawa hadi wanapoagana Maghrib inapoingia.

Mmoja wa wanabarza wa barza hii alikuwa babu yangu Salum Abdallah ambae nyumba aliyokuwa anaishi ilikuwa inatazamana na nyumba ya Kleist. Hawa walikuwa si majirani tu bali hata kazi wanafanya pamoja Tanganyika Railways. Hii ilikuwa miaka ya mwanzo ya 1920. Kleist akiwa Karani wa Mahesabu na babu yangu Mfua Vyuma kwenye karakana ya Railway iliyokuwa Arab Street sasa Mtaa wa Nkrumah. Mle ndani kulikuwa na king’ora kikipigwa saa moja kamili asubuhi barabara na saa saba mchana. King’ora hiki cha Railway kiliwasaidia sana wakazi wa Kariakoo na Ilala kujua majira.

Mtu mwingine maarufu katika ile barza alikuwa Aziz Ali, Mdigo kutoka Moa Tanga. Huyu Aziz Ali alikuwa mwamba katika miamba ya Dar es Salaam. Alikuwa tajiri ‘’contractor,’’ wa kujenga, majumba, Mwafrika wa kwanza kununua gari na kujenga nyumba ya vigae na vioo Mtoni. Nyumba hii hadi leo ipo na sehemu hiyo katika Kilwa Road inaitwa Mtoni kwa Aziz Ali. Lakini katika sifa hizi sifa yake kubwa sana Aziz Ali ilikuwa ujenzi wa misikiti na kuihudumia misikiti. Hii ilikuwa miaka ya 1930 na hapakuwa na umeme Kariakoo. Misikiti ilikuwa ikitumia karabai kuonea. Aziz Ali yeye alinunua karabai kwa kila msikiti na ikifika Maghrib mwanae Hamza alikuwa akizitia mafuta na kuziwasha kisha akizipeleka kila msikiti tayari kwa sala ya Maghrib. Inapomalizika sala ya Isha alikuwa anapita tena katika ile misikiti kukusanya karabai zake na kurudi nazo nyumbani kwao Mtaa wa Mbaruku na Kongo. Hii ndiyo ilikuwa kazi yake kila siku. Aziz Ali alipokufa mwaka wa 1951 miaka miwili baada ya kifo cha rafiki yake Kleist gazeti la Tanganyika Standard liliandika kifo chake kwa maneno haya: ‘’Aziz Ali the Builder of Mosques is Dead,’’ yaani, ‘’Aziz Ali Mjenzi wa Misikiti Amekufa.’’ Iko siku nilimtembela Rose Aziz mjukuu wa Aziz Ali, mtoto wa Hamza Aziz. Rose akanionyesha picha katika ukumbi wake ya mtu amevaa tarabushi akanambia, ‘’Mohamed unamuona mume wangu?’’ Nikiwa katika hali ya kushangaa huku nikiikodolea macho ile picha Rose akaendelea, ‘’Huyu babu yangu Aziz Ali.’’

Aziz Ali alikuwa na nyumba nyingi sana Dar es Salaam na ndiyo zilikuwa moja ya utajiri wake. Katika nyumba hizi nyumba ambayo imaecha historia ya pekee ni hii nyumba ya Mtaa wa Mbaruku na Congo kwa sababu nyumba hii ilikuwa moja ya sehemu ambazo harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika zilianza. Nyumba nyingine ilikuwa Mtaa wa Kipata kwa Ally Sykes, hapo zamani lilipokuwa duka la baba yake na barza ya wazee. Nyumba nyingine ilikuwa Stanley Street kwa Abdul Sykes. Nyumba hii ilikuwa pia ya Kleist na kulikuwa na duka la vifaa vya ujenzi katika uhai wake. Hii ilikuwa mwanzoni mwa mwaka wa 1950. Mambo yalipamba moto sana kuanzia mwaka huo pale vijana wazalendo walipoanza kufanya mipango ya kuunda chama cha siasa halisi kupambana na ukoloni wa Muingereza. Hizi ndizo zikawa nyumba ambazo Nyerere alikuwa akifika kuanzia mwaka wa 1952 kila anapokuja mjini kutokea Pugu alipokuwa akifundisha. Mama Ali mke wa Aziz Ali bado yu hai, Bi Mkubwa huyu ana mengi katika historia ya nyumba ile ya Mbaruku alipokuwa akiishi na mumewe katika miaka ile ya 1940 na akaendelea kuishi hapo na wanawe baada ya kifo cha mumewe. Hivi sasa Mama Ali anaishi Ilala na ni mtu mzima sana.

Angalia picha:Mohamed Said: AZIZ ALI WA GEREZANI NA MTONI DAR ES SALAAM
Mzee wangu Mohamedi Said nakualika ufike katika kijiji chetu cha Moa, Tanga, kijiji maarufu sana kwa mwambao wa kaskazini mwa Tanga, sikua nikijua kuwa Aziz Alli alitokea kijijini kwetu, Subhana Llaah, njoo kuna mzee mmoja ni babu yangu amezaliwa kunano mwaka 1926 au 1927. Bado yu hai na nguvu tele, ana mambo mengi sana unaweza kustafid.
 
Mzee wangu Mohamedi Said nakualika ufike katika kijiji chetu cha Moa, Tanga, kijiji maarufu sana kwa mwambao wa kaskazini mwa Tanga, sikua nikijua kuwa Aziz Alli alitokea kijijini kwetu, Subhana Llaah, njoo kuna mzee mmoja ni babu yangu amezaliwa kunano mwaka 1926 au 1927. Bado yu hai na nguvu tele, ana mambo mengi sana unaweza kustafid.

Duh unaona maajabu ya mtandao hayo akhi
dangadunguri.Maalim Mohamed Saidi kanifungua macho Na historia ambayo nilikuwa siijui.MwenyeEZMungu amlinde maalim wetu Mzee Mohamed Saidi Na husda Na kila balaa
Amen.
 
Mzee wangu Mohamedi Said nakualika ufike katika kijiji chetu cha Moa, Tanga, kijiji maarufu sana kwa mwambao wa kaskazini mwa Tanga, sikua nikijua kuwa Aziz Alli alitokea kijijini kwetu, Subhana Llaah, njoo kuna mzee mmoja ni babu yangu amezaliwa kunano mwaka 1926 au 1927. Bado yu hai na nguvu tele, ana mambo mengi sana unaweza kustafid.
Danga...
Ahsante sana kwa mwaliko.
Nimewahi kufika Moa na kwa kweli ni kijiji cha kiasili.

Nimeona ule msikiti pale na gati ambalo kwa wakati
ule nilipofika lilikuwa limemezwa na bahari lakini bado
linaonekana.
 
Waafrika wanafika sana, walikuwa wanawapinga makaburu halafu wanajibebesha majina ya kikaburu. Mbona makaburu hawakujiita Totsi, au Vusi?
Miafrika tuna mapepo wachafu vichwani
Buibui,
Waafrika kulipa majina ya watawala wao si kwa sababu walikuwa wanafiki.

Hii ni moja ya majanga ya ukoloni.
Hebu angalia hili.

Kleist Sykes katika mswada wake aliandika kuhusu maisha yake na vipi baba yake alikuja Tanganyika akiwa askari mamluki anasema kuwa Herman von Wissman aliweka mkataba nä Affande Plantan kuwa wakiiteka Tanganyika wataitawala kwa ushirika kati ya Wajerumani na Wazulu.

Nani hii leo anaweza kuamini ulaghai kama huu.

Sasa tuangalie nini kilifuata baada ya ushindi wa Wajerumani dhidi ya Abushiri bin Salim Al Harith na Chief Mkwawa.

Wajerumani wakatengeneza jeshi wanaliita Germany Constabulary na Mkuu wa Jeshi hilo akawekwa Affande Plantan.

Jeshi hili likawekwa katika kambi.
Watoto wote waliozaliwa katika kambi za Wajerumani walipewa majina ya Kijerumani.

Lakini wazee wao hawakuridhia wakawa wanawapa majina yao ya asili.
Ndiyo maana unakuta Kleist jina lake ni Abdallah.

Schneider ni Abdillah nk.
 
Back
Top Bottom