Baada ya ACT-Wazalendo kujiunga katika SUK huko Zanzibar, CHADEMA kinakwenda kuwa Chama Kikuu cha Upinzani Zanzibar

Baada ya ACT-Wazalendo kujiunga katika SUK huko Zanzibar, CHADEMA kinakwenda kuwa Chama Kikuu cha Upinzani Zanzibar

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Waswahili wana msemo: "atafutae hachoki, akichoka amepata". Msemo huu utajidhirisha huko Zanzibar kuanzia sasa ambapo Wazanzibar wanaotafuta ukombozi kwa mara ya pili, watatafuta ukombozi huo kupitia chama tofauti na ACT-Wazalendo na chama pekee kitakuwa ni CHADEMA unless CHADEMA nao waonyeshe udhaifu wa kuungana na CCM Bungeni au nje ya Bunge.

Maalim Seif sasa ameshapoteza ushawishi kwa wananchi wa Zanzibar kwa kuwa sehemu ya makubaliano ya kuungana na watesi wao, na zaidi Maalim umri umeshamtupa mkono hivyo wananchi hawawezi tena kumtegemea kuongoza mapambano ya 2025 katika kutafuta dola hivyo Maalim ameshafika mwisho kisiasa.

Kwahiyo, kama ambavyo Wazanzibar walimfuata Maalim ACT, ndivyo sasa watajikuta hawana option zaid ya kusimama na CHADEMA huko Zanzibar wakati wowote kuanzia sasa ambapo tunaweza kushuhudia bendera za ACT-Wazalendo zikishushwa katika maeneo mbalimbali huko Zanzibar na Siku zijazo CHADEMA ndio ikawa mbadala wa ACT kama ambavyo ACT ilivyokuwa mbadala wa CUF.

Pia, Wazanzibar sasa wanakwenda kuacha na siasa za kuwa wafuasi wa mwanasiasa fulani na sasa watakuwa wafuasi wa taasisi za kisiasa(vyama vya siasa) kama ilivyo huku Bara ambapo mwanasiasa wa upinzani akihama upinzani na kujiunga na CCM, ushawishi wake nao unafutika kama tulivyoona kwa Dr. Slaa na sasa Halima Mdee na kundi lake.

Mungu ana makusudi na kila jambo, hivyo maamuzi ya ACT kujiunga katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa huko Zanzibar, yanaweza yakawa ni faida kwa CHADEMA na pigo kwa ACT na viongozi wake.

Wanachopaswa kufanya CHADEMA ni kuendelea kuikataa CCM na makandokando yake kama walivyofanya kwa kuwakataa kina Halima Mdee na kundi lake kwani adui wa CCM kisiasa (CHADEMA), ndio atakuwa/ataendelea kuwa rafiki wa Wazanzibar walio wengi, na rafiki wa CCM kisiasa(sasa ACT), ndie atakuwa /ataendelea kuwa adui wa Wazanzibar walio wengi.

Muda utathibitisha.
 
Kimeshindwa kuwa chama kikuu cha upinzani wakati CUF imesambaratika alafu ije kuwa leo?

Umesahau Lisu alipoenda kujifanya kamati kuu na kumteua Seif kuwa ndio mgombea wenu kule Zanzibar wakati mgombea wenu alikuwepo?
Wazanzibar walikuwa wanamtazama Maalim Seif, mtu ambae sasa anaonekana kuungana na watesi wa Wazanzibar hivyo Wazanzibar sasa watalazimika kusimama na vyama kama taasisi na si tena kusimamia na mwanasiasa mmoja mmoja.
 
Mbona Mbowe anawabania wabunge wa viti malum sasa?

Au kwa kuwa Joyce Mukya ametoswa?
 
Wazanzibar walikuwa wanamtazama Maalim Seif, mtu ambae sasa anaonekana kuungana na watesi wa Wazanzibar hivyo Wazanzibar sasa watalazimika kusimama na vyama kama taasisi na si tena kusimamia na mwanasiasa mmoja mmoja.
Mbona toka miaka ya nyuma inakuwa hivyo?

Kwani Seif kaanza leo kuungana na ccm?

Au umeanza kufuatilia siasa jana?
 
1456109.jpg
 
Mkuu una mawazo mapana Sana, binafsi hii ni fulsa naiyona KWA chadema kusuka mtandao imara visiwani humo na itapasua mawimbi Sana.

Wazanzibar,wanampenda Sana seif,ila kwa hili halitawaacha salama Chadema hii ni fulsa ,so msijidanganye, kwa tathmini ya haraka, mpaka mda huu wananchi wamezidi kuwaelewa kutokana na msimamo wenu, KWA zaidi ya asilimia 85.
 
Maailim ananakwambia"marahii atutokubali ukhanithi"
naona sasa kakubali kuwa khanithi.
Sidhani kama Wazanzibar wataendelea kumuanini tena. Yaliyofanyika mwaka huu huko Zanzibar yanatisha hivyo haingii akilini kuungana na walifanya unyama ule.
 
Mkuu hayo sisi tuliyaona mapema hasa pale Zitto alivyoungana na CUF ya Maalim Seif. Lakini tumemsikia Zitto huyu huyu akitaka Chadema isipeleke wabunge wa viti maalum bungeni tena akiita Chadema a sister party.

Leo yaliotokea ni tofauti. Lakini kumwambia Chadema awe ndio mpinzani Zanzibar HAIWEZEKANI.Kwa sababu siasa za Zanzibar zinajitambulisha kwa Upemba vis Unguja,hakuna ubara hapo.

Mifano ipo wazi tokea Maparara, Lipumba. Chadema ni kutuliza kichwa yapo mambo yanayoweza kushirikiana na ACT-WAZALENDO, au CCM.Sio kila kitu cha CCM,au CUF,au ACT ni kibaya.
 
Back
Top Bottom