Baada ya DR Congo kuingia EAC, sasa changamkieni fursa kama ifuatavyo

vita viko ukraine huko,drc hkn vita

watanzania wamezoea bure.ndo maana nchi inapiga sana mizinga (mikopo)

wananchi wamekalia porojo za simba na yanga.ccm na cdm

zikija fursa sababu zinaanza
Diamond harmonise kafanya nini

Waache uwoga na porojo

Utakuta mtu unampa ramani anabakia mwaka mzima anauliziaa kukoje huko
Badala ya kwenda akaone mwenyewe hali halisi

Ova
 
hahahaha. wanaogoqa kufa? dah dunia ya leo unaogopa kufa?

kwenye vita.mapigano.vurugu niko kule mashariki .wao waje katanga km vp
 
Mkuu Nina mtaji wa 3M hapo katanga nitafanya biashara ngapi kaka?
mkuu umesoma uzi vzr? drc kila kitu wanaagiza nje, kwanza nenda ukafanye tafiti ndogo

kwa mtaji huo kwa mfn unaeza peleka hata toilets paper.kule hawatumii maji chooni.kifupi unaeza uza chochote. huo ni mfn
 
Ona sasa mtu anaulizia vita
Hawajui kwenye machafuko kuna neema

Ova

Tuko nyuma sana mkuu ujue mtu wa namna hiyo anatafuta sababu ya kutotoka kwenda kutafuta chochote kitu nchi za watu
 
Usiwastue waache waendeleee kulaumu Samia na Serikali 😀😀
 
Kazi wanabakia humu wanaishia kulialia mara Sijui January, mgao umeme
Wanaulizia pesa za msaada
Vijana Sahv wamekuwa lonyalonya sana

Ova

Kabisa mkuu kile kizazi cha watu wa Songea waliokua wanazamia machimboni msumbiji na kurudi kwao kujenga majumba hakipo au kile kizazi cha watu wa lindi na mtwara kilichokua kinavuka boda ya tangazo kupeleka ngano na redbull msumbiji kilishapotea saa hizi tuna walalamikaji wa Taifa, Ujasiri kwa watanzania umeisha kabisa
 

Acha kabisa malawi na zambia kulikua na vitu vya maana, wao ilikua landcruiser ikisumbua kidogo wanapaki yaani mafundi walikua hawana hivo wanauza kama chuma chakavu fasta wabongo waliotea hadi magreda huko, spare used ziliingia bongo kama chuma chakavu, respect kwa wana wote waliopuyanga enzi hizo
 
Wkt huo m23 wanacheka tu ihiii hiii hiiiiiiiiiii , wanasema waleteee

Nakupa hii hapa, niliwahi kwenda kuwauzia m23 buti za kijeshi nilizitoa kwenye mitumba nyeusi na zile za kaki kuzipitisha nilinunua udaga maeneo ya masumbwe tani kumi nikafunika vizuri nikazama rwanda, goma hadi maporini kwao vile viatu nilikusanya pea za kutosha hakuna iliyozidi elfu 30 jamaa walinunua kwa laki na 20 , kila pea nilikua navuka na kifuso kama napeleka udaga kumbe udaga kizugio tu sasa acha uoga dogo kapambane, nimekuthibitishia hata hao waasi watu tulifanya nao biashara
 
Kwani unafikiri watu hawajawahi onana nao
Nendeni acheni uoga kamateni fursa

Ova

Nimemuelezea chini kisa changu cha kuonana na hao waasi kwenye pori fulani mbele ya Goma, tatizo watu waoga sana basi tu
 
Sasa ndo uelekeze njia nzuri ni ipi ya kwenda .
Suala la usalamatwa mtu linatakiwa liwe kipaumbele Cha kwanza SIO FURSA.
HAKUNA maduka ya kuuza uhai
Vita ipo lakini sii maeneo yote yana vita ukianza kuwaza hivo hutovuka border
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…