#COVID19 Baada ya kampeni ya chanjo za COVID-19 kudoda, Askofu Gwajima kuwa mbuzi wa kafara?

#COVID19 Baada ya kampeni ya chanjo za COVID-19 kudoda, Askofu Gwajima kuwa mbuzi wa kafara?

Mimi nikitafuta namna nyingine ya kuishi hujui kuwa na wewe itabidi utafute namna nyingine ya kuishi kwa sababu inaonekana maisha yako yanategemea uwepo wa mada zangu hapa Jamiiforums ili uzijibu hata kwa hoja za kijinga kama ulivyofanya ili upate ujira wako!

Nani alikuambia kuwa CCM walikuwa wanadhani kuwa kila mtu anaweza kuwa Rais wa Tanzania. Hujui kuwa wagombea wa Uraia ndani ya CCM mwaka 2015 walikuwa zaidi ya 40 lakini waliofika kwenye mkutano mkuu ni 5

Kama ilivyo kawaida yenu na wauza chanjo, badala ya kushambulia hoja kwa nguvu za hoja badala yake unashambulia mleta hoja kwa matusi na hoja za nguvu.

Mimi nikitafuta namna nyingine ya kuishi hujui kuwa na wewe itabidi utafute namna nyingine ya kuishi kwa sababu inaonekana maisha yako yanategemea uwepo wa mada zangu hapa Jamiiforums ili uzijibu hata kwa hoja za kijinga kama ulivyofanya ili upate ujira wako!

Eti kwa sababu kuna chanjo zaidi ya 60 kwa hiyo wananchi walazimishwe hata chanjo ambazo zimeleta mgawanyiko mkubwa kwa wataalam kule zinakotoka.

Hujui kama chanjo zingine mpaka kupewa binadamu zilipitia mfumo unaotambuliwa kimataifa ambao pia sio mfumo unaotumika sasa wa “emergence administered” ambao dhumuni lake kuu ni uchumi kwanza?

1630596755042.png
 
Kiongozi lazima uwe na team ya ushindi na siyo hawa makanjanja tupu

Inawezekana hata kiongozi akawa ni kanjanja!

Waliosema, the buck stops at the state house nadhani hawakukosea!
 
Magufuli ameshakufa kijana. Tafuta namna nyingine ya kuishi.

Tanzania kuna chanjo zaidi ya 60..

Kila siku wanawakae na watoto wanapokea chanjo kila iitwapo siku na tena wasipozipata wanalalamika.

TT pekee inatolewa mpaka shots nne na watu wanaipata.

Kampeni ya COVID imekuwa ngumu kwasababu ha athari za akili ya kibwenhmgo Magu alizoacha.

Hata CCM wenyeqe naamini wamejifunza siyo kila mtu anaweza kuwa Rais. Magu was a total disaster.
Kama ni hivyo basi nchi nzima hii walimuelewa sana magu
 
Naona sasa ni zamu yako kuleta uzi humu chato gang.

Poleni sana na chuki zenu dhidi ya Samia. Hamjafanikiwa kwenye lolote na hamtafanikiwa kwenye lolote

Na wewe ni zamu yako kujibu uzi wangu!

Sisi “ sukuma gang” hatuwezi kufanikiwa kwa sababu kama asingekuwa Rais Magufuli kuchagua kuwa mgombea mwenza sidhani kama Rais Samia angekuwa ni Rais wa Tanzania!
 
Na wewe ni zamu yako kujibu uzi wangu!

Sisi “ sukuma gang” hatuwezi kufanikiwa kwa sababu kama asingekuwa Rais Magufuli kuchagua kuwa mgombea mwenza sidhani kama Rais Samia angekuwa ni Rais wa Tanzania!
Mjomba umeambiwa utafute namna nyingine ya kuishi,

Kuishi kwa kudanganyana hakupo kama wazungu wanataka kukuua wana njia nyingi za kukuondoa kama walivyomuondoa huyo uliyekuwa unapata riziki kupitia mgongo wake!!
 
nyinyi mataahira mtaacha lini kumwota magufuli!!!!

kwani imeshindikana kabisa kuelewesha watu umuhimu wa chanjo tofauti na walivyoelekezwa na magufuli!!

Badala ya kupambana ili kubadilisha mawazo ya wananchi wengi kuhusu fikra za chanjo za korona, kwa sasa wanachofanya ni kutoa lawama kwa mtu ambaye amemaliza safari yake ya hapa duniani!
 
Usanii zaidi wa hii biashara ya kulazimishana umeonekana Zanzibar ambako chanjo iliyotumika pamoja na kuidhinishwa na WHO haitambuliwi na nchi za Magharibi na Marekani.
Hivyo imepelekea Mahujaji wachanje tena J&J ili waende Saudia nchi mshirika wa Ulaya na Marekani.

Completely business

Hizi chanjo ni biashara lakini mbaya zaidi ni biashara ya kulazimishana!
 
Ukiwa kiongozi ukazungukwa na wanafiki wengi. Ni ngumu kufanikiwa.

Mama ana wasaidizi ambaohata huna uhakika kama wanafanyakazi kwa dhati, au bora liende.
Kinachoendelea serikalini na bungeni ni kutafuta mbuzi wa kafara baada ya “utapeli” wa serikali kuhusu chanjo za korona kushtukiwa na wananchi wengi nchini.

Fikiria chanjo za watu milioni moja ambazo serikali ilipokea kama “msaada” kutoka Marekani mpaka sasa zaidi ya nusu yake bado ziko kwenye “magodauni” zikisubiri watanzania kujitokeza kwenda kupata hizo chanjo!

Kibaya zaidi hizi chanjo za korona zinahitaji uangalifu wa hali ya juu katika utunzaji ili zisiharibike. Kwa sasa ni mwezi mmoja na wiki mbili tokea serikali ilipopata hizi chanjo!

Chanjo za Johnson and Johnson zinapozalishwa zina expire baada ya miezi 4. Kuna uwezekano wa wananchi huko vijijini kupewa chanjo ambazo zime expire au zimeharibika kutokana na utunzaji mbaya.

Ieleweke kuwa chanjo hizi zinatakiwa kwa muda wote ziwe kwenye jokofu(fridge) lenye joto kati ya 2°C na 8°C (36°F na 46°F). Kwa umeme huu wa mgao au majokofu “spear mkononi” kuna uwezekano mkubwa kwa chanjo kuharibika!

Juzi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alitoa wito kwa wakazi wa Jiji la Dar Es Salaam na viunga vyake wajitokeze kwenye uwanja wa uhuru kupata chanjo bila kujali makundi yao lakini mwitikio ulikuwa ni hafifu sana hasa ikichukuliwa Jiji la Dar es Salaam lina watu zaidi ya milioni 6 na wengi wana uelewa na ufahamu zaidi.

Serikali inatumia nguvu nyingi bila maalifa katika kutimiza malengo ambayo wananchi wengi wameyakataa kimya kimya huku wachache kama Askofu Gwajima wakipaza sauti zao.

Kwa sasa mpaka bunge linaanza kutumia nguvu kuisaidis serikali kuwafumba mdomo baadhi ya wananchi/wabunge wanaotoa sababu za kutochanja.

Yaani serikali haitaki mtu aeleze kwa sauti sababu zinazomfanya asichanje lakini serikali hiyo hiyo inataka waliochanjwa wajipige picha/video na kueleza kwa sauti kwa nini wanachanja.

Kama chanjo ni hiari, kwa nini wizara ya afya inatumia pesa za watanzania wote kuwahamasisha watanzania kuchanja chanjo ambazo mpaka sasa zimeleta mgawanyiko mkubwa huko zinakotoka. Kwa lugha nyingine, serikali inatafuta soko la chanjo kwa kutumia pesa na rasilimali za wananchi.

Neno hiari kwa sasa linageuzwa kuwa LAZIMA eti kwa sababu Rais wa Tanzania amechanja.

Kuna Mbunge mmoja anasema eti maneno ya Askofu Gwajima ya kupinga chanjo yanaweza kusababisha serikali ya Rais Samia kupinduliwa! Eti akamatwe kwa kosa la uhaini! Huyu ni aina ya mbunge anayesababisha bunge zima kuonekana kama limejaa wabunge ambao uwezo wao wa kupambanua na kuchambua mambo ni finyu!

Kinachoendelea nchini kuhusu chanjo kinadhihilisha Watanzania sio wajinga au “sell-out”.
Wewe ni muumini wa Self declared Askofu Gwajima.Mwenzenu keshachanja Kenya tangia mwaka jana.Sasa nyie wapumbavu mtaondoka na familia zenu.Nenda kawaulize wanauza Sanda na Majeneza watakujibu.Maelfu wamelazwa na mamia watapoteza maisha kwa ajili ya covid 19.
 
Basi huyu Magu atakua na ushawishi mkubwa sana, suala la chanjo limeigawa dunia kuanzia huko zinakotengenezwa.
Kwetu tuheshimu maamuzi na hiari kama tulivyoambiwa, anaetaka achanje, anaeona tashwishwi asichanje. Hakuna sababu ya ugomvi.

Mleta uzi anaonya athari na kutoa tahadhari kwa wanaochanjwa kwamba kwa mwenendo unavyoenda, huenda dawa zikafikia muda wake wa kwisha matumizi zikiwa bado hazijatumika.

Akatoa wito kampeni na namba bora ya uhamasishaji ifanyike badala ya hii ya awali kutokuonyesha matokeo chanya.

Kwanini tunajikita kumshambulia mtoa hoja badala ya kujadili hoja?

Tumeona hadi sasa hivi ndugu zetu wa Zanzibar waliochoma chanjo ya China kama sehem ya maandalizi ya kwenda hija wameambiwa wanatakiwa wachanje J&J au zingine zinatotambulika Saudia. Hayo ni mambo serikali ilitakiwa iwe mstari wa mbele kutolea ufafanuzi na kueleza nini kifanyike ili kuwatuliza wananchi. Vinginevyo taharuki zitaendelea.

Mkuu, nashukuru kwa mchango wako wenye ukweli na hekima
Kubwa.

Kwa sasa jukwaa hili limebakiwa na watu wachache sana wenye uwezo mkubwa kifikra kama wewe.

Asante
 
Magufuli ameshakufa kijana. Tafuta namna nyingine ya kuishi.

Tanzania kuna chanjo zaidi ya 60..

Kila siku wanawakae na watoto wanapokea chanjo kila iitwapo siku na tena wasipozipata wanalalamika.

TT pekee inatolewa mpaka shots nne na watu wanaipata.

Kampeni ya COVID imekuwa ngumu kwasababu ha athari za akili ya kibwenhmgo Magu alizoacha.

Hata CCM wenyeqe naamini wamejifunza siyo kila mtu anaweza kuwa Rais. Magu was a total disaster.
Hizo chanjo unazosema siyo chanjo za majaribio ni chanjo kamili ,kuhusu chanjo za korona tulisha sema sana sijui hadi tuwatie vidole ndiyo muelewe tumesema uwezi kusema kuna chanjo ya korona wakati ugonjwa upo katika hali ya kubadilika badilika hivyo tukasema tusubiri hadi itakapo patikana chanjo ya uhakika ya kovidi
 
Kwenye chanjo serikali imechemka big time.

Juzi wizara ya afya imesema kwa mwezi mmoja ama siku 32 watu 304,000 ndio walikua wamechanja, kwa maana kua ndani ya mwezi mmoja chanjo ni 33% tu zimetumika.

Kwa hesabu ya haraka chanjo milioni za msaada zitahitaji miezi 3 kumalizika wakati hizo chanjo haijulikani zilizalishwa lini hadi kufika Tanzania na hadi kumalizika zitakua na miezi mingapi, watu watapewa expired shots.

Iwapo mpango wa covax ni kutusaidia chanjo milioni 12, maana yake tutahitaji miezi 36 kuzimaliza hizo chanjo za covax, miaka 3 na ushee. Na wataalam wanashauri ili kujihakikishia ulinzi angalau uchanje 70% ya raia wako, kwa Tanzania ni kama milioni 40, hiyo tutahitaji miaka 10 kumaliza kuchanja 70% ya raia wote.

Hesabu za chanjo zinagoma, tumeingia mkenge wa kukubali kukopeshwa trilioni 2 za kununua madawa ya chanjo lakini iko wazi huu ni usanii.
Wameingia kichwa kichwa ili na wao waonekane. Kwa mwaka moja unahitaj chanjo si chini ya tatu (Case study - UK wanatoa third jab right now) Kuchanja 90% ya watanzania mara tatu zinatakiwa dozi millioni kama 150 na usheee. Je Bei ya booster shots ni sawa na chanjo ya kwanza? Kama ni tofuti ni kwa kiasi gani?



 
Yule "Hero" wako

kichwa ngumu ndie chanzo cha yote, apumzike anapostahili, alifundisha wengi ujinga mwishowe ukamrudia mwenyewe.

Gwajima kukosa ushahidi wa kisayansi kwa zile pumba zake ndio sababu ya kuadhibiwa kwake, nothing else.
Nijibu hii korona inayoua sasa hivi ni ile ya kwanza au yapili maana hizo magufuli alitupitisha ,je kovidi ya kwanza bado ipo ? je kovidi ya pili bado ipo? Je kama hazipo zimeenda wapi maana hatukutumia chanjo yoyote kwa hizo kovidi ,sasa unasemaje magu kichwa ngumu
 
Magufuli ameshakufa kijana. Tafuta namna nyingine ya kuishi.

Tanzania kuna chanjo zaidi ya 60..

Kila siku wanawakae na watoto wanapokea chanjo kila iitwapo siku na tena wasipozipata wanalalamika.

TT pekee inatolewa mpaka shots nne na watu wanaipata.

Kampeni ya COVID imekuwa ngumu kwasababu ha athari za akili ya kibwenhmgo Magu alizoacha.

Hata CCM wenyeqe naamini wamejifunza siyo kila mtu anaweza kuwa Rais. Magu was a total disaster.
Mavi haya
 
Mkuu maelezo yako mazuri sana.

Mleta uzi ni masalia ya lile chizi la chato.

Mpaka leo hawaamini kama amekufa na hatorudi milele.
Muulize mama ikulu hatakuambia kuwa kupambana na wapinzani tz ni wepesi sana kuliko kupambana na legacy ya marehemu magufuli ,mother mwenyewe katii
 
Mkuu, wanaoishi usukumani wanajua.

Mchawi akifa ghafla misukule yake na fisi huwa vinasumbua sana wanakijiji hasa usiku, intangatanga sana kwa njaa.

Hiki ndicho kinachotokea kwasasa.
Je na mitume wakifa uwa kitugani cha hao mitume kinabaki kikisumbua waovu ? Sasa magufuli legacy ni legacy ya kitume inafanya kazi zaidi baada ya yeye kufa wewe subiri miaka miwili ijayo utajua hichi ninacho kuambia wabunge na viongozi wote watasujudia LEGACY YA MAGUFULI ILI WASITILIKE
 
Inatumika nguvu nyingi kumlaumu Magufuli kuliko nguvu hizo kuzitumia kushawishi na kuwaaelimisha watu kukubali kuchanjwa, ukiangalia hakuna jitihada yeyote ya maana kwa serikali inayofanya katika kushawishi watu ila watu kutwa wanamlaumu Magufuli tu.
 
Shida kubwa katika suala la chanjo ni kuwa limechukuliwa kiimani zaidi kuliko kisayansi na hivi vitu viwili haviendi sawa.

Kwa sababu jamii ina watu wenye mitazamo tofauti, Serikali ilifanya uamuzi wa busara kuleta chanjo nchini ili anayeihitaji apate asiyeigitaji aache, kuliko kuegemea upande mmoja tu wa wasioihitaji na hivyo kutoileta.

Ni vizuri kuheshimu pande zote mbili, lakini sio sawa kuilaumu Serikali maana imetimiza wajibu wake.

Inashangaza kwa sasa kuona kuwa serikali ambayo ilifanya suala la chanjo kuwa la hiari lakini kwa sasa inachofanya kinaonyesha sio hiari tena!
 
Back
Top Bottom