Baada ya Kifo cha Rais Magufuli: Nani anafaa kuwa Makamu wa Rais Tanzania?
Nchimbi ni mwana-Siasa mzuri lakini Samiah hawezi kukubali kirahisi hasa ukizingatia Lowassa yupo ndani ya nyumba!!! Kufanya hivyo itakuwa ni kama kukaribisha vuguvugu la urais 2025 kabla ya wakati na hivyo kumfanya Samiah atawale kwa shida wakati bila shaka hata mwenyewe (Samia) angependa agombee hiyo 2025!
Kwanini unazungumzia 2025, hujui katiba inasema nini kuhusu muda wa kukaimu nafasi ya Urais??? Hujui kuna uchaguzi kuchagua Rais?? Mama Samia amewekwa kwa mujibu wa sheria inayotaka Raisi awe amepatikana kwa kuchaguliwa!!
 
Mnamkosea mzee heshima hebu at least kwa kuheshimu mwili..na mazuri aliyofanya tungoje walau apumzishwe ndio muanze kukosoa mki-keep in mind hakuna aliyekamilika..ataingia mwingine mtasema...bora Mzee...tuko hapahapa kikubwa uhai tu..ndio wanadamu hao.
 
Magufuli hakuwa mwana-Mtandao! Kutokuwa kwake mwana-Mtandao kumesaidia nini zaidi ya kuleta madhira kwa wananchi?!
Well said, tuache mambo ya huyu sijui mtandao sijui nini, huyo ambaye sio mtandao ndio aliharibu bora ya wanamtandao. Tunataka tutoke hapa tulipo kwenye huu mkwamo, turudishe umoja na utaifa wetu.
 
Nchimbi atafaa sana
He is corrupt!! He is Rostam’s creature!! Angalieni sana influence ya Rostam katika kushawishi ccm nani awe makamu wa Rais! Kundi la Kikwete la mtandao watakuwa mstari wa mbele kutaka kuweka kinyago chao NCHIMBI!!

Hawa wanamtandao ni waporaji wa rasilimali za nchi: msisahau jinsi walivyo ifilisi nchi enzi za Kikwete na sasa watajipanga kurudi!!
 
Magufuli alipendekezwa kamati kuu baada ya hao wana mtandao kulianzisha mara tu jina la mtu wao (Lowasa) kukatwa! Na huyo Nchimbi alishiriki kwenye ule mkwara ulio wasababishia kamati kuamua bora wakise wote!
Na ndo maana nimesema Mama Samia hawezi kumchagua Nchimbi kirahisi na hasa ukizingatia Lowassa yupo ndani ya nyumba kwa sababu anafahamu kwamba watamsumbua! Lakini kwa upande mwingine, nilitaka kuonesha issue sio kuwa Mwanamtandao au hapana kwa sababu hata JPM mwenyewe hakuwa mwanamtandao lakini aliposhika madaraka bado akatengeneza kimtandao chake ambacho ni hatari zaidi kwa afya pengine kuliko mtandao wa akina Nchimbi ambao purely ilikuwa ni political networking na sio huu wa sasa unaofikia hadi kuua watu!!
 
Kumuongoza kwa maana ya guidance

You are still very wrong. VP hatahitaji guidance at all. Guidance ni kushikwa mkono na ni ule ule mtazamo kuwa mwanamke hawezi kufanikiwa bila kushikwa mkono na mwanaume. Usingesema haya kama angekuwa mwanaume. Haujamtendea haki kwenye hili. Anachohitaji kama Rais yeyote ni ushauri ambao umtasaidia kufanya maamuzi.

Amandla....
 
He is corrupt!! He is Rostam’s creature!! Angalieni sana influence ya Rostam katika kushawishi ccm nani awe makamu wa Rais! Kundi la Kikwete la mtandao watakuwa mstari wa mbele kutaka kuweka kinyago chao NCHIMBI!!
Kuna muda tukubaliane kutokukubaliana. Huyu Rostam unayemsema si ndio amerudi kipindi hiki cha JPM kuwa na influence? Sasa shida nini mbona JPM ndio kamsifia zaidi kuliko hata huko kabla. Na alikaribishwa Ikulu na kushirikiana naye mambo mengi. Hebu tuache akili za kijima, angekuwa ni mbaya hivyo JPM angemu endorse? Mbona wakina Manji walikimbi, wakina Seth na Rugemarila je, na wengine.
 
Kamati kuu inakutana tar 20. Mama Samia hana veto yaa kuteua kwa mapenzi yake. CCM ni taasis. Rejea kauli ya Mama Samia mwenyewe ktk maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2021 akielezea jinsi alivopatikana.
 
He is corrupt!! He is Rostam’s creature!! Angalieni sana influence ya Rostam katika kushawishi ccm nani awe makamu wa Rais! Kundi la Kikwete la mtandao watakuwa mstari wa mbele kutaka kuweka kinyago chao NCHIMBI!!

Hawa wanamtandao ni waporaji wa rasilimali za nchi: msisahau jinsi walivyo ifilisi nchi enzi za Kikwete na sasa watajipanga kurudi!!
Kwanza Rostam na J.K walishafall out muda tu, Rostam kaja kurudi hewani kipindi cha JP, he needed him to defeat Membe and kupata support ya team Edo, ndio hata kumpa Msomali uwaziri. Huo ubaya wa Rostam umerudi ghafla baada ya JP kufariki? Tuache akili za kizamani ndio zilifanya tukapata viongozi wa ajabu, tupate mtu anayeweza kututoa hapa tushakwama, tumeshajuta.
 
Huyo mwigulu nchemba hafai

..hata mimi simkubali Mwigulu Nchemba.

..Mwigulu ana siasa fulani za kihuni-huni.

..nimemtaja kwasababu sasa hivi wako wana-ccm wengi wanapenda siasa za kihuni-huni za watu kama Mwigulu Nchemba.
 
You are still very wrong. VP hatahitaji guidance at all. Guidance ni kushikwa mkono na ni ule ule mtazamo kuwa mwanamke hawezi kufanikiwa bila kushikwa mkono na mwanaume. Usingesema haya kama angekuwa mwanaume. Haujamtendea haki kwenye hili. Anachohitaji kama Rais yeyote ni ushauri ambao umtasaidia kufanya maamuzi.

Amandla....
Wanawake wanaweza wakti mwingine kumzdi hata mwanaume. ndiyo maana nilimtaja na Anne Makinda..

Basi nadhani nilikuwa namaanisha "ushauri" kulingana na angle uliyo angalilia
 
Back
Top Bottom