Baada ya kufika Moscow leo nimeamua kufuatilia saga la Dr. Shika, kumbe anasema ukweli

Baada ya kufika Moscow leo nimeamua kufuatilia saga la Dr. Shika, kumbe anasema ukweli

Baada ya kutazama Video zake,na kusoma huzi huu, bado kunaconnection flan kati yake na wamarecan labda walikuwa wanamtumia kupitishia pesa zao au kutoa pesa zao Urusi, walimtilia shaka sana kuona anapesa nyingi hivyoo, aliposema bado nafwatuliwa na Urusi akaongeza shaka sana sana, hakusema pia spain alienda kufanya nini shaka lingine> ukimwangialia kakatwa vidole viwili, vya mkono wa kulia na kimoja Kushoto, haya tunajua na mateso ya kijasusi, mbavu zote mbovu bado ni mateso ya kijasusi, sisemi moja kwa moja jasusi lakini alikuwa anatumiwa kijasusi, kupitishia pesa zao na NK, NA HILI LA KUSAIDIWA NA UBALOZI WA MAREKANI LINAONGEZA SHAKA ZAIDI ALL IN ALL bado TUNA CHA KUJIFUNZA KWAKO PAMOJA NA KUWA ELIMU YA JUU. LABDA PIA KUNA WATU WANA DETIALS ZAKE WANATAKA KUMTUMIA KUFANYE YAO
Kabisa
 
Huyu bwana ana akili timamu, hajarukwa akili kama wengi tulivyoamini.
Kabisa jamaa anajielewa sana sana sema Tatizo la watanzania wanapenda sana maisha ya kuiga....
Jamaa anaishi kwa utaratibu wake...ndivyo "alivyofundishwa" sasa wengine ukiishi hivyo oooh huna hela,kichaa...ila Mzungu akiishi hivyo hawamshangai sisi banaa....
 
Lancefort Ltd ni kampuni iliyosajiliwa nchini Russia miaka kadhaa iliyopita, na kwasasa haifanyi kazi kwa kipindi kirefu baada ya watendaji wake kupotea gafla kwa mazingira ya kutatanisha.

Kutoka mjini Rostov on don napokaa mpaka Moscow ni mwendo mrefu kidogo ambao ni km 1200 na zaidi, kwa mwendo wa trein ni 5hrs,
nimefika mjini moscow na kuanza kuuliza hasa legality ya kampuni hiyo ndani ya moscow na Urusi kwa ujumla, nimefanikiwa kupata maelekezo ya kukutana na Mtanzania mmoja (Elibariki Dishon) anaisha mtaa wa Tverskaya Street, ambaye kanikaribisha na kuanza kufanya uchunguzi wangu, nikaamua kwanza nipate hifadhi ndani ya hotel ya Sputnik.

Baada ya kwenda kwa watanzania wanaoishi huku nimegundua huyu mzee alipata matatizo kwa kuhisiwa ni spy wa Marekani, ambaye kapandikizwa kutokea Afrika, na amekuwa akitafutwa na kufuatiliwa nyendo zake zote kuanzia kwenye kampuni yake na nyumbani alipokuwa anaishi.
Mke wake bi Luisa Kvonkov ndo alibanwa na kueleza kwao ni Tanzania Magu, Lakini inasemekana kwamba kuna kampuni kubwa la kimarekani aidha shirika la upelelezi ambalo liko nyuma ya kampuni ya Lancefort, ndio chanzo cha kutiwa msuko suko uko alikokuwa anamiliki kampuni hiyo.

Shirika la Lancerfort limekuwa likimiliki asset kubwa nchini urusi na kwingineko duniani wakati chanzo cha hela yao hakijulikani, hivyo moja kwa moja kuhisiwa ni miongoni mwa mashirika ma spy ambao wafadhili wake ni wamarekani ambao wana uhasama wa mda mrefu na Urusi.

Wametelekeza mali nyingi kukiwemo na private jets na magari ya thamani.

Kupitia wapelelezi wa ndani ya urusi ambao walilichunguza shirika ambalo inasemekana rais wake ni Dr Luis Shika kwa kipindi kile, waligundua mawasiliano ya karibu na baadhi ya mashirika yafuatayo AMNESTY INTERNATIONAL, CIA, FBI , HGRE, OKLE, ambayo mara nyingi huwa ni waanzilishi wa upelelezi katiKa nchi nyingi,

Baada ya kugundua hayo walitekwa na kuwekwa mateka na wawili kuuwawa, mmoja wapo akiwa mkenya Edward Koinange na mwingine wa Siera Leone Yunusu AKhbu, Na wawili kukimbilia Tanzania lakini Rais wao akapelekwa hospitali baada ya kuwatoroka akiwa ameumizwa vibaya, hakutibiwa Urusi alitoroshwa kinyemela mpaka mjini Dnipro Ukraine, na kutoroshewa Tanzania,
Baada ya kufika Tanzania hakuenda moja kwa moja kwao akajificha mjini Dar es salaam, (Haya ni maelezo kwa mujibu wa mtu wake wa karibu)
Baadae kutorokea Uhispania Mjini Malaga , amekaa malaga miez 8 Na kurudi Tanzania,

Mwaka 2012 wakaidhinisha malipo kutoka marekani ambayo bado yapo kwenye mlolongo wa
kukamilisha mchakato,

WITO KWA BALOZI ZETU TUNAOMBA MUWASAIDIE HAWA WATANZANIA WANAOKUWA NA MATATIZO MUWASAIDIE

Tukiachana na Shika wapo watanzania wengi wanaokosa msaada wa karibu sana kutoka Kwa balozi zetu hizi ,

Ukisoma ukatafakari haitadhuru

Tufanye nimemaliza

KUNA MENGI SITAYAANDIKA HAPA KUTOKANA NA KUJUA KWAMBA KUMBE HII ISHU NI CRUCIAL , NA KULINDA USALAMA WA DR,

PIA YATAENDELEA KUWA KUMBUKUMBU ZANGU NA KUZIPELEKA MAALI ZITAITAJIKA KWA KUMSAIDIA DR,

USIKURUPUKE KUKOPI HABARI HII, MAANA CODES ZOTE NINAZO MIMI UTASHINDWA KUITETEA,MTU PEKEE MWENYE UWEZO WA KUWEKA EVIDENCE NI MIMI, IKITOKEA UKAKOPI SEMA UMEITOA WAPI,

Britanicca

Kwa maelezo haya (ikiwa yana ukweli) umekumbusha jambo moja muhimu sana: ‘Kwa kila jambo kuna majira yake…’

Nimejaribu kwenda mbali zaidi katika tafakuri (hasa kiimani), naamini kabisa kuwa kila jambo linalokutokea hutokea kwa lengo maalumu (haijalishi unajua au hujui).

Jambo ninaloamini kila siku ni kwamba Mungu anatuwazia mawazo ya amani, kutupatia tumaini katika siku zetu za mwisho.

1 Wakorintho 10:13 – “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.”

Inawezekana kabisa ya kwamba wakati huu unapitia majaribu mengi; kwa mfano magonjwa yameiandama familia yako, unazidi kufeli katika masomo yako, biashara yako imekwama kabisa, kukataliwa kila unakokwenda na kila unalofanya (au kama yaliyomtokea Dk. Luis Shika)… bado Mungu anakuwazia mema.

Kwa nini nimeandika ‘Kwa kila jambo kuna majira yake’? Moja ya mambo ambayo Mungu anayaangalia sana ni suala la Wakati, ndiyo maana anasema: “mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.” – Efeso 5:16. Shida inakuja kwetu wanadamu katika suala la kutambua haya majira na kuwa na tahadhari.

Kwa kila jambo, yanayokupata ni majira tu na yanapita. Kila jambo linakuja katika maisha yako kwa lengo maalumu, ikiwemo kukua kiimani zaidi (kwa watu wa imani za kiroho).

Yusufu (mwana wa Yakobo) baada ya kupitia shida mbalimbali kutoka kwa ndugu zake na pia kule utumwani Misri, Mungu alimstarehesha na kumfanya kuwa wa muhimu sana katika taifa la Misri kwa sababu Majira ya kusumbuka kwake yalikuwa yamepita.

Urefu wa majira katika jambo litakalotokea katika maisha yako ni Mungu ndiye ajuaye, lakini mwisho wa jambo hilo upo… unachotakiwa ni kuwa mwenye Imani na Mvumilivu siku zote (kama ilivyokuwa kwa Dk. Shika – kwa mujibu wa jirani zake anaoishi nao).

Kwa kumalizia, imeandikwa katika: Mhubiri 3.1 – “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.”

Ninaamini kabisa kuwa hiki kilichotokea kwa Dk. Luis Shika kuhusu mnada wa nyumba za Lugumi, kukamatwa kwake na hizi habari zinazotolewa, ni jambo ambalo limetokea kwa kuwa kusudi lake limetimia ili Dk. Luis Shika apate haki yake.
 
Mmh kila jambo mnachomeka siasa tu.
Bwana wee sijui watu wamerogwa sijui mungu wangu Nani atawaondoa katika dhiki hii ya fikra. Leo nilikuwa airport exchange rate ya dollar ni kama zamani katika forex bureau lakini hapa JF ni vurulu vululu tu.
 
Wengi ni wazushi tu mitandaoni na ukute wanalipwa kwa kusambaza uongo.
Bwana wee sijui watu wamerogwa sijui mungu wangu Nani atawaondoa katika dhiki hii ya fikra. Leo nilikuwa airport exchange rate ya dollar ni kama zamani katika forex bureau lakini hapa JF ni vurulu vululu tu.
 
Dr shika spy halafu mpaka sasa urusi wawe wamemuacha huru mbona mbona kama ni magushi haya hv ushawahi kufikiri spy when wanamkamata halafu anapotea mbona hata akili ya kitoto kufikiria haiji kichwani sory [emoji120][emoji120][emoji120] kuwa serous bs na huonuzi wako japo tupe uongo wenye ukweli bs!!!! Dr namashaka bdo tena spy daaah acha masihara haya ila umejitahidi kidogo hayo madomo me nayajua ssana na kama ni kweli hakuna spy mjinga na mpuuz kama yeye kutokea duniani na leo anajiweka wazi kabisa hahhahahahah NOT TRUE•••
Mkuu aliokolewa na cia
 
Kwa maelezo ya britanicca ni kuwa hizo nyumba zimenunuliwa na CIA; Yono hili janga utakula na wa kwenu. Sisi hatumo kabisa, ohooo! Dr. Shika sio kighoma malima haya mie nimewambieni!

Kwa maana nyingine hizi ngeu ni kipigo ka cha lissu kutoka KGB sio?
 
Back
Top Bottom