Baada ya kumsafirisha mke najisikia amani, furaha na wepesi wa kutosha. Ndoa inahitaji umakini usiomithilika

Baada ya kumsafirisha mke najisikia amani, furaha na wepesi wa kutosha. Ndoa inahitaji umakini usiomithilika

WhoWeBe

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2022
Posts
2,299
Reaction score
4,282
Umuofia kwenu!!

Kama mada ilivyo, nimempeleka kwanza kwao kwa muda usiopungua miezi miwili.....akajifunze kitu (kama ni mwenye kujifunza). Siku moja tu baada ya kutoka kwake;

1. Leo kwa mara ya kwanza, katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu, nimefanikiwa kutulia nyumbani saa mbili usiku na kuangalia taarifa ya habari mwanzo mwisho. Kabla, ilikuwa sikai maana nikibadilisha channel tu na kuweka kituo changu pendwa cha Star TV kuangalia taarifa basi manung'uniko yenye kukera huanza kukimbizana kutoka nje ya kinywa chake.

"Tutaacha vp kubadilishiwa channel wakati TV sio yetu na hata bei yake hatuijui..."

"Hata kuzima we zima tu, nini kubalisha channel" Dah

2. Nimepumzika kushuhudia mabega na makwapa ya mke wangu yakionwa na watoto muda wote awapo nyumbani. Jitihada za kumrekebisha ili aendane na desturi yangu, daima huenda sambamba na ugomvi.

3. Nimepumzika kuona sura ya kununanuna pale ninapotoa maelekezo.

4. Udokozi wa vielfu tano tano vyangu katika tigopesa yangu utakoma kwa muda.

5. Nitapumzika kusikia matusi kama 'nyoko we' n.k yanayotolewa kwa watoto kila siku.

6. Nitafurahia vichenji vinavyobaki katika matumizi madogomadogo na kuziweka mezani. Kwa kawaida hivi hutoweka dakika moja tu baaada ya kuviweka, hata kama akiwa amelala basi huamka ghafla na kuvichukua kisha kulala tena.

Mbona nina furaha sana sasa?!!! Atarudi kweli? Arudi ili nije kupata stress tena?

Ndoa..........mh!
 
Nitafurahia vichenji vinavyobaki katika matumizi madogomadogo na kuziweka mezani. Kwa kawaida hivi hutoweka dakika moja tu baaada ya kuviweka, hata kama akiwa amelala basi huamka ghafla na kuvichukua kisha kulala tena.[emoji3064][emoji3064][emoji3064]

Tabia zilizojificha: Chanzo cha migogoro kwenye mahusiano Tabia zilizojificha: Chanzo cha migogoro kwenye mahusiano

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe umeoa gube gube. Huyo hata umuweke kwao miaka 10 hatoacha tabia yake.

Usitarajie mabadiliko yeyote toka nyumbani kwao maana huko ndipo penye chimbuko la tabia zake mbovu. Cha zaidi tarajia kuongezeka kwa tabia mbaya akirudi maana sasa yupo mafunzoni.
 
Kama ana tabia ya kukwapua vijichenji vyako sidhani kama atakuja kuacha, hiyo ndio tabia yake inaonekana halafu anaonekana ni mtu ambae hana malezi bora kabisa, itachukua miaka mingi sana mpaka aje abadilike.
 
Wanawake wana mambo sana, kuna siku kwenye daladala mama mmoja akapiga simu alikuwa anaongea na house girl nadhani, akamuuliza baba kakupata sh ngapi ya matumizi....akaendelea basi sawa tumia elfu saba tu hyo elfu tatu weka pale tunapowekaga. Nilichoka na kuchoka mke anashirikiana na house girl kula ganchi kwa mumewe.
 
Acha pesa kidogo kwenye suluari Kama elfu 20 hivi.

Jifanye huna habari nazo kabisa.
Usiwe siriaz stori zako ziwe za furaha furaha tu.

Hapo utapata habari za nguo kufuliwa vizuri na kupigwa pasi iliyonyooka sana.
 
Wanawake wana mambo sana, kuna siku kwenye daladala mama mmoja akapiga simu alikuwa anaongea na house girl nadhani, akamuuliza baba kakupata sh ngapi ya matumizi....akaendelea basi sawa tumia elfu saba tu hyo elfu tatu weka pale tunapowekaga. Nilichoka na kuchoka mke anashirikiana na house girl kula ganchi kwa mumewe.
Mkuu hiyo yote ni umasikini wa kipato kwa wanawake wake wetu, chanzo chake kutoka kwenye familia yao huko, Yani ata mumewe awe na uchumi wa kati bado mke angemuibia tu.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Umuofia kwenu!!

Kama mada ilivyo, nimempeleka kwanza kwao kwa muda usiopungua miezi miwili.....akajifunze kitu (kama ni mwenye kujifunza). Siku moja tu baada ya kutoka kwake;........

1. Leo kwa mara ya kwanza, katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu, nimefanikiwa kutulia nyumbani saa mbili usiku na kuangalia taarifa ya habari mwanzo mwisho. Kabla, ilikuwa sikai maana nikibadilisha channel tu na kuweka kituo changu pendwa cha StarTv kuangalia taarifa basi manung'uniko yenye kukera huanza kukimbizana kutoka nje ya kinywa chake.......
"Tutaacha vp kubadilishiwa channel wakati TV sio yetu na hata bei yake hatuijui..."
"Hata kuzima we zima tu, nini kubalisha channel" Dah

2. Nimepumzika kushuhudia mabegi na makwapa ya mke wangu yakionwa na watoto muda wote awapo nyumbani. Jitihada za kumrekebisha ili aendane na desturi yangu, daima huenda sambamba na ugomvi....

3. Nimepumzika kuona sura ya kununanuna pale ninapotoa maelekezo....

4. Udokozi wa vielfu tano tano vyangu katika tigopesa yangu utakoma kwa muda....

5. Nitapumzika kusikia matusi kama 'nyoko we' n.k yanayotolewa kwa watoto kila siku....

6. Nitafurahia vichenji vinavyobaki katika matumizi madogomadogo na kuziweka mezani. Kwa kawaida hivi hutoweka dakika moja tu baaada ya kuviweka.....hata kama akiwa amelala basi huamka ghafla na kuvichukua kisha kulala tena.

Mbona nina furaha sana sasa?!!! Atarudi kweli?!!!!! Arudi ili nije kupata stress tena?!!!!!!!

Ndoa..........mh!
Bado mna utoto.Mmeoana mwaka mmoja tu ndiyo unaweweseka?Mkwe bado haujakua.
 
Udokozi wa vielfu tano tano vyangu katika tigopesa yangu utakoma kwa muda....[emoji3064][emoji3064][emoji3064]

Sent using Jamii Forums mobile app
ubahili ndiyo unaomsumbua huyu. Hiyo tigopesa anapata vipi fedha kama hakumpa password mwenyewe?

Hayo ya watoto kutoa matusi alitakiwa na yeye awe na msimamo asiruhusu hivyo vitu.
 
Back
Top Bottom