Baada ya kumsafirisha mke najisikia amani, furaha na wepesi wa kutosha. Ndoa inahitaji umakini usiomithilika

Ndoa ni taasisi inayohitaji uvumilivu na ustahimilivu ili uweze kuifurahia na kuishi humo.........

Ukiondoa changamoto za kiudhaifu wa kibinadamu lakini upendo unafunika mapungufu mengi kwa wanandoa na kuifanya iwe ni taasisi imara na yenye kupendeza.......

Kwa jinsi ulivyo tanabaisha ni dhahiri huyo mkeo ana changamoto ya malezi huko kwao ingawaje ni ngumu kuamua kesi ya upande mmoja..........

Siri ya mtungi aijuaye kata........
 
Umuofia kwenu!!

Kama mada ilivyo, nimempeleka kwanza kwao kwa muda usiopungua miezi miwili.....akajifunze kitu (kama ni mwenye kujifunza). Siku moja tu baada ya kutoka kwake;........

sina details sn ila nahisi unambana sana waifu wako, kiasi anakosa visenti vya matumizi yake madogomadogo (hadi akuibie). hiyo sio poa, maana mwingine akianza kumpa, ndio itakuwa tamati ya hiyo ndoa.

hayo ya kuangalia tv, ni madogo, huna haja ya kushindana nao, ww una options nyingi. wape space, na hizo ndo sacrifice za ndoa.

hayo mengine ya kurudisha mke kwao ndo nayaskia leo, hivi bado yapo miaka hii? ili kitokee nini? na je akipata sweet baby mwingine huko? utarudi hapa kufungua uzi mwingine au utaendeleza huu?
 
Kiongozi bora angebaki tu nyumbani na utumie njia nyingine kumrekebisha.
Huko ulikompeleka ndipo alipokulia na akawa hivyo alivyo. Hapo umeenda tu kumuongezea maujuzi na kumkutanisha na vibwana vyake vya kitaa.
Hapo umeongeza tatizo lingine Atarudi papuchi imechakaa
 
Duh!....huyo mke ulimchagua wewe au uliletewa tu ukaoa ?
 
Tunashauriwa kuweka akiba , sio kupewa hela yote na kuitumia yote bila kubakiza hata senti.
Kama 7000 inatosha kwa chakula ni sahihi alivyofanya. Sasa inategemea hiyo 3000 inaenda kwenye matumizi gani.

Huyo mke ana akili.
 
Na ukiona mke anadokoa visenti vidogo ujue humpi pesa kwaajili ya matumizi yake binafsi.
Next time nunua Tv mbili moja weka chumbani uwe unapumzika huko bila bugudha. Tv ya sebuleni waachie mke na watoto. Ila mke wako ana mdomo nadhani hicho ndo ulimpendea tangu mwanzo.

Wengine tunatamani kupewa likizo hata ya siku mbili twende kwetu hatupewi .
 
Hivi nyie mnafikiri kila mtu ana uwezo wa kua na TV mbili nyumbani, kweli watu wengine ana chumba na sebule hizo kelele za tv mbili utaweza kuzimudu ulipie vinga'mzi viwili, unakipato cha kutosha mpaka kumpa mwanamke pesa zaidi, ninacho fahamu zaidi ya 80% ya wanaumme kipata chao ni hand to mouth economy.........mwanamke mdokozi hata umpe shilling ngapi atadokoa tu.
 
Hivyo visenti anavyolalamika kuibiwa anao uwezo wa Tv mbili. Anaonekana anazo
 
Uweke Tv mbili kwenye chumba na sebule kweli? Hivyo vijisenti vya shilling 300, 700, 150 ndo vinunue TV kweli?
Basi atulie asilalamike. Nimemfungua tu mawazo inawezekana uwezo wa kununua Tv mbili anao lkn hakuwahi kufikiria hilo.

Inawezekana ni kati ya wale wababa wabinafsi ambao akiwepo nyumbani wengine hawaangalii TV ni yeye tu anajipendelea.

ni sawa mke ana mdomo lakini ukute anaongea kitu cha kweli.
 
Omba katika ndoa usije ukapata mwanamke mwenye gubu na mchafu wa mwili na mazingira utasalimu amri tu.........ndoa isikie kwa wezio omba yasikukute.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…