Baada ya kupewa Talaka, Wastara Sasa Hali Mbaya

Baada ya kupewa Talaka, Wastara Sasa Hali Mbaya

Wastara km anataka aheshimike aachane kwanza na hawa wanaume. Ajenge maisha yake mwenyewe. Kuwa na msururu wa list ya wanaume SIYO sifa nzuri.
Sijui tuseme ni fasheni au ni tamaa ya maisha mazuri na pesa? Jamii inakuheshim sana dadaang lakin kwa hii tabia yako inakufanya uonekane jamvi la wageni. Simama kidete jenga maisha yako; hawa wanatosha:

1. Solo Thang
2.Ahmed Kush
3.Sajuki
4.Bond
5.Sadifa
6.Na wengine ambao hta hawajulikani
Mbona wachache sana hao?
Kuna watu wanajaza behewa hata 5 na inakuwa ndio baaadoooo asubuhi kabisaaa
 
Baada ya kupewa talaka kufuatia madai ya kuvunjika kwa ndoa yake na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Donge, Zanzibar, Sadifa Khamis Juma kisha kuzimia na kulazwa hospitalini kwa mshtuko, hali ya kiafya ya staa wa Bongo Muvi, Wastara Juma sasa inadaiwa kuzidi kuwa mbaya.

WASTARA-3.jpg


Akielezea hali ya Wastara, babu wa Wastara aliyelazwa Hospitali ya Misheni ya St. Herry Heath Centre mkoani Morogoro, Abdulaziz Babu ambaye naye ni msanii maarufu wa filamu mkoani hapa alikuwa na haya ya kusema:
“Tangu aolewe na huyo Sadifa, ndoa yake imekuwa na migogoro mingi. Majuzi Wastara aliamua kuachana na mheshimiwa huyo kisha akabeba vitu vyake na kuja kwangu hapa Morogoro.

“Aliamua kuja kwangu kupumzisha akili yake. Chanzo cha mjukuu wangu kuugua ni huyo mheshimiwa aliyekuwa anaposti kashfa kwenye mitandao ya kijamii dhidi ya mjukuu wangu.
“Baada ya kuona hizo kashfa ndipo mjukuu wangu akapatwa na presha na kisukari kisha akapoteza fahamu.

“Niliamua kumkimbiza hapa hospitalini na hali yake ni mbaya kama unavyomuona. Kikweli hali hii inasikitisha na inaniumiza sana lakini najua Mungu anampigania.”
Alipoulizwa kama Wastara akipona na kuweka mambo sawa na Sadifa atarudi kwenye ndoa yake, babu huyo alijibu kwa jazba:
“Hatuko tayari mtoto wetu kuendelea kupata manyanyaso kama aliyokutananayo kwa kipindi kifupi kutoka kwa huyo mwanaume.
“Kwanza Wastara mwenyewe anajuta na ameapa kutorudi tena kwa Sadifa.”

Maneno ya Sadifa:

“Wastara ni mlemavu, hana baba wala mama halafu leo hii aniseme vibaya?”
Alisema kuwa hadi akaamua kumuoa ni kwamba alimpenda hivyo anashangaa kwa nini amseme hivyo.
Wastara amepitia katika uhusiano na ndoa kwa wanaume kadhaa. Awali alizaa na Mwanamuziki wa Kizazi Kipya, Msafiri Kombo ‘Solo Thang’.

Mwaka 2000, alifunga ndoa na Ahmed Kushi kutoka Zanzibar na kuzaa naye mtoto mmoja aitwaye Fares. Baadaye alifunga ndoa na msanii mwenzake, Juma Kilowoko ‘Sajuki’ ambaye kwa sasa ni marehemu na alizaa naye mtoto mmoja aitwaye Farheem kabla ya kufunga ndoa na Sadifa alikuwa katika uhusiano wa kimapenzi na Bond Bin Suleiman.
wizara ya afya lifanyienii kazi hili jambo hasa hasa hii hospitali kanuni na sheria za medicine haziruhusu mgonjwa kupigwa picha na kuanika katika mitandao ya kijamii katika MEDICAL ETHICS yale utakayo yaona ama kuyasikia wakati wa kumhudumia mgonjwa ni siri kati yake na yeyee.. Hii hospitali imekosa maadilii kwa nini wameruhusu upigwaji wa picha kwa mgonjwa na kuanikwa katika mitandao ya kijamii huu ni udharilishaji..serikali ilitizame hili japo .....#HYPOCRATES OATH
 
Hao ndiyo mabinti wa mijini,ushauri kwa vijana kaoe kijijini mtoto aliyelelewa anayeogopa talaka
Mdau,kijiji gani?acha tu usiseme,Mke mwema namna ya kumpata ni kumuomba Allah.
Mjini mbona wapo wenye ethics zao
 
Wabunge wa Tanzania bhana, kutwa kusutana na kinamama huko Instagram lakini wakifika mjengoni kila kitu ndio ndio.
Ha ha haaa,sema wewe.
Nimeona zile comments aisee ni shida kabisa,ukiwaita hapa JF wanang'aa sharubu tu
 
Wastara km anataka aheshimike aachane kwanza na hawa wanaume. Ajenge maisha yake mwenyewe. Kuwa na msururu wa list ya wanaume SIYO sifa nzuri.
Sijui tuseme ni fasheni au ni tamaa ya maisha mazuri na pesa? Jamii inakuheshim sana dadaang lakin kwa hii tabia yako inakufanya uonekane jamvi la wageni. Simama kidete jenga maisha yako; hawa wanatosha:

1. Solo Thang
2.Ahmed Kush
3.Sajuki
4.Bond
5.Sadifa
6.Na wengine ambao hta hawajulikani
Ayajengeje sasa.mdau mpaka hapo anachohitaj ni kuwa kwenye ndoa ndo stara ya mwanadam hyo
 
Huenda wastara alikua anachambwa na mke mwenzie kwa kutumia account ya mme wao , teh hizi ndoa za wake wengi nazo shughuli
Maana nikiposkia anaolewa na nikasoma hapa jamaa ana wake wengine,nilijua hii ndoa haitamove.Halafu pia wastara ni Mtanganyika,jamaa na wakeze ni wapemba (wazenj).Jambo pekee hapo ni kupigania afya yale tu atengemae si kingine,nimeona Riyama Ali (MbongoMuvi) amemchamba huyo jamaa kweli
 
Alisema yy na mke mwenza ni shega tuu hata mwezi haujapita dhambi ya kushabikia ccm ni mbaya sana na iwatafune tuuu kwa maaana hakuna namna bana
 
Mkuu tukirejea kuleeee kwenye ulimwengu wa roho, huyu dada na mwenzie lulu watakuwa na tatizo gani?
Malaika wa kuzimu kwa mtazamo wangu ...kama ni coincidence kwa yale aliyopitia nitakuja kuomba radhi lakini kwasasa huo ndio mtazamo wangu

Sent from my SM-N910X using JamiiForums mobile app
 
Malaika wa kuzimu kwa mtazamo wangu ...kama ni coincidence kwa yale aliyopitia nitakuja kuomba radhi lakini kwasasa huo ndio mtazamo wangu

Sent from my SM-N910X using JamiiForums mobile app

jini mahaba anahusika hapa.
Mkuu fanya mpango wakuleta mada ya kumuelezea huyu jini. Anatesa sana ndoa za watu.
 
Back
Top Bottom