LGE2024 Baada ya kupuuza Ule msemo wa jinsi ya kula na kipofu, Leo wanatafutwa wananchi wa kujiandikisha Kwa tochi ili kura ziibwe!

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Serikali hii ni ya kipuuuzi sana! Mpk kwenye misiba mtu anakurupuka huko anatoa tangazo la kuhamasisha watu kujiandikisha! Pumbavu sana!
imekuwa ndio mtindo kutumia misiba kutoa matamko na matangazo ya serikali huko, tusishangae hata kwenye harusi na sherehe zingine huko zikatumika kama jukwaa la kunadi mambo ya kisiasa
 
Serikali hii ni ya kipuuuzi sana! Mpk kwenye misiba mtu anakurupuka huko anatoa tangazo la kuhamasisha watu kujiandikisha! Pumbavu sana!
siku hizi misiba ndio jukwaa la kupenyeza ajenda za serikali huko. Ni jukwaa la bwerere, unakuta viongozi wa serikali na chama wanatumia mikusanyiko ya misiba kufanya propaganda zao.
 
Juzi kulikuwa na msiba mtaani. kwa bahati mwili wa marehemu ulisafirshwa tukabaki baadhi ya watu kama ilivyo desturi yetu.
mwekiti wa mtaa akajiroga akasema vijana mbona hamjiandikishi?
siku zote nilijua ni mimi tu au tupo wachache sana ambao hatuna muda wa kujiandikisha kumbe vijana karibia wote
hawana mpango wa kujiandikisha.

Aliulizwa maswali yaani bado hajajibu kazomewa na aliambiwa tusikuone kabisa umegombea huu mtaa na ukipita hutaacha kuona kila rangi yetu!

Mimi kwa unyenyekevu nikamuuliza ndg mwenyekiti tangu tukuchague umetufanyia nini maana hata bara bara za mitaa gari hazipiti kipindi kwa sababu ya makorongo na hii ndo ilikuwa ahadi yako ya kuhakikisha bara bara za mtaa zinachimbwa na kuwekwe mifereji ya maji?

Alitamani alie halafu akaniuliza swali badala ya jibu Wewe hujaona nilicho fanya kweli? aisee wanatia huruma sana
kwa sasa baada ya swali hilo alizomewa mno ni aibu tupu
 
Naona unajichekesha. Msipojiandikisha si ndio CCM itashinda kiulaini? Kwanini? Kwasababu wana mtandao wa wanachama hadi ngazi ya balozi. Wakipewa maelekezo wote wataebda kujiandikisha. Wapinzani ndio watakosa wapiga kura. Hivyo bora tu mjitokeze kujiandikisha na kupiga kura.
 
Sisi wananchi sio wajinga.

Walisema wataiba, watatuteka na hata kutuua ikibidi mwisho wa siku wanasema Mungu nisamehe Maisha yanaendelea.
 
Huu uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu unatoa picha ya ajabu ya uchaguzi mkuu ujao mwakani. Kama huu unasuasua, wa mwakani ndio utasuasua zaidi kwani wananchi hawahamasiki kupiga kura ikiwa tayari wanajua nani atakua kiongozi. Wananchi wanaona ni kujisumbua tu kwenda kupiga kura wakati fulani atashinda kwa mbinu zozote hata kama hatapata kura za kutosha
 
Sasa mbona wewe usijiandikishe na kuamua kugombea ili umpige chini? Unajua fikra zingine za wabongo ni mbaya. Kama mnataka mabadiliko ya uongozi mshiriki kwenye michakato ya kidemokrasia!
 
Mnaharibu nchi
 
Sasa mbona wewe usijiandikishe na kuamua kugombea ili umpige chini? Unajua fikra zingine za wabongo ni mbaya. Kama mnataka mabadiliko ya uongozi mshiriki kwenye michakato ya kidemokrasia!
Mkuu kama unavyojiona una akili timamu vivyo hivo nani najiona nina akili timamu.
kwanza kutokujiandikisha ama kupiga kura ni hiari sio lazima.

Nikiwa na akili zangu timamu siwezi enda kujiandikisha wala kupiga kura. huku natambua wazi kabisa ccm
wanaiba kura na Nape amekuwa akisema dhahiri kuwa ushindi wa ccm hautegemei kilichomo ndani ya sanduku
bali hutegemea na anayetangaza matokeo hayo. Nikienda kupiga kura nikateni kichwa

Kuhusu kugombea ni yaleyale maana ccm wanakuwa na mtu wao tiyari na hivyo kuwafanya wananchi ni wajinga
 
Ole wenu nikute jina langu kwenu!!
 
Wameamua kuwaangushia jumba bovu viongozi wao wanaomaliza muda wao kuwa ndiyo wanaovuruga zoezi la uandikishaji wapiga kura wakati ni wao wenyewe walioratibu uhuni huu ili kuficha aibu ya watu kususia kujiandikisha.
 

Attachments

  • CCM.jpeg
    237.7 KB · Views: 3
Mpumbavu wewe!
 
Mimi nimeshuhudia Balozi akihamasisha watu kujiandikisha kwenye msiba wa Mwanangu.Hali ni mbaya sana,Wananchi wamegoma.
Ushauri wa Bure,CCM wajipigie wenyewe kura maana si huwa wanasema ata tusipopiga kura CCM lazima itangazwe mshindi!🤣🤣🤣🤣
 
Ole wenu nikute jina langu kwenu!!
Kuna katibu wa chama mtaani kwetu kachukua majina ya watu wazima wote nyumbani (sikuwepo) sijajua anamaanisha nini ingawa anajua tuliojiandikisha na ambao bado.
Jamaa wamejipanga, wanajua kila kaya waliojiandikisha na ambao bado. Na watakaowapigia kura. Wanapata ushindi kwa forecast kwanza kabla ya siku ya kupoga kura.
 
Hata wakijiandikisha watu buku tu, wanaitosha CCM kuibuka kidedea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…