Baada ya mashambulizi: Tumerejea hewani, Tupo imara zaidi!

Baada ya mashambulizi: Tumerejea hewani, Tupo imara zaidi!

Status
Not open for further replies.
Mimi sometimes naona wanasema 'redirected'
huku JF sipati...
 
Hongereni sana maana jana Jpili ys oct 25 ,2015 mlipata kwikwi sana mpaka
nikaanza kupata wasi wasi kama mko salama.
Hongereni kwa kuonesha werevu wenu katika masuala ya
teknologia hasa wakati wa vipindi vyenye changamoto kama hivi.
Kudos Melo et al.....
 
Mimi sometimes naona wanasema 'redirected'
huku JF sipati...

Hata mimi ina nipa ka ujumbe hako kila ni log-in
sasa sijui uongozi wa JF unatuambiaje.
maana tusijie kuwa IP adress zetu zinapitia kwanza kule
alikosema mbatia ...still skeptic on this alert.
 
@Maxence unadhani lengo la DDoS lilikuwa nini? Kuzuia JF kutangaza matokeo huru ya uchaguzi au kuna lingine?
 
Wakuu salama?
Kumekuwepo na wimbi la watu kupotea kisha kupatikana hai au wakiwa wamekufa. Pia kuna wengine wamepotea na hawajaonekana mpaka sasa. Matukio yote yamekuwa yakiitwa "Kutekwa na watu wasiojulikana".
Kinachoshangaza ni kuona wanaorudi baada ya kupotea wakikaa kimya kama hakuna kilichowatokea. Mfano mzuri ni tukio la kutekwa JamiiForums siku ya Uchaguzi Mkuu 2015.
Kwa kuwa vijana wengi tulikuwa bado sekondari, naomba kujua kama JamiiForums waliita press conference kuelezea watekaji wao walikuwa wanataka nini.
Ufafanuzi huo utatupa mwanga sisi vijana kwa sababu wengi wetu tunaamini watekwaji wa mwanzo walikuwa ni JamiiForums Where We "dare" to talk Openly.
 
Wakuu salama?
Kumekuwepo na wimbi la watu kupotea kisha kupatikana hai au wakiwa wamekufa. Pia kuna wengine wamepotea na hawajaonekana mpaka sasa. Matukio yote yamekuwa yakiitwa "Kutekwa na watu wasiojulikana".
Kinachoshangaza ni kuona wanaorudi baada ya kupotea wakikaa kimya kama hakuna kilichowatokea. Mfano mzuri ni tukio la kutekwa JamiiForums siku ya Uchaguzi Mkuu 2015.
Kwa kuwa vijana wengi tulikuwa bado sekondari, naomba kujua kama JamiiForums waliita press conference kuelezea watekaji wao walikuwa wanataka nini.
Ufafanuzi huo utatupa mwanga sisi vijana kwa sababu wengi wetu tunaamini watekwaji wa mwanzo walikuwa ni JamiiForums Where We "dare" to talk Openly.
Kijana huna kazi yakufanya?
 
Mkuu unadhani jf hawakutoa ufafanuzi wa kilichotekea? Pole, tafuta nyuzi zipo na ufafanuzi ulishatolewa😱
 
JamiiForums Message
Tumerejea: Tupo imara zaidi!

Wakuu,
Tunafarijika kuwafahamisha kuwa tumerejea hewani baada ya kupata mashambulizi ya makusudi yenye kulenga kuzuia upatikanaji wa huduma kwa watumiaji wa JamiiForums (DDOS Attack) kwa takribani masaa 7, kuanzia saa 7 mchana hadi saa 2 usiku.

Mashambulizi haya yaliyolenga kuidhoofisha miundombinu yetu, yamefanywa kwa kupangwa na kwa kiwango tulichobaini kuwa yalifanywa na wataalamu waliobobea katika masuala ya mashambulizi ya kimtandao.

Tunalaani kwa nguvu zetu zote kitendo hiki na vingine vya mwelekeo kama huu vyenye kulenga kunyamazisha sauti za wananchi.

Timu yetu ya wataalamu itaendelea kufanya kazi kwa umakini zaidi katika kipindi hiki cha Uchaguzi na tunaomba ushirikiano wa wanachama na wadau wa JamiiForums pale mtakapoona huduma zetu zinasuasua kwa namna yoyote ile katika upatikanaji. Wasiliana nasi kupitia support@jamiiforums.com

Tunawashukuru sana kwa uvumilivu wenu katika kipindi hiki na tunawatakia kila la heri katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu.

Uongozi,
JamiiForums
 
JamiiForums Message
Tumerejea: Tupo imara zaidi!

Wakuu,
Tunafarijika kuwafahamisha kuwa tumerejea hewani baada ya kupata mashambulizi ya makusudi yenye kulenga kuzuia upatikanaji wa huduma kwa watumiaji wa JamiiForums (DDOS Attack) kwa takribani masaa 7, kuanzia saa 7 mchana hadi saa 2 usiku.

Mashambulizi haya yaliyolenga kuidhoofisha miundombinu yetu, yamefanywa kwa kupangwa na kwa kiwango tulichobaini kuwa yalifanywa na wataalamu waliobobea katika masuala ya mashambulizi ya kimtandao.

Tunalaani kwa nguvu zetu zote kitendo hiki na vingine vya mwelekeo kama huu vyenye kulenga kunyamazisha sauti za wananchi.

Timu yetu ya wataalamu itaendelea kufanya kazi kwa umakini zaidi katika kipindi hiki cha Uchaguzi na tunaomba ushirikiano wa wanachama na wadau wa JamiiForums pale mtakapoona huduma zetu zinasuasua kwa namna yoyote ile katika upatikanaji. Wasiliana nasi kupitia support@jamiiforums.com

Tunawashukuru sana kwa uvumilivu wenu katika kipindi hiki na tunawatakia kila la heri katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu.

Uongozi,
JamiiForums
Wote waliofanya haya.

Watakuwa sisiemu hao.

Kazi hawatupi.

Tukijiajiri wanaleta mgambo.

Tukilima walanguzi wanashusha bei mazao.

Yaani Tarafani.
 
JamiiForums Message
Tumerejea: Tupo imara zaidi!

Wakuu,
Tunafarijika kuwafahamisha kuwa tumerejea hewani baada ya kupata mashambulizi ya makusudi yenye kulenga kuzuia upatikanaji wa huduma kwa watumiaji wa JamiiForums (DDOS Attack) kwa takribani masaa 7, kuanzia saa 7 mchana hadi saa 2 usiku.

Mashambulizi haya yaliyolenga kuidhoofisha miundombinu yetu, yamefanywa kwa kupangwa na kwa kiwango tulichobaini kuwa yalifanywa na wataalamu waliobobea katika masuala ya mashambulizi ya kimtandao.

Tunalaani kwa nguvu zetu zote kitendo hiki na vingine vya mwelekeo kama huu vyenye kulenga kunyamazisha sauti za wananchi.

Timu yetu ya wataalamu itaendelea kufanya kazi kwa umakini zaidi katika kipindi hiki cha Uchaguzi na tunaomba ushirikiano wa wanachama na wadau wa JamiiForums pale mtakapoona huduma zetu zinasuasua kwa namna yoyote ile katika upatikanaji. Wasiliana nasi kupitia support@jamiiforums.com

Tunawashukuru sana kwa uvumilivu wenu katika kipindi hiki na tunawatakia kila la heri katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu.

Uongozi,
JamiiForums
Nakumbuka kile kipindi nadhani lile ndio mojawapo ya mashambulizi mabaya zaidi kuwahi kuikumba JF
 
Na bado ikarudiwa kwa namna ile ile mwaka 2020 siku 7 bila huduma ya internet mpaka utumie Virtual Private Network. Huku mtandao wa Twitter ukiendelea kutopatikana bila hiyo (VPN) kwa zaidi ya miezi mitatu

Haya lazima yawekwe katika kumbukumbu ili kuepusha upotoshaji maana kuna watawala walidhamiria kuzima uhuru wa habari na kutaka nchi iwe ya "one say".
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom