Baada ya miaka 39, Taifa Stars yafuzu kucheza michuano ya AFCON 2019 baada ya uicharaza Uganda goli 3-0, Uwanja wa Taifa-Dar

Baada ya miaka 39, Taifa Stars yafuzu kucheza michuano ya AFCON 2019 baada ya uicharaza Uganda goli 3-0, Uwanja wa Taifa-Dar

Mpo baa gani wadau
IMG-20190324-WA0038.jpeg


Sent using Unknown device
 
ametoa ule mpira upande wa mashariki akapiga locomotive bent bila kusimama ya kwanza alipiga inaitwa reo bent anayumba akiwa amesimama beki akakubali kutoka kwenye njia akaamua kuondoka akajabeki wa pili akapiga locomotive bent huku anaenda kama anataka kupiga back pass akageuka, quick turn "tunaita" quick reflect akapiga mpira mmoja lion pass "stand volley" mpira unaofanana kama chini unapofungia tai hapa basi kilichotokea kwa Aggrey Morris kwenda deep kwenye box akapiga side freak head kwenye paji la uso sio kisogoni sio usoni ngoma ikaenda nyavuni kushoto kwake ambapo ni kulia kwa goalkeeper Dennis Onyango hakuwa chap mpira ulienda taratibu sana lakini vipimo viwango na utulivu wa wa Agrrey Morris overlapping central back.

kwako Jesse John
 
WOW! 39 years? That’s a long time ago Mkuu.

Timu ya Taifa ya Tanzania(Taifa Stars) leo majira ya saa 12:00 jioni katika Uwanja wa Taifa uliopo jijini Dar inacheza na timu ya Taifa ya Uganda(The Cranes) katika mchezo wa kufuzu kucheza Michuano ya Mataifa ya Afrika(AFCON) nchini Misri

Lesotho yenye alama sawa na Tanzania itakuwa ugenini inamenyana na Cape Verde.

Msimamo wa Kundi ulivyo kabla ya Mechi za mwisho leo

Taifa Stars ili kufuzu AFCON pia inategemea na matokeo ya Lesotho ambapo iwapo Lesotho. Taifa Stars itafuzu iwapo itashinda dhidi ya Uganda na Lesotho atoke droo au afungwe na Cape Verde

Lakini iwapo Taifa Stars na Lesotho zote zitashinda badi Stars inabidi ishinde magoli mengi na kukaa juu ya Lesotho kwenye msimamo wa kundi kwa tofauti ya magoli ya kufungwa na kufunga

UPDATES:
Mashabiki wamevunja geti upande uwanja wa Uhuru na NBSP kuingia kwa nguvu kwenye Uwanja wa Taifa kushuhudia mechi ya Taifa Stars na Uganda.

Nguvu ya mashabiki imewashinda polisi na walinzi wengine na kulivunja geti hilo saa 10.33 jioni hali iliyowalazimu polisi kujipanga upya kuzuia hali hilo.

Katika kipindi cha takribani dakika tano kabla ya polisi kuzuia mashabiki wengi tayari walikuwa wameingia na kwenda moja kwa moja jukwaani
***

View attachment 1053045
Mashabiki kutoka sehemu mbalimbali awanaendelea kuingia uwanja
***

Polisi imewatawanya kwa mabomu ya machozi mashabiki waliotaka kuingia uwanjani kwa kupitia uwanja wa Uhuru katika mechi ya Taifa Stars na Uganda, kutokana na msongamano uliopo kwenye mageti ya Uwanja wa Taifa
***

Vikosi vinavyoanza mchezo wa leo



***

Taifa Stars inapata goli la kuongoza dhidi ya Uganda goli lililofungwa dakika ya 21 na Saimon Msuva. Msuva alipokea pasi safi kutoka kwa John Bocco 'Adebayor'

Aidha, katika mchezo mwingine matokeo katika mchezo wa Lesotho na Cape Verde bado ni 0-0
***

MAPUMZIKO: Taifa Stairs inaenda mapumziko ikiwa inaogoza kwa goli 1-0 dhidi ya Uganda. Katika mchezo wa Lesotho na Cape Verde milango bado ni migumu

Stats zilivyo hadi Mapumziko
***


Taifa Stars inapata bao la pili kwa mkwaju wa penati kupitia kwa Erasto Nyoni baada ya beki wa Uganda kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari dakika ya 51.

***

Goli la tatu kwa Tanzania kutoka kwa beki Aggrey Morris akimalizia kwa kichwa pasi ya John Bocco dakika ya 57

***

Stats baada ya mchezo kumalizika leo Machi 24, 2019

Baada ya matokeo ya leo, Tanzania na Uganda zinafuzu ambapo Uganda inaongoza kundi ikiwa na alama 13 na Tanzania ikiwa na alama 8
 
Kwa taarifa yako na Burundi ya Nkurunziza imo!

hahahahaaaaaa

mpaka Burundi?

Nkurunzinza, Museveni, Magu, Kagame, Morsi wa Egypt, Paul Biya wa Cameroon...

Paul Biya ameingia madarakani NOVEMBER 6, 1982!
 
Hahaaa mwalimu kashasha unazungumziaje lile kosa la beki wa Uganda kushika mpira eneo la hatari
ametoa ule mpira upande wa mashariki akapiga locomotive bent bila kusimama ya kwanza alipiga inaitwa reo bent anayumba akiwa amesimama beki akakubali kutoka kwenye njia akaamua kuondoka akajabeki wa pili akapiga locomotive bent huku anaenda kama anataka kupiga back pass akageuka, quick turn "tunaita" quick reflect akapiga mpira mmoja lion pass "stand volley" mpira unaofanana kama chini unapofungia tai hapa basi kilichotokea kwa Aggrey Morris kwenda deep kwenye box akapiga side freak head kwenye paji la uso sio kisogoni sio usoni ngoma ikaenda nyavuni kushoto kwake ambapo ni kulia kwa goalkeeper Dennis Onyango hakuwa chap mpira ulienda taratibu sana lakini vipimo viwango na utulivu wa wa Agrrey Morris overlapping central back.

kwako Jesse John

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wana Jf,

Maendeleo hayana chama ndio ninachoweza kusema kilichotokea kwenye mpira Leo

Shukrani kwa mheshimiwa Makonda pia kwa uhamasishaji,

Rais magufuli wengi walijaribu lakini yeye ameweza ,aliwekeza kwa kocha, matunda yanaonekana

Kuna watu waliombea tufungwe lakini tumeshinda Kama watanzania

Chuki kwa viongozi hazitujengi, Tupongeza yanapofanyika mema
 
Back
Top Bottom