Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

Oooky Inaendelea........

Bado nilikuwa pale getto nikitafakari nisijue nini cha kufanya ikabidi nichote kikombe kingine cha maji ili ni mwagie tena lakini hata nilipoweza fanya hivyo haikusaidia kitu chochote zaidi ya yale maji kuzidi loanisha mashuka.

Basi mimi kwa mawazo yangu nikajua huyu jamaa itakuwa tayari amesha fariki na kwa mazingira yale na ukaribu ule tuliokuwa nae ingeonekana msala wote unaniangukia mimi nikawaza nikimbie nikasema naweza sababisha tatizo lingine wanaweza sema jamaa kaua halafu kakimbia

Pia ni nani atanielewa hata kama nikieleza mbele ya vyombo vya sheria eti tuliweza fanya mambo yote yale tukiwa pamoja nani atanielewa yaani mawazo mengi yaliniijia kichwani nisijue nini cha kufanya. Pia nikiangalia na zile damu kwenye shuka na chini ya uvungu ndio nikasema hapa nimekwisha hii ni kesi ya mauwaji kabisa.

Nilichokifanya nilimbeba agustino nikamuweka chini halafu nikatoa tshirt aliokuwa ameivaa ya rangi ya blue kisha nikamvua viatu alikuwa na viatu vikubwa vya wafanyakazi wa migodini kisha nikatoa yale mashuka yote kwenye kitanda yaliyokuwa yametapakaa damu.

Ndipo nikaangalia vizuri hadi kwenye cover la godoro kulikuwa kuna michirizo ya damu iliyokuwa imepenyeza kwenye shuka hadi kufika kwenye godoro basi nikayaweka kwenye ndoo halafu pia nikaweka na ile tshirt yake nikaanza kusugua cover la godoro kwa dodoki la kuogea

Kisha nikamchukua agustino nikamrudisha kwenye kitanda baadae nikaanza kupiga deki mule ndani piga kila sehemu sugua kila kitu huo huo usiki nikafua mashuka nikayaanika kisha nikarudi mule ndani . Ilibidi nikae chini nianze kujiuliza hivi agustino atakuwa amefariki kweli ndani ya moyo wangu nilikuwa nasema hapana na kama mtu aliyetufanyia hii mikosi sio mwingine atakuwa ni yule mganga maana ule mtaa wote tulikuwa hatuna bifu na mtu.

Ilibidi niwaze tena au ni huyu mama mwenye nyumba maana yeye ikifika saa moja tu tayari ameshajifungia ndani nyumba yake ilikuwa ya ndani kwa ndani na geti kubwa sisi wapangaji ndio tunaishi njee kwenye chumba ambacho jambazi akipiga mlango teke moja tu amekufikia

Lakini sikuwa na uhakika wowote hata siku ile amemtokea agustino kule nyuma ya nyumba nikasikia anakimbia. agustino baada ya kurudi asubuhi aliniambia kuwa hakusikia geti kama limefumguliwa maana lile geti mama mwenye nyumba akifungua hadi mtaa wa pili wanasikia

Basi nikasema ngoja nimtafute yule jamaa wa shinyanga nimwambie hali halisi maana nilijua fika wenyewe wanaweza nisaidia kutatua tatizo daa kushika simu ya agustino sikuona namba hata moja hapo ndio nikachoka nikajua hapa ni ushirikina moja kwa moja nikatoa line yake nikaweka kwenye simu yangu zote zikasoma emergency call .

Hapo nikasema daa mimi jooohs leo nimekamatika siku zote ndege mjanja hunaswa kwenye tundu bovu nilibaki pale chini hadi nikasikia kunaenda pambazuka kuku wanaanza kuwika basi nikaamka fasta pale nilipokuwa nimekaa nikaenda kumuamsha agustino kwa mara nyingine lakini alikuwa kama mtu aliyepooza hapumui wala nini.

Basi nikatoka njee kwenda kukojoa wakati narudi kuangalia yale mashuka pale njee yana alama za damu nikama sikuzifua vizuri basi ikabidi nizianue fasta hivyo hivyo mbichi nikaziingiza ndani nikaziweka kwenye kamba iliyokuwa juu ya dirisha .

Ikabidi nitoke njee nikafunga mlango na kufuli halafu nikatoka njee nikiwa nimemuacha agustino mule ndani nikasema ngoja niangalie usawa wa msosi maana nilikuwa nasikia njaa ya kufa mtu wakati bado nawaza kushika mfukoni sina kitu hata mia mbovu

Ikabidi nirudi getto pale kuchukua nilifungua mlango nikaanza kutafuta wapi nilikuwa nimeweka hela zangu daa sizioni nikapiga mahesabu nikasema jamaa agustino huwa anawaleti tafuta nikaikosa nilikuwa nimemlaza chali ikabidi nimgeuze bado sikuona Walet daa nikasema hapa sijui nifanye nini ikabidi nikae pale chini nikasema niende wapi mimi

Baada ya dakika chache nikasema ngoja nikamtafute kunajamaa alikuwa mshikaji wetu sana alikuwa ni mpishi kwenye ile shule tuliokuwa tunasoma maana tulikuwa tunamsaidia sana na bangi akiwa na uhitaji basi nikamuacha agustino mule ndani nikafunga mlango nikaondoka kuelekea shuleni kumbuka hiyo wiki wanafunzi wameanza kuripoti shule wale kina john visomo

Nilipita pale njia panda nikaona baadhi ya wanafunzi wako kwenye kile kimgahawa wamapiga chai nikapitiliza huku nikitazama mifupa ya wale kuku tulio watupa pale ilivyotapakaa na kuharibika sana kwenye ile bara bara

Basi mimi nikapita tu kama sifahamu kinachoendelea huku moyo wangu ukiwa unaenda mbio hadi mdundo wa mapigo ya moyo nikawa nausikia masikioni niliteremka na barabara hadi nikafika shuleni nikawa naona kwa mbali wenzagu na baadhi ya kidato cha sita wakiwa wanapiga msuli, wengine wanapigiana table teaching daa nikasema mtaka vyote mkosa vyote ndio nisha feli hivyo

Bila kupoteza muda nikapita moja kwa moja hadi jikoni nikamkuta mpishi anahangaika na kuongeza magogo ndani ya jiko huku uji wa mahindi ukiwa unatokota mdogo mdogo ndani ya sufuria basi alivyoniona tukapeana salamu kitu cha kwanza akaniuliza agustino yuko wapi nikamwabia alienda kufata mzigo bado hajarudi maana hiyo ishu ya bangi yule mpishi alikuwa anahijua before hata mimi sijaijua.

Nikamwabia anisaidie kwanza bangi kweli alinipatia kakipisi kadogo nikasogea chemba nikaanza kupuliza baada ya kumaliza wazo likaniijia ebu mwambie huyu mpishi jambo lililomkuta agustino ikabidi niinuke nilipokuwa nimejibanza nikaanza kumfata kule jikoni baada ya kufika nikamwabia nisaidia uji ikabidi achote animiminie kwenye sahani ya plastiki nilikunywa uji mpaka jamaa akabaki anashangaa

Nilipomaliza wazo lingine likakiambia ondoka ila nilimwabia nitarudi jioni kuna mishe nataka tuongee basi nikaondoka kurudi getto hapo mawazo ya kumtoa agustino mule ndani na kumpeleka popote yakanza kuniingia nadhani labda ni kile kibangi nilichokuwa nimevuta wakati natembea kurudi getto nikaanza kupepesa macho ni chaka gani zuri la kwenda kuutupa ule mwili halafu ikiwezekana nikatoe taarifa za kupotea kwake

Nilifikiria nikaona hilo litakuwa wazo zuri wakati nafika pale getto nikamkuta mama mwenye nyumba amekaa njee anatwanga kitu kwenye kinu nikamsalimia hakuitikia nikasema potelea mbali nikaingia na kufungua mlango

Ile nimeingia tu nikakaribishwa na michirizi ya damu kibao pale chini nikaingia ndani fasta nikajifungia kumcheki agustino hana hata dalili ya kuamka nikasema leo usiku ikiwezekana nimbebe nimtupe mahali maana akianza kunuka hapa itakuwa noma kushika simu haina chaji tafuta pesa mule ndani sioni kitu .nikasema nitafanya nini jasho likaanza kunitoka ,nikahisi kuchanganyikiwa nahisi kulia lakini kwa mawazo niliyokuwa nayo hata ningelia isinge saidia kitu

Ilibidi nivue shati nikabaki kifua wazi nikalala pale chini sakafuni huku nikiendelea kujiuliza hizi damu nani anazileta humu ndani nilitamani nitukane matusi ya nguvu ili yule mama hasikie lakini ilibidi nitulie tu

Nililala pale mpaka kwenye majira ya saa kumi hadi nikaanza kuota mpango wa mganga ilifanikiwa tunafanya matanuzi wewe weweee nilikuja kuamshwa pale chini na njaa ya kufa mtu nilivyoamka nikasimama nikaenda kuanza kumchunguza agustino nikaona kweli jamaa amefariki ikabidi nianze kutest kama naweza kumbeba daa alikuwa mzito balaa.

Kisha nikatoka njee nikafata dekio nikaanza kufuta zile damu pale baada ya hapo nikaenda moja kwa moja hadi shuleni hiyo jioni tulipiga story na mpishi huku nikitaka kumueleza shida yangu lakini moyo ulikuwa unasita nilichumguza marafiki pale shuleni kama muddy atakuwa kasha fika lakini niliambulia patupu sasa baada ya kula ikabidi niondoke nikasema leo lazima usiku totoro nitoe ule mwili pale ndani halafu asubuhi nianze gia za kumtafuta

Njiani nilikiwa nimechanganyikiwa kabisa yaani sura yangu ilikuwa inaonesha huyu mtu amekata tamaa yaani nilikuwa nimebaki kama puto muda wowote ule naweza pasuka nilitamani niende hata kwa yule babu anipatie bangi niondoe mawazo lakini nilijua mzigo hana lakini nikasema haina shida nitapiga tu free style

Nilirudi kufungua getto nilikuta kama mwili wajamaa unaanza kama kuharibika huku nikajaribu kiugeuza mwili mgongoni alikuwa kama anavuja damu

Daa nikasema leo sita lala hapa naondoka na mwili halafu nachukua kila kilicho changu nasepa basi nikaendelea kukaa pale chini hadi muda kama saa 6 hivi usiku

Nikavua shati niliokuwanayo nikavua suruari kulikuwa na bukta ya jinsi nikavaa nikachukua vile viatu vya mpira nikavaa kisha nikachukua ule mwili nikauweka chini. Kisha nikasema ngoja nitoke njee nizuge kama naenda chooni nisome mazingira ya kumtoa mwana mule ndani .

Nikafungua mlango taratibu kisha nikatoka njee nikiwa kifua wazi basi nikaenda chooni wakati narudi kupiga chabo kwenye geti la mama mwenye nyumba naona yuko kwa ndani amesimama anachungulia yaani alikuwa amefungua mlango wa mbao kwa ndani ananichungulia kwenye nondo za urembo zilizokuwa juu ya geti .

Basi nikazuga narudi kulala ila nikasema lazima ule mwili utoke mule ndani usiku ule ule





Sent using Jamii Forums mobile app
"kumbuka hiyo wiki wanafunzi wameanza kuripoti shule wale kina john visomo"😂😂
Dah iko kipande kimenifanya nicheke kmoma mana kimenikumbusha mbali balaa ebhana tuauche masihara kuna wajomba wanasoma bhn yn ni ile mtu amepewa wosia wa vipaombele vya Mh Lowasa naukamuingia kwl kwl kwamba Namba moja Elimu namba mbili Elimu namba tatu Elimu
 
Oky Inaendelea..........

Baada ya kutoka pale chooni huku nikiwa kifuawazi na nimesha muona mama mwenye nyumba ananichora asee nilipandwa na hasira nilivuta sura moja ya kibandidu nikasogea mpaka pale mlangoni nikasimama nikamkata jicho lakini hakuonesha mshituko wowote yeye aliendelea kunitazama kwa macho makavu

Basi ikabidi ni ninyooshe mikono juu nikaingia ndani nikajifanya kufunga mlango kwa nguvu lakini nilikuwa bado naendelea kuzuga nikijua yule ni mwanamkee tu atarudi kulala kama mnavyojua kwenye milango mingi kwa juu huwa wanaachaga space wengine wanaweka hata nyavu ikabidi niweke stuli nipandishe kwa juu mdogo mdogo nichungulie kama mama mwenyewe nyumba atakuwa katoka pale mlangoni basi nikaweka stuli nikapanda taratibu sana nikatoa kichwa kidogo nichungulie.

Asee yule mama ni alqaida yani nimetoa jicho sehemu ndogo sana nikaona bado yupo halafu amenikazia jicho sehemu ile ile niliokuwa nachungulia daa nikasema sasa hii ngoma imekuwa ngumu nikakaa pale chini kwa muda kidogo nikaenda kumuangalia agustino nikahisi kama anaanza kutoa harufu daa hapo ndio nikachanganyikiwa nikainama uvunguni kulikuwa na neti inamatobo matobo nikatoa nikajaribu kutandika chini ili nione kama ninaweza uweka ule mwili nikaufunga nikautoa kama mzigo

Hapo hofu inazidi kuniingia niki imagine nimekaa na mtu hadi ameanza kuoza ghafla nilisikia kishindo kama mtu anakaribia mlangoni ikabidi nipande tena juu ya stuli kuchungulia daa namkuta bado yule mama yuko pale pale anachungulia nilizidi kuwaza pale bila kupata majibu ikabidi nibebe tena mwili niuweke juu ya ile neti nikajaribu kufunga mwili naona bado ni kazi bure maana ilikuwa haifuniki mwili vizuri

Nilichoka sana ikabidi nikae pale chini nikasema leo huyu mama amenizidi ujanja wakati huo nazidi kusikia harufu kali inazidi kutoka kwenye kile chumba yaani inatoka halafu inakata ikabidi niuache ule mwili pale chini nikapanda kitandani na viatu hata siku vua

Nilipiga usingizi kama masaa wawili baada ya hapo nikashituka kuangalia mwili unazidi toa harufu mbaya halafu chini kulikuwa na damu nyingi hadi zimetoka chini ya mlango nikasema leo ndio leo hii siku nikipona basi siwezi fanya ujinga tena.

Niliamka pale nikafungua mlango kuangaza huku na huku nikaona hali ni shwali basi nikatoka njee nikachota maji kwenye kidumu nikaweka kwenye ndoo nikavuruta ule mwili kwenda ndani zaidi nikapata space nikafuta zile damu fasta nikaenda mwaga maji kurudi ndani nikasema ngoja niangalie muda nikawasha simu ili niangalie muda yaani imeonesha muda tu ikazima ilikuwa kama saa 10 kasoro nikasema bado ninamuda naweza toa ule mwili ndani.

Basi nikarudi ndani nikajaribu kubeba ule mwili begani ikashindikana yaani ulikiwa mzito balaa nikasema ngoja niuburuze hadi kwenye kingazi cha mlango ili nipate sapoti ya kuunyanyua. Nikaanza kuuvuruta taratibu mlango nikauvuta wote mpaka mwisho nilivyo ufikisha pale kwenye ngazi nikapata balance ya kuubeba ile nimevimba ili ni ubebe ule mwili nilisikia nyuma yangu kishindo cha geti kama linafunguliwa ilibidi ni ruke kwa ndani halafu nikauvuta ule mwili fasta kurudi ndani

Kisha nikatoka nikakaa pale mlangoni lakini nilikaa pale kwa madakika kadhaa sikusikia tena kama mtu anatoka njee nikarudi ndani nikafunga mlango nikajitupa kitandani daa nikajua mambo yameharibika maana nilijua any time yule mama anaweza kunichoma hata kwa askari

Basi kulikucha bado agustino yuko mulemule getto halafu alikuwa ameanza kutoa harufu kama ya mzoga nikasema leo sitoki humu ndani maana unaweza toka mtu akaja kupanda pale kwa juu ya mlango kuchungulia. Pia yule mama hakuwahi hata siku moja kuniuliza eti agustino yuko wapi maana mimi pale nilikuwa sii mpangaji nilikuwa kama mgeni tu.

Basi nimekaa mule ndani naangalia ile maiti mpaka mapua yakazoea ile hewa ya mule nilikuwa nikitoka njee kwenda chooni nikirudi ndio naisikia vizuri .Nilikaa sana mule ndani nisijue la kufanya baada ya njaa kuzidi ndio nikasema ngoja nitoke niende kwa mpishi maana nilikuwa sina hata mia mbovu mfukoni basi nilichukua ule mwili nikaukanyaga kuusukuma uvungumi kisha nikafunga mlango nikasepa

Nilienda hadi shuleni kiukweli nilikuta watu wengi wamesharudi kutoka likizo nilizunguka hadi jikoni nikamfata mlinzi nikamwabia kama anamsosi wowote anisaidie akasema kuna uji msosi mpaka saa 9 hapo ilikuwa mida ya saa 7 akatoa uji kwenye kindoo akanipatia tukaanza kupiga nilitaka nimwabie ishi inayonisibu ila roho ilikata kabisa

Nikamwabia anisaidie ganja alikataa akasema hana basi tuliendelea kupiga story za hapa na pale nikisubiri msosi uive baada ya kazi kuwa nyingi nikaona anatoa kipisi cha bangi mfukoni na mimi akanipatia kimoja msosi ulivyokuwa tayari akapakuwa tukala hadi nikavembewa kisha nikasepa

Niliwahi haraka getto nisijue nini cha kufanya huku ile pisi ya bangi nikasema nitaivuta usiku halafu hata kama yule mama atatoa macho pale njee nitatoka na mwili anaagalia mzima mzima

Basi nikarudi nikakuta chumba kama nilivyokiacha lakini harufu ilizidi kuongezeka ikawa kali kinoma yaani kanakwamba mtu hata akipita dirishani lazima asikie

Yaani ilikuwa harufu kama mzoga wa paka aliyekufa unaona jinsi anavyo chafua mtaa , basi nilijifungia mlango sikutaka kelele na mtu yoyote ila nilikuwa na asilimia mia mchezo wote atakuwa amahusika yule mama kwa namna moja ama nyingine

Nilipiga usingizi kidogo nikiwa na hamu muda uzidi kusogea ili niweze kutoa ule mwili maana angelala tena pale ilikuwa mara ya tatu basi nilikuwa kama nimejiegesha mikaamka muda ulikuwa umeenda kidogo nikachukua simu jaribu kiwasha wapi nikatoa betri paka mate nikarudisha tena wapi sasa ikabidi nikadirie tu muda

Baada kama ya dakika arubini na tano kupita nikachukua ile ganja nikawasha nikapuliza wewe niasikia hadi kichwa kimekuwa kizito basi nikamaliza nikavaa viatu vizuri ,nikafungua mlango hadi mwisho toa ile maiti ndani wakati naivuta pale nikaona masikioni mdomoni na puani anatoa kama ute ute wala sikujali.

Sikuangaika kuangalia nani ananiangalia au nani haniangalii nikashika ile maiti kiunoni kumbuka alikuwa kifua wazi nikainyanyua kwa nguvu zote nikaipandisha hadi mabegani yaani utadhani ni leisner anataka kupiga mtu F5 kisha niaanza mwendo wakati huo sijapanga niwapi nitaenda kuitupa na nitaificha vipi.

Nikaanza kutembe sikuta nifate bara bara nikaingia kwenye njia za mkato nilitembea nikatembea nikatembea nikatembea wakati huo sina tochi nikahisi ule mwili unakuwa mzito nilivyo ingia ndani ndani kwenye vichaka nikasema hii hii ndio sehemu natupa huu mwili basi nikazidi kujongea ile nimefika naenda kutua asee kuangalia shingoni nilikuwa nimebeba mnyama wa ajabu kama nguruwe mwitu

Niliogopa sana nikaanza kukimbia kurudi getto nilikimbia ikafika mahala nikakaribia kufika getto kwa mbali nikaona kama watu wamejaa pale kwenye ile nyumba nikaanza kujiuliza au hii ishi mama mwenye nyumba ameita raia daa nikasema mungu saidia wasije wakawa wameingia kwenye kile chumba maana nilikuw nimekiacha wazi baada ya mzigo kunilemea.

Hazikupita hata dakika 5 kuangalia vizuri naona kimya hakuna watu basi nikaliunga taratibi hadi getto kufika nakuta mlango umefungwa kwa ndani ikabidi nianze kuusukuma kwa nguvu bila kuita mtu yoyote...

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimefanya kosa sana kusoma hii episode usiku huu [emoji45]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu itakuwa ngozi yako ina afya sana.

Maana tukiachana na maswala ya ulozi ile kitu itakuwa inaondoa uchafu sana mwilini

Mtu unachemka jasho linatoka kama unapikwa yaani ilibaki kidogo ni amke nitimue mbio

Asee mvuke unachoma jamani

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji28][emoji28][emoji23][emoji23][emoji23] Yan mkuu ukisema kuhusu kuchomwa na mvuke nacheka sana , hii kweli ni true story

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom