Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

Kwa mashairi haya nisipoangalia naweza jikuta nimesema 'yes I do.!
Ha ha! Why don't you say yes..?

Hiyo yes hujui tu inamaana kubwa Sana kwako na kwangu!
Itafungua kurasa adhimu!,kurasa ya huba ambalo hutoweza kujutia.
Yes yako itakufanya uitwe malaika!,yes yako itatuliza moyo wako kwa kupata huba tamu lisilo vipimo toka kwangu..

Usiutie ukwasi nafasi adhimu,nipe nafasi uone utamu!
Wangu ma baby nikuite lady
Wangu wa huba nikutoe dhoruba😉

Sema nami nitete nawe,nikuite honey uniite nawe😜
 
Mimi nataka mahari tu
Carleen wa @glenn
Ha ha! Why don't you say yes..?

Hiyo yes hujui tu inamaana kubwa Sana kwako na kwangu!
Itafungua kurasa adhimu!,kurasa ya huba ambalo hutoweza kujutia.
Yes yako itakufanya uitwe malaika!,yes yako itatuliza moyo wako kwa kupata huba tamu lisilo vipimo toka kwangu..

Usiutie ukwasi nafasi adhimu,nipe nafasi uone utamu!
Wangu ma baby nikuite lady
Wangu wa huba nikutoe dhoruba[emoji6]

Sema nami nitete nawe,nikuite honey uniite nawe[emoji12]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Oky Inaendelea..........

Basi wakati tuko pale kwa mganga akaendelea kutapa masharti na maelekezo tofauti tofauti huku akitusisitizia sana tufanye kama alivyosema pengine nilidhani labda anahofia umri tuliokuwa nao wakati ule.

Baada ya hapo alichukua kopo la tosi lililokuwa pembeni yake lilikuwa kuukuu akalifungua ndani kulikuwa na visu vya kuchongesha kienyeji yaani ni kipande kidogo cha mti halafu kimechomekwa kichuma flani hivi kwa mbele kama spoku ya baiskeli akatoa viwili akatugawia kila mtu kimoja

Akatuambia kabla hatujapanda mbegu lazima tumwage damu kwenye lile shimo lakini kuku yule hatutakiwi kumchinja kawaida inatakiwa tumtoboe toboe na kile kisu mfano wa bisibisi kuanzia kichwani hadi miguuni mpaka apoteze uhai kisha tupande mbegu tufukie .Mzoga wa yule kuku tukatupe njia panda tena inayopitwa na watu wengi

Basi akatusisitizia kuoga na zile dawa alizokuwa ametupatia kipindi cha nyuma pamoja na kunywa lakini tusioge kwenye bafu ambalo humo humo ni choo bora usubiri usiku ukaoga kibarazani. Kisha akatuambia baada ya lile zoezi kukamilika pesa ndio zitakuwa zinaangaika kututafuta na sio sisi kuziangaikia tena

Baada ya hapo akatutakia safari njema na mafanikio mema na kutuambia tutapata mafanikio kwa haraka na kabla mwezi hauja chomoza tumpelekee zawadi kama malipo yake kisha tukawaaga na wale masela pamoja na yule mkee wa mganga tukasepa.

Tukaenda getto tukawa tumetoa nguo tufue tukakuta majaa wasukuma vijana walikuwa na umri kama wa maika 25 hivi wako pale njee wanapiga story baada ya kupiga nao story ikabidi wafunguke eti kunajamaa wamemleta pale kwa mganga kulingana na tatizo lake wameambiwa usiku wapeleke mbuzi beberu waizike nzima nzima ili jamaa yao apate kupona.

Ilipofika usiku agustino ikabidi amcheki yule jamaa aliyetupeleka akamwabia tumemaliza kazi kesho tunapita kwake kumuaga sisi tunasepa basi usiku ule kila mmoja alitoa vitu vyote na nguo zote kwenye begi lake tukatanguliza kwanza yale madawa tuliokuwa tumepewa ndio tukapanga nguo kwa juu.

Kesho yake bila kupoteza muda tukaenda kwa yule jamaa tulishukia njiani akatufata na gari yake akatupeleka mpaka kwake tulipiga msosi wa nguvu kisha akaanza kutuambia kama mmesha toka kwa mganga kila kitu mmemaliza na kama mkifata alivyoelekeza maisha yenu yataenda kubadilika kabisa baadae akasema atutoe tukatembee kidogo mjini lakini wote tuligoma maana tulikuwa tumechoka balaa

Pia wote baada ya kutoka kwa mganga kila mtu alionekana hana furaha nafsini kwake kwani wakati niko njiani nilikuwa najiuliza hivi nitawezaje kwenda usiku saa 7 tena mimi peke yangu mahali nikachimba kishimo nikapanda mbegu kisha nikauwa kuku mwenyewe hivi nitaweza kweli

Kila muda akili yangu ilikuwa inavuta picha kwenye ule mtaa pale shuleni ni sehemu gani nitaweza fanyia kile kitendo lakini nilikuwa sipati majibu moyo unazidi kujaa hofu lakini nikawa nasema potelea mbali liwalo na liwe

Basi usiku tukaanza kujadiliana lakini jamaa yangu agustino anasema nikitu rahisi sana wale kisinipe mawazo basi mimi nikaamua kujilaza baadae story zikachange tukaanza kukumbushiana mdogo mdogo economics zile topic za mwanzo subject matter na demand n supply mimi kichwa kilikuwa kimesha haribika ila jamaa alikuwa anapenda masomo sijui hata ule moyo wa kukumbushana alikuwa anautoa wapi katika hali ile

Basi kesho yake asubuhi yule jamaa akatupeleka hadi stand kwa gari yake safari ikaanza kurudi kwenye getto la agustino basi ilituchukua zaidi ya masaa 9 mpaka kufika stand tukashuka nikamwabia agustino hapa tutafute boda boda maana mizigo sio mingi ni haya mabegi.

Laķini jamaa akaniuliza sii wewe unapitiliza hadi shuleni hostel daa nikamwabia shule bado hatujafungua na hivi vitu nilivyonavyo humu inatakiwa tufikie getto kwako siunajua form 6 hawajafunga wamebaki pale wakiniona nimefika wanaweza kunipora mizigi yangu basi jamaa akatoa 30000 akanipatia akaniambia lete begi lako nikampatia akaniambia tafuta wanapo uza kuku uchukue hata wa 13000 wawili kama mganga alivyosema mimi natangulia wewe utakuja nao

Basi mimi nikampatia begi langu nikaenda kutafuta kuku mjini nilizunguka nikawa nauliza hadi nikaenda kuwapata kwenye vibanda vya soko nikanunua wawili jumla 24000 basi nikamaliza nikachukua boda boda hadi getto kufika nikamkuta jamaa amechangamka kudeki nyumba basi nikaanza kutafuta kamba ya kufungia jamaa akaniambia kuna net iko chini ya uvungu imechakaa nichukue nikate nitoe kamba

Daa ile nimeinama nikaona matone ya damu ambazo ni mbichi chini ya uvungu asee roho ilitaka kupasuka lakini nilisema uchawi hauwendi kwa mentali nikatoa chandarua nikaanza kutengeneza kamba basi jamaa akafua fua baadhi ya mashuka tukapika msosi tukala tukaelekea shuleni kupiga story na wanaa waliokua hawajaenda likizo huku tukiacha kuku zetu pale njee.

Lakini mawazo yalinijaa kichwani zile damu zinatoka wapi na nini sababu baadae akaniambia turudi geto kabla giza halijazidi tuone nijinsi gani tutachora ramani ya kukamilisha ule mchezo usiku ule siku lala nikawa najiuliza maswali ni alama gani nitaweka kwenye aneo nitakalo panda mbegu zangu ili nisisahau kila sehemu naona haiwezekani

Kesho yake tukaanza survey mtaani njiani tunaulizana hivi pale pata faa basi baada ya kuzunguka sana mimi nikaona muembe mkubwa maeneo ya pale pale yaani ulikuwa ni mkubwa kama mbuyu nikamwabia jamaa yangu mimi nitafanyia pale baada tena ya pita pita yeye kasema ataenda pembeni ya mwamba mkubwa raia wa pale waga wanatumia kuanikia nafaka.

Basi kesho yake akaniacha asubuhi nimelala pale akasema anaenda kumuona pusha flani hivi wa bangi waongee biashara maana alimpigia simu akasema mzigo umeisha wakati najigeuza geuza kwenye kile kitanda nilisikia kama kuna sarafu basi nikaamua kuichukua lakini papasa mkono kumbe jamaa alikuwa ameishonea ndani ya godoro kwa ndani kabisa daa nikasema huyu baharia ni hatari

Baada ya muda nikawaza sana lakini roho ya ujasili iliniingia nikasema nikienda kwenye eneo la tukio kuku ndio mgumu kumuuwa nikasema nguvu zote nitawekeza Kwenye kuuwa kuku

Nilitoka pale kikafunga mlango nikaenda kutafuta kifungua kinywa kunamgahawa flani hivi nikakuta wapiga msuli tunao soma nao wanadiscus tu habari za masomo mara sijui integral sijui differentiation hawakwenda likizo basi baada ya kutoka pale nikarudi getto nikafungua begi kuaandaa zana ili usiku mimi nikamilishe kila kitu.

Nilitoka tena nikaenda pale chini ya muembe kufanya survey ikiwezekana niweke alama kabisa ya wapi nitafaanyia tukio pale chini ya muembe maana eneo la pale lilikuwa kubwa kama unavyojua maeneo ya kijiji ni majani majani marefu na matuta yaliyokuwa yamezunguka ule muembe basi nikabeba jiwe kubwa kiasi nikategesha pembeni ya ule muembe

Nikarudi getto nikamkuta agustino basi nikampanga kila kitu na yeye akaniambia leo usiki tumalize mchezo tukapiga mahesabu kuku tutafanyaje asipige kelele akaniambia tutatumia kamba za manila tuwazibe midomo basi.

Tulienda shuleni tukapoteza muda na wadau halafu tukaondoka tulaelekea kwa yule babu tukavuta bangi za kufa mtu siku hiyo tulipata hadi wanajeshi wanagwanda kabisa wanapuliza tukapeana high tukapiga vitu vyetu tukasepa tukarudi hadi getto kiukweli nilikuwa na ogopa kutoka saa 7 tena kila mtu na njia yake bora hata tungekuwa pamoja lakini baada ya kupiga zile ganja uoga ulipungua sana.

Tulikaa getto tukapiga story huku kuku tumezifunga kamba miguu kichwani na kwenye mabawa ilipofika saa 6 kama na dakika 50 kila mmoja akachukua tochi yake zile za sola udogo mbegu kisu na kuku akapitia njia yake njiani nilikuwa naogopa sana kwani kile kijiji watu wanasema ni mambo ya uchwawi ndio yanafanya kisiendele huku nikiwa nawaza au pale kwenye muembe mkubwa ndio huwa wachawi wa ule mtaa wanafanyai mkutano wao

Nilikuwa natembea haraka haraka huku nikiangalia nyuma tochi nilikuwa nimezima nilifatilia ramani hadi nikafika kwenye ule muembe haraka zangu nikataka nianze kuchimba kuaangalia kwenye ule mfuko niliokuwa nimebeba sioni kitu cha kuchimbia, kuku nilikuwa nimemuweka chini akaanza kutapa tapa nikasema ngoja niwashe tochi nitafute kijiti nianze kuchimba shimo kubwa kiasi ili wakati narudi nisije kupotea mahali nilipo panda mbegu.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Big up mkuu jooohs
Kastory katamu walaqhi'.
Halafu wapenzi wafuatiliaji tupendane tu, tukumbukane katika kutagiana.!
Mkuu inawndelea saa ngapi tena?
Asante mkuu ukiendelea unitag pole kwa masaibu

Sent using Jamii Forums mobile app
Eeh, sipati picha hapo pakwenda kupanda hizo mbeguu yani ni kama unaenda kujua hatma yako,baada ya mihangaiko yote kwa mganga......Niko hapa nasubiri mwendelezo[emoji41]
Huyu jamaa atakua moshi aujatoka kichwani
Mkuu asante kwa kuendelea kunijuza kila unapotoa.

Hizi mambo za chale hizi[emoji38][emoji38][emoji38] unaweza pata demu mgongo una chale kama cutting board

Sent using Jamii Forums mobile app
Ngoja nami nijsajili kupata update naona kuna kitu cha kujifunza hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
Nyie vitoto vya kike mnaopenda hadithi za kichawi huwa naogopa hata kuwaita[emoji12][emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23] Wapenzi wafatiliaji tupo wengi

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji23][emoji23][emoji23] Wapenzi wafatiliaji tupo wengi

Sent using Jamii Forums mobile app
Waganga nyokoooo

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu endelea basi, story nzuri
Mwendelezo jamani

Sent using Jamii Forums mobile app
Agustino aisee ww ndio uliyemdangaya mwenzako aende kwa mganga sio

Sent using Jamii Forums mobile app
Bonge la story mkuu
Duh..... Alikufa nini?

Maana inaonekana ni mtu mwenye itikadi za GET RICH OR DIE TRYING

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimeongezeka.......

Sent using Jamii Forums mobile app
Jamaa alibeba MASTERING HISTORY kwa mganga[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Read my signature below [emoji116]

WANA JAMII FORUMS, TUSIFANYE MAKOSA TENA OCT 2020
Mkuu@jooohs tupe vitu mkuu

House girl(dada wa kazi) Ni binadamu aheshimiwe, apumzike, apewe Uhuru wa kuabudu pia
Mkuu tuendelee na story

Sent using Jamii Forums mobile app
Signature: sic march

Sent using Jamii Forums mobile app
ukiongezea story naomba unitag
Mkuu leta nondo,chai inakaribia kupoa
Hizo kashata mbona haziji kahawa inapoa huku!

Sent using Jamii Forums mobile app
Heading inasanifu hitimisho

Katika maisha watu wanafight sana na maisha ila hola

Kuna maumivu mengi sana katika utafutaji ndo maana huwa ninakanuni ya kuheshimu cha mtu

Maisha yamejaa uchaguzi , ndo maana nikikuta mdada kaamua kutunisha makalio ili aishi mjini kwa kuwa mdangaji- siku hizi nimeacha kabisaa kucoment hisia zangu na kuheshimu maamzi yake

Kwa umbambanani huu haishangazi kuona watu wengine wanaishi peponi uku wengine wanaishi jehanamu



Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu iendelee...
Bila shaka maharagwe yaligoma kuota.
Rejea Kichwa cha Habari.
Pole sana kwa ma swahibu.
.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaendelea........


Nilikaa pele kwenye majani ya migomba kama masaa 3 hivi hadi jua likaanza kuwa kali maana lile jumba lilikuwa liko wazii kwa juu.

Nilikaa pale nikaangalia juu nikawa naona jua linavyo nipiga huku nikiendelea kutoa manyoya ya kuku ambayo yalikuwa yameganda sehemu mbali mbali za kwenye mwili wangu nikaanza kujiuliza hivi kweli ndio nimeamua kupitia njia hii?

Sikuwaza sana wala sikujutia kutokana na maisha ambayo nilikuwa nimepitia hapo nyuma, maisha ya kuomba omba kwa watu na kufanya vibarua vya ajabu ajabu. Ada yenyewe ya masomo nilikuwa mpaka nikapige magoti kwa afisa elimu kama mtoto yatima ndio itolewe .

Wakati bado naendelea kuwaza nikasikia sauti ya yule kibaraka wa mganga ananiambia vaa nguo unifuate basi baada ya hapo nikapelekwa hadi kilingeni nikamkuta mganga akaniambia kaa kwenye kigoda kisha akaniambia vua shati na suruali upandishe hadi magotini.

Baada ya hapo akachukua kibakuli kilikuwa na unga mweusi pia akachukua wembe akaupasua akaanza kunichanja, Alianza kunipiga chanjo mbili mbili kila sehemu kuanzia utosini, kifuasi, nyuma ya shingo, kwenye viwiko vya mkono, kwenye magoti, panapo unganisha mkono na kiganja, pia mwisho wa miguu kwenye maungio ya mguu na kikanyagio.

Alipomaliza akaanza kunipaka ule unga mweusi alipomaliza akaniambia niondoke na nisije nikaoga mpaka kesho yake nirudi kupata maelekezo mengine niliondoka hadi pale tulipopewa chumba nikamkuta jamaa yangu amesha fika na amefanyiwa kama mimi niliyofanyiwa.

Basi tulilala hivyo hivyo kesho yake asubuhi tukawahi kwa mganga baada ya kwenda tuliingia pamoja na agustino kisha tukapatiwa dawa ya kwenda kuogea halafu mganga akatuambia tumebakiza mambo machache tu tukamikishe yaliyotupeleka pale.

Akatuambia siki ile ile tunatakiwa kwenda kati kati ya barabara yaani njia panda majira ya saa saba usiku tufanyiwe dawa halafu itakuwa imebaki hatua moja ili tuweze kuondoka basi tuliondoka tukaenda tukaoga tukapumzika ili ikifika mida mida ya usiku tuanze kwenda kwa yule mganga.

Baada ya muda kufika tulienda kwa mganga akatukabidhi kijakazi wake alitoa zile kaniki nyeusi ambazo tulikuwa tumekwisha zinunua akatuambia tuvae kisha tukaanza safari haikuwa mbali sana kama mita 250 tukawa tumefika.

Baade tulikaa kati kati ya bara bara akatuchanja utosini akafanya madawa yake pale halafu akatoa kijembe kidogo sana unaweza kukishika na mkono mmoja tu akachimba udongo kisha akatuambia kila mmoja achote mchanga tukaweka kwenye mfuko kila mtu tofauti halafu kwenye lile shimo akatoa dawa flani akafukia mule.

Baada ya hapo tukaondoka tukarudi hadi kwa mganga ,tulikuta mganga anashughulikia mama mwingine na watu kadhaa walikuepo sisi yule jamaa akatuambia tuondoke halafu kesho asubuhi turudi tena

Kesho yake asubuhi tukaenda mganga akatuambia imebaki hatua moja pia mizimu na mababu lazima ipate zawadi ambayo ni damu ili ipate furaha itutekelezee jambo letu vizuri tukasema hakuna tatizo tuko tayari basi mganga akatuambia lazima mlipie gharama shillingi 50000 kwa wale vijakazi yeye malipo yake tutarudisha mambo yakiwa sawa basi jamaa yangu bila kusita akatoa pesa yote pale pale.

Kisha wakasema leo usiku ndio tunaenda kumaliza kila kitu tutoe na pesa wakanunue nazi na udi kwa ajili ya kazi yetu baada ya hapo wakatuambia tuondoke turudi usiku maana kazi itaanzaa saa sita usiku.

Basi tulikuwa na furaha tukijua kuwa tunaenda kumaliza kila kitu ili turudi tuendelee hata kupiga msuli maana nakumbuka jamaa alikuwa kwenye begi amabeba mastering history awe anapitia pitia lakini hakuwahi igusa hadi tunatoka pale kwa mganga

Basi usiki kwenye mida ya saa 5 tukajisogeza pale tulikuta jamaa wameandaa vitu kadhaa wamaweka kwenye gunia basi tukaanza safari nilikuwa nadhani tunaelekea njia panda laahaula baada ya kutembea sana kama kilo mita moja tukajikuta tuko eneo la makaburi daa nikaanza kuogoba basi tulivyofika jamaa wakatuambia tubadili nguo yaani zile kaniki nikikumbuka nacheka sana tulikuwa kama bongo movie kisha jamaa akatoa kile kijembe akachimba mbele ya kaburi moja .

Akaniambia chota mchanga na mkono wa kulia basi nikachota nikauweka kwenye kile kimfuko cha kule njia panda halafu akaniambai nilale juu ya lile kaburi pia na jamaa yangu akaambiwa afanye hivyo hivyo basi wakawasha udi kuzungula lile kaburi.

Daa wakangomani ni hatari asikwambie mtu nilisikia wanaanza kuongea lugha nisiyo ielewa wakawa kama wanakemea mapepo yaani zaidi ya walokole wanavyokemea kisha walikuwa na kikamba kama kombeo cha kupasulia nazi wanaingiza nazi ndani yake wakati huo mimi nimelala chali halafu wanapasua nazi juu ya kaburi usiki unasika kama baruti

Kwa kuhesabu haraka haraka walipasua kila mmoja nazi kama saba kisha tukaondoka wakatuambia tuondoke bila kuongea kitu chochote tukafika hadi kwa mganga wakatuambia tuondoke tusiongee jambo lolote hadi kesho asubuhi turudi pale tupewe maelekezo ya mwisho.

Kweli tuliondoka hatukuongea neno lolote kila mmoja alijikausha hakuna ambaye hata alikohoa, asubuhi na mapema tukafika pale kwa mganga tukakuta mabaharia wengine wako pale wanaonge tu habari za madini baadae tuliitwa maana Sisi tulikuwa ni kama tumesha maliza basi.

Mganga sikuio ni kama alikuwa na furaha sana tulionge story za kawaida kisha akatuambia naona kabisa mnaenda kutimiza malengo yenu dawa zote na kila kitu kimeenda sawa sasa ni hivi akatoa ule mchanga ulikuwa katika kila kimfuko akanipatia mimi na agustino pia kisha akatoa mbegu za maharage akanipatia mimi mbili na agustino mbili akazifunga kwenyw karatasi nyeusi .

Kisha akatuambia hizi mbegu mtaondoka nazo kila mmoja kwa wakati wake atanunua jogoo mwekundu halafu mida ya saa saba usiku utaenda upandikize kwa kutumia huu mchanga maji usimwagilizie itakuwa ni damu ya yule kuku kisha utahesabu siku saba utaenda kuangalia kama imeota angalizo nalo wapa usionekane na mtu yoyote yule.

Pia akatuambia baada ya siku saba ukikuta hazija ota usijisumbue kurudi kwangu maana mambo yako yatakuwa yamesha haribika mizimu itakuwa imekukataa sito weza saidia kitu chochote.......






Sent using Jamii Forums mobile app
Kwelii mlidhamiria si Kwa episode hizi duh!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daaaah
Oky Inaendelea..........

Basi wakati tuko pale kwa mganga akaendelea kutapa masharti na maelekezo tofauti tofauti huku akitusisitizia sana tufanye kama alivyosema pengine nilidhani labda anahofia umri tuliokuwa nao wakati ule.

Baada ya hapo alichukua kopo la tosi lililokuwa pembeni yake lilikuwa kuukuu akalifungua ndani kulikuwa na visu vya kuchongesha kienyeji yaani ni kipande kidogo cha mti halafu kimechomekwa kichuma flani hivi kwa mbele kama spoku ya baiskeli akatoa viwili akatugawia kila mtu kimoja

Akatuambia kabla hatujapanda mbegu lazima tumwage damu kwenye lile shimo lakini kuku yule hatutakiwi kumchinja kawaida inatakiwa tumtoboe toboe na kile kisu mfano wa bisibisi kuanzia kichwani hadi miguuni mpaka apoteze uhai kisha tupande mbegu tufukie .Mzoga wa yule kuku tukatupe njia panda tena inayopitwa na watu wengi

Basi akatusisitizia kuoga na zile dawa alizokuwa ametupatia kipindi cha nyuma pamoja na kunywa lakini tusioge kwenye bafu ambalo humo humo ni choo bora usubiri usiku ukaoga kibarazani. Kisha akatuambia baada ya lile zoezi kukamilika pesa ndio zitakuwa zinaangaika kututafuta na sio sisi kuziangaikia tena

Baada ya hapo akatutakia safari njema na mafanikio mema na kutuambia tutapata mafanikio kwa haraka na kabla mwezi hauja chomoza tumpelekee zawadi kama malipo yake kisha tukawaaga na wale masela pamoja na yule mkee wa mganga tukasepa.

Tukaenda getto tukawa tumetoa nguo tufue tukakuta majaa wasukuma vijana walikuwa na umri kama wa maika 25 hivi wako pale njee wanapiga story baada ya kupiga nao story ikabidi wafunguke eti kunajamaa wamemleta pale kwa mganga kulingana na tatizo lake wameambiwa usiku wapeleke mbuzi beberu waizike nzima nzima ili jamaa yao apate kupona.

Ilipofika usiku agustino ikabidi amcheki yule jamaa aliyetupeleka akamwabia tumemaliza kazi kesho tunapita kwake kumuaga sisi tunasepa basi usiku ule kila mmoja alitoa vitu vyote na nguo zote kwenye begi lake tukatanguliza kwanza yale madawa tuliokuwa tumepewa ndio tukapanga nguo kwa juu.

Kesho yake bila kupoteza muda tukaenda kwa yule jamaa tulishukia njiani akatufata na gari yake akatupeleka mpaka kwake tulipiga msosi wa nguvu kisha akaanza kutuambia kama mmesha toka kwa mganga kila kitu mmemaliza na kama mkifata alivyoelekeza maisha yenu yataenda kubadilika kabisa baadae akasema atutoe tukatembee kidogo mjini lakini wote tuligoma maana tulikuwa tumechoka balaa

Pia wote baada ya kutoka kwa mganga kila mtu alionekana hana furaha nafsini kwake kwani wakati niko njiani nilikuwa najiuliza hivi nitawezaje kwenda usiku saa 7 tena mimi peke yangu mahali nikachimba kishimo nikapanda mbegu kisha nikauwa kuku mwenyewe hivi nitaweza kweli

Kila muda akili yangu ilikuwa inavuta picha kwenye ule mtaa pale shuleni ni sehemu gani nitaweza fanyia kile kitendo lakini nilikuwa sipati majibu moyo unazidi kujaa hofu lakini nikawa nasema potelea mbali liwalo na liwe

Basi usiku tukaanza kujadiliana lakini jamaa yangu agustino anasema nikitu rahisi sana wale kisinipe mawazo basi mimi nikaamua kujilaza baadae story zikachange tukaanza kukumbushiana mdogo mdogo economics zile topic za mwanzo subject matter na demand n supply mimi kichwa kilikuwa kimesha haribika ila jamaa alikuwa anapenda masomo sijui hata ule moyo wa kukumbushana alikuwa anautoa wapi katika hali ile

Basi kesho yake asubuhi yule jamaa akatupeleka hadi stand kwa gari yake safari ikaanza kurudi kwenye getto la agustino basi ilituchukua zaidi ya masaa 9 mpaka kufika stand tukashuka nikamwabia agustino hapa tutafute boda boda maana mizigo sio mingi ni haya mabegi.

Laķini jamaa akaniuliza sii wewe unapitiliza hadi shuleni hostel daa nikamwabia shule bado hatujafungua na hivi vitu nilivyonavyo humu inatakiwa tufikie getto kwako siunajua form 6 hawajafunga wamebaki pale wakiniona nimefika wanaweza kunipora mizigi yangu basi jamaa akatoa 30000 akanipatia akaniambia lete begi lako nikampatia akaniambia tafuta wanapo uza kuku uchukue hata wa 13000 wawili kama mganga alivyosema mimi natangulia wewe utakuja nao

Basi mimi nikampatia begi langu nikaenda kutafuta kuku mjini nilizunguka nikawa nauliza hadi nikaenda kuwapata kwenye vibanda vya soko nikanunua wawili jumla 24000 basi nikamaliza nikachukua boda boda hadi getto kufika nikamkuta jamaa amechangamka kudeki nyumba basi nikaanza kutafuta kamba ya kufungia jamaa akaniambia kuna net iko chini ya uvungu imechakaa nichukue nikate nitoe kamba

Daa ile nimeinama nikaona matone ya damu ambazo ni mbichi chini ya uvungu asee roho ilitaka kupasuka lakini nilisema uchawi hauwendi kwa mentali nikatoa chandarua nikaanza kutengeneza kamba basi jamaa akafua fua baadhi ya mashuka tukapika msosi tukala tukaelekea shuleni kupiga story na wanaa waliokua hawajaenda likizo huku tukiacha kuku zetu pale njee.

Lakini mawazo yalinijaa kichwani zile damu zinatoka wapi na nini sababu baadae akaniambia turudi geto kabla giza halijazidi tuone nijinsi gani tutachora ramani ya kukamilisha ule mchezo usiku ule siku lala nikawa najiuliza maswali ni alama gani nitaweka kwenye aneo nitakalo panda mbegu zangu ili nisisahau kila sehemu naona haiwezekani

Kesho yake tukaanza survey mtaani njiani tunaulizana hivi pale pata faa basi baada ya kuzunguka sana mimi nikaona muembe mkubwa maeneo ya pale pale yaani ulikuwa ni mkubwa kama mbuyu nikamwabia jamaa yangu mimi nitafanyia pale baada tena ya pita pita yeye kasema ataenda pembeni ya mwamba mkubwa raia wa pale waga wanatumia kuanikia nafaka.

Basi kesho yake akaniacha asubuhi nimelala pale akasema anaenda kumuona pusha flani hivi wa bangi waongee biashara maana alimpigia simu akasema mzigo umeisha wakati najigeuza geuza kwenye kile kitanda nilisikia kama kuna sarafu basi nikaamua kuichukua lakini papasa mkono kumbe jamaa alikuwa ameishonea ndani ya godoro kwa ndani kabisa daa nikasema huyu baharia ni hatari

Baada ya muda nikawaza sana lakini roho ya ujasili iliniingia nikasema nikienda kwenye eneo la tukio kuku ndio mgumu kumuuwa nikasema nguvu zote nitawekeza Kwenye kuuwa kuku

Nilitoka pale kikafunga mlango nikaenda kutafuta kifungua kinywa kunamgahawa flani hivi nikakuta wapiga msuli tunao soma nao wanadiscus tu habari za masomo mara sijui integral sijui differentiation hawakwenda likizo basi baada ya kutoka pale nikarudi getto nikafungua begi kuaandaa zana ili usiku mimi nikamilishe kila kitu.

Nilitoka tena nikaenda pale chini ya muembe kufanya survey ikiwezekana niweke alama kabisa ya wapi nitafaanyia tukio pale chini ya muembe maana eneo la pale lilikuwa kubwa kama unavyojua maeneo ya kijiji ni majani majani marefu na matuta yaliyokuwa yamezunguka ule muembe basi nikabeba jiwe kubwa kiasi nikategesha pembeni ya ule muembe

Nikarudi getto nikamkuta agustino basi nikampanga kila kitu na yeye akaniambia leo usiki tumalize mchezo tukapiga mahesabu kuku tutafanyaje asipige kelele akaniambia tutatumia kamba za manila tuwazibe midomo basi.

Tulienda shuleni tukapoteza muda na wadau halafu tukaondoka tulaelekea kwa yule babu tukavuta bangi za kufa mtu siku hiyo tulipata hadi wanajeshi wanagwanda kabisa wanapuliza tukapeana high tukapiga vitu vyetu tukasepa tukarudi hadi getto kiukweli nilikuwa na ogopa kutoka saa 7 tena kila mtu na njia yake bora hata tungekuwa pamoja lakini baada ya kupiga zile ganja uoga ulipungua sana.

Tulikaa getto tukapiga story huku kuku tumezifunga kamba miguu kichwani na kwenye mabawa ilipofika saa 6 kama na dakika 50 kila mmoja akachukua tochi yake zile za sola udogo mbegu kisu na kuku akapitia njia yake njiani nilikuwa naogopa sana kwani kile kijiji watu wanasema ni mambo ya uchwawi ndio yanafanya kisiendele huku nikiwa nawaza au pale kwenye muembe mkubwa ndio huwa wachawi wa ule mtaa wanafanyai mkutano wao

Nilikuwa natembea haraka haraka huku nikiangalia nyuma tochi nilikuwa nimezima nilifatilia ramani hadi nikafika kwenye ule muembe haraka zangu nikataka nianze kuchimba kuaangalia kwenye ule mfuko niliokuwa nimebeba sioni kitu cha kuchimbia, kuku nilikuwa nimemuweka chini akaanza kutapa tapa nikasema ngoja niwashe tochi nitafute kijiti nianze kuchimba shimo kubwa kiasi ili wakati narudi nisije kupotea mahali nilipo panda mbegu.



Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom