Baada ya Wife kuniweka Lockup naona kama natengenezewa mazingira ya ku react nichukue hatua kali

Tulikuuliza sababu ya kumchapa makofi ukaficha kumbe ni picha za uchi! Duu pole huyo wala siwezi mtetea.
 
Hili nalo nenoπŸ˜ƒ, kabla hajatoa talaka aombe DNA πŸ’― Fanton Mahal pindua meza baba ukienda kwenye shauri la talaka omba DNA ya watoto
Hii maana yake nani atakua responsible kwenye hilo zoezi kuthibitsha watoto ni wangu?? Maana uliposema niombe DNA maana yake ni yeye atatakiwa kuthibitisha au ni mimi?
 
Pamoja chief. Ahsante
 
Mkuu kwanza hongera kwa ukimya na huu ukimya ndio unaomtesa,kikubwa mpe kila kitu hamna haja ya 50:50 kwa ajili ya watoto alafu jikatae usiwahi hata kumuona.
N.B:hawa viumbe hawapumzikagi had waone umeingia kaburini.
 
Hii maana yake nani atakua responsible kwenye hilo zoezi kuthibitsha watoto ni wangu?? Maana uliposema niombe DNA maana yake ni yeye atatakiwa kuthibitisha au ni mimi?
mahakamani utaambiwa uende ustawi wa jamii kuchukua kibali na utaratibu jinsi ya kupima na gharama zake ni laki moja kupima,ila muhimu kujiongeza kwa wale maafisa wa ustawi ili jambo liende kiuwepesi afu kama mkeo alikuchezea rafu lazima alete upinzani kwenye hilo jambo na lazima atajaribu kuhonga, embu mpe na yeye heka heka kidogo na ikiwezekana kabla ya mahakamani watafute maafisa wa ustawi wa jamii uongee nao kabisa then ukifika mahakamani katika kujieleza sema ya kwako na usikubaliane na talaka moja kwa moja we kazia kwanza kwenye DNA ili mnapoachana uwe na uhakika unahudumia damu yako kiroho safi. Natamani kungekuwa na voice note nikuhadithie kisa cha jamaa yangu jinsi alivyolea mtoto si wake na huyo mwanamke walikutana chuo mwaka wa pili sijui ndo kuzaa kumbe alibambikiwa mimba sasa kaja kupata safari ya marekani yani kuhamia huko pale ubalozi lazima watoto wapimwe DNA kujiridhisha ni watoto wake huwezi amini huyo mwanamke alikataa kabisa mwanae kupimwa DNA , ikabidi jamaa atumie mbinu mbadala dah majibu yanatoka sio mtoto wake.
 
USHAURI WA BURE KWENU NYOTE MLIOPO HAPA
Haijalishi kama mko kwenye ndoa au ni mahusiano ya kawaida, mpenzi wako akitamka kwamba HAKUTAKI, usilazimishe na usipoteze muda, kwa upole, kubali matokeo, mpe anachotaka na endelea na maisha yako. Kutamka maneno kama SIKUTAKI, NAOMBA UNIACHE, NIPE TALAKA YANGU, USINITAFUTE, USINIPIGIE SIMU, FUTA NAMBA YANGU, n,k yanatoka moyoni mwake na ana sababu zake kutamka maneno hayo, hivyo ukilazimisha kutaka kuwa naye, ataendelea 'kukukataa kwa matendo' yake na si maneno tena, na hayo matendo yatakutesa sana, kwa akili yake yeye ni kwamba, 'mimi nilishasema kwamba sikutaki' na likiharibika jambo tafsiri yake ni 'uliyataka mwenyewe'.

Ukishakaa mbali naye, jipe muda wa kukaa peke yako bila mahusiano mapya, jikite katika kujijenga wewe binafsi na maisha yako kwanza, usikimbilie kuanza mahusiano mengine, kuwa mwenyewe kwa muda jifanyie tathimini ya maisha yako, jiulize unachotaka maishani mwako na katika mahusiano badala ya kukurupuka na kukimbilia mahusiano mapya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…