JF na ndoto za alinacha!!! Million moja itoshe? ThubutuMstafu yoyote asipofanya chochote kwa hela zake,atazila mpaka kufa.Mfano Mama yangu alikuwa Mwalimu mafao yake alipata 92.5M na fedha ya kila mwezi anapata 500K.
Alisitafu na 55,ukiweka makadirio kuwa ataishi 25 yrs to come maana yake ataishi mpaka 80 yrs.Akisema atumie 92.5 kwa miaka hiyo 25 kila mwaka atatumia 3.7M wastani wa 308,000 kwa mwezi,fedha hii ukijumuisha na 500K anayopata kila mwezi maana yake kila mwezi atakuwa na kipato cha 800K.
Kwa mstafu anayeishi wilayani 800,000 ni hela nyingi sana,ukitegemea hana mtoto hata moja anamtegemea.
Of course hela ya kustaafu si hela ya kuchezea. Ni hela ya kununua Bond tu. Siye tulistaafu miaka 6 iliyopitaMtumishi una uwezo wa kukopeshwa na Benki Kwa dhamana ya mshahara
Lakini ukishaanzisha biashara, unakopea biashara yako pia
Ukisema usubiri Mtaji uupate baada ya kulipwa kiinua mgongo, lazima maisha yakuchakaze Mkuu
Tuchukue tahadhali
Pension pekee haitoshi, ndiyo maana tunashauri kuweza kujiongeza Kwa kufanya UwekezajiJF na ndoto za alinacha!!! Million moja itoshe? Thubutu
Mshindweeee!Hahaha................kuwa na imani na Wazee 😅
Wazee wa hovyo!Kuwa na huruma na Wazee 🤗
Mtakula wenyewe!Nimesikia hakuna chakula unapenda kama Makande si ni kweli Mjukuu
Ukija kutusalimia, nitamwambia Bibi yenu awapikie chungu kizima 😜
Unawazo zuri sana lakini shughuli unazopendekeza ni ngumu kwa wastafu hasa wa hali ya chini... Me mtendaji wa kijiji nikafungue kampuni ya kitalii? Au niwekeze mtandaoniSalaam,
Kila mtumishi aliyeajiriwa, akumbuke itafikia wakati atalazimika kustaafu kazi. Kustaafu huku inaweza kuwa ni kwa hiari ama kulazimishwa kutokana na Umri (Miaka 60 ama 65 kwa Wakufunzi wa Vyuo Vikuu) ama sababu za Ulemavu ama Maradhi yasiyotibika.
Kwa kujua huku kwamba kuna siku tutalazimika kustaafu na kupisha damu changa kwenye utumishi wetu, ndiyo maana inashauriwa kuanza kujiwekeza tangu tarehe ya kwanza unapokea mshahara wako wa kwanza.
Kama mnavyofahamu, Mtumishi akisha staafu, hunufaika na kulipwa kiasi cha 1/3 ya Mshahara wake aliokuwa anapokea wakati anastaafu. Mathalani ikitokea unastaafu ukiwa unapokea mshahara wa shilingi za Kitanzania 1,500,000 kwa Mwezi (Gross Salary) basi ukisha staafu utaanza kulipwa kiasi cha shilingi 500,000 tu hadi siku unaaga Dunia (Kufariki).
Pamoja na hilo, mtumishi huyu atalipwa kiiunua mgongo chake ambacho kwa kikokotoo kipya atalipwa 33% ya fedha zake za Mkupuo.
Kwa taarifa ambazo sio rasmi, watumishi wengi sasa wanapokea fedha zao za Mkupuo unao-range kati ya shilingi 25,000,000 hadi 200,000,000 kulingana na kiwango chako cha mshahara.
Kwa kutambua hili, napenda kuwasisitiza wastaafu watarajiwa, kuhakikisha mnajenga nyumba zenu za kuishi ukiwa bado upo kazini. Ili utakapolipwa fedha zako za kiinua mgongo, basi uzitumie kwenye shughuli nyingine lakini isiwe kujenga.
Kupitia andiko hili, tunaweza kupeana dondoo za aina ya miradi inayoweza kufanywa na Wastaafu ili kujikidhi na maisha yao ya baada ya kustaafu.
Kumbukeni, Uzee bila hela ni changamoto, utaanza kula kwa shida ya kukosa chakula, kukosa matibabu,kukosa sehemu nzuri ya kulala, kukosa hata fedha ya kwenda mapumziko ya Mwisho wa Mwaka. Anza kuwekeza sasa ili uepuke kutokupokelewa kwa simu zako, ukiwapigia Watoto wako, Ndugu,Jamaa na marafiki, bila kusahau kuepuka kuitwa Mchawi (Hakuna mtu mwenye kipato cha wastani/juu akaitwa Mchawi).
- Uwekezaji kupitia Kilimo Biashara; Ufugaji wa Nyuki,mazao ya chai, matunda, Ufugaji na Kuku wa Kisasa kwaajili ya Mayai na Nyama.
- Uwekezaji kupitia biashara ya Majengo(Real Estates); Biashara ya GuestHouses, Biashara ya kununua na kuuza viwanja, Nyumba za Kupangisha n.k
- Biashara mtandao ya kununua na kuuza iwe ni vifaa vya Umeme ama vya nyumbani
- Biashara kupitia Teknolojia; Kuna baadhi ni wataalamu wa Tehama kama vile Website development, Apps n.k. bila kusahau biashara ya fedha mtandao mfano Mpesa,Airtel Money,CRDB Wakala n.k.
- Unaweza kuwekeza kwenye Utalii, kwa kufungua kampuni ya Utalii (Safari Tours) n.k, hii ni kwa wale wanaofanya kazi sekta ya Utalii ama wengine wowote.
- Uwekezaji kupitia Usafirishaji; Iwe Uber/Bolt ama biashara ya kusafirisha mizigo ama parcels
- Uwekezaji kupitia Vituo vya Elimu, iwe ni daycare centers, Tuitions centers hii ni maalumu kwa Walimu n.k
- Kuwekeza kupitia huduma za afya iwe ni Maabara binafsi, maduka ya madawa, ama utoaji wa huduma tembezi ya kuwafikia wagonjwa majumbani (Mobile Health clinics)
- Uwekezaji kupitia Ujenzi; Unaweza kufanya uwekezaji kwa kujisajiri kama Local Fundi na kisha kuanza kuchukua tenda za Ujenzi wa Miradi ya Serikali ama Binafsi, wakati mwingine unaweza kufanya biashara ya kuuza vifaa vya Ujenzi (Hardwares), kiwanda cha kuzalisha tofali n.k
- Uwekezaji kupitia huduma za Kisheria (Kuanzisha Ofisi za Uwakili) n.k
- Kufungua kampuni za Ulinzi, kwa wale wenzetu walioajiriwa kwenye idara za Ulinzi na Usalama
Kila la Kheri Wazee na Wastaafu wenzangu watarajiwa
Humu sijabahatika Mzee mwenzangu, maombi yangu yote yamekuwa rejectedLakini mzee mwenzangu hujawahi kuniambia nani hasa anaufubaza moyo wako humu🤣🤣🤣au hutaki ijulikane ili uendelee kula mema ya jf🏃🏃🏃
Shukrani MkuuUnawazo zuri sana lakini shughuli unazopendekeza ni ngumu kwa wastafu hasa wa hali ya chini... Me mtendaji wa kijiji nikafungue kampuni ya kitalii? Au niwekeze mtandaoni
Hela huwa haitoshi ujue. Na gharama za uzee ni kubwa ajabu.Hongera sana Mkuu kuweza kustaafu na kuwekeza pia
Shukrani sana Kwa mchango wako MkuuHela huwa haitoshi ujue. Na gharama za uzee ni kubwa ajabu.
Jambo la msingi katika kujiandaa kustaafu ni pamoja na kuwafunza wategemezi wako kuwa hakuna urithi. Hakikisha kila mmoja ajifunze kujitegemea. Utapata shida sana iwapo kila mmoja anasubiri pension yako. Ukiwa na wategemezi au ndugu hata watoto wanauliza zitaingia lini, juwa chamoto unacho. Hata wewe binafsi, kama unasikilizia zitaingia lini, juwa kustaafu ni kugongwa na kitu kizito kichwani.
Imagine hata shemeji yako anayeoa dada yako anakuuliza lini utapokea pension yako.
Uanzishwaji wa miradi ni jambo jema isipokuwa kitu uaminifu ni tatizo kwa sasa.
Nipende kusema kuwa maisha hayana fomula, kama wengi hapa JF tunavyofikiria, after all hapa JF mwanamme anaanzisha nyuzi kuhusu wanawake wanavyojihisi wakati hajawahi kuwa kuwa mwanamke. Vijana wanaongelea maisha ya kustaafu wakati sasa hivi anatafuta ajira baada ya kutoka chuo, n.k.
Wewe unaweza kuyapenda!!! Aaah hapana jamani🤣🤣Usiniambie huyo Mpare ameshindwa kukushawishi kupenda Makande
Ila huyo Mpare ametushangaza sana, Siku ile ya harusi tulilishwa pilau/biriyani na Kuku Choma za kutoshaWewe unaweza kuyapenda!!! Aaah hapana jamani🤣🤣
Ni huzuni babu😭😭😭Ila huyo Mpare ametushangaza sana, Siku ile ya harusi tulilishwa pilau/biriyani na Kuku Choma za kutosha
Na alihaidi nawe Mjukuu, ungeenda kula hayo masotojo
Sasa hii ya kukulisha Makande ya Upareni hatukuitegemea 😜
🤣🤣🤣🤣 hunitakii mema babu!!Ila hata ungeolewa na yule Kijana wa Njombe, bado ungelishwa Makande
Useme Makande ya Njombe ungelishwa na Maparachichi 😜