Baadhi ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambavyo ni magodauni na magofu

Baadhi ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambavyo ni magodauni na magofu

..kwanza sio kweli kwamba ubinafsishaji haukuwa na tija.

..pili sio kweli kwamba ubinafsishaji uliua viwanda.

..tatu zoezi lilifanyika kwa muda mrefu na kulikuwa na muda wa kutafakari, kushauriana, na kupima matokeo.

..kwa maoni yangu, ubinafshaji ulichelewa kufanyika, matokeo yake tukawa tunabinafsisha viwanda vilivyokufa.

..Zipo taarifa kwamba wataalamu toka SWEDEN waliishauri serikali ya awamu ya kwanza kuendesha viwanda kwa ubia ili kuviokoa lakini wazo hilo lilikataliwa.
Naona unatetea mpaka unajichanganya. Uliyokubali kabla sasa unayakataa. Mnufaika wa huo utaratibu hatuwezi kubadilisha mawazo yake. Its impossible!
 
Hiyo siyo sababu ya uamauzi na utekelezaji hafifu namna ile bila kujali Taifa. Nikuulize swali, TANESCO ilikuwa inaliingizia nini Taifa? Kwanini hiyo hawakudhubutu basi kuibinafsisha?

..Tanesco sio sawa na kiwanda cha chibuku au tumbaku ndio maana mpaka leo haijabinafsishwa.
 
Naona unatetea mpaka unajichanganya. Uliyokubali kabla sasa unayakataa. Mnufaika wa huo utaratibu hatuwezi kubadilisha mawazo yake. Its impossible!

..tatizo lako unatoa statement za jumla-jumla na kusema uongo wakati mwingine.
 
Ni awam ya tatu ndio iliua kila kitu

..hapana.

..viwanda vilikuwa na matatizo tangu awamu ya kwanza.

..ndio maana kulikuwa na foleni za mkate wa boflo, sukari, unga wa sembe, mafuta ya kupikia, sabuni, etc.
 
Ni kweli kabisa. Mwalimu alijitahidi sana.. hata kama viwanda alivyopewa/uziwa vilikuwa tayari vimepitwa na wakati. Laiti kama Mwalimu angelijuwa kuwa alikuwa anaongoza watu wa aina gani, angeamua tu kula bata kama Mobutu

Mosi.. watz wa nyakati zile, kama walivyo wa sasa hawakuwa watu wa kupiga kazi.. walijaa uvivu tuuu, kulalamika na uzembe. Ili viwanda visonge mbele na kuzalisha faida, ilitakiwa mali ghafi. Katika sekta ya uzalishaji mali ghafi, mambo yaliharibika pindi mkoloni alipoondoka hususa baada ya Azimio la Arusha, 1967. Watz wakiwa na jembe la mkono huko mashambani na wengine wakiwa na elimu duni katika masuala mazima ya uchumi ea viwanda, hakuna cha maana ambacho kingefanýika. Ni uvivu kwa kwenda mbelee..
Baadaye ghafla chama kikashika hatam.. balaa la uharibifu likapanuka.. meneja wa kiwana cha Bucop anapewa amri ya kutoa milioni 30 kugharamia safari ya Kawawa mkoani Kagera, bila vielelezo wala nyaraka stahiki.. naye meneja anajiongezea zake milioni 5.. na kila mahala ilikuwa hivyo..
Kwa muktadha huo, uongozi wa wakati ule unapswa kulaumiwa sehemu kwa kushindwa kufuata miiko ya kiviwanda..
Ikawaje Waasia na waarabu wakavigeuza magodown? Ni uozo tu katika nchi.. Mh Ben (RIP) anarithi mahame/mapango wananchi waliopigika kisawa sawa.. wenye kaunafuu ni wahindi kwa vile wana uwezo wa kupata vijimikopo kutoka India.. ndo ikawa hivyo..

Kazi sana kuendeleza nchi ambako watu wake hawapendi kazi.. wanapenda kula kuliko kazi..
Hii dhana mpaka sasa ipo ila wamei dilute ukiwa na biashara kubwa kuletewa barua uchangie chama au mwenge hata kama sio mwanachama [emoji23][emoji23] tena barua rasmi toka wilayani na mhuri juu, nchi ina mambo ya ajabu hii, kama unahisi naongopa kipindi cha mwenge au ziara ya kiongozi wa chama kupigwa mzinga uchangie ndio zao sasa ole wako ukatae utaona cha mtema kuni mbona biashara utafunga [emoji3525]
 
Kinachosikitisha sana ni kwamba vimekaliwa na Waasia na matajiri wengine wenye asili ya kiarabu wakitumia kama ma Godown ya kuhifradhia bidhaa wanazoagiza kutoka nje ambazo wala hazifikii ubora wa zile zilizokuwa zinazalishwa na hivyo viwanda. Kwa maksudi kabisa ya kulihujumu Taifa.

Haya mambo yako wazi kabisa, wanasiasa wakiamua kuyafanyia uchunguzi ukweli wote utabainika na hatua stahiki kuweza kuchukuliwa. Hapo ndiyo pale baadhi ya viongozi walijaribu kufahamu nini kilichoko nyuma ya huo uhujumu uchumi, lakini wakaishia kukiri kuwa makaburi mengine ni hatari kuyafukua.

Hapo ikimaanisha kuwa kuna baadhi ya watu hapa nchini ambao wako juu ya sheria na HNi vingaapi "awagusiki!
Ni vingaapi kati yao "vimekaliwa na Waasia na matajiri wengine wenye asili ya kiarabu" ? Tuletee data kama unazo badala ya kutumia maneno ya kibaguzi ili kuficha ujinga
 
Aliyeruhusu ulaji wa chips yai ndiye aliyeharibu akili za WA Tanganyika.
 
Ni vingaapi kati yao "vimekaliwa na Waasia na matajiri wengine wenye asili ya kiarabu" ? Tuletee data kama unazo badala ya kutumia maneno ya kibaguzi ili kuficha ujinga
Wanaoelewa wameshanielewa, na kila uchao mambo yanazidi kudhihirika, matusi yako wala hayatabadilisha jambo. Ubaguzi si jambo ninaloliamini, ila inatosha kusema umekurupuka.
 
Back
Top Bottom