antimatter
JF-Expert Member
- Feb 26, 2017
- 47,274
- 126,778
Angalau hao siyo wanafiki, wanapombeka hadharani.View attachment 3189715
Gazeti la Mwananchi limeonyesha kabisa Waamini wa Kanisa la Mtakatifu Joseph Dar es Salaam wakinywa Konyagi Kanisani.
Haaa bwasheee, YESU ndio Njia ,Kweli na Uzima ,MTU haendi Kwa Baba Mungu bila kupita Kwa YESU.Leta ushahidi wakanisa lako likiwa limemfikisha muumin wake huko kwababa mungu
Ukristo halisi ukoje?Kwa wakatoliki unywaji wa pombe yoyote (hata gongo!) sio dhambi. Na wakatoliki wanajivunia kunywa pombe popote ikiwemo hata kanisani, wao wanasema wanakunywa kistaarabu.
Pale ukatolikini hakuna ukristo halisi, ni upagani wa Kiitaliano ulioboreshwa kwa tamaduni zilizoupokea ukristo wa kale na kuueneza duniani chini ya mwamvuli wa kanisa.
Mlio... tatizo kamdomoSiku nyingine jifunze kusoma Bible, ili ujifunze kutofautisha mambo.
Ulichokileta hapo siyo maagizo, hivyo jifunze kwa kutofautisha kati ya parables na instructions.
Ndiyo maana hauoni popote pale wakristu kuwahi kukitumia hicho kifungu sababu kwao siyo agizo.
Kingine, Mkristo kabla ya kuyafuata maandiko kichwakichwa, huwa anatakiwa kuushirikisha vyema ubongo wake na wakati mwingine hutakiwa kuomba ili aangaziwe kuweza kuyaelewa maandiko.
Mkristo akisoma maandiko, kabla ya kufuata hutakiwa kuangalia, mazingira, nyakati na hata utamaduni. Ndiyo maana Wakristo wanahimizwa kusoma na kutafuta maarifa
Hahahah Biblia ya Wakatoliki, Ina vitabu 72 ππ utasikia Sira, Sijui nani nani, vitabu vya kininadam vyenye Maneno yaloandikwa yoyote na WANADAM.
RC na maji ni kama mchagga na mbegeView attachment 3189715
Gazeti la Mwananchi limeonyesha kabisa Waamini wa Kanisa la Mtakatifu Joseph Dar es Salaam wakinywa Konyagi Kanisani.
kwa hiyo pia halisemi pia kuwa alikuwa rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi, au sio?Andiko hilo halihalarishi pombe, wala halisemi Yesu alikuwa mnywaji wa pombe, bali linatoa tafsiri ya maisha ya ujumla jumla ya Yohana vs Yesu.
nikweli nimeshuhudia kuna jirani yangu ni mkatoliki akiwa anaenda kanisani anapita vilabuni anakunywa pombe wakitoka anapita tena anakunywa pombe nilikuwa nafikiria sipati majibu leo nimepata ukweli nikama chanda na pete.Huyo mwandishi kilaza kweli kweli. Anachikuwa mafundidho anayodanganywa kwenye dini yake anadhani wakatoliki wapo hivyo?
Toka enzi na enzi pombe kwa mkatoliki ni sehemu ya chakula na lazima skibariki kala jajanywa kama chakula kingine. Iwe kanisani au sehemu yoyote kwenye sherehe. za wakatoliki pombe ni kiungo muhimu na hata kitimoto ( nguruwe) ndio nyama Yao pendwa na kubatilisha uongo unaohubiriwa na eahubiri uchwara kuwa ulinuwa pombe su Kila kiti moto utakuga haraka, hutakuwa na maendeleo, hitayenda mema nk .lakini kinyume chake makabila wanaokunywa pombe na Kila kitimoto wanaishije umri mrefu na Wana maendeleo makubwa na wanatenda mema Sana na hao wanaojifanya kuwa pombe na kitimoto ni dhambi wanawazunguka kueaomba msaada
Wewe mzima kweli, unayoyaandika tu yanaashiria ulishaamua ku left group kwa hiariMlio... tatizo kamdomo
Dini ya Uyahudi pombe ni sehemu ya ibada yao na chakula chao. Divai ni pombe siku zote, sio juice ya zabibu.Hivi unajua nuhu alizaliwa na aliishi katika tamaduni za kibagani japokuwa alisikia sauti ya Mungu ikimwambia atengeneze Safina na akatii? Hata unywaji wa pombe wa Nuhu haukuwa mpango wa Mungu na mwisho wa siku ulizaa aibu, laana na utukufu kwa shetani. Mungu hawezi kuruhusu jambo lenye kuzaa uovu katika maisha ya watu.
Kitamaduni za kiitaliano na ibada zao za kibagani zinaruhusu unywaji wa pombe popote pale, Ukristo wa kale ulipotua Italy uliingizwa katika falme zao na kuboreshwa ili kuweza kuchangamana na tamaduni za kibagani za kiitaliano na kutokea hapo ukaenezwa duniani kwa mwamvuli wa kanisa. Leo hii ndio tunauita ukatoliki.
Ukristo halisi na unywaji wa pombe wapi na wapi?
Yesu alibadilisha maji na kuwa divai (kinywaji) na sio divai (Pombe). Kwanini? Huwezi ukabadilisha maji yakawa pombe kwenye sherehe, halafu watu wote wakanywa mpaka kutosheka halafu hapo hapo tukio hilo limrudishie Mungu utukufu. Unywaji wowote wa pombe vya kutosha huzaa aibu, upotofu na utukufu wa shetani.
Lakini muujiza wa kwanza wa Yesu ulikuwa kubadili maji kuwa divai harusini Kana (tazama Yohana 2:1-11).Yesu hakuwa mlevi wala mnywaji wa pombe. Acha kumsingia uongo.
kwa hiyo pia halisemi pia kuwa alikuwa rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi, au sio?
Acha kuleta ujinga wako jukwaani. Hii pia sio ya kuleta jukwaa la siasa.Gongo?!
Hata hivyo 66 unavyoita vya Mungu ni subset ya vitabu 72 ambavyo Luther alivichukua kama vilivyo kwa Wakatoliki.Hahahah Biblia ya Wakatoliki, Ina vitabu 72 ππ utasikia Sira, Sijui nani nani, vitabu vya kininadam vyenye Maneno yaloandikwa yoyote na WANADAM.
Biblia ya Mungu Ina vitabu 66 tu.
Habari zote za Nuhu nimetoa kwenye biblia. Habari kamili za ukatoliki zipo kwenye vitabu na maandiko ya kikatoliki, kwa kuwa ukatoliki umejengwa katika maandiko tofauti tofauti, na sio lazima yawe maandiko ya kibiblia. Msingi mkuu wa ukatoliki upo kwenye mapokeo (matamko, maagizo, matangazo, mafundisho ya wakuu wa kanisa katoliki kule Italy)Dogo mimi nimeandika yaliyomo kwenye Biblia Takatifu. Wewe unaandika kwa hisia. Huoni tofauti hapo?
Hata ibada zao zinatumia kiswahili tofautiHahahah Biblia ya Wakatoliki, Ina vitabu 72 ππ utasikia Sira, Sijui nani nani, vitabu vya kininadam vyenye Maneno yaloandikwa yoyote na WANADAM.
Biblia ya Mungu Ina vitabu 66 tu.
Mathayo na Yohana ni miongoni mwa hivyo vitabu 66 vya Mungu au ni miongoni mwa vile vya kibadamu vya Wakatoliki?Biblia ya Mungu Ina vitabu 66 tu.
Ukristo halisi uko ndani ya Yesu pekee yake. Mfuatilie Yesu kupitia Biblia takatifu ndio utaujua ukristo halisi, na sio kufuatilia hizi hadithi za haya madhehebu mbali mbali.Ukristo halisi ukoje?
Sasa ndugu yangu Mungu mwenye Rehema atashindwaje kuwa na huruma na kiumbe chake alichokiumba mwenyewe na kukipa mzigo wa utashi? Mawazo, shida, chuki na misuguano mingine ya kibinadamu inahitaji walau mara moja moja nati zilegezwe; nyinyi wenzetu naona bado mnaishi kwa misingi ya agano la kale ambapo Baba muumba ilibidi awe mkali sana maana kumstaarabisha binadamu kwa mazingira ya jangwani sio kazi ndogoKwa wakatoliki unywaji wa pombe yoyote (hata gongo!) sio dhambi. Na wakatoliki wanajivunia kunywa pombe popote ikiwemo hata kanisani, wao wanasema wanakunywa kistaarabu.
Pale ukatolikini hakuna ukristo halisi, ni upagani wa Kiitaliano ulioboreshwa kwa tamaduni zilizoupokea ukristo wa kale na kuueneza duniani chini ya mwamvuli wa kanisa.
Waliookoka ni wale wanauza maji na udongo wa uzima?wale hawajaokoka, habari za wokovu wako mbali nazo, dhambi zimewajaa, kunywa pombe kwao ni kawaida na dhamiri zao haziwashitaki kuwa wanatenda dhambi kwa ulevi