Baba mtoto kanitelekeza

Baba mtoto kanitelekeza

Miaka minane uko na mlevi anaefukuzwa kazi kila siku
Halafu anakuomba muuwe kichanga muendelee na mapenzi yenu daa
Dunia hii kuna watu huwa hata ushauri wanaukataa na hawaulizi wazazi yaani wanakuwa vipofu wa mahaba

Kwa ushauri ukimpenda mtu ujue weaknesses zake kama yuko ok basi haraka aende kwa wazazi
Au huwa hamna wazazi?
Sio kwa ubaya ila ni vizuri kuolewa kuliko kukaa na mahusiana miaka kibao na sababu huwa sijui kwa kweli
Maisha mafupi sana haya kama unaona ana tabia za kishenzi piga chini songa mbele
Muwe mnashirikisha hata na mama zenu bila kuwaficha maana mama atakupa ushauri mzuri kuliko rafiki
 
Hongera sana Mkuu! Maisha lazima yasonge ..huyo achana nae we lea mtoto wako kama ndoa ipo ipo tuu…
Hongera sana wewe pambana kivyako kama ataamua kurudi utaamua mwenyewe ! Uzuri una kazi achana na mawazo ya kusema umetelekezwa….!
Hongera sana
 
Kuna vitu 3 nimevipata kwenye mada yako ambavyo vinasumbua sana waafrika na kuwafanya kuendelea kuwa maskini.

(a) Jamaa ana 36 mke ana 32 lkn bado wanajitafuta. Mpk mkajipate mngefikisha miaka 50. Hii ndiyo Afrika. Halafu utasikia kuna kuku anaongea eti life begins at 40.

2. Kigugumizi ulichokuwa nacho kwenye kufanya maamuzi ya kumuacha mlevi asiyejielewa na anayedanga na videnti vya chuo kimekuponza.

3. Kupata mtoto ni jambo jema. Lkn tuzingatie misingi na kanuni za kupata mtoto kutoka kwenye mbegu bora (mtu mwenye sifa bora). Hivi mwanao akija kuwa mlevi na asiye na msaada kwako utalalamika? Maana mtoto wako katika kwa baba mlevi, mzinzi na asiye na msimamo na maisha. Mtoto akiwa na tabia hizo utalaumu??
Duu…
 
Kuna vitu 3 nimevipata kwenye mada yako ambavyo vinasumbua sana waafrika na kuwafanya kuendelea kuwa maskini.

(a) Jamaa ana 36 mke ana 32 lkn bado wanajitafuta. Mpk mkajipate mngefikisha miaka 50. Hii ndiyo Afrika. Halafu utasikia kuna kuku anaongea eti life begins at 40.

2. Kigugumizi ulichokuwa nacho kwenye kufanya maamuzi ya kumuacha mlevi asiyejielewa na anayedanga na videnti vya chuo kimekuponza.

3. Kupata mtoto ni jambo jema. Lkn tuzingatie misingi na kanuni za kupata mtoto kutoka kwenye mbegu bora (mtu mwenye sifa bora). Hivi mwanao akija kuwa mlevi na asiye na msaada kwako utalalamika? Maana mtoto wako katika kwa baba mlevi, mzinzi na asiye na msimamo na maisha. Mtoto akiwa na tabia hizo utalaumu??
Hii ndio sababu kubwa inayonifanya niwe proud kuwa mbali naye. Ninaamini nikijitahidi kumlea Kwa msaada wa Mungu kuliko baba yake, itakuwa vema kwa ajili yake.
 
Nimependa hapo mwishoni ulivojifariji na kibendi chako, wanaume hatukosei wa kuzaa nao, ukiona tumelea mimba tumeuelewa mziki ujue unafaa kuwa maza hausi
 
Ana uhakika ila ni muoga sana wa maisha. Ni kawaida yake kuwapa wanawake zake dawa za kuua watoto Kwa kisingizio kuwa hana maisha. Aliwahi kuwa na mtoto mmoja ambaye hajui ada wala chakula. Kiufupi ni mtu asiyependa majukumu. Yeye anachojua ni pombe.
Na umedumu naye miaka 8 yote....na mimba ukabeba?
Hapo mkizaa mnatengeneza bond ambayo haifutiki....mtoto atawaunganisha mtake msitake
 
Umesema kakutelekeza maana yake alikuwa responsible kipindi fulani...sasa inawezekana kuna tabia zako bado zinamfukuza mbali na wewe,inawezekana uchumi wake haupo stable kwa kipindi hiki(ufumilivu huna)..kingine kutakuwa na mambo kadha ya kadha umeficha nyuma ya pazia...may be ulevi wake ulisababishwa na mamno yenu kipindi fulani,ukimkuta sasa hivi sio mlevi basi ujue we ulihusika kuwa chachu ya ulevi wake.

Na kama kweli ulikuwa unampenda ulifanya juhudi gani kama maombi,ushauri ya yeye kuachana ulevi...?

Nakutabiria from January atakutumia matumizi na pia nakushuri kama atahitaji mtoto wake mpatie maana umesema huna feeling naye tena.

Pia, ongera sana kwa kufanya maamuzi ya busara wa kumzalia mtoto.
 
Sio Kukaa tu, kukaa na kuchanua miguu hadi ujauzito akapata. Hawa wanawake bhn, hawajui nini wanataka kiukweli
Hakuna sehemu niliyosema ilikua Bahati mbaya mkuu. Siku hizi wanawake tunajitambua ila wanaume waliobaki Ni wachache mno.
 
Habarini?

Ninaomba nieleweke kwamba mimi si mgeni, nimekua nikisoma mijadala mbalimbali lakini leo nami nimewiwa nilete kisa changu ambacho ninaamini kwa namna moja au nyingine kitawasaidia watu kadhaa.

Mimi mwanamke wa miaka 32, nimeajiriwa mahala Fulani. Kiukweli, nilikua kwenye mahusiano Kwa muda mrefu sana tangu nikiwa chuo hadi hivi majuzi. Hali ya mahusiano yetu yalikua ya kusuasua mno. Leo mko poa, kesho majanga hali ambavyo ilinikatisha tamaa sana. Ingawa jamaa alinitamkia ndoa wakati Fulani lakini binafsi kwa tabia za jamaa, sikuona hata kivuli endapo tungefunga ndoa.

Mwenzangu kwanza ni mnywaji sana wa pombe kiasi kwamba mara kadhaa ilimletea shida kwenye ajira yake na alisimamishwa mara nyingi sana. Mbali na hiyo, ni mtu ambaye bado hajui anataka nini. Leo mtapanga hiki, kesho mtagombana muanze upya so mnakua mara kadhaa hakuna mtakachokamilisha.

Mara nyingine anadai anataka kuoa mtu wa kabila lake, mara anaweza kuanzisha mahusiano na vitoto vya chuo ingawa yeye ana 36 years.

Kwa mahusiano yetu ya miaka Zaidi ya nane, hatukuwai kujaliwa mtoto ingawa jamaa alinitamkia mara moja akisema ananiacha sababu simpi mtoto then baadaye akaomba msamaha na maisha yakaendelea.

Mungu si Athuman! Mwezi wa tano nilijigundua ni mjamzito. Nikamshirikisha mwenzangu ambaye hakuwa na furaha nayo kabisa. Akanishauri sana tutoe tukizingatia bado tunajitafuta and blablabla.

Kiukweli mimi nilifurahi mno nilipojigundua ni mjamzito. Hata wazo la kutoa sikua nalo kichwani. Niliamua moyoni hata kama jamaa ataamua kuondoka lakini priority ya kwanza ni mtoto wangu.

Kweli, jamaa alihangaika sana kunishawishi kutoa ili tuendeleze mahusiano (ambayo hayana dura) nikaamua kuweka msimamo wangu kwamba akijisikia kuondoka, aondoke ila mtoto kama lolote likitokea basi liwe limepangwa na Mungu ila sipo yeye. Aliamua kuondoka na wala sikujushughulisha naye kabisa.

Ninamshukuru sana Mungu kwa kunisaidia safari yangu ya ujauzito hadi sasa, hakuna kilichonisumbua. Kiukweli, nina furaha na amani zote, sielewi ni kwa nini. Nimejikuta natamani kuwaambia wanawake wenzangu, wasikubali kuendeshwa na wanaume wa namna hii ili kuendeleza mahusiano.

Focus na unachokichagua kwani hata ningetoa, sio kweli kwamba mahusiano yangeboreka, tena yangekua mabaya zaidi. Ninamshukuru sana na niwatakie jioni njema.
Mama Mtoto naona umekuja kunisema!

Karibu Burindi.
 
Aise
Habarini?

Ninaomba nieleweke kwamba mimi si mgeni, nimekua nikisoma mijadala mbalimbali lakini leo nami nimewiwa nilete kisa changu ambacho ninaamini kwa namna moja au nyingine kitawasaidia watu kadhaa.

Mimi mwanamke wa miaka 32, nimeajiriwa mahala Fulani. Kiukweli, nilikua kwenye mahusiano Kwa muda mrefu sana tangu nikiwa chuo hadi hivi majuzi. Hali ya mahusiano yetu yalikua ya kusuasua mno. Leo mko poa, kesho majanga hali ambavyo ilinikatisha tamaa sana. Ingawa jamaa alinitamkia ndoa wakati Fulani lakini binafsi kwa tabia za jamaa, sikuona hata kivuli endapo tungefunga ndoa.

Mwenzangu kwanza ni mnywaji sana wa pombe kiasi kwamba mara kadhaa ilimletea shida kwenye ajira yake na alisimamishwa mara nyingi sana. Mbali na hiyo, ni mtu ambaye bado hajui anataka nini. Leo mtapanga hiki, kesho mtagombana muanze upya so mnakua mara kadhaa hakuna mtakachokamilisha.

Mara nyingine anadai anataka kuoa mtu wa kabila lake, mara anaweza kuanzisha mahusiano na vitoto vya chuo ingawa yeye ana 36 years.

Kwa mahusiano yetu ya miaka Zaidi ya nane, hatukuwai kujaliwa mtoto ingawa jamaa alinitamkia mara moja akisema ananiacha sababu simpi mtoto then baadaye akaomba msamaha na maisha yakaendelea.

Mungu si Athuman! Mwezi wa tano nilijigundua ni mjamzito. Nikamshirikisha mwenzangu ambaye hakuwa na furaha nayo kabisa. Akanishauri sana tutoe tukizingatia bado tunajitafuta and blablabla.

Kiukweli mimi nilifurahi mno nilipojigundua ni mjamzito. Hata wazo la kutoa sikua nalo kichwani. Niliamua moyoni hata kama jamaa ataamua kuondoka lakini priority ya kwanza ni mtoto wangu.

Kweli, jamaa alihangaika sana kunishawishi kutoa ili tuendeleze mahusiano (ambayo hayana dura) nikaamua kuweka msimamo wangu kwamba akijisikia kuondoka, aondoke ila mtoto kama lolote likitokea basi liwe limepangwa na Mungu ila sipo yeye. Aliamua kuondoka na wala sikujushughulisha naye kabisa.

Ninamshukuru sana Mungu kwa kunisaidia safari yangu ya ujauzito hadi sasa, hakuna kilichonisumbua. Kiukweli, nina furaha na amani zote, sielewi ni kwa nini. Nimejikuta natamani kuwaambia wanawake wenzangu, wasikubali kuendeshwa na wanaume wa namna hii ili kuendeleza mahusiano.

Focus na unachokichagua kwani hata ningetoa, sio kweli kwamba mahusiano yangeboreka, tena yangekua mabaya zaidi. Ninamshukuru sana na niwatakie jioni njema.
Njoo tulee mtoto pamoja mama
 
Eti focus focus,, ya nk... Huyo soon anakuja kuomba msamaha ba hautachomoa, na ndio utakuwa mwisho wa hiyo focus
 
Mtoa mada
Ajira ulonayo na Mtoto visikudanganye,
Hili kosa ulofanya utalijutia sana maishani[emoji29]
 
Back
Top Bottom