Mkuu mtoa uzi kwanza pile kwa hayo maswaibu japo ni mambo ya kawaida kwa jamii ya sasa. Kuna mambo nahisi hayapo sawa kwako na kwake pia, kama ni kweli basi akiyarebisha au mkiyarwbisha, basi ataolewa.
1. Inawezekana anatafuta mtu wako hadhi yake kulingana na elimu, kazi na kipato chake. Na hii ndio maana anaangukia kwa watu wenye familia kwa maana kuwa anapowaona for the first time anaona wa hadhi yake, wana maisha, wana kazi nzuri pengine wana push ndinga za maana. Naamini kabisa anatobgozwa na watu wengi ila nadhani atakua ana evaluyna kuona huyu hapana. Kama ndivyo basi aelewe kuwa, asilimia kubwa ya hao anaosema hapana, ndio waowaji ila hawajajipata tu. Aamini kuwa ipo siku nao watajipata watakua kama hao waume za watu wanaomvutia.
2. Kuna uwezekana upo nae karibu sanaa kiasi kwamba watu anaowapata wanapata mashaka juu ya ukaribu wenu. Ni kawaida mtoto wa kike kuwa karibu na mama na kumshiriksha mambo ya siri kama haya ila si kawaida kwa mtoto wa kike ku share mambo ya ndaani kama haya na baba yake, hii ni kwa mujibu wa mila zetu watu weusi. Sasa kama umemfanya sana kuwa mtoto wa baba, basi wanaume anaowapata huamininkabisa kuwa wakimuoa kuna external force itakua inashiriki kuendesha familia ambayo ni wewe baba yake. Wanaume hupenda kutawala kwenye familia zao na sio kuwa na mtu mwingine mwenye kuendesha kwa mfano wa rimont. Yaani kuna uwezekana kuna mambo huwa wanazungumza kama wapenzi halafu binti anasema ngoja nitaongea na baba, sio kitu kibaya ila ikizidi inaleta wasiwasi wa huko mbele itakuaje nikimuoa. Kama hilo lipo basi mzee wangu ni la kurekebisha tu na mambo yatakaa sawa.
Pole tena mkuu. Sema msiwe na hafu kiasi hicho. Wewe ukiwa hivi na hofu kubwa kiasi hiki nani atamwambia kuwa usiogope mambo yatakua sawa?