Baba wa kambo jela kwa kumuambukiza mtoto UKIMWI kwa makusudi

Baba wa kambo jela kwa kumuambukiza mtoto UKIMWI kwa makusudi

Mbona adhabu ndogo sana, aisee nimetetemeka mimi kwa alichofanya huyo mzee.
 
Ikiwa nitazaa watoto wa kike kisha mama zao wakaenda kuishi kwa wanaume wengine na watoto lazima niwape semina ya kuishi na baba wa kambo ili wakwepe kufanyiwa vitendo vya kikatili na hao baba wa kambo. Kwanza wasiingilie ugomvi wa mama yao na mume wake, pili mahusiano ya mama yao na baba wa kambo yakiharibika hata kwa dakika moja watoroke haraka sana kwenda kwa bibi zao au kwa dada zangu hadi ugomvi wa mama yao na mume wake uishe na amani irejee. Mabinti zangu huko wanakoishi na mama zao wawaheshimu baba wa kambo wasijibizane nao ili kumsaidia mama yao. Ni bora wanawake wanaolewa wakiwa na watoto wawaache kwa bibi zao ili wakaanzishe familia mpya huko kwingine japo si vizuri kutenga watoto. Usalama wa watoto uzingatiwe katika mahusiano mapya kwa baba wa kambo
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mara imemuhukumu kwenda jela miaka saba Msirari Muhere (60) mkazi wa Wilaya ya Tarime baada ya kupatikana na hatia ya kumuambukiza ugonjwa wa Ukimwi mtoto wa miaka sita kwa makusudi.

Hukumu hiyo imetolewa mjini hapa leo Mei 31, 2023 na Hakimu Mkazi Mkuu mwenye mamlaka ya ziada ya kusikiliza mashauri ya Mahakama Kuu, Timoth Swai baada ya kuridhishwa na ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo.

Awali kesi hiyo ya jinai namba 7/2023 ilifunguliwa katika Mahakama ya Wilaya ya Tarime Juni 2021 na kutolewa humu Novemba 2022 ambapo hakimu wa mahakama hiyo ya Tarime aliamuru mshtakiwa huyo kulipa faini ya Sh200,000 au kwenda jela miaka mitano katika kesi hiyo iliyosajiliwa kwenye mahakama hiyo kwa namba 186/2021.

Kufuatia hukumu hiyo mshtakiwa huyo alilipa faini na kisha kuwa huru.

Hakimu Swai amesema kuwa kutokana na hukumu hiyo, Jamhuri ilikata rufaa Mahakama Kuu baada ya kutokuridhishwa na hukumu kwa maelezo ilikuwa kinyume cha Sheria ya Kuzuia Maambukizi ya Ukimwi namba 28 ya mwaka 2008.

"Sheria hii inatamka kuwa mtu yeyote atakayepatikana na hatia ya kusambaza Ukimwi kwa makusudi hukumu yake ni kifungo cha kati ya miaka mitano hadi 10 jela na hakuna chaguo la faini,"amesema.

Akitoa maelezo ya tukio hilo, hakimu Swai amesema kuwa mwaka 2018 Muhere alioa mke wa pili ambaye alikuwa na watoto watatu ambao aliamua kuishi nao pamoja na mama yao.

Amefafanua kuwa baadaye wanandoa hao waligombana hali iliyopelekea kutengana huku mwanamke huyo akiwaacha watoto wake watatu na baba yao huyo wa kufikia.

Ameongeza kuwa baadaye wanandoa hao walimaliza tofauti zao na kuanza kuishi tena pamoja kama mke na mume na kwamba baada ya muda mwanamke huyo aligundua kuwa mume wake aliwaambukiza watoto wake Ukimwi kwa makusudi.

"Ushahidi umeonyesha kuwa Muhere alichukua sindano na kunyonya damu kutoka kwa mtoto wa mke wake mkubwa ambaye alikuwa ameathirika kisha kuanza kuwadunga watoto wawili wa huyu mke wake wa pili na uchunguzi wa kitabibu umebaini kuwa kati ya hao watoto wawili mmoja wa kiume ameambukizwa ugonjwa wa Ukimwi," amesema.

"Muhere na mke wake mkubwa ni waathirika wa Ukimwi na binti yao alizaliwa na ugonjwa huo kwa hiyo baada ya kutofautiana na mke mdogo aliamua kumkomesha kwa kuwaambukiza watoto wake Ukimwi labda kwasababu hawakuwa wa kwake (Muhere) wa kuzaa," ameongeza.

Katika kesi ya awali jumla ya mashahidi sita walitoa ushahidi wao akiwemo mama pamoja na mtoto ambapo katika rufaa hiyo upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Mawakili wa Serikali, Felix Mshama na Joyce Matimbwi.

MWANANCHI
hivi kwanini hii tabia wanayo wazee???kuanzia 55+
 
Adhabu ya kijinga sana kwa kosa hilo. Nawaasa muwe makini sana na watu wa vijijini, ni wapumbavu sana.
 
Kwahiyo kawachoma sindano yenye damu yenye virusi watoto wote wawili ila aliyepata maambukizi ni mmoja.hii inawezekanaje?
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mara imemuhukumu kwenda jela miaka saba Msirari Muhere (60) mkazi wa Wilaya ya Tarime baada ya kupatikana na hatia ya kumuambukiza ugonjwa wa Ukimwi mtoto wa miaka sita kwa makusudi.

Hukumu hiyo imetolewa mjini hapa leo Mei 31, 2023 na Hakimu Mkazi Mkuu mwenye mamlaka ya ziada ya kusikiliza mashauri ya Mahakama Kuu, Timoth Swai baada ya kuridhishwa na ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo.

Awali kesi hiyo ya jinai namba 7/2023 ilifunguliwa katika Mahakama ya Wilaya ya Tarime Juni 2021 na kutolewa humu Novemba 2022 ambapo hakimu wa mahakama hiyo ya Tarime aliamuru mshtakiwa huyo kulipa faini ya Sh200,000 au kwenda jela miaka mitano katika kesi hiyo iliyosajiliwa kwenye mahakama hiyo kwa namba 186/2021.

Kufuatia hukumu hiyo mshtakiwa huyo alilipa faini na kisha kuwa huru.

Hakimu Swai amesema kuwa kutokana na hukumu hiyo, Jamhuri ilikata rufaa Mahakama Kuu baada ya kutokuridhishwa na hukumu kwa maelezo ilikuwa kinyume cha Sheria ya Kuzuia Maambukizi ya Ukimwi namba 28 ya mwaka 2008.

"Sheria hii inatamka kuwa mtu yeyote atakayepatikana na hatia ya kusambaza Ukimwi kwa makusudi hukumu yake ni kifungo cha kati ya miaka mitano hadi 10 jela na hakuna chaguo la faini,"amesema.

Akitoa maelezo ya tukio hilo, hakimu Swai amesema kuwa mwaka 2018 Muhere alioa mke wa pili ambaye alikuwa na watoto watatu ambao aliamua kuishi nao pamoja na mama yao.

Amefafanua kuwa baadaye wanandoa hao waligombana hali iliyopelekea kutengana huku mwanamke huyo akiwaacha watoto wake watatu na baba yao huyo wa kufikia.

Ameongeza kuwa baadaye wanandoa hao walimaliza tofauti zao na kuanza kuishi tena pamoja kama mke na mume na kwamba baada ya muda mwanamke huyo aligundua kuwa mume wake aliwaambukiza watoto wake Ukimwi kwa makusudi.

"Ushahidi umeonyesha kuwa Muhere alichukua sindano na kunyonya damu kutoka kwa mtoto wa mke wake mkubwa ambaye alikuwa ameathirika kisha kuanza kuwadunga watoto wawili wa huyu mke wake wa pili na uchunguzi wa kitabibu umebaini kuwa kati ya hao watoto wawili mmoja wa kiume ameambukizwa ugonjwa wa Ukimwi," amesema.

"Muhere na mke wake mkubwa ni waathirika wa Ukimwi na binti yao alizaliwa na ugonjwa huo kwa hiyo baada ya kutofautiana na mke mdogo aliamua kumkomesha kwa kuwaambukiza watoto wake Ukimwi labda kwasababu hawakuwa wa kwake (Muhere) wa kuzaa," ameongeza.

Katika kesi ya awali jumla ya mashahidi sita walitoa ushahidi wao akiwemo mama pamoja na mtoto ambapo katika rufaa hiyo upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Mawakili wa Serikali, Felix Mshama na Joyce Matimbwi.

MWANANCHI
Hii Kanda ya ziwa Ina matatizo, nasisitiza tu, hii Kanda Ina ukatili wa Hali ya juu yaani utu haupo kabsaaa
 
Sema huyo mama aliyeondoka akawacha watoto wadogo kwa baba wa kambo nae anakesi ya kujibu
 
Why huo mkoa kila siku unaongoza kwa visa vya kikatili hivi?yan kama sio binadam hakuna huruma,mtoto amekukosea nn?
 
Mnalalamikia Sheria ikiwa watunga Sheria ni akina musukuma na babu tale mnategemea nn? S
 
wangemdunga sindano zenye vimelea vya Gono na Bawasiri kwa pamoja
kisha wamfungie kwa room akojoe uji mzito mwaka mzima uku akijitia vidole kukuna mkvndv
 
30 michache sana, kama kweli amefanya hayo (hajasingiziwa), basi kifungo cha maisha jela ni haki yake.., yaani ingekuwa mimi huyo angekula shaba ya kichwa
Afungwe miaka 30 kwa gharama za nani? Kwa zuri lipi alilolifanya hata akatunzwe kwa muda wote huo?
 
Unatafuta kuhamisha mada kwa kuleta habari za gender?
Kwani ni gender gani hutumbukiza watoto vyooni au huchokonoa mimba?
Nitajie matukio ya kutumbukiza watoto chooni na kuchokonoa mimba nikutajie matukio yaliyofanywa na hiyo gender kwa mwezi mmoja tu.
 
Back
Top Bottom