Baba wa kambo jela kwa kumuambukiza mtoto UKIMWI kwa makusudi

Baba wa kambo jela kwa kumuambukiza mtoto UKIMWI kwa makusudi

Daah aisee matukio ya Watanzania ukiyasikia yanatisha sana wana Unyama huyo mnyama mwenyewe anasubiri mbali sana...
 
Sheria bado ni nyepesi mno.

Kwa muktadha huo atakaa gerezani kwa miaka minne na point. Wakati ukatili aliowafanyia watoto ni wa maisha.

Sheria inabidi iongezewe meno. 30 years at least.

Hata hiyo 30 bado ni midogo. Hapo irekebishwe iwe kifungo cha maisha, na itapendeza zaidi ikiwa ni kunyongwa mpaka kufa. Maana kafanya kwa makusudi.
 
Aiseee,
Hivi huwaga ni magonjwa ya Akili au Ukatili wa namna gani???

Mtoto wa miaka 6 kweli ????
Umaskini/ufukara,ujinga,hapa lazima ubongo ushindwe kufanya kazi vzr,unakuwa mtu asiyejielewa,
Unakuta tamaa,unakuwa katili,unaona kila mtu ndio kakusababishia hiyo hari,
Kwa wale tuliowahi kuvamiwa na vibaka,Hawa madogo Huwa hawana huruma,macho yao Huwa yamejaa chuki,kutokana na maumivu ya umaskini,kupoteza mwelekeo wa maisha,
Unakuta wameishakusaula kila kitu,cm,pochi,begi,viatu,lakini hawakuachi,unaachiwa ngeu!
Nikala mtama,tofauli likatua usoni,damu kibao,nikapata wenge,sauti haitoki,fahamu ziliporudi nilikimbia kama husein bolt!wakawa wananifata
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mara imemuhukumu kwenda jela miaka saba Msirari Muhere (60) mkazi wa Wilaya ya Tarime baada ya kupatikana na hatia ya kumuambukiza ugonjwa wa Ukimwi mtoto wa miaka sita kwa makusudi.

Hukumu hiyo imetolewa mjini hapa leo Mei 31, 2023 na Hakimu Mkazi Mkuu mwenye mamlaka ya ziada ya kusikiliza mashauri ya Mahakama Kuu, Timoth Swai baada ya kuridhishwa na ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo.

Awali kesi hiyo ya jinai namba 7/2023 ilifunguliwa katika Mahakama ya Wilaya ya Tarime Juni 2021 na kutolewa humu Novemba 2022 ambapo hakimu wa mahakama hiyo ya Tarime aliamuru mshtakiwa huyo kulipa faini ya Sh200,000 au kwenda jela miaka mitano katika kesi hiyo iliyosajiliwa kwenye mahakama hiyo kwa namba 186/2021.

Kufuatia hukumu hiyo mshtakiwa huyo alilipa faini na kisha kuwa huru.

Hakimu Swai amesema kuwa kutokana na hukumu hiyo, Jamhuri ilikata rufaa Mahakama Kuu baada ya kutokuridhishwa na hukumu kwa maelezo ilikuwa kinyume cha Sheria ya Kuzuia Maambukizi ya Ukimwi namba 28 ya mwaka 2008.

"Sheria hii inatamka kuwa mtu yeyote atakayepatikana na hatia ya kusambaza Ukimwi kwa makusudi hukumu yake ni kifungo cha kati ya miaka mitano hadi 10 jela na hakuna chaguo la faini,"amesema.

Akitoa maelezo ya tukio hilo, hakimu Swai amesema kuwa mwaka 2018 Muhere alioa mke wa pili ambaye alikuwa na watoto watatu ambao aliamua kuishi nao pamoja na mama yao.

Amefafanua kuwa baadaye wanandoa hao waligombana hali iliyopelekea kutengana huku mwanamke huyo akiwaacha watoto wake watatu na baba yao huyo wa kufikia.

Ameongeza kuwa baadaye wanandoa hao walimaliza tofauti zao na kuanza kuishi tena pamoja kama mke na mume na kwamba baada ya muda mwanamke huyo aligundua kuwa mume wake aliwaambukiza watoto wake Ukimwi kwa makusudi.

"Ushahidi umeonyesha kuwa Muhere alichukua sindano na kunyonya damu kutoka kwa mtoto wa mke wake mkubwa ambaye alikuwa ameathirika kisha kuanza kuwadunga watoto wawili wa huyu mke wake wa pili na uchunguzi wa kitabibu umebaini kuwa kati ya hao watoto wawili mmoja wa kiume ameambukizwa ugonjwa wa Ukimwi," amesema.

"Muhere na mke wake mkubwa ni waathirika wa Ukimwi na binti yao alizaliwa na ugonjwa huo kwa hiyo baada ya kutofautiana na mke mdogo aliamua kumkomesha kwa kuwaambukiza watoto wake Ukimwi labda kwasababu hawakuwa wa kwake (Muhere) wa kuzaa," ameongeza.

Katika kesi ya awali jumla ya mashahidi sita walitoa ushahidi wao akiwemo mama pamoja na mtoto ambapo katika rufaa hiyo upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Mawakili wa Serikali, Felix Mshama na Joyce Matimbwi.

MWANANCHI
Aaarrrgh!! 😫 What a nonsense!! Huyu mbuzi alistahili kifungo cha miaka 10, na siyo 7.
 
Nchi hii Kuna sheria nyingine zinatungwa mpaka unajiuliza hawa waliotunga walikuwa na akili kweli!?? Huyu anatakiwa kuhukumiwa kunyongwa kabisaa! Hivi huyo mtoto akikua akakutana na hii story halafu akalipa kisasi kwa kumuua huyu mhusika Kuna atakayekuja kumlaumu..!?? Huyu mtoto akikua atakuwa na Hasira mara 100 zaidi akimuona muhusika yupo nje. Tuna watunga sheria wa ajabu Sana nchi hii...
 
I wish ninge....
Unamnyofoa kiungo kimoja kimoja bila ganzi. Au unamtupa mbele ya fisi wenye njaaa wanamtafuna anajiona. Shetani ndani ya kiwili wili cha binadamu.
 
Ingewezekana angefungwa maisha, huwezi kumsababishia mtoto mdogo aanze kumeza ARVs kwa makusudi yake.

Huu ni uuwaji
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mara imemuhukumu kwenda jela miaka saba Msirari Muhere (60) mkazi wa Wilaya ya Tarime baada ya kupatikana na hatia ya kumuambukiza ugonjwa wa Ukimwi mtoto wa miaka sita kwa makusudi.

Hukumu hiyo imetolewa mjini hapa leo Mei 31, 2023 na Hakimu Mkazi Mkuu mwenye mamlaka ya ziada ya kusikiliza mashauri ya Mahakama Kuu, Timoth Swai baada ya kuridhishwa na ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo.

Awali kesi hiyo ya jinai namba 7/2023 ilifunguliwa katika Mahakama ya Wilaya ya Tarime Juni 2021 na kutolewa humu Novemba 2022 ambapo hakimu wa mahakama hiyo ya Tarime aliamuru mshtakiwa huyo kulipa faini ya Sh200,000 au kwenda jela miaka mitano katika kesi hiyo iliyosajiliwa kwenye mahakama hiyo kwa namba 186/2021.

Kufuatia hukumu hiyo mshtakiwa huyo alilipa faini na kisha kuwa huru.

Hakimu Swai amesema kuwa kutokana na hukumu hiyo, Jamhuri ilikata rufaa Mahakama Kuu baada ya kutokuridhishwa na hukumu kwa maelezo ilikuwa kinyume cha Sheria ya Kuzuia Maambukizi ya Ukimwi namba 28 ya mwaka 2008.

"Sheria hii inatamka kuwa mtu yeyote atakayepatikana na hatia ya kusambaza Ukimwi kwa makusudi hukumu yake ni kifungo cha kati ya miaka mitano hadi 10 jela na hakuna chaguo la faini,"amesema.

Akitoa maelezo ya tukio hilo, hakimu Swai amesema kuwa mwaka 2018 Muhere alioa mke wa pili ambaye alikuwa na watoto watatu ambao aliamua kuishi nao pamoja na mama yao.

Amefafanua kuwa baadaye wanandoa hao waligombana hali iliyopelekea kutengana huku mwanamke huyo akiwaacha watoto wake watatu na baba yao huyo wa kufikia.

Ameongeza kuwa baadaye wanandoa hao walimaliza tofauti zao na kuanza kuishi tena pamoja kama mke na mume na kwamba baada ya muda mwanamke huyo aligundua kuwa mume wake aliwaambukiza watoto wake Ukimwi kwa makusudi.

"Ushahidi umeonyesha kuwa Muhere alichukua sindano na kunyonya damu kutoka kwa mtoto wa mke wake mkubwa ambaye alikuwa ameathirika kisha kuanza kuwadunga watoto wawili wa huyu mke wake wa pili na uchunguzi wa kitabibu umebaini kuwa kati ya hao watoto wawili mmoja wa kiume ameambukizwa ugonjwa wa Ukimwi," amesema.

"Muhere na mke wake mkubwa ni waathirika wa Ukimwi na binti yao alizaliwa na ugonjwa huo kwa hiyo baada ya kutofautiana na mke mdogo aliamua kumkomesha kwa kuwaambukiza watoto wake Ukimwi labda kwasababu hawakuwa wa kwake (Muhere) wa kuzaa," ameongeza.

Katika kesi ya awali jumla ya mashahidi sita walitoa ushahidi wao akiwemo mama pamoja na mtoto ambapo katika rufaa hiyo upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Mawakili wa Serikali, Felix Mshama na Joyce Matimbwi.

MWANANCHI
Jamaa roho ya korosho
 
Akirudi uraiani ataendelea kuambukiza na wengine..

Hata huyo mama akapime...

Huyu Ni wa kumfunga maisha ..alime na kulala tu jela!
 
Lakini mama nae ana makosa na alaumiwe tena sana unaachaje watoto wadogo tena kwa baba wa kambi ihali mmegombana??
Baba mzazi tuu siwezi achia mtoto mdogo tukigombana sembuse baba wa kambo?? Kina mama tujitafakari pia
 
Huyo anafaa kunyongwa kabisa, hafai kuishi, hata huko gerezani anaweza kuwaqmbukiza wenzake kwa maksudi.
 
Back
Top Bottom