Informer
JF-Expert Member
- Jul 29, 2006
- 1,606
- 6,672
Mizengwe na fitna havikuanza baada ya Baba wa Taifa kuondoka madarakani. Hata wakati wake, wapo waliojaribu kuanzisha mizengwe na fitna za kisiasa. Tofauti ya wakati ule na huu wetu ni moja tu. Wakati wa Baba wa Taifa, mizengwe na fitna ilianzishwa na wapambe na makanda bila kumhusisha. Alipoigundua, aliikemea na kuikomesha. Wakati fulani alimwajibisha kada wake kipenzi (Sozigwa) alipogundua kuwa anawalazimisha watu kuchangia harambee ya ujenzi wa kanisa fulani huko Dodoma kwa kisingizio cha kumuunga mkono Baba wa Taifa.
Wakati wetu, wapanga mizengwe na fitna wanadiriki ama kuwahusisha wakuu wa mihimili au wanaanzisha mizengwe na fitna na hawawajibishwi. Mizengwe na fitna hizo, vinawachonganisha wakuu wetu na wananchi au hata kuwachafua kuwa wakuu ndio wamewatuma hao wafanya mizengwe na fitna. Imewapasa wakuu wetu kukemea mizengwe na fitna kwa namna ambayo haiachi mashaka kuwa wanahusika na mizengwe hiyo. "Mtu akiwatazama usoni ajue kuwa wanamaanisha wanachokikemea". Hii ni kwa sababu baadhi ya mizengwe na fitna ina sura ya kijinai, mingine inavunja katiba, na mingine inapungua viwango vya kimaadili. Kibaya zaidi, baadhi ya mizengwe na fitna vinafanyika ndani vyombo vyenye utakatifu wa taifa letu.
Katika kukemea na kujitenga na mizengwe hiyo, Baba wa Taifa daima alizingatia mambo matano:
1. Ikulu ni mahali patakatifu. Utakatifu wa Ikulu haukutokana na utakatifu wa Baba wa Taifa bali msimamo wa wazi kuwa yeyote atumikaye Ikulu na aendaye ikulu atatenda na kutendewa haki, si pungufu ya haki. Kwa muda mrefu na kwa nyakati tofauti wakati wa Mwalimu, Mzee Timothy Apiyo na John Rupia walikuwa kama makuhani wa madhabahu ya Ikulu. Chochote kinyonge na kisicho cha nuru hakikuhusishwa na Ikulu. Waliofuata waliiga mfano huu isipokuwa hawakuwa waangalifu katika uteuzi wa "makuhani".
2. Chama kilikuwa kisafi kuliko serikali na Mwalimu alilalamika kuwa matendo ya serikali yalikuwa yanakichafua chama. Msimamo wa kutenganisha chama na serikali ulilenga kukifanya chama kuwa mfano na kielelezo kwa serikali. Kivukoni, JKT na madarasa ya itikadi vililenga kutatua kasoro hii.
3. Pamoja na uwepo wa washauri wa rais, Mwalimu alipata ushauri wake wa msingi kutoka kwa watu wa kawaida. Aliwauliza wapishi, wafagiaji, wakulima shambani, wacheza bao, madereva, wanafunzi na waumini wa kawaida kanisani Butiama ikiwa waliuelewa ujamaa na Azimio la Arusha. Nyakati fulani alimwuliza hata mama yake mzazi. Hekima ya kweli imesheheni katika watu wa kawaida na ndio maana Mungu ameumba wengi mno. Jilindeni na chachu ya watu kutoka Jalalani hata kama elimu yao ni muhimu pia.
4. Mwalimu aliwasikiliza washauri wake rasmi kwa kila sekta bila yeye kuwashauri. Wakati mwingine alifanya kama utani na kukaa na kuwaita waje kumshauri na aliwasikiliza na kuwauliza maswali magumu baada ya kuwasikiliza. Matokeo yake, washauri wake walilazimika kuandika ripoti zao na kumpa mapema azisome. Alizisoma na kuzichafua kwa kalamu ili kuwaonyesha alipokuwa na mashaka.
5. Kwa sababu za kihistoria, Mwalimu aliona maadui wengi nje kuliko ndani. Maadui wa nje aliona ni mabeberu/mabepari. Maadui wa ndani aliona ni viongozi/vibaraka. Alitumia muda mwingi na timu ya mambo ya nje kutafakari matishio ya nje kuliko ya ndani. Hii ilimsaidia kuwatania watanzania aliowaita "waswahili" ambao aliona wanasumbuliwa zaidi na ushamba, ujinga, maradhi na umaskini. Kundi la pili la maadui wa taifa aliona ni viongozi vibaraka kuliko "waswahili".
Sikumbuki wakati wowote Mwalimu alipoona wananchi ni tatizo na kuwatungia sheria ya kuwadhibiti. Aliwakomalia viongozi ambao daima aliona wanataka kutumia ujinga wa wananchi ili kuwanyonya na kuwakandamiza.
Kutokana na misimamo hii ya Mwalimu, yafuatayo yalitokea:
1. Kuna watu walikufa wakaandika urithi wa mali zao kwa serikali au kwa chama tawala. Serikali na chama vilikuwa na hadhi sawa na dini.
2. Watu waliwekesha mali zao serikalini na kwenye chama. Watu walilaza magari yao kwenye viwanja na ofisi za TANU/CCM kuliko kuyalaza kanisani au msikitini.
3. Watu walipeleka mashauri yao TANU/CCM kuliko kuyapeleka mahakamani.
4. Kadi ya TANU/CCM ilikuwa na uzito kuliko passport au degree ya chuo kikuu.
5. Tulifuta ujinga kitaifa tukiwa na chuo kikuu kimoja, lakini hivi sasa tuna vyuo vikuu zaidi ya 50 ila tuna wajinga wengi!
Ukiona wazee kama mimi tuna kumbukumbu nyingi kuliko ndoto za kesho, ujue kuwa kuna jambo lisilo sawa. Kutukanwa ni halali yangu maana nimepitwa na wakati. Nikiitwa mzee mzima ovyo nitakuwa nimependelewa.
What went wrong? Nini kilienda mrama?
Wakati wetu, wapanga mizengwe na fitna wanadiriki ama kuwahusisha wakuu wa mihimili au wanaanzisha mizengwe na fitna na hawawajibishwi. Mizengwe na fitna hizo, vinawachonganisha wakuu wetu na wananchi au hata kuwachafua kuwa wakuu ndio wamewatuma hao wafanya mizengwe na fitna. Imewapasa wakuu wetu kukemea mizengwe na fitna kwa namna ambayo haiachi mashaka kuwa wanahusika na mizengwe hiyo. "Mtu akiwatazama usoni ajue kuwa wanamaanisha wanachokikemea". Hii ni kwa sababu baadhi ya mizengwe na fitna ina sura ya kijinai, mingine inavunja katiba, na mingine inapungua viwango vya kimaadili. Kibaya zaidi, baadhi ya mizengwe na fitna vinafanyika ndani vyombo vyenye utakatifu wa taifa letu.
Katika kukemea na kujitenga na mizengwe hiyo, Baba wa Taifa daima alizingatia mambo matano:
1. Ikulu ni mahali patakatifu. Utakatifu wa Ikulu haukutokana na utakatifu wa Baba wa Taifa bali msimamo wa wazi kuwa yeyote atumikaye Ikulu na aendaye ikulu atatenda na kutendewa haki, si pungufu ya haki. Kwa muda mrefu na kwa nyakati tofauti wakati wa Mwalimu, Mzee Timothy Apiyo na John Rupia walikuwa kama makuhani wa madhabahu ya Ikulu. Chochote kinyonge na kisicho cha nuru hakikuhusishwa na Ikulu. Waliofuata waliiga mfano huu isipokuwa hawakuwa waangalifu katika uteuzi wa "makuhani".
2. Chama kilikuwa kisafi kuliko serikali na Mwalimu alilalamika kuwa matendo ya serikali yalikuwa yanakichafua chama. Msimamo wa kutenganisha chama na serikali ulilenga kukifanya chama kuwa mfano na kielelezo kwa serikali. Kivukoni, JKT na madarasa ya itikadi vililenga kutatua kasoro hii.
3. Pamoja na uwepo wa washauri wa rais, Mwalimu alipata ushauri wake wa msingi kutoka kwa watu wa kawaida. Aliwauliza wapishi, wafagiaji, wakulima shambani, wacheza bao, madereva, wanafunzi na waumini wa kawaida kanisani Butiama ikiwa waliuelewa ujamaa na Azimio la Arusha. Nyakati fulani alimwuliza hata mama yake mzazi. Hekima ya kweli imesheheni katika watu wa kawaida na ndio maana Mungu ameumba wengi mno. Jilindeni na chachu ya watu kutoka Jalalani hata kama elimu yao ni muhimu pia.
4. Mwalimu aliwasikiliza washauri wake rasmi kwa kila sekta bila yeye kuwashauri. Wakati mwingine alifanya kama utani na kukaa na kuwaita waje kumshauri na aliwasikiliza na kuwauliza maswali magumu baada ya kuwasikiliza. Matokeo yake, washauri wake walilazimika kuandika ripoti zao na kumpa mapema azisome. Alizisoma na kuzichafua kwa kalamu ili kuwaonyesha alipokuwa na mashaka.
5. Kwa sababu za kihistoria, Mwalimu aliona maadui wengi nje kuliko ndani. Maadui wa nje aliona ni mabeberu/mabepari. Maadui wa ndani aliona ni viongozi/vibaraka. Alitumia muda mwingi na timu ya mambo ya nje kutafakari matishio ya nje kuliko ya ndani. Hii ilimsaidia kuwatania watanzania aliowaita "waswahili" ambao aliona wanasumbuliwa zaidi na ushamba, ujinga, maradhi na umaskini. Kundi la pili la maadui wa taifa aliona ni viongozi vibaraka kuliko "waswahili".
Sikumbuki wakati wowote Mwalimu alipoona wananchi ni tatizo na kuwatungia sheria ya kuwadhibiti. Aliwakomalia viongozi ambao daima aliona wanataka kutumia ujinga wa wananchi ili kuwanyonya na kuwakandamiza.
Kutokana na misimamo hii ya Mwalimu, yafuatayo yalitokea:
1. Kuna watu walikufa wakaandika urithi wa mali zao kwa serikali au kwa chama tawala. Serikali na chama vilikuwa na hadhi sawa na dini.
2. Watu waliwekesha mali zao serikalini na kwenye chama. Watu walilaza magari yao kwenye viwanja na ofisi za TANU/CCM kuliko kuyalaza kanisani au msikitini.
3. Watu walipeleka mashauri yao TANU/CCM kuliko kuyapeleka mahakamani.
4. Kadi ya TANU/CCM ilikuwa na uzito kuliko passport au degree ya chuo kikuu.
5. Tulifuta ujinga kitaifa tukiwa na chuo kikuu kimoja, lakini hivi sasa tuna vyuo vikuu zaidi ya 50 ila tuna wajinga wengi!
Ukiona wazee kama mimi tuna kumbukumbu nyingi kuliko ndoto za kesho, ujue kuwa kuna jambo lisilo sawa. Kutukanwa ni halali yangu maana nimepitwa na wakati. Nikiitwa mzee mzima ovyo nitakuwa nimependelewa.
What went wrong? Nini kilienda mrama?