Baba yake Mbowe kusaidia kudai Uhuru sio defence ya Mbowe kutofanya uhalifu, tutumie busara kujenga hoja

Mbowe kwa sasa ni mtuhumiwa. Kosa ni watu wanaohusisha msaada wa baba yake kudai uhuru na makosa yake. Kosa kubwa sana.
 
Sahihi kamanda uko sawa mahakama ziachwe zifanye kazi yake. Hakuna aliye na kinga.
 
Nyerere alisaidiwa na watu wengi tu kuna wengine walimasaidia mpaka sehemu ya kulala na kula mpaka nguo za kuvaa sasa unataka Mbowe apambane na rais aachwe kisa baba yake alikuwa anajuana la Nyerere
Rubbish
Si utoe mifano, kama nani, tunajua mtu aliyempa pesa na mali ni John Rupia, nyie wote uongo mtupu, mbowe hapo juu kaweka hadi picha, huyo mama kwanza hata uchungu wa Tanganyika haujui, si Mpemba huyo? Yeye na Mbowe nani big time??
 
Element za ubambikiaji zimewajaa wengine hivyo siii wa kuwashangaa Sana ni sehemu ya weledi wa kibongo.
 
Mbowe kwa sasa ni mtuhumiwa. Kosa ni watu wanaohusisha msaada wa baba yake kudai uhuru na makosa yake. Kosa kubwa sana.
Mkuu, hiyo haiepukiki! Kama mzazi wa Mbowe angekuwa alikuwa kibaka bado watu wangehusianisha! Vyovyote vile, kama historia ya familia yako inafahamika kwa mabaya au mema ukipatwa na jambo liwe baya au jema watu watahusianisha tu!
Mkuu, mbona hiki kitu ni cha kawaida sana?! Kwa nini ituume hivyo?! Sasa hapa umeandika kuwa ni kosa kubwa.....kweli?! Kwa sheria ipi mkuu?!
 
Rubbish
Si utoe mifano, kama nani, tunajua mtu aliyempa pesa na mali ni John Rupia, nyie wote uongo mtupu, mbowe hapo juu kaweka hadi picha, huyo mama kwanza hata uchungu wa Tanganyika haujui, si Mpemba huyo? Yeye na Mbowe nani big time??
Pointless
 
Gaidi ni ccm tumeona gaidi kutoka ccm likiuwa askari wetu wasio na hatia,halafu mnapakazia mbowe wakati magaidi wa kweli ni CCM
 
Wanaccm ni mara ngapi Mbowe amewekwa jela na Chadema iko palepale, hivi sasa mmemuweka ndani kisha mnakwenda kuhakiki kama chama kina mwenyekiti na msipomkuta ofisini mnaifuta Chadema kwa kukosa mwenyekiti! Mkishaifuta Chadema Tanzania itapaa kimaendeleo na kuwa dunia ya kwanza.
 
Nani mwanaCcm?
 
Mimi kwa mtazamo wangu Mbowe angejaliwa hekima angekuwa ameshaachana siasa kitambo tu. Maana hata madai ya kudai katiba mpya muda wake haujafika. Hatuwezi kudai katiba mpya huku chama chenye mlengo na maslahi mapana ya nchi ni kimoja. Kila chama cha upinzani kina mlengo finyu na kina maslahi ya kibaguzi. Nakubali CCM ina madhaifu lakini maendeleo ya nchi hayawezi kupatikana nje ya CCM. Hivyo basi inanidi CCM ijitathmini na ijipange upya na pia wapinzani wasiwe wabaguzi. Inabidi tuwe na chama cha upinzani ambacho kinaiwakilisha vyema nchi, chama cha upinzani ambacho maamuzi ya chama hayafanywi na mtu mmoja. Na viongozi wanawakilisha nchi na sio kanda flani ya nchi.Tukumbuke pia jamii nzima inaweza kukosea(the mob is not always right). Nahitimisha hivi, kwa mtazamo wangu huu sio muda sahihi wa kupata katiba mpya na kwa maslahi mapana ya nchi kijengwe chama pinzani chenye taswira ya chama tawala lakini malengo au mikikati endelevu mingine. Kwa mtanzania mwenye kuipenda nchi na kujua nini maana ya dola hawezi kusimama na kudai katiba mpya kwa sasa.
 
Picha hii ilipigwa mwaka gani? Inaonekana kama ni ya miaka ya hamsini hivi, umri wa Mbowe ni miaka mingapi kwa sasa.
Baba yake Mbowe alikuwa mtanzania wa kwanza kumiliki hoteli ya kitalii (SPLENDID) katikati ya jiji la Dar mahali ambapo lipo jengo la Extelecom mtaa wa Samora.
 
Yaani utadhani at maamuzi ya CCM huwa yanafanywa na watu wote. Wakati wa JPM si wote mlifyata mikia mkawa mnamsifia kwa kila kitu, mkawa mnaumizana wenyewe kwa wenyewe na kuchongeana, lile (JPM) lilikuwa dume lenu. Wakati wote wa Nyerere nani aliweza kubisha kitu? Mwongo mkubwa wewe, congenital liar
 
Pumbavu tena yawezekana aliyoyafanya Baba yangu ( Unsung Hero ) si tu kwa Tanzania yako hii bali hata Uganda, Rwanda, Burundi, Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibja ni makubwa na ya Thamani kuliko hata hayo aliyoyafanya Baba yake huyu Mbowe wenu.

Katika Sherehe Mbili Kubwa za Uhuru wa Uganda pale Kololo Kampala na ile ya Rwanda pale Amahoro Stadium na moja Afrika Kusini mbele ya Rais Mstaafu Kikwete Marais wa Uganda Museveni, wa Rwanda Kagame na wa Afrika Kusini wakati huo Mbeki walimpa Tuzo za Heshima ( Mzazi wangu ) pamoja na Wenzake akina Dkt. Salim Ahmed Salim, Hayati Rais Mkapa, CDF Mstaafu Jenerali David Bugozi Msuguri, Marehemu Brigedia Ngwilizi na Mzee Butiku kwa kujitoa Kwao Kuzipambania hizo nchi hadi leo hii kuwa Huru na Amani hii.

Dhumuni langu si kutaka Kujitapa hapa kwa aliyoyafanya Mzee wangu ( Baba yangu ) Mzazi kwani hayo ni machache mno yapo mengi isipokuwa nimesema haya ili Kutaka Kujibu kuwa Tanzania nzima si tu sijui Baba yake Freeman Mbowe ndiyo Kaipigania Tanzania bali wapo Wengine kwa Kushirikiana na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere hawakuipambania tu Tanzania bali hata nchi mbalimbali Barani Afrika.

Mpuuzi mkubwa Wewe!!!
 
Tupo wengi ambao babu zetu wameshiriki kwa karibu na mwalimu Nyerere kudai uhuru na mapicha picha yapo,na tukizingua sero zinatuhusu,kwa Mbowe isiwe ajabu sana.
 
Sasa hata kama hataki sifa wewe tu ungemtaja huyo baba yako hata kwa jina tu, kutokumtaja jina na kuongea bila evidence unataka tu kumdhalilisha tu Freeman Mbowe na wivu wako.
Pumbavu sina Shobo hizo au Ushamba huo ila Rais wako Mstaafu Kikwete na Hayati Mkapa bila kumsahau aliyekuwa Katibu Mkuu wa iliyokuwa OAU Dk. Salim Ahmed Salim wanamjua. Ndiyo alikuwa Mmoja wa Nyerere's Think Tanks katika Utawala wake.

Sina haja ya Kumtaja kwani haitokusaidia kivile ila aliyoyafanya kwa Tanzania yako hii na nchi nyingi za Barani Afrika ni ya Kishujaa na Kizalendo kweli kweli.

Na siandiki ( sijibu ) hivi kama labda Kujitapa kama ambavyo Wapumbavu wachache wa Mfano wako mnadhani bali imenilazimu kuja na haya ili kuonyesha ( kuwaonyesha ) kuwa wapo Watanzania wengi waliofanya makubwa na ya Thamani kwa Tanzania yetu hii kuliko hata huyo Baba yake Mzazi Freeman Mbowe.

Kwa Mfano kuna Mtu kama Nape Nnauye huyu nikiambiwa kuwa Baba yake Mzazi Brigedia Nnauye kafanya mengi na makubwa kwa Tanzania, Msumbiji na hata Afrika Kusini na anastahili Sifa kuliko Baba yake Mzazi Freeman Mbowe wenu nitakubali kwa 100%.

Tanzania ina Unsung Heroes wengi kuliko hawa mnaowasikia na bahati nzuri wenyewe huwa hawapendi Publicity bali wanafurahi kuona Tanzania walioipambania katika Mazingira magumu na ya Hatari leo iko hivi.

Nimemaliza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…