Baba yangu kachomwa nusu kaputi Jumatano hajazinduka mpaka leo, bado yupo ICU

Pole sana Manka, Mungu amuweke mahali pema peponi baba yetu!
 
Reactions: RWE
Oooh masikini pole my dia.May his soul rest in peace baba yetu mpendwa
 
jamani pole mkuu nimekuja kuuliza vipi .. alale kwa amani
 
Wapendwa Mungu kampenda zaidi baba yangu
Pole sana ndugu...Mungu akutie moyo wa ujasiri ili uweze kupita salama kipindi hiki kigumu. Hiyo ndiyo njia yetu sote, tunapishana muda tu. Pole sana Manka.
 
Pole Sana Mkuu, umoja katika familia Ni muhimu sana kama Mzee alivyowalea kwa nguvu zake Basi bakieni wamoja daima.
 
pole sana mkuu may his soul rest in peace kikubwa usimlaumu sana madaktari kwa yaliyowakuta mpeni sifa na utukufu Mungu wetu
 
Kwake tumetoka na kwake ndio marejeo yetu,

Pole sana kwa msiba mzito Manka.
 
Mungu ndiye mwenye enzi yote na mamlaka, madaktari nao humtegemea yeye maana ndiye mponyaji mkuu
 
Bwana ametoa bwana ametwaa jina lake lihimidiwe!!
 
Pole sana ndugu. Umenikumbusha mbali sana, mzazi mwezangu nyuzi zilifumka akiwa na mwezi amefanyiwa operation ya uzazi, damu zilikuwa nyingi, nafika hospital Dr. anaagiza apelekwe ICU, aisee nilikuwa nikiagizwa kifaa sijui nilikuwa natembea kama jini kuwahisha mahitaji. Mungu ni mwema atazinduka tu.
 
Oh men, thats so sad. Pole sana naomba kwa dhati Mungu awe mfariji wenu na kuwapa tumaini pole Sana Manka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…