Baba yangu kachomwa nusu kaputi Jumatano hajazinduka mpaka leo, bado yupo ICU

Baba yangu kachomwa nusu kaputi Jumatano hajazinduka mpaka leo, bado yupo ICU

Pole sana ndugu. Umenikumbusha mbali sana, mzazi mwezangu nyuzi zilifumka akiwa na mwezi amefanyiwa operation ya uzazi, damu zilikuwa nyingi, nafika hospital Dr. anaagiza apelekwe ICU, aisee nilikuwa nikiagizwa kifaa sijui nilikuwa natembea kama jini kuwahisha mahitaji. Mungu ni mwema atazinduka tu.

Mkuu huyu mgonjwa inasemekana ameshafariki
 
Wapendwa Mungu kampenda zaidi baba yangu

Pole sana ndugu. Umenikumbusha mbali sana, mzazi mwezangu nyuzi zilifumka akiwa na mwezi amefanyiwa operation ya uzazi, damu zilikuwa nyingi, nafika hospital Dr. anaagiza apelekwe ICU, aisee nilikuwa nikiagizwa kifaa sijui nilikuwa natembea kama jini kuwahisha mahitaji. Mungu ni mwema atazinduka tu.
Pole sana, niliposti pasipo kufahamu kama baba ameshatutoka!! Ni muda mgumu sana lkn pia ni muda ambao familia inatakiwa kuwa na mshikamano. Ni muda pia wanandugu wasio na imani kupenyeza imani za kishirikina na mwisho ni kuleta mtafaruku ndani ya familia. Sote tu mavumbi ndugu
 
Pole Manka.
Baba apumzike kwa amani kwa mapenzi yake MUUMBA.

Nasi tuliobaki atupe mioyo na subra atuepushe na fikra za kumsaka mchawi.
Wala asitokee miongoni mwetu wa kumnyooshea mtu kidoole. Na asitupungukie kitu kwenye uhitaji wetu.
AMEN
 
Aliye mpiga sindano ya nusu kaputi ni Daktari, Nurse au - kama tatizo lilikuwa,kwenye titi kwa nini apigwe sindano ya kumfanya apote fahamu kabisa badala ya kufanya sehemu ya titi tu ndiyo iwekwe ganzi na so mwili mzima.
This post values are outdated
 
Pole sana mkuu, kuna daktari mmoja aliwahi kuniambia kitaalamu kuna vipimo huwa vinatakiwa kuchukuliwa kabla mgonjwa hajachomwa sindano ya nusu kaputi ila madaktari wengi huwa hawazingatii hilo na inaweza kua na reaction mbaya kwa mgonjwa ila kwa sababu ni makosa yao hawawezi kukwambia. Kikubwa muombe mungu mkuu yeye ndo muamuzi wa kila jambo.

Ni kweli na hicho ndio kilicho tokea!! Wanadamu tuneumbwa tofauti, kuna wengine ukimpiga sindano ya penicillin inaweza kumletea reaction mbaya sana wakati mwingine kupoteza maisha, kuna wengine ukimpiga sindano ya kwinini anapoteza maisha, wengine seprin na dawa nyingine zenye sulphur nk.

Cha muhimu hapa wahusika walipashwa kufanya jaribio kwanza kabla ya kutumia dawa.
 
Huenda walizidisha kipimo cha nusu kaputi ila naamini atapata fahamu tu kama dawa bado inafanya kazi.
 
Pole sana, mungu akutie nguvu katika kipindi hiki kigumu
 
Apumzike kwa Amani. Poleni sana
 
mmh pole, au wamekosea vipimo, au kuna vipimo hawakufanya kabisa, kwanini asiamke baada ya operation?
 
Pole sana kuna vitu unpredictable huwa vinatokea, positively or negatively kama kwenye kazi nyengine yoyote, ndio maana kabla ya kupewa dawa ya usingizi mgonjwa husaini concert form, Mungu awape nguvu katika kipindi kigumu hata maandiko yanasema "usilaumu usije ukalaumiwa.."
 
Sisi sote tuliumbwa kwa udongo, tutaurudia udongo, lakini ipo habari njema kwamba siku moja waliolala wote wataamshwa
 
Jamani[emoji24][emoji24][emoji24]....
Mungu akutie nguvu ktk kipindi hiki kigumu...

Pia aipumzishe roho ya marehemu mahala pema..

Pole sana jamani,it hurts trully...
 
Back
Top Bottom