Ukikaa kwenye nafasi ya huyu bwana, huwezi kufikiri hivi aisee. Najua anayopitia, tuna kesi ya namna hii iko mahakamani tangu 2015, hukumu inatoka, inapingwa, inatoka, inapingwa, mnasogezwa juu na juu zaidi, wapi! Watu wanaanza kupoteza maisha, mvurugano moja kwa yote.
Na bora hawa kwamba mali za baba alizochuma na mama wote. Watu wanagombea mpaka maeneo ya mke mkubwa ambayo alipewa na wazazi wake kabla ya ndoa, mke mdogo na watoto wake wanayataka hayo pia!
Mtoa mada, kuna vyeti vya ndoa kwa wake wote wawili? Wakati wapili anaolewa, zipi ni mali zilikuwepo? Na zipi ni mali zilizokuja baada ya ndoa ya pili?
Kulikuwa na maelewano mazuri baina ya watoto wote kabla ya mzee kufa?
Choreni mstari, kuna wakati haya mambo myamalize kindugu, kijamaa na kijamii, mahakama haziondoi kila mgogoro na zaidi zinavunja vingi!
Mwisho wa siku, kila kitu kinatafuta na kama kiko kwenye mkondo wako kitakuja tu! Kisicho ridhiki hakiriki.