michael nyalusi
Member
- Jul 19, 2013
- 38
- 21
habari nilizozipata ivi punde zinasema babu seya kaachiliwa huru
naomba usibitisho jamani
==========
TAHADHARI: UVUMI SI WA KWELI
Picha inayosambazwa kwenye mitandao ni ya Oktoba 2013 wakati wakitoka Mahakamani pia tetesi hizi si za kweli.
Kilichosambazwa na blogs nyingi ni mipango yao wakifika uraiani kama watatoka kwa msamaha wa Raisi ikiwa na kichwa cha habari kisichoakisi maelezo ya ndani kuvutia wasomaji
naomba usibitisho jamani
==========
TAHADHARI: UVUMI SI WA KWELI
Picha inayosambazwa kwenye mitandao ni ya Oktoba 2013 wakati wakitoka Mahakamani pia tetesi hizi si za kweli.
Kilichosambazwa na blogs nyingi ni mipango yao wakifika uraiani kama watatoka kwa msamaha wa Raisi ikiwa na kichwa cha habari kisichoakisi maelezo ya ndani kuvutia wasomaji
![]()
Hivi sasa kuna taarifa zimesambaa kupitia Ujumbe mfupi wa simu (SMS) na mitandao ya kijamii zikihusisha kuachiliwa huru kwa wafungwa wawili wanaotumikia Kifungo cha Maisha gerezani. Wafungwa hao wanaotajwa ni Nguza Vicking(Maarufu kwa jina Babu Seya) na Johnson Nguza(Maarufu kwa jina la Papii Kocha).
Napenda kuufahamisha Umma wa Watanzania kuwa taarifa hizo zote zilizotolewa kupitia njia hizo ni za Uongo na uzushi mkubwa na zinalenga kuipotosha jamii kwani wafungwa hao wapo gerezani na wanaendelea kutumikia adhabu ya kifungo cha Maisha gerezani kwa mujibu wa Sheria.
Jeshi la Magereza nchini linatoa onyo kali kwa watu kujiepusha na uhalifu huo na linawataka wale wote wanaotumiwa ujumbe wa aina hiyo waepuke kuusambaza ujumbe huo kwa wengine bali waufute, kwani kuendelea kuusambaza ni kosa kisheria.
Aidha, Jeshi la Magereza linaendelea na uchunguzi wa kina ili kuwabaini wanaosambaza ujumbe huo likishirikiana na Vyombo vingine muhimu kwa lengo la kuwakamata wahalifu hao ili mkondo wa Sheria uchukue nafasi yake.
Imetolewa na;
Lucas Mboje, Mkaguzi wa Magereza,
Afisa Habari wa Jeshi la Magereza,
Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
DAR ES SALAAM.
Septemba 8, 2014.