Bado Km 51 ili Kigoma-Dar iwe lami. Rais Samia anaenda kuunganisha mikoa yote kwa lami

Bado Km 51 ili Kigoma-Dar iwe lami. Rais Samia anaenda kuunganisha mikoa yote kwa lami

Ukuu wa propaganda 🤣🤣 Onyesha Mikoa mliyounganisha na lami maana Samia atasema nilikuta Kigoma-Tabora hakuna lami nikaunganisha 😂😂

Na tuzo ya nini alipewa? wapi? na nani aliyempa? Na lini alipewa? Ebu chawa wa mama tujuze tujue tusiojua
Tuzo ipi aliyopewa na n
 
Utakuwa unaishi Canada.Nyie mlikuwa mnaishi Kwa propaganda za Mwendazake.

Sasa Kwa taarifa Yako Barabara zifuatazo ni vumbi tupu.

Kigoma-Tabora
Mpanda-Sumbawanga
Kigoma-Mpanda
Morogoro -Songea
Mbeya-Tabora
Mbeya-Singida
Arusha-Musoma
Arusha-Simiyu
Njombe-Morogoro via Ifakara.
Mtwara-Masasi via Tandahimba
Morogoro -Lindi
Kigoma-Kagera

Hiyo ni Baadhi tuu ya Barabara kuu za Mikoa kwa Mikoa ambazo zimejaa mavumbi au Baadhi ya vipande Bado ni mavumbi.
Kigoma-Tabora ndiyo hiyo inazungumziwa hapo. Hiyo hesabu ni lami tayari; Mpanda-Kigoma ni lami; Mpanda Sumbawanga ni lami. Upande wa barabara Serikali imepiga hatua kwa kweli!
 
Kigoma-Tabora ndiyo hiyo unazungumzia hapo. Hiyo hesabu ni lami tayari; Mpanda-Kigoma ni lami; Mpanda Sumbawanga ni lami. Uoande wa barabara Serikali imepiga hatua kwa kweli!
We mbumbumbu acha kuongeza takataka zako.Mimi Niko Kigoma Sasa sijui unaongea nini.

Sikiliza hata video basi kama kuambiwa huelewi
 
20230215_120116.jpg
 
Mambo ya kijinga sn, miaka 62 ya uhuru bado tunahangaika kuunganisha mikoa kwa lami badala ya kuunganisha kata kwa lami
 
Bangi unayovuta itakua imeanza kukupalia, kipande cha barabara cha kuanzia kasulu hadi kakonko na hicho kipande cha kuelekea tabora vilianza kujengwa na magufuli, huyo bibi chaudele amekuja kuendelea na kazi aliyo anazisha mwamba hata kama ulikua unamchukia mwamba usimsee uongo
 
S
Tukiwaambia kwamba hakuna alichofanya Cha maana Mwendazake kwenye Barabara za lami wakati wa Uongozi wake muwe mnaelewa.

Imagine Hadi Leo hii huwezi fika Kigoma bila kutembea kwenye mavumbi na hali Iko hivyo kwenye Mikoa Mingi sana.

Sasa kipele kimepata mkunaji ambao km 51 zilizosalia zinaenda kukamilika kabla ya desemba 2024 hivyo Kigoma-Dar itakuwa lami.Kazi hii ya kutukuka anaifanya Rais Samia.

View attachment 2764695
View attachment 2764700

BADO KM 51.1 KUUNGANISHA TABORA-KIGOMA KWA LAMI

IMEELEZWA kuwa bado kilomita 51.1 ili kuunganisha mikoa ya Tabora na Kigoma kwa barabara ya lami na hivyo kuandika historia ya aina yake nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya alipokagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Tabora- Kigoma sehemu ya Kazilambwa-Chagu yenye urefu wa KM 36 na Malagarasi-Ilunde-Uvinza KM 51.1.

“Kwa kweli nimeridhika na kasi ya ujenzi sehemu ya Kazilambwa-Chagu yenye urefu wa KM 36 ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 99”, amesema Eng. Kasekenya.

Naibu Waziri huyo amemtaka mkandarasi STECOL Cooperation Ltd anayejenga sehemu ya Malagarasi-Ilunde-Uvinza KM 51.1 kufanya kazi usiku na mchana ili kuandika historia ya kuunganisha mikoa ya Tabora na Kigoma kwa lami mapema iwezekanavyo.

Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Kigoma Eng. Narcis Choma amesema ujenzi huo umefikia asilimia 45 na watamsimamia kikamilifu mkandarasi ili maeneo yanayoweza kuathiriwa na mvua yakamilishwe mapema ili kuepuka visingizio na kuwawezesha wasafiri na wasafirishaji wa mikoa hiyo kunufaika na barabara ya kisasa.

Zaidi ya shilingi bilioni 62.7 zinatumika katika ujenzi huo ambazo ni matapo ya ndani na mkopo nafuu kutoka mifuko ya OPEC na Abu Dhabi.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Kasekenya amemtaka Mbunge wa Urambo Mhe. Margareth Sitta kuhamasisha wananchi wa jimbo hilo kulinda miundombinu inayojengwa katika jimbo hilo ikiwemo taa na alama za barabarani ili kuepusha ajali na kuendana na kasi ya Serikali ya kupendezesha barabara nchini.

“Tunawajengea barabara na mzunguko wa kisasa round about ili kupunguza ajali eneo lililokuwa na kona kali na kutengeneza taswira nzuri ya Urambo hivyo hakikisheni miundombinu hii inalindwa na kuendelezwa kwani inatumia fedha nyingi za Serikali “, amesisitiza Naibu Waziri Kasekenya.

Kwa upande wake Mhe. Margareth Sitta ameishukuru Serikali kwa uwekezaji mkubwa wa miundombinu ya kisasa katika wilaya ya Urambo na kuahidi kutoa elimu kwa wananchi kuthamini uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali ili kuchochea maendeleo ya wananchi.

View: https://youtu.be/wmpjkZkgfR4?si=PuPssK4vU2XqJbXx

Nawakumbusha tuu mradi ulianza tarehe 7/10/2021 baada ya Rais Samia kuingia madarakani,hakuna Cha Mwendazake kuanzisha na blaa blaa kama hizo,huku section ya kwanza Kigoma-Malagarasi alijenga JK

View: https://youtu.be/MfRWwiENKz8?si=S4TOiH1TvwP7NTKs

Sema serikali. What.is samia by the way?
 
Back
Top Bottom