Bado ni kitendawili waliofaidi mabilioni ya Justine Kasusura

Bado ni kitendawili waliofaidi mabilioni ya Justine Kasusura

2

Bado ni kitendawili waliofaidi mabilioni ya Justine Kasusura



Justine Kasusura akitoka katika jengo la Mahakama kuu jijini Dar es Salaam ambapo rufaa yake ya kwanza ilisikilizwa na kutupwa.



Muktasari:

Kiasi cha fedha alichodaiwa kupora, staili aliyotumia na ukubwa ambao tukio hilo lilipewa na vyombo vya habari kumelifanya lisifutike kirahisi kwenye kumbukumbu za wengi.

Kwa miezi 12 baada ya Ijumaa ya tarehe 2 Agosti, 2001, hakuna jina lililotawala vyombo vya habari kama la Justine Kasusura, aliyedaiwa kupora dola za Marekani milioni mbili (Sh4.4 bilioni) bila kutumia nguvu kubwa.

Kasusura aliyekuwa ameajiriwa na kampuni ya ulinzi ya Knight Support alidaiwa kupora fedha hizo muda mfupi baada ya kuzipokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) akiwa njiani na mfanyakazi mwenzake kuelekea benki ya Citibank.

Kiasi cha fedha alichodaiwa kupora, staili aliyotumia na ukubwa ambao tukio hilo lilipewa na vyombo vya habari kumelifanya lisifutike kirahisi kwenye kumbukumbu za wengi.





Hadi kesi dhidi ya Kasusura aliyekamatwa miezi mitano baada ya tukio inamalizika, Jeshi la Polisi lilidai kuambulia Sh256,000 tu mikononi mwake.

Kutopatikana fedha hizo kumeacha fumbo. Ni wapi fedha hizo zinazotosha kumlipa mkandarasi atakayejenga upya miundombinu ya eneo zima la Jangwani ziliishia? Ni nani hasa waliofaidi fedha hizo?


Uporaji ulivyotekelezwa

Tukio zima lilianza hivi; asubuhi ya tarehe 2 Agosti 2001, Kasusura na mfanyakazi mwenziwe, Said Hamisi, walioajiriwa na Knight Support walielekezwa na meneja wa kampuni hiyo aliyeitwa Doren kwenda Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam kupokea mzigo na kuupeleka katika benki ya Citibank katikati ya jiji la Dar es Salaam.

Kama ilivyokuwa kawaida ya kampuni hiyo, Kasusura, aliyeajiriwa kama dereva, alikabidhiwa bastola na risasi kadhaa huku mwenzake akikabidhiwa simu ya mkononi ili kufanikisha mawasiliano.

Safari kutoka makao makuu ya Knight Support iliyokuwa eneo la Victoria ilianza vizuri. Wakiwa njiani kuelekea uwanja wa ndege walisimama mara moja tu kujaza mafuta.

Wakiwa uwanja wa ndege, walikutana na maofisa wa kampuni ya Dahaco iliyoshughulika na mizigo ya kutoka nje ya nchi. Baada ya mazungumzo mafupi majira ya saa nne asubuhi Kasusura aliitwa na kusaini nyaraka kadhaa kabla ya kukabidhiwa mzigo walioufuata.

Kasusura aliuweka mzigo huo nyuma ya nyuma ya gari hilo aina ya Toyota Hilux Double Cabin lililofunikwa pande zote na kufunga kwa ufunguo. Wakati wakiondoka, Kasusura alimfahamisha Doren kwa njia ya simu kuwa walikuwa wakiondoka uwanjani hapo na kwamba aliweka mzigo huo nyuma ya gari na kufunga kwa ufunguo.

Walipotoka eneo la uwanja wa ndege, waliona gari likiwa limeegeshwa pembeni mwa barabara. Kasusura alikwenda moja kwa moja na kuliegesha gari akiendesha mbele ya gari hilo aina ya Toyota Land Cruser.

Hapa Kasusura alimweleza mfanyakazi mwenzake kuwa “biashara imekwisha” na kumtaka afungue boksi walilopokea uwanja wa ndege huku akimwelekezea bastola.

Alipoona mwenzake anasuasua, Kasusura alichukua funguo na simu ya mkononi kutoka kwa mwenzake na kuchukua ule mzigo akisaidiwa na watu wengine wawili waliokuwa kwenye gari walilolikuta pale.

Baada ya Kasusura na wenzake kutoweka na wenzake, Hamis aliomba msaada na kuripoti tukio hilo kituo cha Polisi Stakishari.


Taifa lashtuka

Siku iliyofuata aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Alfred Tibaigana aliutangazia umma tukio la uporaji wa fedha za Citibank.

Alisema tayari askari walikuwa wamejipanga kila kona ya nchi kumsaka mhalifu huyo, huku akiwaambia kutoa taarifa endapo watamwona au watahisi uwepo wake mahali popote.


Kasusura akamatwa Mbeya

Miezi mitano ilipita bila Kasusura kukamatwa. Habari zake ziliendelea kutawala vyombo vya habari

Taarifa za uwepo wa Kasusura mkoani Mbeya zilitolewa na msiri wa polisi.

Akiwa nyumbani kwake majira ya saa tatu usiku tarehe 24 Disemba 2001, Inspekta wa Polisi Richard Tadei alipokea taarifa kuwa katika nyumba ya kulala wageni ya Three in One iliyoko eneo la Soweto mkoani Mbeya alikuwapo mhalifu hatari aliyekuwa akitafutwa na polisi.

Baada ya kufanya ufuatiliaji na kujiridhisha kuwa mtu aliyekuwa akiishi katika hoteli hiyo alikuwa Kasusura, Inspekta Richard aliandaa askari wenzake na kuweka mtego wa kumnasa Kasusura.

Bila kujua siku zake zinahesabika, usiku wa manane siku ya mkesha wa Krismasi ya tarehe 24 Desemba, 2001, Kasusura aliingia kwenye chumba chake namba 101k hotelini hapo akiambatana na mwanamke.

Alipofungua mlango alikutana na askari ambao tayari walikuwa wamejificha sehemu mbali mbali ndani ya chumba hicho. Wengine walikuwa wameizingira hoteli. Alipofungua tu mlango, Kasusura alijikuta akiangukia mikononi mwa askari.

Ushahidi uliotolewa mahakamani na nyaraka nyingine zinaonyesha Kasusura alikutwa na Sh256,000 tu baada ya kupekuliwa.


Haikuwa mara ya kwanza kukamatwa

Kabla ya kukamatwa Kasusura, uvumi ulisambaa kuwa Kasusura amewahi kukamatwa mara kadhaa lakini amekuwa akiponyoka mikononi mwa polisi kwa nguvu ya fedha.

Taarifa hizo zilizidi kuvuma kiasi cha kumuibua hadharani aliyekuwa mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Omar Mahita na kutangaza kuwa askari watano walikuwa wakihojiwa kwa tuhuma za kumkamata na kumwachia Kasusura.

Siku chache baadaye aliyekuwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, Adadi Rajabu, alitangaza kufukuzwa kazi kwa askari wote waliotuhumiwa kumkamata na kumwachia Kasusura.


Ashtakiwa Kisutu

Tarehe 7 Januari, 2002 Kasusura na wenzake sita walishtakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam katika kesi ambayo ilivuta hisia za watu wengi.

Walishtakiwa kwa kosa la kula njama, unyang’anyi wa kutumia silaha, wizi na kupokea mali ya wizi.

Ahukumiwa

Ijumaa ya tarehe 30 Machi, 2007, Hakimu Mkuu Mfawidhi Sivangilwa Mwangesi ambaye sasa ni jaji wa Mahakama ya Rufani alimhukumu Kasusura kifungo cha miaka 35 jela kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha na wizi. Pia, alihukumiwa kuchapwa viboko 12.


Mahakama Kuu yatupa rufaa yake

Mara tu baada ya kuhukumiwa, Kasusura alikata rufaa Mahakama Kuu kupinga kutiwa hatiani na kufungwa. Mwezi Juni, 2010, Jaji Thomas Mihayo alitupilia mbali rufaa hiyo ikidai haikuwa na hoja za kutosha kuishawishi kutengua uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu.

Kutupwa kwa rufaa yake hakukumkatisha tamaa. Juni 4, 2015, Kasusura alikata rufaa ya pili katika Mahakama ya Rufani huku akiwasilisha sababu tisa kwa nini anapinga kifungo dhidi yake.


Ashinda rufaa

Tarehe 3 Mei, 2016 Mahakama ya Rufani ilikubaliana na hoja za Kasusura kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilikosea kumhukumu miaka 30 jela.

Ilisema wakati akidaiwa kutenda kosa hilo mabadiliko ya Sheria ya Kanuni ya Adhabu yanayoelekeza kifungo cha miaka 30 kwa mtu anayetiwa hatiani kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha yalikuwa hayajaanza kutumika. Mahakama ilikubali hoja ya Kasusura kuwa maelezo yake ya onyo alimodaiwa kukiri kosa yalipokelewa mahakamani kinyume cha utaratibu uliowekwa na Sheria Mwenendo wa Makosa ya Jinai. Mahakama iliona maelezo ya onyo ya Kasusura yalikuwa batili kwa kuwa yalirekodiwa baada ya muda wa kisheria kupita.

Kasusura alikamatwa tarehe 24 Disemba, 2001 lakini maelezo yake yalichukuliwa tarehe 26 Disemba, 2001.

Mahakama pia ilikubaliana na Kasusura kuwa kushindwa kwa upande wa mashtaka kuwaita maofisa wa benki ya Citibank waliokuwa wamiliki wa mzigo ulioibwa kulileta shaka kubwa kuhusu aina na kiasi cha fedha zilizokuwa ndani na mzigo huo.

Uamuzi wa kuwachia Kasusura ulitolewa na majaji Mbarouk Mbarouk, Sauda Mjasiri na Semistocle Kaijage ambaye sasa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Ni nani aliyefaidi mabilioni yaliyodaiwa kuporwa na Kasusura? Si Kasusura wala Jeshi la Polisi wameweza kujibu swali hili miaka 20 tangu tukio hilo litokee.
 
Nimeisahau hii kesi..hivi hukumu yake ilikuwaje‽
Hukumu ya kwanza alifungwa miaka 35, wakili akakata rufaa mahakama kuu akapewa miaka 30, baadae Kasusura akaingia front mwenyewe bila Wakili akakata rufaa mahakama ya rufaa na kuorodhesha vipengele 9 ikiwemo kukosekana shahidi upande wa pesa zilizoibwa yaan bank ya Citibank, hivyo mahakama ya rufaa ikamuachia huru, hapo alikua ameshatumikia jela miaka 15,

Hajafa yupo hai isipokua mke wake ndie alikufa kipindi kesi bado mbichi na aliomba akamzike mahakama ikamkatalia,

Credit: Michuzi Blog
 
Mtu kama huyu Kasurura ni kwamba hakuwa smart, sema dodo lilimdondokea akashindwa kucheza kama pele....

Waafrika wengi weusi hatujui kucheza na pesa vilivyo hasa tunapo piga tukio, wazungu, waarabu, wachina na hawa wasomali hapa afrika akiotea dodo ni ngumu sana kumkamata though wanaintelejensia wao wapo vizuri sana kwenye kuwasachi.

Tukio umepiga miezi kadhaa unaenda guest bubu na kimwana asee hii ni hollshit alafu unaenda lewa na kurudi chakariii, haya ndiyo yale ya Hushpupy yaani he caughted red handed na pesa kibao.

Pesa kwa mtu mweusi haijifichi kabisa showoff na blabla kibao..... bilioni 4.4 za mwaka 2001 yaani nimefanikiwa kutokomea niambia ndugu yangu mwaminifu anichimbie Andaki langu kabisa [emoji16]

Ikishindikana kuchimbiwa Andaki najibadilisha mwonekano wote kabisa, yaani napita hapo JNIA na mkinijua lazima mtoke jasho.
Kama i was Christian i must be a muslim......change the full identities....ndevu za bandia, kama ni mweusi najikoboa kuwa white, milioni $2 si mchezo.
Ishu ukiiba pesa na kufanikiwa kutokomea kama mwamba hapo inatakiwa u stay low key uwe mvumilivu hata miaka ipite ndio uanze ku spend....

Sio mda wa kulewa ni mda wa act upo choka mbaya unalima vibarua mashamban huko had joto lipoe
 
Ishu ukiiba pesa na kufanikiwa kutokomea kama mwamba hapo inatakiwa u stay low key uwe mvumilivu hata miaka ipite ndio uanze ku spend....

Sio mda wa kulewa ni mda wa act upo choka mbaya unalima vibarua mashamban huko had joto lipoe
Kwamba ulikuwa mwenyewe? Hio pesa lazima ushiriki na watu na mgawane
 
Ishu ukiiba pesa na kufanikiwa kutokomea kama mwamba hapo inatakiwa u stay low key uwe mvumilivu hata miaka ipite ndio uanze ku spend....

Sio mda wa kulewa ni mda wa act upo choka mbaya unalima vibarua mashamban huko had joto lipoe
Yaani una kibunda kinono umekisunda harafu ujitese hivyo inahitaji moyo wa chuma aisee.
 
Hukumu ya kwanza alifungwa miaka 35, wakili akakata rufaa mahakama kuu akapewa miaka 30, baadae Kasusura akaingia front mwenyewe bila Wakili akakata rufaa mahakama ya rufaa na kuorodhesha vipengele 9 ikiwemo kukosekana shahidi upande wa pesa zilizoibwa yaan bank ya Citibank, hivyo mahakama ya rufaa ikamuachia huru, hapo alikua ameshatumikia jela miaka 15,

Hajafa yupo hai isipokua mke wake ndie alikufa kipindi kesi bado mbichi na aliomba akamzike mahakama ikamkatalia,

Credit: Michuzi Blog
Na unajua kwanini Citibank waligoma kwenda mahakamani kutoa ushahidi?

Wao walipaswa kuwa washitakiwa no 1 kwakuwa walivunja utaratibu wa kuhamisha pesa (IMT) International Money transfer act

Hizo pesa zilipaswa kuhamishwa kupitia BOT ama kwa kibali maalum cha serikali kupitia BOT lakini Citibank wakafanya uhuni kwa nia ya kukwepa tozo, kodi na kamisheni za serikali
Jela kuna kila aina ya ujuzi na elimu.. Kasusura baada ya kulijua hili alishikilia hapo hapo
 
Hukumu ya kwanza alifungwa miaka 35, wakili akakata rufaa mahakama kuu akapewa miaka 30, baadae Kasusura akaingia front mwenyewe bila Wakili akakata rufaa mahakama ya rufaa na kuorodhesha vipengele 9 ikiwemo kukosekana shahidi upande wa pesa zilizoibwa yaan bank ya Citibank, hivyo mahakama ya rufaa ikamuachia huru, hapo alikua ameshatumikia jela miaka 15,

Hajafa yupo hai isipokua mke wake ndie alikufa kipindi kesi bado mbichi na aliomba akamzike mahakama ikamkatalia,

Credit: Michuzi Blog
Napenda mwanaume anayejiamini kama hivi....!
 
Kasusura alikamatwa na mzigo wa kutosha, akapelekwa kote alikokuwa kahifadhi mzigo, washkaji wakatembea nao kwa maelekezo maalum
Wale wote waliofykuzwa kazi bila kushtakiwa inasemekana walipata mgao wa kutosha sana

Kuna mmoja mtani wangu.. Au basi[emoji1544][emoji1544][emoji1550]mdomo koma!
 
Jumapili January 17 2021

Kwa miezi 12 baada ya Ijumaa ya tarehe 2 Agosti, 2001, hakuna jina lililotawala vyombo vya habari kama la Justine Kasusura, aliyedaiwa kupora dola za Marekani milioni mbili (Sh4.4 bilioni) bila kutumia nguvu kubwa.

Kiasi cha fedha alichodaiwa kupora, staili aliyotumia na ukubwa ambao tukio hilo lilipewa na vyombo vya habari kumelifanya lisifutike kirahisi kwenye kumbukumbu za wengi.

Kwa miezi 12 baada ya Ijumaa ya tarehe 2 Agosti, 2001, hakuna jina lililotawala vyombo vya habari kama la Justine Kasusura, aliyedaiwa kupora dola za Marekani milioni mbili (Sh4.4 bilioni) bila kutumia nguvu kubwa.

Kasusura aliyekuwa ameajiriwa na kampuni ya ulinzi ya Knight Support alidaiwa kupora fedha hizo muda mfupi baada ya kuzipokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) akiwa njiani na mfanyakazi mwenzake kuelekea benki ya Citibank.

Kiasi cha fedha alichodaiwa kupora, staili aliyotumia na ukubwa ambao tukio hilo lilipewa na vyombo vya habari kumelifanya lisifutike kirahisi kwenye kumbukumbu za wengi.

Hadi kesi dhidi ya Kasusura aliyekamatwa miezi mitano baada ya tukio inamalizika, Jeshi la Polisi lilidai kuambulia Sh256,000 tu mikononi mwake.

Kutopatikana fedha hizo kumeacha fumbo. Ni wapi fedha hizo zinazotosha kumlipa mkandarasi atakayejenga upya miundombinu ya eneo zima la Jangwani ziliishia? Ni nani hasa waliofaidi fedha hizo?

Uporaji ulivyotekelezwa

Tukio zima lilianza hivi; asubuhi ya tarehe 2 Agosti 2001, Kasusura na mfanyakazi mwenziwe, Said Hamisi, walioajiriwa na Knight Support walielekezwa na meneja wa kampuni hiyo aliyeitwa Doren kwenda Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam kupokea mzigo na kuupeleka katika benki ya Citibank katikati ya jiji la Dar es Salaam.

Kama ilivyokuwa kawaida ya kampuni hiyo, Kasusura, aliyeajiriwa kama dereva, alikabidhiwa bastola na risasi kadhaa huku mwenzake akikabidhiwa simu ya mkononi ili kufanikisha mawasiliano.

Safari kutoka makao makuu ya Knight Support iliyokuwa eneo la Victoria ilianza vizuri. Wakiwa njiani kuelekea uwanja wa ndege walisimama mara moja tu kujaza
Mafuta

Wakiwa uwanja wa ndege, walikutana na maofisa wa kampuni ya Dahaco iliyoshughulika na mizigo ya kutoka nje ya nchi. Baada ya mazungumzo mafupi majira ya saa nne asubuhi Kasusura aliitwa na kusaini nyaraka kadhaa kabla ya kukabidhiwa mzigo walioufuata.

Kasusura aliuweka mzigo huo nyuma ya nyuma ya gari hilo aina ya Toyota Hilux Double Cabin lililofunikwa pande zote na kufunga kwa ufunguo. Wakati wakiondoka, Kasusura alimfahamisha Doren kwa njia ya simu kuwa walikuwa wakiondoka uwanjani hapo na kwamba aliweka mzigo huo nyuma ya gari na kufunga kwa ufunguo.

Walipotoka eneo la uwanja wa ndege, waliona gari likiwa limeegeshwa pembeni mwa barabara. Kasusura alikwenda moja kwa moja na kuliegesha gari akiendesha mbele ya gari hilo aina ya Toyota Land Cruser.

Hapa Kasusura alimweleza mfanyakazi mwenzake kuwa “biashara imekwisha” na kumtaka afungue boksi walilopokea uwanja wa ndege huku akimwelekezea bastola.

Alipoona mwenzake anasuasua, Kasusura alichukua funguo na simu ya mkononi kutoka kwa mwenzake na kuchukua ule mzigo akisaidiwa na watu wengine wawili waliokuwa kwenye gari walilolikuta pale.

Baada ya Kasusura na wenzake kutoweka na wenzake, Hamis aliomba msaada na kuripoti tukio hilo kituo cha Polisi Stakishari.

Taifa lashtuka

Siku iliyofuata aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Alfred Tibaigana aliutangazia umma tukio la uporaji wa fedha za Citibank.

Alisema tayari askari walikuwa wamejipanga kila kona ya nchi kumsaka mhalifu huyo, huku akiwaambia kutoa taarifa endapo watamwona au watahisi uwepo wake mahali popote.

Kasusura akamatwa Mbeya

Miezi mitano ilipita bila Kasusura kukamatwa. Habari zake ziliendelea kutawala vyombo vya habari

Taarifa za uwepo wa Kasusura mkoani Mbeya zilitolewa na msiri wa polisi.

Akiwa nyumbani kwake majira ya saa tatu usiku tarehe 24 Disemba 2001, Inspekta wa Polisi Richard Tadei alipokea taarifa kuwa katika nyumba ya kulala wageni ya Three in One iliyoko eneo la Soweto mkoani Mbeya alikuwapo mhalifu hatari aliyekuwa akitafutwa na polisi.

Baada ya kufanya ufuatiliaji na kujiridhisha kuwa mtu aliyekuwa akiishi katika hoteli hiyo alikuwa Kasusura, Inspekta Richard aliandaa askari wenzake na kuweka mtego wa kumnasa Kasusura.

Bila kujua siku zake zinahesabika, usiku wa manane siku ya mkesha wa Krismasi ya tarehe 24 Desemba, 2001, Kasusura aliingia kwenye chumba chake namba 101k hotelini hapo akiambatana na mwanamke.

Alipofungua mlango alikutana na askari ambao tayari walikuwa wamejificha sehemu mbali mbali ndani ya chumba hicho. Wengine walikuwa wameizingira hoteli. Alipofungua tu mlango, Kasusura alijikuta akiangukia mikononi mwa askari.

Ushahidi uliotolewa mahakamani na nyaraka nyingine zinaonyesha Kasusura alikutwa na Sh256,000 tu baada ya kupekuliwa.

Haikuwa mara ya kwanza kukamatwa

Kabla ya kukamatwa Kasusura, uvumi ulisambaa kuwa Kasusura amewahi kukamatwa mara kadhaa lakini amekuwa akiponyoka mikononi mwa polisi kwa nguvu ya fedha.

Taarifa hizo zilizidi kuvuma kiasi cha kumuibua hadharani aliyekuwa mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Omar Mahita na kutangaza kuwa askari watano walikuwa wakihojiwa kwa tuhuma za kumkamata na kumwachia Kasusura.

Siku chache baadaye aliyekuwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, Adadi Rajabu, alitangaza kufukuzwa kazi kwa askari wote waliotuhumiwa kumkamata na kumwachia Kasusura.

Ashtakiwa Kisutu

Tarehe 7 Januari, 2002 Kasusura na wenzake sita walishtakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam katika kesi ambayo ilivuta hisia za watu wengi.

Walishtakiwa kwa kosa la kula njama, unyang’anyi wa kutumia silaha, wizi na kupokea mali ya wizi.

Ahukumiwa

Ijumaa ya tarehe 30 Machi, 2007, Hakimu Mkuu Mfawidhi Sivangilwa Mwangesi ambaye sasa ni jaji wa Mahakama ya Rufani alimhukumu Kasusura kifungo cha miaka 35 jela kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha na wizi. Pia, alihukumiwa kuchapwa viboko 12.


Mahakama Kuu yatupa rufaa yake

Mara tu baada ya kuhukumiwa, Kasusura alikata rufaa Mahakama Kuu kupinga kutiwa hatiani na kufungwa. Mwezi Juni, 2010, Jaji Thomas Mihayo alitupilia mbali rufaa hiyo ikidai haikuwa na hoja za kutosha kuishawishi kutengua uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu.

Kutupwa kwa rufaa yake hakukumkatisha tamaa. Juni 4, 2015, Kasusura alikata rufaa ya pili katika Mahakama ya Rufani huku akiwasilisha sababu tisa kwa nini anapinga kifungo dhidi yake.


Ashinda rufaa

Tarehe 3 Mei, 2016 Mahakama ya Rufani ilikubaliana na hoja za Kasusura kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilikosea kumhukumu miaka 30 jela.

Ilisema wakati akidaiwa kutenda kosa hilo mabadiliko ya Sheria ya Kanuni ya Adhabu yanayoelekeza kifungo cha miaka 30 kwa mtu anayetiwa hatiani kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha yalikuwa hayajaanza kutumika. Mahakama ilikubali hoja ya Kasusura kuwa maelezo yake ya onyo alimodaiwa kukiri kosa yalipokelewa mahakamani kinyume cha utaratibu uliowekwa na Sheria Mwenendo wa Makosa ya Jinai. Mahakama iliona maelezo ya onyo ya Kasusura yalikuwa batili kwa kuwa yalirekodiwa baada ya muda wa kisheria kupita.

Kasusura alikamatwa tarehe 24 Disemba, 2001 lakini maelezo yake yalichukuliwa tarehe 26 Disemba, 2001.

Mahakama pia ilikubaliana na Kasusura kuwa kushindwa kwa upande wa mashtaka kuwaita maofisa wa benki ya Citibank waliokuwa wamiliki wa mzigo ulioibwa kulileta shaka kubwa kuhusu aina na kiasi cha fedha zilizokuwa ndani na mzigo huo.

Uamuzi wa kuwachia Kasusura ulitolewa na majaji Mbarouk Mbarouk, Sauda Mjasiri na Semistocle Kaijage ambaye sasa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Ni nani aliyefaidi mabilioni yaliyodaiwa kuporwa na Kasusura? Si Kasusura wala Jeshi la Polisi wameweza kujibu swali hili miaka 20 tangu tukio hilo litokee.
Yuko wapi huyo kasusura

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu kama huyu Kasurura ni kwamba hakuwa smart, sema dodo lilimdondokea akashindwa kucheza kama pele....

Waafrika wengi weusi hatujui kucheza na pesa vilivyo hasa tunapo piga tukio, wazungu, waarabu, wachina na hawa wasomali hapa afrika akiotea dodo ni ngumu sana kumkamata though wanaintelejensia wao wapo vizuri sana kwenye kuwasachi.

Tukio umepiga miezi kadhaa unaenda guest bubu na kimwana asee hii ni hollshit alafu unaenda lewa na kurudi chakariii, haya ndiyo yale ya Hushpupy yaani he caughted red handed na pesa kibao.

Pesa kwa mtu mweusi haijifichi kabisa showoff na blabla kibao..... bilioni 4.4 za mwaka 2001 yaani nimefanikiwa kutokomea niambia ndugu yangu mwaminifu anichimbie Andaki langu kabisa [emoji16]

Ikishindikana kuchimbiwa Andaki najibadilisha mwonekano wote kabisa, yaani napita hapo JNIA na mkinijua lazima mtoke jasho.
Kama i was Christian i must be a muslim......change the full identities....ndevu za bandia, kama ni mweusi najikoboa kuwa white, milioni $2 si mchezo.
Alifanya hivyo lkn nakumbuka waliomuangusha ni ndugu wa karibu.

Nakumbuka alipokwapua ule mzigo alikwenda nyumbani kwa kaka yake fulani kisha kumkabidhi mzigo wote wa USD 2m kisha yeye kubaki na kiasi fulani cha Tshs na kutokomea zake. Tatizo lilikuwa kwa upande wa mke wa Kaka yake. Kaka yake alikuwa ni miongoni mwa waliokamatwa kusaidia Polisi hivyo mzigo wote ulikuwa mikononi mwa mke wake (mke wa Kaka yake Kasusura).

Yule mama alikuwa mwenyeji wa Arusha, hivyo alikimbilia huko na ule mzigo pamoja na ndugu zake wengine. Wakati huo Arusha kulikuwa na hoteli maarufu ya kitalii ijulikanayo kama Impala. Ule mzigo ulikuwa ukibadilishiwa pale in terms of Tshs.

Walinunua gari fulani minibus [emoji604]. Kazi kubwa ya gari lile ni kuwajaza marafiki zao na kwenda kula BATA. Hapo mkumbuke kuwa Kasusura katokomea gizani huku Kaka yake kawekwa korokoroni. Mama alikuwa huru na Michepuko pamoja na baadhi ya maafisa usalama waliokuwa wameahidi kumsaidia mumewe aweze kutoka korokoroni.

Nakumbuka Yule mama alikuwa na wadogo zake wawili, wa kike na wa kiume wote waliokuwa kwenye ndoa lkn wote waliwatelekeza wenza wao kwasababu ya ulimbukeni wa mpunga mrefu.

Fedha zile hazikuwa tofauti na maji ya mvua yasababishayo mafuriko Jijini. Jua likiwaka kwa saa kadhaa hukauka. Fedha nazo zilikata paap. Walichoka mbaya kisha kuuza lile gari na kurudi Jijini.

Ninachotaka kusema ni kwamba Kasusura aliangushwa na Shemeji yake yaani mke wa kaka yake.
 
Ilikuwa Ijumaa ya Augost 3, 2001 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, ALFRED TIBAIGANA, alitangaza kutokea unyan'ganyi wa fedha kiasi cha U$D 2 Milioni (Tsh 4,400,000,000/=) uliofanyika majira ya saa 5 asubuhi nje kidogo ya "Airport" ya JKIA Augost 2, mwaka huo.

RPC TIBAIGANA alimtaja mtuhimiwa was wizi huo ni JUSTINE KAKURU KASUSURA, ambaye aliiuwa dereva wa gari la Kampuni ya Ulinzi ya Knight Support yenye makao makuu yake eneo la Victoria, Dar es salaam.

Kamanda TIBAIGANA alisema mtuhumiwa huyo ametoweka na fedha hizo kusiko julikana na msako mkali umeanza nchi nzima hususan maeneo ya mipakani.

Aidha alitoa rai kwa wananchi na wasamaria wema kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kufanikisha kumkamata mtuhumiwa huyo. Lakini ilipita miezi 5 bila kukamatwa.

Kipindi cha miezi 5 bila kukamatwa kilizuwa gumzo kwa wananchi wengi wakiamini kuwa huenda kakimbilia nje ya nchi, lakini taarifa za siri zilipatikana na kusaidia kukamatwa kwake usiku wa manane, Jumatatu ya Desemba 24, mwaka 2001 katika Hoteli ijulikanayo kama "Three In One" iliyoko maeneo ya Soweto, Mbeya.

Inadaiwa KASUSURA alifika hotelini hapo siku ya Jumapili, Desemba 23, 2001 saa 12 jioni akitokea Sumbawanga akijifanya mfanyabishara akiwa amevalia kofia kubwa kuficha uso wake na kupewa chumba Na. 101K ambapo katika rejista alijisajili kwa jina bandia la JOHN LAIZER na kulipia chumba malazi ya siku moja kwa Sh 3,500/=.

Jioni yake baada ya kakamilisha taratibu za chumba alitoka kwenda kujivinjari na ndipo Askari walipoingia chumbani kwakwe kukuwekea mtego was kumnasa.

KASUSURA akiwa amekwisha ianza Kristmas alirejea huku usiku akiwa kalewa na kimwana wake na mara baada ya kuingia ndani, alikutana uso kwa uso na askari walioibuka kutoka uvunguni na kabatini na kumtia nguvuni kilaini.

Hate hivyo baada ya upekuzi alikutwa na akiwa na Sh 200.000/= tu.!.View attachment 2615019View attachment 2615020



Bado ni kitendawili waliofaidi mabilioni ya Justine Kasusura

Justine Kasusura akitoka katika jengo la Mahakama kuu jijini Dar es Salaam ambapo rufaa yake ya kwanza ilisikilizwa na kutupwa.

[emoji1541][emoji1541][emoji1541]

Kiasi cha fedha alichodaiwa kupora, staili aliyotumia na ukubwa ambao tukio hilo lilipewa na vyombo vya habari kumelifanya lisifutike kirahisi kwenye kumbukumbu za wengi.

Kwa miezi 12 baada ya Ijumaa ya tarehe 2 Agosti, 2001, hakuna jina lililotawala vyombo vya habari kama la Justine Kasusura, aliyedaiwa kupora dola za Marekani milioni mbili (Sh4.4 bilioni) bila kutumia nguvu kubwa.

Kasusura aliyekuwa ameajiriwa na kampuni ya ulinzi ya Knight Support alidaiwa kupora fedha hizo muda mfupi baada ya kuzipokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) akiwa njiani na mfanyakazi mwenzake kuelekea benki ya Citibank.

Kiasi cha fedha alichodaiwa kupora, staili aliyotumia na ukubwa ambao tukio hilo lilipewa na vyombo vya habari kumelifanya lisifutike kirahisi kwenye kumbukumbu za wengi.

Hadi kesi dhidi ya Kasusura aliyekamatwa miezi mitano baada ya tukio inamalizika, Jeshi la Polisi lilidai kuambulia Sh256,000 tu mikononi mwake.

Kutopatikana fedha hizo kumeacha fumbo. Ni wapi fedha hizo zinazotosha kumlipa mkandarasi atakayejenga upya miundombinu ya eneo zima la Jangwani ziliishia? Ni nani hasa waliofaidi fedha hizo?

Uporaji ulivyotekelezwa

Tukio zima lilianza hivi; asubuhi ya tarehe 2 Agosti 2001, Kasusura na mfanyakazi mwenziwe, Said Hamisi, walioajiriwa na Knight Support walielekezwa na meneja wa kampuni hiyo aliyeitwa Doren kwenda Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam kupokea mzigo na kuupeleka katika benki ya Citibank katikati ya jiji la Dar es Salaam.

Kama ilivyokuwa kawaida ya kampuni hiyo, Kasusura, aliyeajiriwa kama dereva, alikabidhiwa bastola na risasi kadhaa huku mwenzake akikabidhiwa simu ya mkononi ili kufanikisha mawasiliano.

Safari kutoka makao makuu ya Knight Support iliyokuwa eneo la Victoria ilianza vizuri. Wakiwa njiani kuelekea uwanja wa ndege walisimama mara moja tu kujaza mafuta.

Wakiwa uwanja wa ndege, walikutana na maofisa wa kampuni ya Dahaco iliyoshughulika na mizigo ya kutoka nje ya nchi. Baada ya mazungumzo mafupi majira ya saa nne asubuhi Kasusura aliitwa na kusaini nyaraka kadhaa kabla ya kukabidhiwa mzigo walioufuata.

Kasusura aliuweka mzigo huo nyuma ya nyuma ya gari hilo aina ya Toyota Hilux Double Cabin lililofunikwa pande zote na kufunga kwa ufunguo. Wakati wakiondoka, Kasusura alimfahamisha Doren kwa njia ya simu kuwa walikuwa wakiondoka uwanjani hapo na kwamba aliweka mzigo huo nyuma ya gari na kufunga kwa ufunguo.

Walipotoka eneo la uwanja wa ndege, waliona gari likiwa limeegeshwa pembeni mwa barabara. Kasusura alikwenda moja kwa moja na kuliegesha gari akiendesha mbele ya gari hilo aina ya Toyota Land Cruser.

Hapa Kasusura alimweleza mfanyakazi mwenzake kuwa “biashara imekwisha” na kumtaka afungue boksi walilopokea uwanja wa ndege huku akimwelekezea bastola.

Alipoona mwenzake anasuasua, Kasusura alichukua funguo na simu ya mkononi kutoka kwa mwenzake na kuchukua ule mzigo akisaidiwa na watu wengine wawili waliokuwa kwenye gari walilolikuta pale.

Baada ya Kasusura na wenzake kutoweka na wenzake, Hamis aliomba msaada na kuripoti tukio hilo kituo cha Polisi Stakishari.

Taifa lashtuka

Siku iliyofuata aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Alfred Tibaigana aliutangazia umma tukio la uporaji wa fedha za Citibank.

Alisema tayari askari walikuwa wamejipanga kila kona ya nchi kumsaka mhalifu huyo, huku akiwaambia kutoa taarifa endapo watamwona au watahisi uwepo wake mahali popote.

Kasusura akamatwa Mbeya

Miezi mitano ilipita bila Kasusura kukamatwa. Habari zake ziliendelea kutawala vyombo vya habari

Taarifa za uwepo wa Kasusura mkoani Mbeya zilitolewa na msiri wa polisi.

Akiwa nyumbani kwake majira ya saa tatu usiku tarehe 24 Disemba 2001, Inspekta wa Polisi Richard Tadei alipokea taarifa kuwa katika nyumba ya kulala wageni ya Three in One iliyoko eneo la Soweto mkoani Mbeya alikuwapo mhalifu hatari aliyekuwa akitafutwa na polisi.

Baada ya kufanya ufuatiliaji na kujiridhisha kuwa mtu aliyekuwa akiishi katika hoteli hiyo alikuwa Kasusura, Inspekta Richard aliandaa askari wenzake na kuweka mtego wa kumnasa Kasusura.

Bila kujua siku zake zinahesabika, usiku wa manane siku ya mkesha wa Krismasi ya tarehe 24 Desemba, 2001, Kasusura aliingia kwenye chumba chake namba 101k hotelini hapo akiambatana na mwanamke.

Alipofungua mlango alikutana na askari ambao tayari walikuwa wamejificha sehemu mbali mbali ndani ya chumba hicho. Wengine walikuwa wameizingira hoteli. Alipofungua tu mlango, Kasusura alijikuta akiangukia mikononi mwa askari.

Ushahidi uliotolewa mahakamani na nyaraka nyingine zinaonyesha Kasusura alikutwa na Sh256,000 tu baada ya kupekuliwa.

Haikuwa mara ya kwanza kukamatwa

Kabla ya kukamatwa Kasusura, uvumi ulisambaa kuwa Kasusura amewahi kukamatwa mara kadhaa lakini amekuwa akiponyoka mikononi mwa polisi kwa nguvu ya fedha.

Taarifa hizo zilizidi kuvuma kiasi cha kumuibua hadharani aliyekuwa mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Omar Mahita na kutangaza kuwa askari watano walikuwa wakihojiwa kwa tuhuma za kumkamata na kumwachia Kasusura.

Siku chache baadaye aliyekuwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, Adadi Rajabu, alitangaza kufukuzwa kazi kwa askari wote waliotuhumiwa kumkamata na kumwachia Kasusura.

Ashtakiwa Kisutu

Tarehe 7 Januari, 2002 Kasusura na wenzake sita walishtakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam katika kesi ambayo ilivuta hisia za watu wengi.

Walishtakiwa kwa kosa la kula njama, unyang’anyi wa kutumia silaha, wizi na kupokea mali ya wizi.

Ahukumiwa

Ijumaa ya tarehe 30 Machi, 2007, Hakimu Mkuu Mfawidhi Sivangilwa Mwangesi ambaye sasa ni jaji wa Mahakama ya Rufani alimhukumu Kasusura kifungo cha miaka 35 jela kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha na wizi. Pia, alihukumiwa kuchapwa viboko 12.

Mahakama Kuu yatupa rufaa yake

Mara tu baada ya kuhukumiwa, Kasusura alikata rufaa Mahakama Kuu kupinga kutiwa hatiani na kufungwa. Mwezi Juni, 2010, Jaji Thomas Mihayo alitupilia mbali rufaa hiyo ikidai haikuwa na hoja za kutosha kuishawishi kutengua uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu.

Kutupwa kwa rufaa yake hakukumkatisha tamaa. Juni 4, 2015, Kasusura alikata rufaa ya pili katika Mahakama ya Rufani huku akiwasilisha sababu tisa kwa nini anapinga kifungo dhidi yake.

Ashinda rufaa

Tarehe 3 Mei, 2016 Mahakama ya Rufani ilikubaliana na hoja za Kasusura kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilikosea kumhukumu miaka 30 jela.

Ilisema wakati akidaiwa kutenda kosa hilo mabadiliko ya Sheria ya Kanuni ya Adhabu yanayoelekeza kifungo cha miaka 30 kwa mtu anayetiwa hatiani kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha yalikuwa hayajaanza kutumika. Mahakama ilikubali hoja ya Kasusura kuwa maelezo yake ya onyo alimodaiwa kukiri kosa yalipokelewa mahakamani kinyume cha utaratibu uliowekwa na Sheria Mwenendo wa Makosa ya Jinai. Mahakama iliona maelezo ya onyo ya Kasusura yalikuwa batili kwa kuwa yalirekodiwa baada ya muda wa kisheria kupita.

Kasusura alikamatwa tarehe 24 Disemba, 2001 lakini maelezo yake yalichukuliwa tarehe 26 Disemba, 2001.

Mahakama pia ilikubaliana na Kasusura kuwa kushindwa kwa upande wa mashtaka kuwaita maofisa wa benki ya Citibank waliokuwa wamiliki wa mzigo ulioibwa kulileta shaka kubwa kuhusu aina na kiasi cha fedha zilizokuwa ndani na mzigo huo.

Uamuzi wa kuwachia Kasusura ulitolewa na majaji Mbarouk Mbarouk, Sauda Mjasiri na Semistocle Kaijage ambaye sasa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Ni nani aliyefaidi mabilioni yaliyodaiwa kuporwa na Kasusura? Si Kasusura wala Jeshi la Polisi wameweza kujibu swali hili miaka 20 tangu tukio hilo litokee.
Huyu nae alishindwa vipi kwenda hata south Africa na hela zote hizo.

Anyways, yuko wapi kwa sasa...baada ya kushinda kesi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Napenda mwanaume anayejiamini kama hivi....!
Jela kuna wanasheria wafungwa huwasaidia wafungwa wanaokata rufaa, jinsi ya kuiframe kesi, jinsi ya kujibu maswali, muonekano wa muhusika siku ya kwenda kusikiliza kesi ya rufaa, n.k,

Mahakama za rufaa hua wanamjali zaidi mkata rufaa anayesimama mwenyewe bila Wakili, ndio maana Rufaa ya kwanza alikua na Wakili wakaangukia pua, Rufaa ya pili baada ya kuivishwa jela akasimama mwenyewe akatoka.

Kujiamini kunasaidia sana.
 
Alifanya hivyo lkn nakumbuka waliomuangusha ni ndugu wa karibu.

Nakumbuka alipokwapua ule mzigo alikwenda nyumbani kwa kaka yake fulani kisha kumkabidhi mzigo wote wa USD 2m kisha yeye kubaki na kiasi fulani cha Tshs na kutokomea zake. Tatizo lilikuwa kwa upande wa mke wa Kaka yake. Kaka yake alikuwa ni miongoni mwa waliokamatwa kusaidia Polisi hivyo mzigo wote ulikuwa mikononi mwa mke wake (mke wa Kaka yake Kasusura).

Yule mama alikuwa mwenyeji wa Arusha, hivyo alikimbilia huko na ule mzigo pamoja na ndugu zake wengine. Wakati huo Arusha kulikuwa na hoteli maarufu ya kitalii ijulikanayo kama Impala. Ule mzigo ulikuwa ukibadilishiwa pale in terms of Tshs.

Walinunua gari fulani minibus [emoji604]. Kazi kubwa ya gari lile ni kuwajaza marafiki zao na kwenda kula BATA. Hapo mkumbuke kuwa Kasusura katokomea gizani huku Kaka yake kawekwa korokoroni. Mama alikuwa huru na Michepuko pamoja na baadhi ya maafisa usalama waliokuwa wameahidi kumsaidia mumewe aweze kutoka korokoroni.

Nakumbuka Yule mama alikuwa na wadogo zake wawili, wa kike na wa kiume wote waliokuwa kwenye ndoa lkn wote waliwatelekeza wenza wao kwasababu ya ulimbukeni wa mpunga mrefu.

Fedha zile hazikuwa tofauti na maji ya mvua yasababishayo mafuriko Jijini. Jua likiwaka kwa saa kadhaa hukauka. Fedha nazo zilikata paap. Walichoka mbaya kisha kuuza lile gari na kurudi Jijini.

Ninachotaka kusema ni kwamba Kasusura aliangushwa na Shemeji yake yaani mke wa kaka yake.
Aisee hii dunia taabu sana tena sana.
Sasa hizi $ mingi hivi unakubali kumpa brother ambaye haaminiki alafu brother anampa demu wake asee mimi ni huyu kasusura lazima ningetoka shavu.
 
Back
Top Bottom