Bado zipo sababu kwa familia ya Lissu kuishi Ulaya? Je Lissu haoni kuwa jambo hili linampunguzia uzito kisiasa?

Bado zipo sababu kwa familia ya Lissu kuishi Ulaya? Je Lissu haoni kuwa jambo hili linampunguzia uzito kisiasa?

Nsanzagee

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2023
Posts
2,209
Reaction score
4,769
Najua,

Wengi wenu badala ya kujikita kwenye hoja, mtanijadiri na tena siyo tu kunijadiri, ila ni kwa kutoa matusi!

Ni kweli hatuwezi kuwa na mtazamo sawa, na hii inakuja ili kutufanya tuonekane ni wanadamu na mambo yetu ili yawe sawa, tunahitaji kuwa na migongano ya kifikra na hatimaye kwenda sawa

Naam!

Mh makamu mwenyekiti Chadema bwana Tundu Lissu, tangu aondoke nchini kwa matibabu huko Ughaibuni, na baada ya kukaa huko kwa mda mrefu akitibiwa, alirejea nchini kwa ajili uchaguzi mkuu 2020

Hata hivyo, hakuja na familia yake, nadhani kwa kipindi hicho, haukuwa wakati sahihi wa kuuliza juu ya kwa nini kaiacha familia yake ulaya kwa sababu kuu moja kwamba, bado alikuwa kwenye matazamio ya kiafya

Mpaka hii leo, tunazungumza miaka mitano mingine inakaribia kupita tokea uchaguzi wa 2020 alipokuwa mgombea wa nafasi ya Urais kupitia chama chake, bado shida ya matazamio inaendelea?

Jambo hili halimfanyi kutokueleweka na kuaminika vizuri kwenye nyanja za kisiasa?

Kuhusu Sheria za Nchi au Katiba inasema nini kuhusu wagombea mbalimbali wa nafasi hasa ya Urais inapotokea mgombea mmoja wapo familia yake haikai nchini!

Jambo lingine la pili, Vuguvugu ambalo chadema wanaonekana kuliamsha ni la wananchi wenyewe kuingia mtaani kudai katiba, yaweza kuwa ni mbinu nzuri, Je, wananchi wanapofika mahali wajiulize, waanzishaji wa vuguvugu hili, wao ni kama wahamiaji tu nchini, likitokea la kutokea, wao wanapanda pipa na kwenda makwao ulaya, Chadema hawaoni kuwa jambo hili linawarudisha nyuma wanavuguvugu wa katiba?
 
Jambo hili halimfanyi kutokueleweka na kuaminika vizuri kwenye nyanja za kisiasa?
Toka lini ukamuamini Lissu? Huyu yupo kimaslahi, tena ya kwake na familia yake. Jikomboe, usidanganyike... Lissu hakukomboi hata siku moja.
Utachoweza kufanya ni kumpuuza na kumtosa kwa kila asemalo. Hafai kabisa huyuuuu.
 
Kutokana na hali mbovu ya usalama na vitisho dhidi ya Lissu na familia yake ni sawa kabisa kwa Lissu kuishi Ulaya, tena amefanya ujasiri wa ajabu kuja Tz na kuendelea na siasa, ni hatari mno kwa usalama wake na famila yake kwa wanasiasa tulionao nchini!
 
KWANI ANAZUITO GANI? ANAKUJA KUDANGANYA WASIO NA AKILI WANAOMFUATA KISHA ANARUDI KWA MME WAKE ULAYA
 
Toka lini ukamuamini Lissu? Huyu yupo kimaslahi, tena ya kwake na familia yake. Jikomboe, usidanganyike... Lissu hakukomboi hata siku moja.
Utachoweza kufanya ni kumpuuza na kumtosa kwa kila asemalo. Hafai kabisa huyuuuu.
Unazo sababu kwa vidokezo vyako hivi, ila kishawishi cha hiki unachokisema, umebaki nacho kwenye akili yako

Funguka mkuu, kwa nini unasema Lissu amekuja ili ajipe manufaa yeye na siyo Watanzania wote?
 
Wewe unaogopa kujadiliwa ila unamjadili lissu tena kwa maelezo marefuuuuuuu

Usivyopenda kujadiliwa wewe jiepushe na kujadili wengine.

We tuambie kwanza familia yako inaishi wapi na kwanini?? Kwanini usiishi masasi?
 
KWANI ANAZUITO GANI? ANAKUJA KUDANGANYA WASIO NA AKILI WANAOMFUATA KISHA ANARUDI KWA MME WAKE ULAYA
Kwani ni lazima uchangie uzi mkuu? Mbona matusi tena!

Hii ni Tanzania bhana, ni nchi ambayo tunaishi kidugu, hapa siyo Kenya
 
Haya maneno ya familia inaishi wapi hata wewe pia yanakuhusu, ipo siku yatakurudia na watu watasema urudi kwenu kule ndani ndani panapoitwa, " Pangu Pakavu Tia Mchuzi".
 
Anapata malipo ya watu wasiojiweza
Lissu ni mjanja flani chadema wenyewe hawajamshtukia hana tofauti na yule mwanasiasa jauko wa kenya anayetukana jukwaani ndio maana lissu lazima aanze na kitu cha bob marley kutukuza yale mafusho!
 
Back
Top Bottom