Bakhresa, Mo Dewji na GSM wajitosa kuwekeza kwenye SGR

Bakhresa, Mo Dewji na GSM wajitosa kuwekeza kwenye SGR

Mmoja tu kutoka ccm asimame athibitishe kwamba yeye ni msomi, anauchungu na nchi pia anaweza kuitoa nchi hapa ilipo na kuipeleka kwenye maendeleo ni nani nauliza?

Hayupo hata mmoja, walioko huko wote wanawaza ni namna ipi wafanye ili wapate nafasi ya kuiba na kulihujumu taifa
Hapo wanaiba nini? Kwani kuleta treni yako ili utoe huduma kuna dhambi gani?
 
Hapo wanaiba nini? Kwani kuleta treni yako ili utoe huduma kuna dhambi gani?
Nashangaa

Reli ni barabara tu mwenye chombo chake Cha kupita humo ruksa Kwa makubaliano tu ya malipo ya kutumia hiyo reli
Tatizo watazania Wengine wamezoea Biashara vidogo vidogo visivyokua hivyo akiona biashara kubwa hivi anashangaa ohh itakuwaje
 
Watanzania angalieni yaliyojiri kwenye Mwendokasi! Mimi naona akikipewa Baresa ni poa ila atoe shares ili nasi tushiriki
 
Ni vema ukayafahamu haya mapema kwa faida yako

Bali wadau wengi wanajiuliza kwamba ni kitu gani ambacho Serikali ya Tanzania inaweza kufanya, maana unaambiwa ni afadhali hata mtoto mwenye Polio waweza kumpa Magongo akatembea mwenyewe

Kampuni sita za Kitanzania ni miongoni mwa kampuni kadhaa ambazo zimeonyesha nia ya kushirikiana na serikali katika kuendesha Reli ya Standard Gauge (SGR).

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa kufuatia kutangazwa kwa Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma Binafsi za mwaka 2024.

Akizungumza na Mwananchi leo Juni 19, 2024, Kadogosa amezitaja kampuni hizo kuwa ni GSM, Bakhresa Group, Mohammed Enterprises Company Limited, Lake Oil, Azania na Jambo.

Orodha hiyo pia inajumuisha kampuni kadhaa kutoka China na Ulaya.

“Kati ya kampuni zilizotajwa hapo juu, Jambo ndiyo kampuni pekee ya Kitanzania ambayo imeonyesha nia ya kuanzisha treni ya kifahari ya abiria kwa ajili ya watalii. Asilimia 99 iliyobaki wana hamu ya kuwekeza kwenye usafirishaji wa mizigo,” amesema.

Amesema kwa sasa TRC inajitahidi sana kuhakikisha ujenzi wa sehemu zote za SGR unakamilika ifikapo 2028 ili wawekezaji watumie fursa hiyo na kutoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi.
Nani kawazuia matajiri wasio wahindi,Waarabu na Waislamu wasiwekeze kwenye reli hii?
Taratibu unaiingiza ubaguzi wa rangi na dini kama Lema.
 
Screenshot_20240620-020735.jpg

Dah jiwe
 
Sioni tatizo, kama wanaweza kuwekeza wawekeze tu. Money is Money.
Ilimradi sheria na taratibu za uwekezaji zifuatwe, wasipewe favors.
 
Wamejazwa wajinga kuendesha chombo cha kisasa, unategemea nini zaidi?

Tegemea mashine zote za tiketi na malipo ya kupitia simu kutokufanya kazi ndani ya miezi mitatu.
Hapana.
Sijui kwa nini napishana fikra nawe mara nyingi hivi, hata katika mambo rahisi kama hili hapa, ambapo katika hali ya kawaida kabisa tungeweza kuwa upande mmoja. Mimi hapa sioni "ujinga", bali naona kukosa mwongozo na uongozi wa kuhakikisha hali hiyo uliyo ielezea isiwepo.
Kila mtu atimize wajibu wake kama alivyo pangiwa, na wanaosimamia nao wahakikishe wamesimamia ipasavyo.

Hivi sisi tutakuwa watu wa kuwategemea wengine hadi lini?
 
Serikali imekopa matrilioni zitakazolipwa na tozo za wananchi - halafu leo mabepari wanavamia na kufaidi uwekezaji wa serikali
Kwanini wasijenge hao matajiri?
 
Hapana.
Sijui kwa nini napishana fikra nawe mara nyingi hivi, hata katika mambo rahisi kama hili hapa, ambapo katika hali ya kawaida kabisa tungeweza kuwa upande mmoja. Mimi hapa sioni "ujinga", bali naona kukosa mwongozo na uongozi wa kuhakikisha hali hiyo uliyo ielezea isiwepo.
Kila mtu atimize wajibu wake kama alivyo pangiwa, na wanaosimamia nao wahakikishe wamesimamia ipasavyo.

Hivi sisi tutakuwa watu wa kuwategemea wengine hadi lini?
Hadi tukifuta ujinga.
 
HONGERA SANA KUFIKIA MAAMUZI SAHIHI ya kuruhusu sekta binafsi kutoa huduma ya usafiri wa treni kwa kutumia miundombinu ya reli ya serikali. Nilishasema humu ya kwamba kwa mfumo wa sheria za utumishi wa umma zilivyo, ni vigumu sana sector ya umma kutoa huduma y viwango na ya uhakika ya usafiri wa treni, hasa ya SGR. Ingekufa tu mapema sana. Uamuzi huo ni mzuri sana unaenda kuleta ushindani,ubora na uhakika wa usafiri wa treni, hasa SGR.
 
Serikali imekopa matrilioni zitakazolipwa na tozo za wananchi - halafu leo mabepari wanavamia na kufaidi uwekezaji wa serikali
Kwanini wasijenge hao matajiri?
Kwani matabaka katika jamii hujengwa vipi?

Hawa matajiri sasa wanayo serikali yao. Hawa ndio kipaumbele cha serikali. Wao wana sauti nzito zaidi serikalini kuliko hao akina hohehahe.
Hawa ndio wanaoiamrisha serikali ifuate mipango yao, ya kuwafaidisha zaidi kupitia mgongoni kwa hahehoi.
 
Pamoja na kukubaliana na wewe kwa kiasi fulani; lakini haina maana huduma hizo haziwezi kufanywa kwa ufanisi na mashirika ya kiserikali. Hii dhana potofu ya kufikiri serikali haina uwezo wa kufanya kitu kwa ufanisi. imekuwa mzigo mzito sana katika akili zetu siku hizi.

Ethiopian Airways ni shirika linaloingiza faida kila mwaka, ni shirika la serikali. Hapo Kenya SGR yao inaendeshwa na shirika lao la kiserikali; wamefunzwa vyema na waChina, hadi sasa wanakwenda vizuri
Mashirika mengi ya kiChina yapo kila mahali duniani, yanafanya kazi kibiashara kwa ufanisi.

Sijatamka popote kwamba sekta binafsi isihusishwe, lakini ni lazima pia kujuwa athari zinazotokana na kutegemea kila kitu, hasa maeneo nyeti hiyo sekta. Wananunua serikali kwa manufaa yao, kama tunavyoona inafanyika sasa hivi.

Hizo huduma nafuu unazozililia utazisikia tu, hutaziona.
Nakuelewa Mzee wa Malumbano ya hoja
 
Back
Top Bottom