Bakhresa, Mo Dewji na GSM wajitosa kuwekeza kwenye SGR

Bakhresa, Mo Dewji na GSM wajitosa kuwekeza kwenye SGR

Pamoja na kukubaliana na wewe kwa kiasi fulani; lakini haina maana huduma hizo haziwezi kufanywa kwa ufanisi na mashirika ya kiserikali. Hii dhana potofu ya kufikiri serikali haina uwezo wa kufanya kitu kwa ufanisi. imekuwa mzigo mzito sana katika akili zetu siku hizi.

Ethiopian Airways ni shirika linaloingiza faida kila mwaka, ni shirika la serikali. Hapo Kenya SGR yao inaendeshwa na shirika lao la kiserikali; wamefunzwa vyema na waChina, hadi sasa wanakwenda vizuri
Mashirika mengi ya kiChina yapo kila mahali duniani, yanafanya kazi kibiashara kwa ufanisi.

Sijatamka popote kwamba sekta binafsi isihusishwe, lakini ni lazima pia kujuwa athari zinazotokana na kutegemea kila kitu, hasa maeneo nyeti hiyo sekta. Wananunua serikali kwa manufaa yao, kama tunavyoona inafanyika sasa hivi.

Hizo huduma nafuu unazozililia utazisikia tu, hutaziona.
Mashirika ya serikali mangapi tuliyokuwa nayo toka tumepata Uhuru hadi hii leo? Lipi lililofanya kazi kwa faida?
 
Lini Watanzania walimfuta adui ujinga?

BRT imewashinda kuendesha, mtaweza SGR?
Unawadharau waTanzania, huku unasahau wanao wasababishia kudharauliwa?
Ungekuwa umefuta ujinga ungejuwa wapi pa kuelekeza lawama zako, lakini najuwa ujinga ni mzigo mkubwa. kwako.
 
Mashirika ya serikali mangapi tuliyokuwa nayo toka tumepata Uhuru hadi hii leo? Lipi lililofanya kazi kwa faida?
Huu nao ni mjadala unaotaka tutumie muda mwingi kuujadili?
Katika muda huo wakati mashirika hayo yakifa, ni matajiri gani wakubwa walioibuka na kushamiri bila ya kuitegemea serikali hiyo hiyo; kwa kuiibia, au kushiriki katika kuuwa hayo mashirika ya umma!
 
Ni vema ukayafahamu haya mapema kwa faida yako

Bali wadau wengi wanajiuliza kwamba ni kitu gani ambacho Serikali ya Tanzania inaweza kufanya, maana unaambiwa ni afadhali hata mtoto mwenye Polio waweza kumpa Magongo akatembea mwenyewe

Kampuni sita za Kitanzania ni miongoni mwa kampuni kadhaa ambazo zimeonyesha nia ya kushirikiana na serikali katika kuendesha Reli ya Standard Gauge (SGR).

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa kufuatia kutangazwa kwa Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma Binafsi za mwaka 2024.

Akizungumza na Mwananchi leo Juni 19, 2024, Kadogosa amezitaja kampuni hizo kuwa ni GSM, Bakhresa Group, Mohammed Enterprises Company Limited, Lake Oil, Azania na Jambo.

Orodha hiyo pia inajumuisha kampuni kadhaa kutoka China na Ulaya.

“Kati ya kampuni zilizotajwa hapo juu, Jambo ndiyo kampuni pekee ya Kitanzania ambayo imeonyesha nia ya kuanzisha treni ya kifahari ya abiria kwa ajili ya watalii. Asilimia 99 iliyobaki wana hamu ya kuwekeza kwenye usafirishaji wa mizigo,” amesema.

Amesema kwa sasa TRC inajitahidi sana kuhakikisha ujenzi wa sehemu zote za SGR unakamilika ifikapo 2028 ili wawekezaji watumie fursa hiyo na kutoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi.
🙋‍♂️👍👌🤝👏👊🙏💐🎁🛡️

⚖️Justice for Asimwe#
 
Mimi naona sawa tu! Kama serikali inaona haiwezi kuiendesha SGR bora itafute wawekezaji!
 
Ni vema ukayafahamu haya mapema kwa faida yako

Bali wadau wengi wanajiuliza kwamba ni kitu gani ambacho Serikali ya Tanzania inaweza kufanya, maana unaambiwa ni afadhali hata mtoto mwenye Polio waweza kumpa Magongo akatembea mwenyewe

Kampuni sita za Kitanzania ni miongoni mwa kampuni kadhaa ambazo zimeonyesha nia ya kushirikiana na serikali katika kuendesha Reli ya Standard Gauge (SGR).

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa kufuatia kutangazwa kwa Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma Binafsi za mwaka 2024.

Akizungumza na Mwananchi leo Juni 19, 2024, Kadogosa amezitaja kampuni hizo kuwa ni GSM, Bakhresa Group, Mohammed Enterprises Company Limited, Lake Oil, Azania na Jambo.

Orodha hiyo pia inajumuisha kampuni kadhaa kutoka China na Ulaya.

“Kati ya kampuni zilizotajwa hapo juu, Jambo ndiyo kampuni pekee ya Kitanzania ambayo imeonyesha nia ya kuanzisha treni ya kifahari ya abiria kwa ajili ya watalii. Asilimia 99 iliyobaki wana hamu ya kuwekeza kwenye usafirishaji wa mizigo,” amesema.

Amesema kwa sasa TRC inajitahidi sana kuhakikisha ujenzi wa sehemu zote za SGR unakamilika ifikapo 2028 ili wawekezaji watumie fursa hiyo na kutoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi.

View: https://twitter.com/Sisimizi3/status/1803480214581678486?t=5E4D54qSElTJnCjtgg9LqA&s=19
 

Mi kwa maoni yangu naona bora kwa miaka 5 kwanza Serikali isimamie yenyewe.

Ikifanya hivyo itajua ups and down za SGR na kujua namna ya kufanya.

Katika kipindi hicho wakiona hawaiwezi hiyo SGR wa-outsource makampuni yenye sifa wasimamie na wampe target mfano makusanyo ya Bil100 kwa mwezi baada kwa kuzingatia trend ya makusanyo waliyokutana nayo ndani ya hiyo miaka 5

Tena hyo kampuni itakayopata zabuni, isipewe kila kitu,wazipe zabuni kampuni tofauti tofauti kwa kandarasi tofauti tofauti,mfano Ticketing,service za train,n.k ili kuleta ufanisi na ushindani,na wote wapewe targets.
 
Mi kwa maoni yangu naona bora kwa miaka 5 kwanza Serikali isimamie yenyewe.

Ikifanya hivyo itajua ups and down za SGR na kujua namna ya kufanya.

Katika kipindi hicho wakiona hawaiwezi hiyo SGR wa-outsource makampuni yenye sifa wasimamie na wampe target mfano makusanyo ya Bil100 kwa mwezi baada kwa kuzingatia trend ya makusanyo waliyokutana nayo ndani ya hiyo miaka 5

Tena hyo kampuni itakayopata zabuni, isipewe kila kitu,wazipe zabuni kampuni tofauti tofauti kwa kandarasi tofauti tofauti,mfano Ticketing,service za train,n.k ili kuleta ufanisi na ushindani,na wote wapewe targets.
Uko sahihi.

Ila Mimi msimamo wangu ni ule ule,hiyo Sgr ni cosmetic project ya kupigia picha ,haiwezi na haitakuja kurudisha hela achilia mbali kuleta faida.
 
Ni jambo zuri kwani serikali ingekaa kando tu kwenye miradi hii mikubwa maana upigaji ni mwingi kuliko faida
Kama wanawekeza ni sawa tu wawe na shares
 
Hao ni wahujumu au wawekezaji?

Yaani wamiliki wa biashara ya mabasi na maroli ya mizigo ndio wawekeze sgr?

Hao wanakuja kuua treni na kuhujumu Miundombinu!!

The good thing is, 2025 tuna Rais mpya.

Watashindana lakini hawatoshinda.
 
Hakuna jambo linalo kosa mwisho mkuu
Basi nimekuelewa.
Kwamba mwisho unaweza kuwa kila mmoja wetu hii leo atakapofikia ukomo wa maisha yake. Hapo ndipo itakuwa mwisho wa maumivu chini ya CCM, ndani ya Tanzania.

Mimi nisingependa mwisho huo. Mwisho ninaoutafuta ni kuondokana na CCM wakati wa uhai wangu, na itapendeza zaidi isiendelee kuwepo madarakani 2025 chini ya uongozi huu uliopo sasa. Hilo ndilo tamanio langu kuu kwa manufaa ya taifa letu.
 
Back
Top Bottom