zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 20,537
- 31,729
Hapo wanaiba nini? Kwani kuleta treni yako ili utoe huduma kuna dhambi gani?Mmoja tu kutoka ccm asimame athibitishe kwamba yeye ni msomi, anauchungu na nchi pia anaweza kuitoa nchi hapa ilipo na kuipeleka kwenye maendeleo ni nani nauliza?
Hayupo hata mmoja, walioko huko wote wanawaza ni namna ipi wafanye ili wapate nafasi ya kuiba na kulihujumu taifa
NashangaaHapo wanaiba nini? Kwani kuleta treni yako ili utoe huduma kuna dhambi gani?
Tayari ameshakabidhiwa mkandarasi Toka Dubai Mwaka huu anaanzaWawape na Mwendokasi.
Umesahau "UCHAWA"?Awamu ya Sita hatuwezi kila kitu
Karabashi wale makaburu wapo Serious sana, kuanzia muda mpaka uharaka wa kushusha mzigoSio rahisi kama unavyowaza wewe mzee ila Kuna watu wanaitwa karabashi freight hao wapo tazara wanatumia reli mpk inasema kama wale wangechukua sgr ingekuwa jambo zuri maana tazara ukilitimba umezidi manina
Nani kawazuia matajiri wasio wahindi,Waarabu na Waislamu wasiwekeze kwenye reli hii?Ni vema ukayafahamu haya mapema kwa faida yako
Bali wadau wengi wanajiuliza kwamba ni kitu gani ambacho Serikali ya Tanzania inaweza kufanya, maana unaambiwa ni afadhali hata mtoto mwenye Polio waweza kumpa Magongo akatembea mwenyewe
Kampuni sita za Kitanzania ni miongoni mwa kampuni kadhaa ambazo zimeonyesha nia ya kushirikiana na serikali katika kuendesha Reli ya Standard Gauge (SGR).
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa kufuatia kutangazwa kwa Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma Binafsi za mwaka 2024.
Akizungumza na Mwananchi leo Juni 19, 2024, Kadogosa amezitaja kampuni hizo kuwa ni GSM, Bakhresa Group, Mohammed Enterprises Company Limited, Lake Oil, Azania na Jambo.
Orodha hiyo pia inajumuisha kampuni kadhaa kutoka China na Ulaya.
“Kati ya kampuni zilizotajwa hapo juu, Jambo ndiyo kampuni pekee ya Kitanzania ambayo imeonyesha nia ya kuanzisha treni ya kifahari ya abiria kwa ajili ya watalii. Asilimia 99 iliyobaki wana hamu ya kuwekeza kwenye usafirishaji wa mizigo,” amesema.
Amesema kwa sasa TRC inajitahidi sana kuhakikisha ujenzi wa sehemu zote za SGR unakamilika ifikapo 2028 ili wawekezaji watumie fursa hiyo na kutoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi.
Wamejazwa wajinga kuendesha chombo cha kisasa, unategemea nini zaidi?Una-print ticket ya nini mkuu, si nenda na simu janja yako isomwe wakati unaingia?, au nako ni shida?
Hapana.Wamejazwa wajinga kuendesha chombo cha kisasa, unategemea nini zaidi?
Tegemea mashine zote za tiketi na malipo ya kupitia simu kutokufanya kazi ndani ya miezi mitatu.
Hadi tukifuta ujinga.Hapana.
Sijui kwa nini napishana fikra nawe mara nyingi hivi, hata katika mambo rahisi kama hili hapa, ambapo katika hali ya kawaida kabisa tungeweza kuwa upande mmoja. Mimi hapa sioni "ujinga", bali naona kukosa mwongozo na uongozi wa kuhakikisha hali hiyo uliyo ielezea isiwepo.
Kila mtu atimize wajibu wake kama alivyo pangiwa, na wanaosimamia nao wahakikishe wamesimamia ipasavyo.
Hivi sisi tutakuwa watu wa kuwategemea wengine hadi lini?
Mimi sijawahi kuwa mjinga hata mara moja. Kwa hiyo futa huo ujinga ulio nao wewe.Hadi tukifuta ujinga.
Kwani matabaka katika jamii hujengwa vipi?Serikali imekopa matrilioni zitakazolipwa na tozo za wananchi - halafu leo mabepari wanavamia na kufaidi uwekezaji wa serikali
Kwanini wasijenge hao matajiri?
Nakuelewa Mzee wa Malumbano ya hojaPamoja na kukubaliana na wewe kwa kiasi fulani; lakini haina maana huduma hizo haziwezi kufanywa kwa ufanisi na mashirika ya kiserikali. Hii dhana potofu ya kufikiri serikali haina uwezo wa kufanya kitu kwa ufanisi. imekuwa mzigo mzito sana katika akili zetu siku hizi.
Ethiopian Airways ni shirika linaloingiza faida kila mwaka, ni shirika la serikali. Hapo Kenya SGR yao inaendeshwa na shirika lao la kiserikali; wamefunzwa vyema na waChina, hadi sasa wanakwenda vizuri
Mashirika mengi ya kiChina yapo kila mahali duniani, yanafanya kazi kibiashara kwa ufanisi.
Sijatamka popote kwamba sekta binafsi isihusishwe, lakini ni lazima pia kujuwa athari zinazotokana na kutegemea kila kitu, hasa maeneo nyeti hiyo sekta. Wananunua serikali kwa manufaa yao, kama tunavyoona inafanyika sasa hivi.
Hizo huduma nafuu unazozililia utazisikia tu, hutaziona.