Bakwata uislaam huo mmeutoa wapi? Kumbukeni moto ni mkali sana mtaenda chomwa

Bakwata uislaam huo mmeutoa wapi? Kumbukeni moto ni mkali sana mtaenda chomwa

Nidyo, nyie ni wapigaji hivyo muache upigaji. Msiwadhulumu wenzenu.

Uislamu ni mzuri ila nyie ndio mnauchafua

Hapa ni jukwaa sahihi kabisa na lengo la mtoa mada ni kutujuza na kuwaelimisha wanawake kuwa Bakwata Kata hawana mamlaka hivyo waende tu kwa kadhi wa Wilaya na wakiambiwa kuhusu hela wahoji kama hawana wafanyeje!
Sawa.
 
Hakuna mahala nilipoandika nimebuni, hakuna mahala nilipoandika uniwekee risiti ya malipo ya bank! Bali nilichokihitaji kutoka kwako ni yakini.
Allah shAhidi wa haya
 
Kama hali ipo hivyo si vyema kutupa shutuma. Ni vyema kuwa nasihi na kuwapa ushauri. Quran imetupa sifa ya tunaoneana huruma na Quran yenyewe inatutaka tuaidhiane kwa hekima.
Wenyewe waonewe huruma wakati ambao wao hawajamuonea huruma mwanamke...

Na hiyo ndio hekima yake.. .
 
Usiwe ni mwenye ghadhabu.

Usiwe ni mwenye kuhukumu watu! Umejikita kuhukumu watu, haujajikita kuogopa kwa unachokifanya bali umejipa yakini kwa unachokifanya. Dini yetu ni ya Mungu tuwe na heshima na viumbe vyake.
Subiri siku ya KUDHULUMIWA mama yako au bint yako ndio utaona ni ghadhabu ama la!
 
Usiwe ni mwenye ghadhabu.

Usiwe ni mwenye kuhukumu watu! Umejikita kuhukumu watu, haujajikita kuogopa kwa unachokifanya bali umejipa yakini kwa unachokifanya. Dini yetu ni ya Mungu tuwe na heshima na viumbe vyake.
Siku Musa alivyomvuta ndevu Harun akimkaba kwa hasira ungekuwepo ungesema Musa hana hekima
 
Nidyo, nyie ni wapigaji hivyo muache upigaji. Msiwadhulumu wenzenu.

Uislamu ni mzuri ila nyie ndio mnauchafua

Hapa ni jukwaa sahihi kabisa na lengo la mtoa mada ni kutujuza na kuwaelimisha wanawake kuwa Bakwata Kata hawana mamlaka hivyo waende tu kwa kadhi wa Wilaya na wakiambiwa kuhusu hela wahoji kama hawana wafanyeje!
BAARAKALLAH FIYK... NAOMBA MODS HII COMMENT MUIPIN. ..

HILI NDIO LENGO..
 
Wenyewe waonewe huruma wakati ambao wao hawajamuonea huruma mwanamke...

Na hiyo ndio hekima yake.. .

DsmicSound itimilize haki ya Allah kwa kuwaelekeza watu waelekee kwake. Uovu hauondoshwi kwa uovu. Itangulize mbele huruma kutoka ndani ya moyo wako. Mtume rehma na amani ziwe juu yake alimkubalia Wahshi kuingia kwenye Uislam ijapokuwa Wahshi alimuulia Mtume uncle wake Hamza r.a ijapokuwa Mtume rehma na amani ziwe juu yake alionelea ngumu kumtizama usoni pindi anasilimu. Hii nayo ni sunnah ya Mtume, tuifuate.

Ikiwa Allah anatuambia waja wake waliyokuwa na israfu ya madhambi wasikate tamaa kwenye rehma yake ni huruma ya namna gani hiyo? Tuwe na huruma na waliyopo chini, tutaonewa huruma na aliyepo juu.
 
Subiri siku ya KUDHULUMIWA mama yako au bint yako ndio utaona ni ghadhabu ama la!
Kama familia tulishadhulumiwa millioni 300 unajua ni nini tulichokifanya? Usiruhusu matamanio ya nafsi yakuchukue.
 
Siku Musa alivyomvuta ndevu Harun akimkaba kwa hasira ungekuwepo ungesema Musa hana hekima
Kadhia iliyomfanya Nabii Musa A.S amvute nduguye Nabii Haaruun A.S ndevu utainasibisha na ya kwako?
 
Kadhia iliyomfanya Nabii Musa A.S amvute nduguye Nabii Haaruun A.S ndevu utainasibisha na ya kwako?
Hivi unaijua vizuri kadhia ya Musa na Harun.. .?

Mpuuzi wewe umekuja hapa kwa lengo la kujifanya una upole.. Kwenye Maasi juu ya Allah...

Hekima ni kulifanya jambo kwa kila jambo pahala pake. ..

Kuna mahala pa upole na kuna mahala pa ukali...

Uislaam ni wa katikati. . . Usijikute unaigiza au unaniletea UKHURAFI HAPA.. .

KWANZA HATA UAMBIWEJE UMEWEKA USUSUAVU WA MOYO HUTOKUBALIANA NA MIMI SHIA WEWE NA BABA ZAKO AKILA ALHADI...

KAA MBALI NA MIMI KHURAFI MKUBWA WEWE.. ..
 
Kadhia iliyomfanya Nabii Musa A.S amvute nduguye Nabii Haaruun A.S ndevu utainasibisha na ya kwako?
Tatizo lako nishalijua tayari.. . Hutaweza kuelewana. .. Una yako kichwani. .. SIONGEI NA WEWE TENA. ..
 
Nakusihi pamoja na kuisihi nafsi yangu, livue vazi la kujioni ni msafi katika imani/dini.
Ndio mimi nipo njia salama kwa sababu kigezo changu ni Mtume na maswahaba zake.. . Wewe kabaki na quraniyyuun mwenzako faizafoxy na mashia wenzako. .. Achana na hii post kama inakuuma au kama baba yako yupo bakwata mpe ujumbe huu mwambie aache dhulma.. .
 
Hizi nasaha zako zingekuwa ni nzuri laiti kama ungelizifikisha mahali husika na sio kuja kulaumu mtandaoni.

Kwa BAKWATA hizi ni nasaha zako kwao, na kwa sisi wengine utatufanya tuzidi kuwaona wapigaji tu, kama ulivyosema.

Au ulitaka tujifunze nini kwa haya uliyoyasema?
Kwa mtazamo huu, hakuna kitakachoandikwa JF... Maana kila kiandikwacho kina pahala pa kupeleka.. JF SI PA MAMBO YASIYO NA KWA KWENDA PEKEE.... Wakati mwingine huko kunakotakiwa kupelekewa mambo fulani kuna tatizo linaoloathiri unachokipeleka
 
Wewe ndiye unaona hana sehemu nyingine ya kulalamikia ila hapa.

Je unauhakika kuwa hao wahusika wapo humu? na kama unauhakika kwa nini asiwa PM ili ujumbe uwafikie.

Nauliza tena kunafaida gani ya yeye kutuambia haya aliyosema, zaidi ya kutufanya kuzidi kuwaona wapigaji?

Hebu soma comments za wadau ujionee.
Uhakika kwamba fulani yupo humu tunao kwa VERIFIED MEMBERS PEKEE.. eg Zitto etc.. sisi wengine hatujui kama na JPM yumo personally au la..!! hivyo bado naitazama kuwa ni sahihi kuandika humu...

UNAKUMBUKA WAKATI WA KIPINDI CHA PILI CHA JK, PIUS MSEKWA ALIITAJA JF KAMA SABABU YA KUPUNGUA KWA KURA ZA JK KWA KIPINDI CHA PILI...?? Kwani Pius Msekwa hadi atamke vile, alikuwe/yumo humu?
 
Nakusihi pamoja na kuisihi nafsi yangu, livue vazi la kujioni ni msafi katika imani/dini.
Unanisihi nini wakati ulikuwa unapinga. .. Baada ya kukwambia shahidi ni Allah na nikakwambia nikuletee docs za bank. .. Sasa unanisihi... Basi HUKUWA NA LENGO LA KUJUA UKWELI ILA ILIKUWA NI KUPINGA TU KWA MASLAHI YAKO...

KUTOKUJUA KAMA NI MSAFI AU KUTOKUWA MSAFI NDIO NIFUNGE MLANGO WA KUKEMEA MUNKARI. ..

UISLAAM HAUPO HIVYO.. .

LENGO LA HUU UZI NI KUWEKA BAYANA UBAATWIL WA GHARAMA ZINAZOTOZWA NA BAKWATA KWA WANAWAKE DHAIFU. .. NA KUUWEKA WAZI USITOE HIZO GHARAMA HAZIHUSIANI...
 
TANBIHI: Mods naomba uzi huu msiufute na mkiuhamisha basi nifahamisheni mmehamishia wapi?

Nayaandika haya nikiwa na uchungu mkubwa rohoni mwangu. .. Nikiangalia wale walio pewa mamlaka ya usimamizi wa sheria ya Allah wanafanya mambo mazito ya kumuasi Allah na kudhulumu watu...

Kwanza nibainishe MIMI SIO MTU WA KUENDESHWA NA MIHEMKO YA KIHARAKATI... SINA CHUKI JUU YA BAKWATA NA NAWAHESHIMU SANA KWA SABABU NDIO CHOMBO TEGEMEWA CHA KUWASEMEA WAISLAAM NCHINI NA KUISIMAMISHA SHERIA YA ALLAH. .. LAZIMA TUKITII NA TUKIHESHIMU BILA SHAKA. .. NA NAKITII NA KUKIHESHIMU CHOMBO HIKI. ..

Bakwata Mashaa Allah, Allah amejaalia lwa serikali hii kuruhusu WAISLAAM kujihukumia mambo yao msingi ya kijamii yenyewe na MIFUMO YA KIDOLA ikazitambua na kuzirasimisha sheria hizo(NDOA, TALAKA NA MIRATHI). . . NA HUKUMU ITAKAYOTOLEWA NA BAKWATA KWENYE MASUALA HAYO MAHAKAMA ZA NCHI HAZIWEZI INGILIA.. .

TUMSHUKURU ALLAH KWA HILO.. . Ni jambo mlilolipigania kwa muda mrefu kupata mahakama ya Qadhi, ili waislaam tujihukumie mambo yetu wenyewe bila kuingiliwa kwenye ibada hizo. ..

Kumbe bhanaa wenzetu BAKWATA na BAADHI viongozi Wake waliliangalia kwa jicho la kimaslahi(LA KIUPIGAJI) . .. MCHENI ALLAH NYIE WATU.. . ADHABU YA ALLAH NI CHUNGU. ..HAMTOOKOKA NA VIREMBA VYENU WALA VYETI VYENU VYA THANAWY MLIVYOVIPATIA TANGA...

Mathalani. .. KWENYE MASUALA YA NDOA. .. SIKU ZOTE UKIONA SUALA HILO LIMEFIKA KWA QADHI UJUE MLETAJI NI MWANAMKE(MKE). ..

Kwa sababu Kisheria MWANAUME hapati shida amepewa Mamlaka, YAKIMKERA ANAACHA TU(TALAKA). ..

Ila mwanamke hana uwezo wa kutoa Talaka, Suluhisho lake ni kwa Qadhi...

Na kwa mfumo wenu wa uendeshaji QADHI MMEMUWEKA KUANZIA WILAYA kisha MKOA kisha TAIFA. ..

LAKINI wa kumpata huyo QADHI sasa ndio unaleta ukakasi. ..

Binti akiwa na tatizo kwenye ndoa yake na Mumewe anabidi aanzie shauri lake BAKWATA KATA ili lifike kwa QADHI WA WILAYA. ..

Huko KATA sasa ETI BINTI MASKINI ANATOZWA KUANZIA SH. 15,000/- Ili tu shauri lake lifunguliwe na lisikilizwe. ..

Tujue kabisa OFISI YA BAKWATA KATA HAINA MAMLAKA YA KUSIKILIZA NA KUIAMUA KESI ILI WATAPOTEZA TU MUDA WAKO ILA MWISHO WA SIKU UTAPEWA BARUA UENDE BAKWATA WILAYANI. ..

Ukifika BAKWATA WILAYA kabla hawajakusikiliza lolote... NENDA KADEPOSIT SH. 30,000/-...

ILA KUMBUKA MWENYE MAMLAKA YA KUSIKILIZA NA KUAMUA NI QADHI NA SI BAKWATA(Si sheikh wa wilaya wala katibu wake). . . Ila hela yako wanaitaka...

Kwahiyo mwisho wa siku lazima upelekwe kwa Qadhi. ..

Sijajua na hadi kufika huko kwa Qadhi nako inabidi utoe kiasi gani!

KINACHONIUMA ROHO SIO HELA WANAYOIPIGA. ..

Ila ni HUYU MWANAMKE aliyepeleka Kesi huko. .. KUMBUKA KISHERIA YA KIISLAAM MWANAMKE ANATAKIWA AKAE NYUMBANI NA WATOTO ALEE FAMILIA NA AMTII MUMEWE TU. .. Suala ya kufanya kazi limeruhusiwa kwa mwanamke ila INATILIWA NGUVU ZAIDI ASIFANYE KAZI. ..

ANAYEMHUDUMIA MWANAMKE NI MUMEWE. ..

SASA FIKIRIA Mwanamke amegombana na Mumewe anayemhudumia. .. Ikafikia hatua anahitaji msaada kutoka kwenu BAKWATA. .. LAKINI NINYI MNAMCHAJI OVER SHS. 45,000/- ILI APATE HUDUMA NA MSAADA WENU ILI APATE HAKI YAKE. ..

Sasa hiyo hela anaitoa wapi MDHAIFU HUYU. ..? BADALA YA KUMSAIDIA KUMPA HAKI YAKE MNAMUONGEZEA MATATIZO?

UISLAAM WENU MMEUTOA KWA SHEITWAANI GANI?

MBONA HATA HAMUMUOGOPI ALLAH... HIVI HATA MTUME ANGEKUWA ANAFANYA HUU UPUMBAVU WENU. .. HUU UISLAAM USINGEFIKA HAPA ULIPO. ..

MTUME AMESEMA "ZICHENGUENI HAKI ZA MADHAIFU WAWILI HAWA, NAO NI WANAWAKE NA MAYATIMA".

Lakini ninyi mnashiriki kuwakandamiza. ..

Mcheni Allah ndugu zangu. ..

MTAFANYA WAUKIMBIE UISLAAM NA WAULALAMIKIE UISLAAM KWA TAMAA ZENU ZA MAISHA YA DUNIA YASIYO CHOCHOTE. ..

MNATUPELEKA WAPI NYIE WATU MSIOMUOGOPA ALLAH. ..

MNA TOFAUTI GANI NA WAPIGA DILI WA RICHMOND NA WALA RUSHWA. ..

NYINYI MTACHOMWA KWA KUDHULUMU MALI ZA WATU KWA KUZILA PASIPO HAKI. ..

KAMA MLITAKA KIPATO MNGEKUWA NA SUBRA MKAMSIKILIZA HUYO DHAIFU ALAFU MWISHO MTWANGENI HIZO GHARAMA MWANAUME. .. ILA MWANAMKE MNAMUONEA ANAZIPATA WAPI?

AKIWA HANA MAANA YAKE AKAENDELEE KUMUASI ALLAH KWA ZINAA KWA MLOLONGO WENU KWA KUDHULUMU WATU. ..

mwisho:
NITOE TANBIHI NYINGINE... UISLAAM NA SHERIA ZAKE HAZINA SHIDA KABISA WALA HAZINA KASORO.. .

NA UKIZIFUATA NA ZIKASIMAMISHWA VIZURI KWA UADILIFU UTAUPENDA NA KUUFURAHIA UISLAAM. .. UTA ENJOY NA KUJIVUNIA KUWA MUISLAAM.

ILA HAWA WAPIGA DILI HAWA NDIO WANAOUCHAFUA UISLAAM...

NIMUOMBE MUFTI.. . BARAZA LAKO UNALOJITAHIDI KULISAFISHA NA KULIRUDISHA KWA UMMA... KUNA WATU WA MASLAHI WANAKUANGUSHA.. . WANALICHAFUA BARAZA KWA TAMAA ZAO ZA MATUMBO... MIJITU IMEJAZA VITAMBI NJAA ZIMEWAJAA HAWANA HOFU YA ALLAH... ADHABU YA ALLAH YAWANGOJA WASIPOTUBU. .. ALLAH AWAONGOZE. ..

NB: MODS TAFADHALI UZI HUU USIFUTWE MUHIMU SANA KWA UMMA...
Inamaana mahaka ya Qadhi Tanzania imeanzishwa?
 
Kwa mtazamo huu, hakuna kitakachoandikwa JF... Maana kila kiandikwacho kina pahala pa kupeleka.. JF SI PA MAMBO YASIYO NA KWA KWENDA PEKEE.... Wakati mwingine huko kunakotakiwa kupelekewa mambo fulani kuna tatizo linaoloathiri unachokipeleka
Hao wanaosema uwapelekee huko wenyewe wako tayari kupokea? Wamefungua mlango wa nasaha kupokea?
 
TANBIHI: Mods naomba uzi huu msiufute na mkiuhamisha basi nifahamisheni mmehamishia wapi?

Nayaandika haya nikiwa na uchungu mkubwa rohoni mwangu. .. Nikiangalia wale walio pewa mamlaka ya usimamizi wa sheria ya Allah wanafanya mambo mazito ya kumuasi Allah na kudhulumu watu...

Kwanza nibainishe MIMI SIO MTU WA KUENDESHWA NA MIHEMKO YA KIHARAKATI... SINA CHUKI JUU YA BAKWATA NA NAWAHESHIMU SANA KWA SABABU NDIO CHOMBO TEGEMEWA CHA KUWASEMEA WAISLAAM NCHINI NA KUISIMAMISHA SHERIA YA ALLAH. .. LAZIMA TUKITII NA TUKIHESHIMU BILA SHAKA. .. NA NAKITII NA KUKIHESHIMU CHOMBO HIKI. ..

Bakwata Mashaa Allah, Allah amejaalia lwa serikali hii kuruhusu WAISLAAM kujihukumia mambo yao msingi ya kijamii yenyewe na MIFUMO YA KIDOLA ikazitambua na kuzirasimisha sheria hizo(NDOA, TALAKA NA MIRATHI). . . NA HUKUMU ITAKAYOTOLEWA NA BAKWATA KWENYE MASUALA HAYO MAHAKAMA ZA NCHI HAZIWEZI INGILIA.. .

TUMSHUKURU ALLAH KWA HILO.. . Ni jambo mlilolipigania kwa muda mrefu kupata mahakama ya Qadhi, ili waislaam tujihukumie mambo yetu wenyewe bila kuingiliwa kwenye ibada hizo. ..

Kumbe bhanaa wenzetu BAKWATA na BAADHI viongozi Wake waliliangalia kwa jicho la kimaslahi(LA KIUPIGAJI) . .. MCHENI ALLAH NYIE WATU.. . ADHABU YA ALLAH NI CHUNGU. ..HAMTOOKOKA NA VIREMBA VYENU WALA VYETI VYENU VYA THANAWY MLIVYOVIPATIA TANGA...

Mathalani. .. KWENYE MASUALA YA NDOA. .. SIKU ZOTE UKIONA SUALA HILO LIMEFIKA KWA QADHI UJUE MLETAJI NI MWANAMKE(MKE). ..

Kwa sababu Kisheria MWANAUME hapati shida amepewa Mamlaka, YAKIMKERA ANAACHA TU(TALAKA). ..

Ila mwanamke hana uwezo wa kutoa Talaka, Suluhisho lake ni kwa Qadhi...

Na kwa mfumo wenu wa uendeshaji QADHI MMEMUWEKA KUANZIA WILAYA kisha MKOA kisha TAIFA. ..

LAKINI wa kumpata huyo QADHI sasa ndio unaleta ukakasi. ..

Binti akiwa na tatizo kwenye ndoa yake na Mumewe anabidi aanzie shauri lake BAKWATA KATA ili lifike kwa QADHI WA WILAYA. ..

Huko KATA sasa ETI BINTI MASKINI ANATOZWA KUANZIA SH. 15,000/- Ili tu shauri lake lifunguliwe na lisikilizwe. ..

Tujue kabisa OFISI YA BAKWATA KATA HAINA MAMLAKA YA KUSIKILIZA NA KUIAMUA KESI ILI WATAPOTEZA TU MUDA WAKO ILA MWISHO WA SIKU UTAPEWA BARUA UENDE BAKWATA WILAYANI. ..

Ukifika BAKWATA WILAYA kabla hawajakusikiliza lolote... NENDA KADEPOSIT SH. 30,000/-...

ILA KUMBUKA MWENYE MAMLAKA YA KUSIKILIZA NA KUAMUA NI QADHI NA SI BAKWATA(Si sheikh wa wilaya wala katibu wake). . . Ila hela yako wanaitaka...

Kwahiyo mwisho wa siku lazima upelekwe kwa Qadhi. ..

Sijajua na hadi kufika huko kwa Qadhi nako inabidi utoe kiasi gani!

KINACHONIUMA ROHO SIO HELA WANAYOIPIGA. ..

Ila ni HUYU MWANAMKE aliyepeleka Kesi huko. .. KUMBUKA KISHERIA YA KIISLAAM MWANAMKE ANATAKIWA AKAE NYUMBANI NA WATOTO ALEE FAMILIA NA AMTII MUMEWE TU. .. Suala ya kufanya kazi limeruhusiwa kwa mwanamke ila INATILIWA NGUVU ZAIDI ASIFANYE KAZI. ..

ANAYEMHUDUMIA MWANAMKE NI MUMEWE. ..

SASA FIKIRIA Mwanamke amegombana na Mumewe anayemhudumia. .. Ikafikia hatua anahitaji msaada kutoka kwenu BAKWATA. .. LAKINI NINYI MNAMCHAJI OVER SHS. 45,000/- ILI APATE HUDUMA NA MSAADA WENU ILI APATE HAKI YAKE. ..

Sasa hiyo hela anaitoa wapi MDHAIFU HUYU. ..? BADALA YA KUMSAIDIA KUMPA HAKI YAKE MNAMUONGEZEA MATATIZO?

UISLAAM WENU MMEUTOA KWA SHEITWAANI GANI?

MBONA HATA HAMUMUOGOPI ALLAH... HIVI HATA MTUME ANGEKUWA ANAFANYA HUU UPUMBAVU WENU. .. HUU UISLAAM USINGEFIKA HAPA ULIPO. ..

MTUME AMESEMA "ZICHENGUENI HAKI ZA MADHAIFU WAWILI HAWA, NAO NI WANAWAKE NA MAYATIMA".

Lakini ninyi mnashiriki kuwakandamiza. ..

Mcheni Allah ndugu zangu. ..

MTAFANYA WAUKIMBIE UISLAAM NA WAULALAMIKIE UISLAAM KWA TAMAA ZENU ZA MAISHA YA DUNIA YASIYO CHOCHOTE. ..

MNATUPELEKA WAPI NYIE WATU MSIOMUOGOPA ALLAH. ..

MNA TOFAUTI GANI NA WAPIGA DILI WA RICHMOND NA WALA RUSHWA. ..

NYINYI MTACHOMWA KWA KUDHULUMU MALI ZA WATU KWA KUZILA PASIPO HAKI. ..

KAMA MLITAKA KIPATO MNGEKUWA NA SUBRA MKAMSIKILIZA HUYO DHAIFU ALAFU MWISHO MTWANGENI HIZO GHARAMA MWANAUME. .. ILA MWANAMKE MNAMUONEA ANAZIPATA WAPI?

AKIWA HANA MAANA YAKE AKAENDELEE KUMUASI ALLAH KWA ZINAA KWA MLOLONGO WENU KWA KUDHULUMU WATU. ..

mwisho:
NITOE TANBIHI NYINGINE... UISLAAM NA SHERIA ZAKE HAZINA SHIDA KABISA WALA HAZINA KASORO.. .

NA UKIZIFUATA NA ZIKASIMAMISHWA VIZURI KWA UADILIFU UTAUPENDA NA KUUFURAHIA UISLAAM. .. UTA ENJOY NA KUJIVUNIA KUWA MUISLAAM.

ILA HAWA WAPIGA DILI HAWA NDIO WANAOUCHAFUA UISLAAM...

NIMUOMBE MUFTI.. . BARAZA LAKO UNALOJITAHIDI KULISAFISHA NA KULIRUDISHA KWA UMMA... KUNA WATU WA MASLAHI WANAKUANGUSHA.. . WANALICHAFUA BARAZA KWA TAMAA ZAO ZA MATUMBO... MIJITU IMEJAZA VITAMBI NJAA ZIMEWAJAA HAWANA HOFU YA ALLAH... ADHABU YA ALLAH YAWANGOJA WASIPOTUBU. .. ALLAH AWAONGOZE. ..

NB: MODS TAFADHALI UZI HUU USIFUTWE MUHIMU SANA KWA UMMA...


Mada nzuri sana na inafikirisha lakini ngoja waje watu na busara zao, Sheikh Kipozeo karibu huku mtaani kwetu
 
Back
Top Bottom