Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Yani ni miradi hewa ila anaiendeleza?

Ujinga mzigo
 
Watu wengine wajinga Sana mkuu anadhani anadanganya watoto tofauti ya Deni hili na Yale anayodhani yalikuwa madogo Ni fedha ilitumika kufanyia Nini, Kuna wakati tulifika mahali tukawa tunakopa ili kulipa mishahara. Kwa ujumla bin adamu Hana shukurani.
 
Swali pesa zimetumika kinyume na matumizi au vitu vinaonekana nafikiri hata wewe mwandishi umekiri vitu vilifanyika ila hasira zako ni kuwa hukuambiwa ukweli kama ni mkopo!
 
Halafu hajasema kuwa deni la Kikwete na Mkapa kuiva kwake kunachangia kiasi gani kwenye hizo 78.2T.

Halafu eti yeye ndiye kasababisha Samia kuapishwa Qyummae zake huyu mbwa kasoro mkia!
Kuiva kwa deni maana yake muda wa kuanza kulipa deni lako na riba yake umefika. Haimaanishi kuwa hilo sasa ni deni jipya on top of that.

Na tunapocalculate deni la Taifa maana yake vitu vyote hivyo unavyovisema tumeshaviinclude ndani yake.

Kwa hiyo ukiambiwa mwaka 2005 Kikwete alikuta deni la Trillion 20, basi hilo ndo deni alilolikuta, akizembea kulipa linajiaccumulate, na hiyo accumulation inaongezwa kwenye deni, na kile atajachokopa yeye nacho kinaongezwa kwenye deni.

Kwa hiyo kama Magufuli alikuta deni la Trillion 42 mwaka 2015, basi ndo deni hilo alilokuta limeshainclude vyote (riba na mkopo wa JK), Sasa na yeye Magufuli kaavha deni la Trillion 70, maana yake kaongeza Trilion zake za kutosha tu kwenye deni alilokuta. Yeye kama rais ilibidi Alipe, hakuna excuse kuwa ni madeni ya watangulizi wangu. Kwani Mkapa, JK hawakuwa na watangulizi?, Mbona wao rate ya ukuaji wa deni haikuwa kama ya Magufuli?
 
Ugaidi wa Mbowe unaingiaje kwenye hii mada? Inaonesha mlikuwa mnamchukia "kweri kweri" huyo Mbowe! Magufuli hajawahi kuwa mtendaji ila ni maneno mengi mdomoni na kuwafunga watu midomo wasiseme kwa kutumia mabavu!! Kifupi kichwani alikuwa empty, one man show aliyeamini yeye ni Mungu mtu!! Ila sioni kama ni afya sana kumzungumzia kwa sasa, kwani kwa kupigwa kwake tayari taifa limepona.
 
Vitu vinaonekana, kwa mfano uwanja wa ndege Chato. Ule ni bonge la mradi! 😁
 
Mwenda wazimu huyo!
 
Zama zile ukiandika habari kama hii yatakupata mzito, hivyo Sasa ndio muda sahihi wa kuandika na hakuna tatizo kufanya hivyo.
 
Kwani deni linalipwa na pesa za nje?

Ni msaada tu ndio huwa za nje, borrowed zote ni za ndani. Unachanga unalipa... ukikamilisha mradi ni wako.

We ukikopa ukajenga nyumba then ukikamilisha mkopo ni bank imekujengea au we mwenyewe?
Barabara za mitaani ni pesa ya metropolitan project (world bank ) pesa zilisainiwa kipindi Cha Kikwete

Umeme vijijini tunachangia wananchi kwa kukatwa kwenye Luku / ila zamani ilikuwa MCC project ndio inafund.

Madaraja ya Dar Ni pesa za mjapani.
 
"Haya yote tunayafanya kwa fedha zetu wenyewe"

 
Hizo hospital za kanda unazoengelea ulishawahi kuzitembelea au unaziona kwenye picha,
Majengo yake ni uchafu mtupu, je kuna huduma gani za maana katika majengo hayo?.

Mbona mbeya alishindwa kuifanya iwe kama Bugando,Kcmc na Muhimbili?.

Tumekulia maisha ya umaskini hivyo hudhani gorofa/jengo ndiyo kiwango cha huduma.

Jamaa vitu vyake vyote alivyovifanya uongo ulikuwa mwingi sana, wala hakuwa na uchungu na fedha ya nchi yetu bali aliangalia kuufurahisha moyo wake uliojaa maisha ya sifa.
 
Kwa hiyo Mkuu unapenda utawala wa "One Man Show"? Kila kitu aamue Rais? Ni ngumu sana kwa nchi kubwa kama TZ!! May be inaweza kuwa sababu ya kuuchokonoa moyo wake kwa miaka 5 tu ya kwanza, huwezi ukabeba matatizo ya watanzania yote kwenye moyo mmoja!! Ila nakumbuka alisema analala na mafaili kitandani, which is not healthy!! Haijalishi watu wako wapo corrupt/wazembe kiasi gani lazima uwe na watu katika hao uwaamini na wakusaidie, atayezingua nawe unamzingua
 
Magufuli alikuwa anakopa kinyemela na kuna kipindi alikuwa black listed na WB kuwa amevuka threshold. Amekopa sana AfDB na commercial banks kama StanChart na Credit Suisse.
 
Raisi kuwa mahala pote kwa wakati mmoja aliwezekani na Magufuli hakuwa ‘one man show’ it’s just a label ya watu ambao hawakuzoea kusimamiwa.

Boss ndio mwenye mamlaka ya ku set agenda (pamoja na ilani ya chama) kwa maana hiyo anaweza amua namna kazi itakavyofanyika kufikia malengo.

Tatizo huo ulikuwa ni utaratibu mpya wa uwajibikaji ambao watu serikalini awakuzoea na kwenye chama watu kutotaka reforms.

But otherwise pamoja na mapungufu yake Magufuli alikuwa anaipeleka nchi kwenye right direction.

Anyway asubuhi njema.
 
Ila watanzania mna ujinga Sana sijui ni madhara ya elimu tunayopata Hadi tunAshindwa kutafuta taarifa.

Barabara za lami na mataa unayoyaona mitaani kwenye majiji yote Ni mradi wa Dar metropolitan project , huu mradi aliusaini kikwete na unaenda kuisha mwaka 2022. Ni pesa za world bank. Sijui kwanini sifa mnampa Magufuli peke Yake. Ingia hapa world usome mwenyewe. Development Projects : Dar es Salaam Metropolitan Development Project - P123134

Sipingi uchapakazi wa Magufuli ila tuache kupotosha.

Mradi wa umeme vijijini kikwete aliuacha ukiwa unakuwa financed na MCC PROJECT ya Marekani na lengo ilikuwa vijiji vyote viwe na umeme mpaka 2020. Ila Magufuli alipokonywa huo mradi wa MCC na Marekani, leo tunakatwa hela za REA kila tukinunua Luku.


Daraja la Ubungo upembuzi yakinifu na mkopo wa pesa zake umeanza kuanzia kipindi Cha kikwete. Naomba uchukue muda kusoma hii article TANROADS – Ubungo Interchange – Dar es Salaam
 
Hoja ya kipuuzi kabisa! Unasema miaka uote hakuna kilichofanyika! Nini kikubwa cha pekee kikubwa alichofanya marehemu ambacho kilikuwa hakijafanyika?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…