a4afrika
JF-Expert Member
- Apr 13, 2012
- 1,456
- 1,459
Asante Mkuu wangu Mchambuzi kwa kunielewa.
UCHANGA wa Taifa! Tunapozungumza Uchanga moja kwa moja tunagusa Ukomavu. Je, vigezo gani vitumike? Binafsi naona hivi viwili;-
1. Uwezo wa Taifa Kujiendesha lenyewe! Uchanga ni utepetepe, kama ni mtoto hawezi hata kukaa chini mwenyewe. Ukomavu ni KUJIMUDU, kama ni mtoto ni yule anayeweza kukaa ama kusimama mwenyewe pasi kushikiliwa! Sasa sisi kama Taifa, kipi tunaweza kujidai nacho kuwa tunajimudu nacho? Je, ni siasa zetu hizi za kusikiliza mzungu anatakaje? Ama Uchumi wetu huu wa kuamuliwa na mzungu? (copy and paste style) Hata tamaduni zetu wenyewe hatuwezi kuzifanya zisimame, TUMEKOMAA NINI? Je, sisi si kama mtoto amtegemeae mamaye kumkalisha ama kumsimamisha?
2. Uzoefu: Hapa tunaweza kupima uchanga ama ukomavu wa Taifa kwa kuangalia Umri! "Ukiona nyani mzee ujue amekwepa mishale mingi". Miaka 50 si haba kuitwa mkomavu! Maana ndaniye, kama Taifa tume-experience mengi mno...njaa, magonjwa, na hata vita, sera na mifumo tofauti tofauti, itikadi mbalimbali, imani, sayansi na teknolojia n.k...vyote tumevishuhudia! Je, yatosha kusema TUMEKOMAA kwakuwa tu UMRI WETU umeruhusu kushuhudia MAMBO MENGI? Binafsi ninahofu kigezo hicho, kwani inaweza tokea ya mfyatua tofali la udongo, anayesubiri wiki moja kwenda kunyanyua tofali kujengea, kumbe kuna mwenye HILA naye ambaye tangu siku ya kwanza amekuwa akilimwagia maji tofali lisikauke hadi siku ya saba. Ole kwa mnyanyua tofali, akidhani limekomaa na kulinyanyua kwa pupa kwakuwa tu limeshafikisha wiki, LITAMPASUKIA MIKONO na kubaki mdomo wazi! Na hiyo ndio Tanzania. "UKOMAVU WA TAIFA UTAPIMWA NA FIKRA ZA WATU WAKE KATIKA KUAMUA NAMNA BORA YA KULI-TREAT TAIFA LAO WENYEWE, KULINGANA NA MAZINGIRA NA NYAKATI ZAO WENYEWE" tukifikia hapo, ni sahihi kusema tumekomaa!
*Mkuu wangu Mchambuzi, nimefurahi sana kueleweka kuhusu Demokrasia na anguko lake. Inquality, poverty, ethnic, religious polarization, fragmentation, e.t.c kama vyanzo vya anguko la Demokrasia...vyote hivyo vinadhihirisha "IRRELEVANCE OF DEMOCRACY" katika mataifa yetu Afrika! Mfumo usiosadifu jinsi tulivyo utatufikisha wapi? Mfano wa kutosadifu kwa huu upuuzi, INQUALITY haikuanza leo, tangu ukoloni. Tunajua kwamba yapo maeneo ambyo yalipata huduma za kijamii mapema sana, mfano shule na hospitali. Lakini yapo maeneo pia ambayo yalipata kujua shule na hospitali miaka 10-20 baada ya uhuru. Leo demokrasia inataka watu hao wawili tofauti, wa-be treated sawa! Kama ni fursa ya ajira washindanishwe, biashara, uongozi, kula, kuvaa na kulala kwao kuwekwe kwenye sahani moja wajinyakulie. Tumesahau kuwa kipindi A anaenda shule B alikuwa shambani analima ama udongoni amejilaza na maumivu ya kichwa! No Consideration, na watu wanakenua meno. Itaachaje kuzua machafuko?
Hapa umenena maneno mazito sana mkuu wangu, katika nchi changa, "Wanasiasa wanatafuta kuungwa mkono by exploiting nationalism and unity exaggreting internal threats kwa umma" cha kusikitisha zaidi system imewaruhusu kufanya hayo kwa madai ya uhuru wa kuropoka! TUNAENDA WAPI NDUGU ZANGU? Hakika hilo linadhihirisha uchanga wetu. Maana katika ukomavu wa taifa kinachopimwa ni FIKRA za watu wake sio umri! Kama wenyenchi wenyewe wanashindwa kutofautisha kujenga na kubomoa nchi, kipi kilichokomaa kwao? Labda tuite UCHANGA ULIOKOMAA.
Katiba Mpya na matumaini ya watanzania hii ni HATARI lakini salama, maana wengi wataamka na kujua thamani yako katika maendeleo yetu. Niliwahi kusema hivi, katiba ni maafikiano yanayorasimisha SERA juu ya mfumo fulani kutoka Falsafa/Itikadi fulani. Mifumo iliyopo leo imeoza na ndiyo hiyo ifungayo zoezi la kupata katiba mpya. Hakuna misingi mikuu ya kulijenga taifa, ndio maana tunahitaji "REFORMATION OF STATE, OUR OWN STATE" Mkuu Mchambuzi ulishanena hili, leo limerudi tena, hapo ndipo napoichukia JF maana litapita tena. Upi uwe mwisho wa kelele hizi tupigazo?
Mungu wetu yu tayari kutushindia vitani.
Anaita sasa!
UCHANGA wa Taifa! Tunapozungumza Uchanga moja kwa moja tunagusa Ukomavu. Je, vigezo gani vitumike? Binafsi naona hivi viwili;-
1. Uwezo wa Taifa Kujiendesha lenyewe! Uchanga ni utepetepe, kama ni mtoto hawezi hata kukaa chini mwenyewe. Ukomavu ni KUJIMUDU, kama ni mtoto ni yule anayeweza kukaa ama kusimama mwenyewe pasi kushikiliwa! Sasa sisi kama Taifa, kipi tunaweza kujidai nacho kuwa tunajimudu nacho? Je, ni siasa zetu hizi za kusikiliza mzungu anatakaje? Ama Uchumi wetu huu wa kuamuliwa na mzungu? (copy and paste style) Hata tamaduni zetu wenyewe hatuwezi kuzifanya zisimame, TUMEKOMAA NINI? Je, sisi si kama mtoto amtegemeae mamaye kumkalisha ama kumsimamisha?
2. Uzoefu: Hapa tunaweza kupima uchanga ama ukomavu wa Taifa kwa kuangalia Umri! "Ukiona nyani mzee ujue amekwepa mishale mingi". Miaka 50 si haba kuitwa mkomavu! Maana ndaniye, kama Taifa tume-experience mengi mno...njaa, magonjwa, na hata vita, sera na mifumo tofauti tofauti, itikadi mbalimbali, imani, sayansi na teknolojia n.k...vyote tumevishuhudia! Je, yatosha kusema TUMEKOMAA kwakuwa tu UMRI WETU umeruhusu kushuhudia MAMBO MENGI? Binafsi ninahofu kigezo hicho, kwani inaweza tokea ya mfyatua tofali la udongo, anayesubiri wiki moja kwenda kunyanyua tofali kujengea, kumbe kuna mwenye HILA naye ambaye tangu siku ya kwanza amekuwa akilimwagia maji tofali lisikauke hadi siku ya saba. Ole kwa mnyanyua tofali, akidhani limekomaa na kulinyanyua kwa pupa kwakuwa tu limeshafikisha wiki, LITAMPASUKIA MIKONO na kubaki mdomo wazi! Na hiyo ndio Tanzania. "UKOMAVU WA TAIFA UTAPIMWA NA FIKRA ZA WATU WAKE KATIKA KUAMUA NAMNA BORA YA KULI-TREAT TAIFA LAO WENYEWE, KULINGANA NA MAZINGIRA NA NYAKATI ZAO WENYEWE" tukifikia hapo, ni sahihi kusema tumekomaa!
*Mkuu wangu Mchambuzi, nimefurahi sana kueleweka kuhusu Demokrasia na anguko lake. Inquality, poverty, ethnic, religious polarization, fragmentation, e.t.c kama vyanzo vya anguko la Demokrasia...vyote hivyo vinadhihirisha "IRRELEVANCE OF DEMOCRACY" katika mataifa yetu Afrika! Mfumo usiosadifu jinsi tulivyo utatufikisha wapi? Mfano wa kutosadifu kwa huu upuuzi, INQUALITY haikuanza leo, tangu ukoloni. Tunajua kwamba yapo maeneo ambyo yalipata huduma za kijamii mapema sana, mfano shule na hospitali. Lakini yapo maeneo pia ambayo yalipata kujua shule na hospitali miaka 10-20 baada ya uhuru. Leo demokrasia inataka watu hao wawili tofauti, wa-be treated sawa! Kama ni fursa ya ajira washindanishwe, biashara, uongozi, kula, kuvaa na kulala kwao kuwekwe kwenye sahani moja wajinyakulie. Tumesahau kuwa kipindi A anaenda shule B alikuwa shambani analima ama udongoni amejilaza na maumivu ya kichwa! No Consideration, na watu wanakenua meno. Itaachaje kuzua machafuko?
Hapa umenena maneno mazito sana mkuu wangu, katika nchi changa, "Wanasiasa wanatafuta kuungwa mkono by exploiting nationalism and unity exaggreting internal threats kwa umma" cha kusikitisha zaidi system imewaruhusu kufanya hayo kwa madai ya uhuru wa kuropoka! TUNAENDA WAPI NDUGU ZANGU? Hakika hilo linadhihirisha uchanga wetu. Maana katika ukomavu wa taifa kinachopimwa ni FIKRA za watu wake sio umri! Kama wenyenchi wenyewe wanashindwa kutofautisha kujenga na kubomoa nchi, kipi kilichokomaa kwao? Labda tuite UCHANGA ULIOKOMAA.
Katiba Mpya na matumaini ya watanzania hii ni HATARI lakini salama, maana wengi wataamka na kujua thamani yako katika maendeleo yetu. Niliwahi kusema hivi, katiba ni maafikiano yanayorasimisha SERA juu ya mfumo fulani kutoka Falsafa/Itikadi fulani. Mifumo iliyopo leo imeoza na ndiyo hiyo ifungayo zoezi la kupata katiba mpya. Hakuna misingi mikuu ya kulijenga taifa, ndio maana tunahitaji "REFORMATION OF STATE, OUR OWN STATE" Mkuu Mchambuzi ulishanena hili, leo limerudi tena, hapo ndipo napoichukia JF maana litapita tena. Upi uwe mwisho wa kelele hizi tupigazo?
Mungu wetu yu tayari kutushindia vitani.
Anaita sasa!