Balozi wa Kenya aishambulia Russia kwa kuyatambua kama majimbo huru ya Ukraine

Balozi wa Kenya aishambulia Russia kwa kuyatambua kama majimbo huru ya Ukraine

Kuna mmoja ambaye alipewa kiti cha kuazima kama ilivyo kenya, yaani mwanachama wa muda wa baraza la usalama, alipinga kitu cha marekani. Marekani alikuwa na kitu chake, akawa anafanya ushawishi wa kukipitisha kwenye baraza. Huyo wa kiti cha kuazima, akapiga kura ya hapana. marekani wakamuambia, hiyo kura yako ina gharama kubwa sana. Itakugharimu sana. Baada ya muda, akashangaa miradi ambayo ilikuwa inafadhiriwa na marekani nchini mwake ikanyimwa fedha, mambo mengi ya misaada yakasitishwa. Mpaka ile nchi ikasema, tungejua wala tusingegombea kupata hicho kiti. 😂 🤣 😛
Taja jina la nchi hiyo.
 
Kuna mmoja ambaye alipewa kiti cha kuazima kama ilivyo kenya, yaani mwanachama wa muda wa baraza la usalama, alipinga kitu cha marekani. Marekani alikuwa na kitu chake, akawa anafanya ushawishi wa kukipitisha kwenye baraza. Huyo wa kiti cha kuazima, akapiga kura ya hapana. marekani wakamuambia, hiyo kura yako ina gharama kubwa sana. Itakugharimu sana. Baada ya muda, akashangaa miradi ambayo ilikuwa inafadhiriwa na marekani nchini mwake ikanyimwa fedha, mambo mengi ya misaada yakasitishwa. Mpaka ile nchi ikasema, tungejua wala tusingegombea kupata hicho kiti. [emoji23] [emoji1787] 😛
Pia......hata Salim Ahmed Salim ...aliwahi kuipinga USA ....ilivyokuwa inakataa
Kuitambua PRC ( China) Kama nchi mwanachama wa UN .........

Kipind kiti cha China kilikua kinashikiriwa na TAIWAN.....chin ya Chiang kai shek
 
Mpaka sasa mataifa yaliyounga mkono kwa uwazi utambuzi wa majimbo hayo kuwa ni "huru" ni Venezuela, Cuba, Nicaragua na Syria ya Assad. Bado nasubiri statements za mataifa mengine.

Waingereza wana msemo wao maarufu sana unasema: Birds of a feather flock together!
taarifa hizi nzuri huwa hazisemwi na marekani na washirika wake
 
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilifanya mkutano wa dharura baada ya Rais wa Urusi Vladimir Putin kusema kwamba sasa anatambua sehemu ya Ukraine kama Urusi na atatuma wanajeshi wake kuwa walinzi wa amani katika majimbo hayo mawili.

Uingereza ilichukua hatua ya haraka kutangaza vikwazo. Urusi ilikemewa na nchi nyingi zikiwemo Mexico, Ireland, Norway, Ghana, na nyinginezo. Lakini ni Kenya ndio iliyojitokeza kwa makali yake kwa jinsi ilivyojibu hatua hiyo ya Urusi.

Balozi wake kwa Umoja wa Mataifa Martin Kimani alitoa hotuba ambayo wengi wamejitokeza kuisifia kama iliyoeleza kwa urahisi na ukali unaostahiki ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa ambao urusi imetekeleza.

"Uhuru wa eneo na mamlaka ya Ukraine yamevunjwa," alisema Balozi Martin Kimani.

"Mkataba wa Umoja wa Mataifa unaendelea kudhoofika chini ya shambulio hilo lisilo na huruma. Kwa wakati mmoja unatolewa kwa heshima na nchi zile zile ambazo kisha zikaupa kisogo katika kutekeleza malengo yanayopinga amani na usalama.... Kenya inasikitishwa sana na tangazo lililotolewa na Urusi la kutambua maeneo ya Ukraine kama mataifa huru'

Aliendelea kusema kuwa Kenya ina wasiwasi mkubwa juu ya athari ambayo Urusi inaweza kuwa nayo ikiwa itaruhusiwa na UN kushambulia na kunyakua nchi zingine.

Mfano wake ni kwamba mipaka ya Afrika ilikubaliwa na nchi zote za huko, licha ya mipaka hiyo kulazimishwa na wakoloni. Alieleza kuwa mataifa ya Afrika yalifanya uamuzi huo badala ya kuwa na vita visivyoisha.

"Tulikataa upanuzi kwa misingi yoyote, ikiwa ni pamoja na rangi, kabila, au kitamaduni," Kimani alisema. "

Baada ya hotuba yake hiyo ,maoni yalianza kutolewa huku akisifiwa kwa hotuba yake hiyo .Watumiaji wa mitandao ya kijamii walituma jumbe za kuonyesha 'makali' ya ujumbe wake na jinsi Kimani alivyojieleza na kuwakilisha msimamo wa kenya kuhusu hatua ya Urusi ;

Balozi Martin Kimani ni nani?

Balozi kimani aliteuliwa kuwa mwakilishi wa Kudumu wa Kenya katika Umoja wa mataifa mwaka wa 2020 .

Kabla ya uteuzi wake wa hivi punde zaidi, Bw. Kimani alikuwa Mjumbe Maalumu wa Rais wa Kukabiliana na Itikadi kali na Mkurugenzi wa Kituo cha Kitaifa cha Kupambana na Ugaidi nchini Kenya kuanzia Septemba 2015.

Pia aliwahi kuwa Katibu wa Mikakati katika Ofisi ya Mtendaji wa Rais kuanzia Disemba 2018.

Bw. Kimani alikuwa Mwakilishi wa Kudumu wa Kenya katika Umoja wa Mataifa huko Nairobi, Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa (UNEP) na Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Makazi (UN-Habitat) kati ya Desemba 2012 na Septemba 2015.

Mapema katika taaluma yake, Bw. Kimani alikuwa Mkurugenzi katika Mamlaka ya Kiserikali juu ya Maendeleo (IGAD) nchini Ethiopia, kuanzia Aprili 2011 hadi Disemba 2012.

Bw. Kimani alipata PhD na shahada ya uzamili katika masomo ya vita katika Chuo cha King's College, Chuo Kikuu cha London, mwaka wa 2010 na 2003, mtawalia, na pia shahada ya kwanza katika Chuo Kikuu cha New Hampshire mwaka wa 1996

Source bbc swahili

Je, kiutalaamu hili limekaaje ....au ni sawa na sisimizi kumpiga biti tembo[emoji23][emoji23]
View attachment 2127616
kenya imeonyesha dhahiri kujikomba kwa ulaya na us, mambo yake mengi ya ndani yamewashinda ikiwamo njaa, mgogoro na somalia, ukabila, ugaidi .....wanaenda kujikomba, njaa mbaya sana
 
Back
Top Bottom