Balozi wa Kenya nchini Tanzania: Hatuiangalii Tanzania kama jirani bali kama Ndugu. Sisi sio maadui, adui yetu ni Corona

Porojo tu, hakuna hoja hapo, huwezi kujiamulia kupima mtu against his will
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao hata KUB kwenye mabunge yao hawi mtu " mbabaishaji" kama kule bongoland!
 
Hao wakenya wanajua udhaifu wetu sana wanatumia diplomasia kutukosoa sana wamejishusha wakati wanajua sisi tunafanya maamuzi kwa mihemko bila logic hawawezi kumjibu chochote Kenya intaendelea kutunyoonya paka pale tutakapo pata viongozi wanao jua PR unaona wakuu wamikoa watanzania kama laymen hawana lolote kichwani duh Mungu ibariki Tz Mungu ibariki Africa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Balozi wa Kenya nchi Tanzania anazungumza na Vyombo vya habari muda huuu kahusiana na sitofahamu kati ya Tanzania na Kenya
Hii sitofahamu kaiona leo? Hivi hawa wakenya wanajifanya wanakili sana? Madereva wetu walivyokuwa wanateseka mpakani hiyo haikuwa sintofaham? Hiyo sintofahamu kaiona jana ndio kaamua kuitolea maelezo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
“Rais Kenyatta amenituma hapa, anasema Kenya haiiangalii Tanzania kama jirani bali kama Ndugu, sisi sio maadui, adui yetu ni corona, ndio maana alikuwa Rais wa kwanza kuingia Chato kumsalimia JPM, akachukua dhahabu akasema mpelekeeni Magufuli” -Dany Kazungu, Balozi wa Kenya nchini Tanzania


“Bila hii corona April 26 mwaka huu Kenyatta alipanga aje asherehekee na Watanzania Muungano, alipanga awe na ziara ya muda mrefu hapa TZ kuliko Rais yeyote, uamuzi ambao Kenya imechukua kuhusu safari za mipakani sio kwasababu ya Tanzania bali adui yetu ni kirusi”-Balozi Kazungu

“Hakuna Mkenya anayemuombea mabaya Mtanzania, Wakenya tunawaombea Watanzania mpigane na janga hili, na sisi pia mtuombee, tusianze kukorogwa na kirusi hiki, tusianze kugongana kisa corona, Watu watulie, Viongozi wetu watakutana na tutalimaliza” -Balozi Kazungu
#MillardAyoUPDATES
 
Tunasubiri hotuba ya Mbowe kuijibu hotuba hii ya balozi wa Kenya, faster faster.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…