Balozi wa Uturuki: Shule za Feza zinaidanganya Tanzania, naamini Serikali itachukua hatua

haya ya balozi,ss kwetu watz tunasema ni umbea na kuchomeana. Tulishakubaliana sote kila mtu ale kutokana na urefu wa kamba yake!! Kama baloz na rais wake eldogan hawaliziki na urefu wa kamba zao ,basi wakae kimya!!!

Ugomvi wao ,hautuhusu ,wamalizane huko huko kwao uturuki,kwetu hakuna mahali wamevunja Sheria za nchi!!
 
Mnapigwa au mnafata elimu bora kwa walimu wanaolipwa vizuri? Acha kuiga kama huyawezi!
 
aibu mgeni anakuja kuwafundisha jiographia yenu, kiswahili chenu, siasa zenu, historia yenu vizuri kuliko wenyewe mnavyoweza kujifundisha
 
Mpumbavu huyo, amesahau Erdogan alikuja kipindi fulan akamletea jiwe hizo stori lakin jiwe akamtolea nje, sasa kama jiwe mwenyewe aliona ni upuuzi sembuse mama!!!!
 
Heshima yako ndugu. Ni faida kupata watu wanaojua Mambo hivi
 
Na yeye Sasa hivi anajitadi sana kwenye dini
Agenda ya Uturuki, lengo sio kuonekana mtu wa dini bali kueneza dini na kuwapa watu wanachokitaka. Utawaona wapenda dini kama wewe unaona dini muhimu, utawaona ni msaada wako wakati wa vita, etc. Uturuki ilisambaza dini enzi za zamani. Waturuki kina Mehmet walipigana vita mpaka wakafikisha Uislamu Ulaya hadi nchini Spain. Wakatishia kuiteka Vatican wakafeli kwa kutumia nguvu badala ya akili.

Uturuki ina historia iliyoshuba na sasa hivi wanatamani kurudisha heshima yao. Walianza wakiwa centre of Byzantine Empire baada ya Roman Empire kudondoka, wakaja kuwa centre of Ottoman empire. Hata mji wao mkubwa na wa kihistoria wa Constantinople una asili ya dini mbili Ukristo na Uislamu. Nadhani unasema anajitahidi kwenye dini kwa sababu alirudisha msikiti wa Hagia Sofia kwa Waislamu. Hilo ni kosa la kihistoria alifanya kufurahisha raia, hana mwamko wowote wa kidini.

Viongozi wengi huko duniani hawana muda na mambo ya dini, ni kutafuta popularity kama kuitwa Chifu Hangaya. Saudi Arabia pale hawafatili dini kabisa na kuswali yawezekana hawaswali wale. Unahisi kwanini members wengi wa familia ya kifalme wanamiliki majumba ya kifahari Ulaya hasa Ufaransa kwenye raha, tena majumba yamejitenga uko ni sababu kule wako free kufanya mambo ya ajabu ajabu yasiyopatikana kwao kisa sheria na watu watanionaje. Syria pale Assad havai kanzu ni mwendo wa suti kali slim fit nyeusi hata mke wake hafuniki nywele mara nyingi tu. Wananchi ndio wanakesha msikitini
 
Sisi kama taifa tuamue kubaki na kashule kamoja ili tukose mengi ya serikali ya Uturuki au tulazimishe kauzwe ili tupate la kuanzia kutynufaisha. Uturuki ni nchi inarespond haraka sana ukiomba msaada wa kiteknolojia, sayansi, elimu, etc.
 

πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘ Umenena vizuri kabisa.

Uhasimu wa kisiasa kati ya Rais wa Uturuki na mfanya biashara na mwanasiasa maarufu wa upinzani wa Uturuki Gulan, ndio maana balozi wa Uturuki kasema hivyo, sbb balozi ni kibaraka wa serikali ya Rais Erdogan, hivyo serikali ya Erdogan inataka kufilisi mali za Gulan kokote kule duniani, ila imeshindwa.
 
kwa stail hii inabid watu wajiongeze
 
na siku zote watu wenye nguvu huwa wapo vizur kifedha
 
hii vita itachukua mda kuisha na kuisha kwake mpaka mmoja atakaposhindwa na hakuna anayekubali kushindwa
 
Ya dini yametoka wapi? Nimekujibu hoja yako, pls usiniharibie siku,
 
Hizi shule zinamilikiwa na mpinzani wa serikali yaa uturuki anaeishi uhamishoni nchini marekani kwahiyo hilo tangazo la balozi halina maajabu yeyote. Feza schools kazeni buti nawakubali sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…