Banc ABC wamekataa kulipwa, msaada wenu unahitajika

Banc ABC wamekataa kulipwa, msaada wenu unahitajika

Ni baada ya kuhangaika huku na huko bila kupata mkopo wa kuendeleza biashara yangu hatimae nikakutana na hii Banc ABC wakanipatia mkopo wa miaka miwili Ila kwa makubaliano kuwa nikipata pesa yao kabla ya huo muda naweza kulipa pesa yao tukaachana.

Kweli nilipambana kwa namna yangu na Hali yangu Hadi nikapata pesa yao baada ya miezi mitatu tu na biashara yangu inaendelea.

Tatizo limeanza pale niliporudi kwao Banc ABC kutaka balance yangu ili niwalipe tuachane.

Ni mwezi wa nne Sasa tangu niombe kulipa Deni kuanzia mwezi wa tano Hadi wa Tisa (mwezi huu) wananisumbua, hawataki kunipatia balance (kiasi kilichobakia).

Msaada tafadhari nifanyeje nilipe Deni?

Sitaki kudaiwa Ila wananilazimisha, Wazo langu ilikuwa niwapeleke mahakamani Ila nimewaza huenda Kuna sehemu naweza kuanzia kuepusha lawama zisizo na msingi.

Msaada wa hatua za kuanzia...
Neenda BOT mkuuu wapigie chapu wanakupa soon
 
nafikiri tatizo hapo ni wao tu kukuelewesha mmalizane.
Mfano: Kama ulichukua milioni mbili ila kwa miaka miwili utarejesha milioni tatu
Wanachotakiwa kukuambia hapo ni kuwa, uwarejeshee milioni tatu zao yaishe. Haijalishi umerudisha haraka kiasi gani kwani ulisaini mkataba wa marejesho ya miaka miwili.
We mpare unatutia aibu wapare wenzako. Hiyo miaka mitatu ina include na riba. Jamaa anatakiwa alipe hadi sasa adaiwacho.
 
nafikiri tatizo hapo ni wao tu kukuelewesha mmalizane.
Mfano: Kama ulichukua milioni mbili ila kwa miaka miwili utarejesha milioni tatu
Wanachotakiwa kukuambia hapo ni kuwa, uwarejeshee milioni tatu zao yaishe. Haijalishi umerudisha haraka kiasi gani kwani ulisaini mkataba wa marejesho ya miaka miwili.
Hapana tulikubalia muda ndiyo unaamua kiasi Cha malipo.
 
Ni baada ya kuhangaika huku na huko bila kupata mkopo wa kuendeleza biashara yangu hatimae nikakutana na hii Banc ABC wakanipatia mkopo wa miaka miwili Ila kwa makubaliano kuwa nikipata pesa yao kabla ya huo muda naweza kulipa pesa yao tukaachana.

Kweli nilipambana kwa namna yangu na Hali yangu Hadi nikapata pesa yao baada ya miezi mitatu tu na biashara yangu inaendelea.

Tatizo limeanza pale niliporudi kwao Banc ABC kutaka balance yangu ili niwalipe tuachane.

Ni mwezi wa nne Sasa tangu niombe kulipa Deni kuanzia mwezi wa tano Hadi wa Tisa (mwezi huu) wananisumbua, hawataki kunipatia balance (kiasi kilichobakia).

Msaada tafadhari nifanyeje nilipe Deni?

Sitaki kudaiwa Ila wananilazimisha, Wazo langu ilikuwa niwapeleke mahakamani Ila nimewaza huenda Kuna sehemu naweza kuanzia kuepusha lawama zisizo na msingi.

Msaada wa hatua za kuanzia...
Leta mkataba wa mkopo, otherwise kuchangia hapa itakuwa useless
 
Nenda BOT,kuna jamaa yangu pia alikuwa anasumbuliwa na letshego,walikuwa hawataki kumpa balance,alivyopeleka malalamuko BOT, balance allipata faster
Nipo mikoani huku hakuna BOT Ila wakizidi nitapanda Basi nienda DAR kuisaka haki yangu.
 
Hao hawatakiwi hekima wala kubembelezwa. Wana msemo wao mmoja kuwa hawataki kupoteza mteja.

Wakati nafanya kazi serikalini nilipata msiba wa mzee. Msiba ule ulikuwa wa ghafla sana nikatakiwa nisafiri toka kanda ya ziwa to nyumbani Mtwara nami ndio mkubwa ikabidi niongeze nguvu kidogo.

Nikaenda wanikope 1,200,000 na wakaingizia makato kwenye mshahara wangu na nilikubaljana nao niilipe hiyo kwa miezi 6. Kweli wakaingiza mzigo nikiwa nyumbani na ulinisaidia kwenye msiba hadi ukaisha fresh.

Baada ya mwezi 1 nikapata pesa yao nikasema niwarudidhie na wanitoe kama mteja wako. Ilikuwa ni mbinde, nikasema hawa nikiwachekea hawatanitoa. Niliwawashia moto pale Mwanza mpaka wakanitoa na HRO nae akawawashia moto kuwa hataingiza makato ya mtu mwingine toka kwenye taasisi yetu awe mteja wao hadi wanitoe.

Usiwaendekeze, kawawashie moto watakutoa wapuuzi hao.
 
Hao hawatakiwi hekima wala kubembelezwa. Wana msemo wao mmoja kuwa hawataki kupoteza mteja.

Wakati nafanya kazi serikalini nilipata msiba wa mzee. Msiba ule ulikuwa wa ghafla sana nikatakiwa nisafiri toka kanda ya ziwa to nyumbani Mtwara nami ndio mkubwa ikabidi niongeze nguvu kidogo.

Nikaenda wanikope 1,200,000 na wakaingizia makato kwenye mshahara wangu na nilikubaljana nao niilipe hiyo kwa miezi 6. Kweli wakaingiza mzigo nikiwa nyumbani na ulinisaidia kwenye msiba hadi ukaisha fresh.

Baada ya mwezi 1 nikapata pesa yao nikasema niwarudidhie na wanitoe kama mteja wako. Ilikuwa ni mbinde, nikasema hawa nikiwachekea hawatanitoa. Niliwawashia moto pale Mwanza mpaka wakanitoa na HRO nae akawawashia moto kuwa hataingiza makato ya mtu mwingine toka kwenye taasisi yetu awe mteja wao hadi wanitoe.

Usiwaendekeze, kawawashie moto watakutoa wapuuzi hao.
Vipi nikishirikiana na mahakama?
 
Back
Top Bottom