Banc ABC wamekataa kulipwa, msaada wenu unahitajika

Banc ABC wamekataa kulipwa, msaada wenu unahitajika

Ni baada ya kuhangaika huku na huko bila kupata mkopo wa kuendeleza biashara yangu hatimae nikakutana na hii Banc ABC wakanipatia mkopo wa miaka miwili Ila kwa makubaliano kuwa nikipata pesa yao kabla ya huo muda naweza kulipa pesa yao tukaachana.

Kweli nilipambana kwa namna yangu na Hali yangu Hadi nikapata pesa yao baada ya miezi mitatu tu na biashara yangu inaendelea.

Tatizo limeanza pale niliporudi kwao Banc ABC kutaka balance yangu ili niwalipe tuachane.

Ni mwezi wa nne Sasa tangu niombe kulipa Deni kuanzia mwezi wa tano Hadi wa Tisa (mwezi huu) wananisumbua, hawataki kunipatia balance (kiasi kilichobakia).

Msaada tafadhari nifanyeje nilipe Deni?

Sitaki kudaiwa Ila wananilazimisha, Wazo langu ilikuwa niwapeleke mahakamani Ila nimewaza huenda Kuna sehemu naweza kuanzia kuepusha lawama zisizo na msingi.

Msaada wa hatua za kuanzia...
Nenda pale BOT mkuu.

Hizi bank si rafiki kwa wakopaji. Ukichelewesha jau
Ukiwahisha jau
Hawana jema
 
Ni baada ya kuhangaika huku na huko bila kupata mkopo wa kuendeleza biashara yangu hatimae nikakutana na hii Banc ABC wakanipatia mkopo wa miaka miwili Ila kwa makubaliano kuwa nikipata pesa yao kabla ya huo muda naweza kulipa pesa yao tukaachana.

Kweli nilipambana kwa namna yangu na Hali yangu Hadi nikapata pesa yao baada ya miezi mitatu tu na biashara yangu inaendelea.

Tatizo limeanza pale niliporudi kwao Banc ABC kutaka balance yangu ili niwalipe tuachane.

Ni mwezi wa nne Sasa tangu niombe kulipa Deni kuanzia mwezi wa tano Hadi wa Tisa (mwezi huu) wananisumbua, hawataki kunipatia balance (kiasi kilichobakia).

Msaada tafadhari nifanyeje nilipe Deni?

Sitaki kudaiwa Ila wananilazimisha, Wazo langu ilikuwa niwapeleke mahakamani Ila nimewaza huenda Kuna sehemu naweza kuanzia kuepusha lawama zisizo na msingi.

Msaada wa hatua za kuanzia...
uza deni hilo aidha kwa CRDB,NMB au bank yeyote alafu utawalipa hao walionunua hilo deni.

Hivyo Bank ABC watalipwa na bank husika sio wewe tena.
 
Banc ABC na Bayport, tofauti yao ni majina tu. Ukikubali kuingia nao mkataba, basi utambue fika maelekezo waliyokuambia kupitia mdomo, ni tofauti kabisa na yale ya kwenye mkataba wao.

Pole sana mtoa mada.
 
Poa poa, watumie e mail now. Nakuhakikishia hadi kufika jumatatu benki yako watakua wamekupigia simu na ku resolve the issue. Hawa BoT ndo kiboko ya mabenki wahuni wahuni. Mimi tangu nigundue hilo, dealings zangu na benki zimekua rahisi sana. Mgaa gaa upwa
Usisahau kutuletea mrejesho pia ukifanikisha.
Nakuhakikishia mrejesho nitaleta maana wamenisumbua mno.
 
Naona imejibadilisha yenyewe
Screenshot_20240906-125127.png
 
Bank inakutumiaje nyaraka Whatsapp.

Mtaalam kusanya document zako hakikisha Watu zaidi wanajua hili ndani ya bank na upande wako.

Pia tumia email mara zote kwenye mambo ya kiofisi
Ndiyo maana nilikuwa na mpango wa kuanzia mahakamani kufungua shauri la madai ya mkataba hard copy.
 
Hapa Tanzania ukitaka upewe huduma kwa haraka bila kubabaisha jitahidi sana siku ya kwanza kabisa waseme "HUYU MTEJA/JAMAA SIO MWELEWA"... Ukiwa mstaarabu utaonewa sana. Kwenye biashara hakuna kuoneana huruma wala haya. Wakikuona sio mwelewa siku nyingine ukienda watakuhudumia haraka ili kuepusha shari.

Halafu wewe ni mfanyabiashara wa aina gani unachukua mkopo wa miaka miwili na kurejesha ndani ya miezi mitatu? Ina maana biashara yako haikuhitaji kukuzwa zaidi? Au uli-bet ukapata hela ya kulipa? Wewe pia upande wako kuna ukakasi. Benki kukataa kulipwa hela zao zote na riba ya miaka miwili ndani ya miezi mitatu watakuwa hawana akili timamu. Hiyo hela yako ukiwapa mapema wataizungusha tena na kupiga hela zaidi. Mteja anayelipa fasta huwa anapendwa mno na mabenki.
 
Hapa Tanzania ukitaka upewe huduma kwa haraka bila kubabaisha jitahidi sana siku ya kwanza kabisa waseme "HUYU MTEJA/JAMAA SIO MWELEWA"... Ukiwa mstaarabu utaonewa sana. Kwenye biashara hakuna kuoneana huruma wala haya. Wakikuona sio mwelewa siku nyingine ukienda watakuhudumia haraka ili kuepusha shari.

Halafu wewe ni mfanyabiashara wa aina gani unachukua mkopo wa miaka miwili na kurejesha ndani ya miezi mitatu? Ina maana biashara yako haikuhitaji kukuzwa zaidi? Au uli-bet ukapata hela ya kulipa? Wewe pia upande wako kuna ukakasi. Benki kukataa kulipwa hela zao zote na riba ya miaka miwili ndani ya miezi mitatu watakuwa hawana akili timamu. Hiyo hela yako ukiwapa mapema wataizungusha tena na kupiga hela zaidi. Mteja anayelipa fasta huwa anapendwa mno na mabenki.
Nilichukua pesa yao nikaweka kwenye biashara yangu ya uchuuzi wa mazao, yaani miezi miwili tu kwa kuzungusha kijijini kuleta mjini tayari nimepata faida na mtaji umesimama,

Si unajua huku tunaishi na mazao ya msimu
 
Nenda BOT mkuu kila mkoa wapo alafu usiwe mstarabu sana sometimes jifanye fyatu fyatu nchi ngumu hii
 
Back
Top Bottom