Iselamagazi
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 6,020
- 6,161
What a poor argument!Mbona Mwalimu Nyerere aliishi kwenye Ikulu iliyojengwa na Mkoloni.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
What a poor argument!Mbona Mwalimu Nyerere aliishi kwenye Ikulu iliyojengwa na Mkoloni.
Mzee pekee anayezeeka vizuri ni Mzee Hashim Rungwe.Huyo Mzee ameshaona amezeeka, hivyo hana ulazima wa kumlamba miguu
Uislam wake unatusaidia nini sisi?Kisa Rais ni muislamu basi mtaongea sana, kisa mwekezaji ni muarabu basi mtaongea sana, lakini wapo ambao sio waislamu lakini wanaunga mkono suala la DP, Mungu ambariki mama samia, Mungu awabariki wawekezaji
Sio
Raisi amepokewa kwa mapenzi makubwa sana na Watanganyika, na ni kati ya Marais wanaopendwa sana.
Ni kwamba tunamsaidia ili tuzidi kumpenda.
Mtoto kipenzi lazima umchape fimbo anapokosea ili aende sawa.
Mzee Rungwe amekomenti Chochote juu ya Bandari zetu kuuzwa?Mzee pekee anayezeeka vizuri ni Mzee Hashim Rungwe.
Uislam wake unatusaidia nini sisi?
Mzee katupandisha mpaka kwenye suala la MuunganoDr. Slaa anauliza swali gumu sana hapa kuhusu DG wa Bandari Zanzibar. Inabidi wakajipange
HahahahMimi nimeshaanza taratibu za kwenda kuomba Uraia Zanzibar, huku bara si hatujielewi wacha tuuzwe na Viongozi wetu aina ya Chifu Mangungo [emoji2957]
Una hoja hata yule Mwarabu wa Arab Contractors aliyepewa kazi na Magufuli bila kushindanishwa kwenye zabuni ingekuwa ni Samia matusi yangenyesha kama mvua.Mfano ingetokea mzungu amepewa unadhani kelele hizi zingekuwepo!!! Refer migodi ya dhahabu na almasi n.k lawama hizi na matusi kem kem yalikuwepo!! Kisa mwarabu amepewa!!!
Imefikia mtu anamtukana mama Rais wetu Samia Suluh hassan, Allah amlinde na amuepushe na watu wabaya
View attachment 2656188
Mokaze adriz imhotep zitto junior Zitto zuberi kabwe
Una hoja hata yule Mwarabu wa Arab Contractors aliyepewa kazi na Magufuli bila kushindanishwa kwenye zabuni ingekuwa ni Samia matusi yangenyesha kama mvua.
Balozi Dkt. Willibrod Slaa anazungumza na Wanahabari Jijini Dar es Salaam, leo Juni 13 2023 kuhusu hati ya makubaliano yaliyoingiwa kati ya Tanzania na DP World.
=======
Dkt. Slaa: Hadi kufikia hatua ya azimio hili kuridhiwa na Bunge, ikumbukwe makubaliano ya awali yalifanyika tarehe 28 February, kampuni ya DP World na bandari waliingia kwenye makubaliano yalitokana na shughuli iliyofanyika Dubai expo 2022, hatujaambiwa ni tathmini gani au utafiti gani ulifanyika
Kwenye expo, kwenye maonesho kama yale ya sabasaba Dar es Salaam watu wanaingia kwenye mkataba mkubwa wa kulifunga Taifa, nadhani mnaelewa hiyo maana yake ni nini!
Hadi wakati huu Taifa na watanzania walikuwa hawajapewa taarifa yoyote ile inayohusu mkataba mkubwa wa aina hiyo.
Naomba kuwakumbusha pia kuwa pamoja na mkataba huu, katika Dubai 2020 Serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Rais mwenyewe kulisainiwa mikataba 17, nani kati yenu hadi leo hii anaifahamu mikataba 17 inahusu nini, ni usiri mtupu, ni nchi inaingizwa kwenye giza, Rais wa Nchi amehudhuria lakini mambo hayo yote yako ndani ya giza.
Waliohudhuria maonesho ni viongozi wa Serikali, wamesafiri, wamelala hoteli, wamekula chakula kwa kodi ya watanzania, ni Tanzania pekee ambako Serikali haiwajibiki kwa wananchi wake, jambo ambalo katika hatua hii, jambo ambalo linalazimisha kuwakumbusha uhitaji wa haraka wa katiba mpya na bora.
Hii taarifa tunayozungumzia hatukuipata Serikalini, tumepata taarifa iliyovuja. Ni nchi gani duniani tunasubiri taarifa ivuje tuanze kuizungumzia. Siku siku 30 zilizotajwa kwenye mkataba na Bunge, kwa maneno mengine umeridhiwa ndani ya siku 30 lakini umekuja kuridhiwa baada ya miezi takribani 8, kwa hali hiyo tuna uhakika gani Tanzania ina uwezo wa kutimiza mkataba huu kama mwanzo tayari ni mbaya na hakuna anayeeleza uchelewashaji huo unatokana na nini.
Dkt. Slaa ametoa hoja zifuatazo
Dkt. Slaa: Niseme yafatayo
- Dkt. Slaa: Nchi inayojulikana kisheria ni United Arab Emirates, Je Dubai ni Serikali? Dubai ni mji unaojiongoza, sisi ni nchi ya Jamhuri ambayo maamuzi yetu yanafanyika kwa kutumia Bunge. Bunge lilitangaza wanataka maoni ya wananchi tarehe 5 Juni wanaotoka maeneo mbalimbali wawe wamefika bungeni tarehe 6. Kwa saa 24 mtanzania gani anafika Dodoma na kutoa maoni yake. Ni dhahiri kuliwa na hila na Serikali haikuwa na nia ya kushirikisha wananchi wake. Hatukushirikishwa na imepelekwa bungeni na mjadala ulivyokuwa bungeni ulikuwa ni mjadala wa ki-mangimushi
- Aidha ikumbukwe Serikali iliyopo ina legitimacy ya wasiwasi kutokana na uchaguzi wa 2019 na 2020. Simung'unyi maneno, uchaguzi wa 2019 na 2020 inaweza kuwa na legitimacy lakini sina hakika kama uchaguzi huo ulikuwa sahihi, najua ulivurugwa kwa makusudi na chama cha mapinduzi na vyombo vyake. Mwenye macho haitaji kuambiwa kuhusu hilo na wananchi wote ni mashahidi.
- Kwa mujibu wa kifungu cha nne cha IGA kinatamka wazi rasilimali zote zilizotajwa zinakabidhiwa kwa Serikali ya kigeni. Rasilimali hizo ni bandari zote za nchi nzima(bahari, maziwa, mito, zitakazokuwepo hata kwenye mabwawa) yale yote yaliyokuwepo leo na hata yatakayokuja. Huu ni uuzaji wa nchi, hakuna mtanzania mwenye akili atakaekubali jambo hilo bila uhakika wa rasilimali zake hizo.
- Serikali ya awamu ya nne wakati inataka kutaifisha mashirika muhimu ikiwemo bandari, aliyetupa taarifa alifukuzwa kazi. Alitupa taarifa ya kutokubali kuyataifisha kutokana umuhimu wake kwa usalama wa Taifa.
Dkt. Slaa ameongelea mfano wa mbia katika kampuni ya mafuta wakati wa vita ya Uganda ambapo Tanzania ilikuwa inamiliki 51% katika kampuni hiyo huku mbia akiwa na 49% lakini aliweka ngumu kwasababu alidai mtu tunayepigana nae ni mbia wake pia hivyo. Slaa amedai kwa siku 5 vifaa havikuweza kuondoka kwasababu ya mafuta wakati nchi inaendelea kupigwa.- Slaa pia ametoa mfano wa 'Entebbe Raid' ambapo amesema ndege ya Air France ilitekwa nyara na wapiganaji wa Palastine wakishinikiza mambo yao ya kisiasa ndani ikiwa na waisraiel ilitua uwanja wa Entebbe. Slaa amedai Waisrael iliwachukua chini ya dakika 90 kuwakomboa watu wao na amedai iliwezekana kwasababu wao ndio waliojenga uwanja na ramani zote walikuwa nazo ikiwepo sehemu ya kuingilia na kutokea.
- Slaa amesema sababu hapo juu pia ilisababisha Serikali ya awamu ya tano itumie wajenzi wa ndani kujenga Ikulu lakini sasa bandari zote zinakabidhiwa kwa mgeni.
- Dkt. Slaa: Mkataba unaotoa 'exclusive rights' daima uogope, inatoa pia kifungu baadae yatakayojadiliwa kwenye mikataba midogo midogo, unatoa kwanza mali yako, unajuaje wakifika kwenye hiyo mikataba midogo midogo wakikutalia! Una nguvu gani, ulishasain 'exclusive rights'
- Utekelezaji wa DP World sio kwamba unaanza Tanzania, katika Afrika peke yake tuna migogoro mingi. Nenda nchi za Ulaya, Brussels ni ya Ulaya lakini wako mahakamani, karibu kote kunakogombaniwa ni rushwa, kuna wabungwe walipelekwa, wakalishwa, wakapewa posho ya dola 2000 yote hiyo ni rushwa. Kama ingekuwa nchi nyingine, hizo zinatosha kufuta mkataba huu na kapeleka hata hiyo kampuni mahakamani.
- Sijawahi kuona mkataba(IGA) Marekani na Ulaya ambao una lugha kama hii ya kwetu, waathirika tumewaandaaje mfano ujenzi wa reli bandarini mpaka airport. Tumeona barabara ya Kibaha watu walivyolia Kimara. Mikataba hii lazima iwe ya tahadhari sana.
- Tunayasema haya kwa nia njema lakini tunashangazwa na kutishwa na propaganda ambayo Serikali inafanya, jambo jema huwa haliendeshwi kwa propaganda, ukiona mtu anafanya propaganda ikiwa ni pamoja na kwenda kwenye madhehebu ya dini anza kuweka mashaka, kuna maslahi gani nyuma ya makubaliano hayo!
Dkt. Slaa: Natoa wito kwa watanzania wote kwa pamoja tusikubali kupokea upotoshwaji aina yoyote katika mambo yanayotuhusu sisi wenyewe na vizazi vyetu vijavyo. Mkataba huu ujadiliwe upya, uangaliwe upya tuweze kukubaliana vitu gani vifanyike.
- Kwa lugha rahisi, taarifa hii haina lengo la kupinga. Hoja ya msingi ni kukosekana kwa uwazi katika namna ya kushughulia rasimali ya nchi yetu
- Vifungu vingi vinavyotia mashaka vinahitaji kuangaliwa upya hata kama mkataba ni mzuri au mbaya, unaweza kuboreshwa kwa kushauriana na wananchi wake. Mkataba wowote hata kama ni mbaya, mzuri unaweza kuboreshwa. Mkataba huu utazamwe upya ili vipengele vyote vyenye utata viondolewe.
Mfano tunaona mkataba huu wanasema ni nchi nzima, bandari zote. Kwanini tusiseme bandari ya Dar es Salaam, mengine yote tutaingia wakati tumeridhika.
Mkataba hauweki muda maalum, kwanini tusiseme tutakuwa na mkataba wa bandari kwa miaka 10, tena kuna kifungu kinazungumza hatutaweza kuondoa. Halafu kuna masharti kama tunataka kuondoa tufanye nini, unaweka masharti. Haya masharti yote wanajua ni ya kutupiga, hata mkienda kwenye mahakama ya malalamiko tumeshapigwa tayari. Hata Serikali ikibadilika hatuwezi kuondoa mkataba huu.
- Bandari inazungumzia upande mmoja wa Tanzania, nimeshangaa na watu hawakosei. Wanasema Rais ni kutoka upande mmoja wa muungano, waziri wake ni kutoka upande huo huo wa muungano. Tafsiri za watu huwezi kuzifungia kwenye sanduku, huwezi kuzuia watanzania wasifikiri kwasababu Rais anatoka upande huu, waziri wake ndio maana wameuza bandari zetu, mbona zile hazikuuzwa.
Slaa amesema suala la bandari ni la muungano lakini ameshangazwa kwa Zanzibar kuwa na sheria ya bandari yao. Slaa ameshangazwa na nchi moja kuwa na bandari mbili ilhali sheria ni moja.
Dkt: Slaa: Mbona hawalielezi hata bungeni hilo, kumbe kuna mambo mengi hata bunge limefichwa na bunge letu jinsi lilivyo la hovyo, naomba radhi sana na waniite kwa hilo, kilichofanyika juzi ni uhuni.
Tuseme LC300 V6. Maana LC300 hazina V8 engineHakuna V8 mpya na Msukuma hajanunua V8 mwaka 2023
Ameukaribisha uwekezaji kwenye Bandari zetu lakini amesema CCM daima huungia Mikataba mibovu.Mzee Rungwe amekomenti Chochote juu ya Bandari zetu kuuzwa?
Sijamsikia bado
Naona Unataka upate chako mapema Mkuu 🙌
Mbona hapo ni kama ameridhia tuuzweAmeukaribisha uwekezaji kwenye Bandari zetu lakini amesema CCM daima huungia Mikataba mibovu.
Watukanaji wengi hawana hoja hawaziwezi hoja na wamejifijicha kwenye Udini na chuki dhidi ya Wanawake.Yani basi tu, wanakera sana
Balozi Dkt. Willibrod Slaa anazungumza na Wanahabari Jijini Dar es Salaam, leo Juni 13 2023 kuhusu hati ya makubaliano yaliyoingiwa kati ya Tanzania na DP World.
=======
Dkt. Slaa: Hadi kufikia hatua ya azimio hili kuridhiwa na Bunge, ikumbukwe makubaliano ya awali yalifanyika tarehe 28 February, kampuni ya DP World na bandari waliingia kwenye makubaliano yalitokana na shughuli iliyofanyika Dubai expo 2022, hatujaambiwa ni tathmini gani au utafiti gani ulifanyika
Kwenye expo, kwenye maonesho kama yale ya sabasaba Dar es Salaam watu wanaingia kwenye mkataba mkubwa wa kulifunga Taifa, nadhani mnaelewa hiyo maana yake ni nini!
Hadi wakati huu Taifa na watanzania walikuwa hawajapewa taarifa yoyote ile inayohusu mkataba mkubwa wa aina hiyo.
Naomba kuwakumbusha pia kuwa pamoja na mkataba huu, katika Dubai 2020 Serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Rais mwenyewe kulisainiwa mikataba 17, nani kati yenu hadi leo hii anaifahamu mikataba 17 inahusu nini, ni usiri mtupu, ni nchi inaingizwa kwenye giza, Rais wa Nchi amehudhuria lakini mambo hayo yote yako ndani ya giza.
Waliohudhuria maonesho ni viongozi wa Serikali, wamesafiri, wamelala hoteli, wamekula chakula kwa kodi ya watanzania, ni Tanzania pekee ambako Serikali haiwajibiki kwa wananchi wake, jambo ambalo katika hatua hii, jambo ambalo linalazimisha kuwakumbusha uhitaji wa haraka wa katiba mpya na bora.
Hii taarifa tunayozungumzia hatukuipata Serikalini, tumepata taarifa iliyovuja. Ni nchi gani duniani tunasubiri taarifa ivuje tuanze kuizungumzia. Siku siku 30 zilizotajwa kwenye mkataba na Bunge, kwa maneno mengine umeridhiwa ndani ya siku 30 lakini umekuja kuridhiwa baada ya miezi takribani 8, kwa hali hiyo tuna uhakika gani Tanzania ina uwezo wa kutimiza mkataba huu kama mwanzo tayari ni mbaya na hakuna anayeeleza uchelewashaji huo unatokana na nini.
Dkt. Slaa ametoa hoja zifuatazo
Dkt. Slaa: Niseme yafatayo
- Dkt. Slaa: Nchi inayojulikana kisheria ni United Arab Emirates, Je Dubai ni Serikali? Dubai ni mji unaojiongoza, sisi ni nchi ya Jamhuri ambayo maamuzi yetu yanafanyika kwa kutumia Bunge. Bunge lilitangaza wanataka maoni ya wananchi tarehe 5 Juni wanaotoka maeneo mbalimbali wawe wamefika bungeni tarehe 6. Kwa saa 24 mtanzania gani anafika Dodoma na kutoa maoni yake. Ni dhahiri kuliwa na hila na Serikali haikuwa na nia ya kushirikisha wananchi wake. Hatukushirikishwa na imepelekwa bungeni na mjadala ulivyokuwa bungeni ulikuwa ni mjadala wa ki-mangimushi
- Aidha ikumbukwe Serikali iliyopo ina legitimacy ya wasiwasi kutokana na uchaguzi wa 2019 na 2020. Simung'unyi maneno, uchaguzi wa 2019 na 2020 inaweza kuwa na legitimacy lakini sina hakika kama uchaguzi huo ulikuwa sahihi, najua ulivurugwa kwa makusudi na chama cha mapinduzi na vyombo vyake. Mwenye macho haitaji kuambiwa kuhusu hilo na wananchi wote ni mashahidi.
- Kwa mujibu wa kifungu cha nne cha IGA kinatamka wazi rasilimali zote zilizotajwa zinakabidhiwa kwa Serikali ya kigeni. Rasilimali hizo ni bandari zote za nchi nzima(bahari, maziwa, mito, zitakazokuwepo hata kwenye mabwawa) yale yote yaliyokuwepo leo na hata yatakayokuja. Huu ni uuzaji wa nchi, hakuna mtanzania mwenye akili atakaekubali jambo hilo bila uhakika wa rasilimali zake hizo.
- Serikali ya awamu ya nne wakati inataka kutaifisha mashirika muhimu ikiwemo bandari, aliyetupa taarifa alifukuzwa kazi. Alitupa taarifa ya kutokubali kuyataifisha kutokana umuhimu wake kwa usalama wa Taifa.
Dkt. Slaa ameongelea mfano wa mbia katika kampuni ya mafuta wakati wa vita ya Uganda ambapo Tanzania ilikuwa inamiliki 51% katika kampuni hiyo huku mbia akiwa na 49% lakini aliweka ngumu kwasababu alidai mtu tunayepigana nae ni mbia wake pia hivyo. Slaa amedai kwa siku 5 vifaa havikuweza kuondoka kwasababu ya mafuta wakati nchi inaendelea kupigwa.- Slaa pia ametoa mfano wa 'Entebbe Raid' ambapo amesema ndege ya Air France ilitekwa nyara na wapiganaji wa Palastine wakishinikiza mambo yao ya kisiasa ndani ikiwa na waisraiel ilitua uwanja wa Entebbe. Slaa amedai Waisrael iliwachukua chini ya dakika 90 kuwakomboa watu wao na amedai iliwezekana kwasababu wao ndio waliojenga uwanja na ramani zote walikuwa nazo ikiwepo sehemu ya kuingilia na kutokea.
- Slaa amesema sababu hapo juu pia ilisababisha Serikali ya awamu ya tano itumie wajenzi wa ndani kujenga Ikulu lakini sasa bandari zote zinakabidhiwa kwa mgeni.
- Dkt. Slaa: Mkataba unaotoa 'exclusive rights' daima uogope, inatoa pia kifungu baadae yatakayojadiliwa kwenye mikataba midogo midogo, unatoa kwanza mali yako, unajuaje wakifika kwenye hiyo mikataba midogo midogo wakikutalia! Una nguvu gani, ulishasain 'exclusive rights'
- Utekelezaji wa DP World sio kwamba unaanza Tanzania, katika Afrika peke yake tuna migogoro mingi. Nenda nchi za Ulaya, Brussels ni ya Ulaya lakini wako mahakamani, karibu kote kunakogombaniwa ni rushwa, kuna wabungwe walipelekwa, wakalishwa, wakapewa posho ya dola 2000 yote hiyo ni rushwa. Kama ingekuwa nchi nyingine, hizo zinatosha kufuta mkataba huu na kapeleka hata hiyo kampuni mahakamani.
- Sijawahi kuona mkataba(IGA) Marekani na Ulaya ambao una lugha kama hii ya kwetu, waathirika tumewaandaaje mfano ujenzi wa reli bandarini mpaka airport. Tumeona barabara ya Kibaha watu walivyolia Kimara. Mikataba hii lazima iwe ya tahadhari sana.
- Tunayasema haya kwa nia njema lakini tunashangazwa na kutishwa na propaganda ambayo Serikali inafanya, jambo jema huwa haliendeshwi kwa propaganda, ukiona mtu anafanya propaganda ikiwa ni pamoja na kwenda kwenye madhehebu ya dini anza kuweka mashaka, kuna maslahi gani nyuma ya makubaliano hayo!
Dkt. Slaa: Natoa wito kwa watanzania wote kwa pamoja tusikubali kupokea upotoshwaji aina yoyote katika mambo yanayotuhusu sisi wenyewe na vizazi vyetu vijavyo. Mkataba huu ujadiliwe upya, uangaliwe upya tuweze kukubaliana vitu gani vifanyike.
- Kwa lugha rahisi, taarifa hii haina lengo la kupinga. Hoja ya msingi ni kukosekana kwa uwazi katika namna ya kushughulia rasimali ya nchi yetu
- Vifungu vingi vinavyotia mashaka vinahitaji kuangaliwa upya hata kama mkataba ni mzuri au mbaya, unaweza kuboreshwa kwa kushauriana na wananchi wake. Mkataba wowote hata kama ni mbaya, mzuri unaweza kuboreshwa. Mkataba huu utazamwe upya ili vipengele vyote vyenye utata viondolewe.
Mfano tunaona mkataba huu wanasema ni nchi nzima, bandari zote. Kwanini tusiseme bandari ya Dar es Salaam, mengine yote tutaingia wakati tumeridhika.
Mkataba hauweki muda maalum, kwanini tusiseme tutakuwa na mkataba wa bandari kwa miaka 10, tena kuna kifungu kinazungumza hatutaweza kuondoa. Halafu kuna masharti kama tunataka kuondoa tufanye nini, unaweka masharti. Haya masharti yote wanajua ni ya kutupiga, hata mkienda kwenye mahakama ya malalamiko tumeshapigwa tayari. Hata Serikali ikibadilika hatuwezi kuondoa mkataba huu.
- Bandari inazungumzia upande mmoja wa Tanzania, nimeshangaa na watu hawakosei. Wanasema Rais ni kutoka upande mmoja wa muungano, waziri wake ni kutoka upande huo huo wa muungano. Tafsiri za watu huwezi kuzifungia kwenye sanduku, huwezi kuzuia watanzania wasifikiri kwasababu Rais anatoka upande huu, waziri wake ndio maana wameuza bandari zetu, mbona zile hazikuuzwa.
Slaa amesema suala la bandari ni la muungano lakini ameshangazwa kwa Zanzibar kuwa na sheria ya bandari yao. Slaa ameshangazwa na nchi moja kuwa na bandari mbili ilhali sheria ni moja.
Dkt: Slaa: Mbona hawalielezi hata bungeni hilo, kumbe kuna mambo mengi hata bunge limefichwa na bunge letu jinsi lilivyo la hovyo, naomba radhi sana na waniite kwa hilo, kilichofanyika juzi ni uhuni.
Ni huyu johnthebaptistWEKENI
Updates za maandishi msiwe kama yule jamaa anayependa kuweka bandiko ili awe wa kwanza na andiko lisilo na maelezo ya kina.