Bandari ya Dar es Salaam ina changamoto za Mafanikio

Makala imeonyesha hatua zote ambazo Bandari inapitia. msongamano na wingi wa wateja ni vitu viwili tofauti
 
Inawezekana sana tu na inaendelea kufanywa na watanzania. wawekezaji wanaoimbwa wamekaribishwa katika GATI NNE tu au TANO kati ya GATI 12 tulizonazo pale DAR PORT
 
Tungepata uchambuzi kama huu wakati wa DP wala tusingehamaki aisee. mnajifichaga wakati wa songombingo kukipoa ndio mnajitokeza na data za hivi. Mungu anawaona
 
Makala imeonyesha hatua zote ambazo Bandari inapitia. msongamano na wingi wa wateja ni vitu viwili tofauti

..makala uliyoileta inajenga picha kwamba MSONGAMANO ktk bandari yetu ni jambo la kujivunia, na huduma nzuri kwa WATEJA.
 
BANDARI YA DSM NA CHANGAMOTO ZA MAFANIKIO
  • Ni baada ya ukamilishaji wa mradi wa DMGP, uimarishaji wa mifumo na utekelezaji wa maelekezo na matamanio ya Rais Dkt. Samia katika mapinduzi ya Bandari

Tuwasiliane :- shaibusufiani@gmail.com
Theoretically uko sawa, lakini bado kuna uzembe kwenye upakuaji meli. Meli kwa Dar es Salaam inachukua hadi siku 16 kupakuliwa wakati Mombasa ni siku 2. Wakenya wanatucheka sana. Tena wanadai kuna Watanzania wameamua kupitisha mizigo yao Mombasa.

Bandari yetu ya Dar es salaam iko karibu na Congo, Zambia, Malawi, Burundi, Rwanda na Uganda kuliko Bandari ya Mombasa. Bandari hii inazidiwa na Mombasa mara 2 kiufanisi Kama Serikali ingefanya kazi vizuri Bandari hii inaweza kuchangia Trilion 6- 8 kwa mwaka
 
BANDARI YA DSM NA CHANGAMOTO ZA MAFANIKIO
  • Ni baada ya ukamilishaji wa mradi wa DMGP, uimarishaji wa mifumo na utekelezaji wa maelekezo na matamanio ya

Shaibu Sufiani

Tuwasiliane :- shaibusufiani@gmail.com
Hakika ndugu mtoa uzi umeandika vizuri sana na hizi zote ni juhud za Rais Samia na zinapaswa kuungwa mkono na kila mtanzania japo wapo wale wazee wa kupinga kila kitu wakija humu na kuona mazuri ya bandari yetu watasema unalipwa kusemea mema na mafaniko ya bandarin yetu ya DAR
 
..makala uliyoileta inajenga picha kwamba MSONGAMANO ktk bandari yetu ni jambo la kujivunia, na huduma nzuri kwa WATEJA.
hapo mtoa uzi kazungumzia wakati wa sasa na ule uliopita na kulinganisha mazuri na mabovu yote lakini kaona kwa sasa utendaji wetu wa bandari ni wa kuungwa mkono na kupongezwa kwa juhud hizi zinazoendelea kuoneshwa
 
Sidhani kama ni uzembe ni swala dogo sana na jepesi kuhusu namba. kama magati yapo 12 na meli zilizotia nanga ni 30 automatically meli 16 plus zitakuwa zinasubiri wenzake washushe...a simple logic ni kama shuleni tu tunavyopeanaga zamu wengine wanaingia asubuhi wengine mchana. kwenye Bandari tufurahie hatua ya kwanza soo limefunguka vyema. sasa hatua ya pili tuone maboresho zaidi na zaidi yakitokea ikiwemo kuongeza magati nakadharika
 
Kinacho kosekana ni nia madhubuti ya kuwekeza katika vitendea kazi ili huo utanisi au upakuaji wa mizigo uwe wa haraka, na usafirishaji wa kutumia treni.
 
Kinacho kosekana ni nia madhubuti ya kuwekeza katika vitendea kazi ili huo utanisi au upakuaji wa mizigo uwe wa haraka, na usafirishaji wa kutumia treni.
Na hizo ndio fursa ambazo watanzania na wasio watanzania tunapaswa kuzichungulia kwa haraka.
 
hapo mtoa uzi kazungumzia wakati wa sasa na ule uliopita na kulinganisha mazuri na mabovu yote lakini kaona kwa sasa utendaji wetu wa bandari ni wa kuungwa mkono na kupongezwa kwa juhud hizi zinazoendelea kuoneshwa

..MSONGAMANO maana yake ni inefficiency.

..hivi unafikiri WATEJA wa bandari yetu wanafurahia msongamano?

.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…